Mika 5 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mika 5:1-15

Mtawala Aliyeahidiwa Kutoka Bethlehemu

15:1 Ay 16:10; Mt 27:30; Mao 3:30Panga majeshi yako, ee mji wa majeshi,

kwa kuwa kuzingirwa kumepangwa dhidi yetu.

Watampiga mtawala wa Israeli

shavuni kwa fimbo.

25:2 Yn 7:42; Mwa 35:19; 48:7; 1Sam 13:14; Hes 24:19; 2Sam 6:21; 2Nya 7:18; Za 90:2; 132:6; 102:25; Isa 9:6; Mit 8:22; Yn 1:1; Mt 2:6“Lakini wewe, Bethlehemu Efrathi,

ingawa u mdogo miongoni mwa koo za Yuda,

kutoka kwako atatokea kwa ajili yangu

yeye atakayekuwa mtawala katika Israeli,

ambaye asili yake ni kutoka zamani,

kutoka milele.”

35:3 Yer 7:29Kwa hiyo Israeli utaachwa mpaka wakati

mwanamke aliye na utungu atakapozaa

na ndugu zake wengine warudi

kujiunga na Waisraeli.

45:4 Isa 40:11; 49:9; 52:13; Za 72:8; Zek 9:10; Mik 7:14; Eze 34:11-15; Lk 1:32Atasimama na kulichunga kundi lake

katika nguvu ya Bwana,

katika utukufu wa jina la Bwana Mungu wake.

Nao wataishi kwa usalama, kwa kuwa wakati huo

ukuu wake utaenea hadi miisho ya dunia.

55:5 Isa 8:7; 9:6; 10:24-27; Lk 2:14; Efe 2:14; Kol 1:19-20Naye atakuwa amani yao.

Ukombozi Na Uharibifu

Wakati Mwashuru atakapovamia nchi yetu

na kupita katika ngome zetu,

tutawainua wachungaji saba dhidi yake,

hata viongozi wanane wa watu.

65:6 Mwa 10:8; Sef 2:13; Lk 1:71; Nah 2:11-13Wataitawala nchi ya Ashuru kwa upanga,

nchi ya Nimrodi kwa upanga.

Atatuokoa kutoka kwa Mwashuru

atakapoivamia nchi yetu

na kuingia katika mipaka yetu.

75:7 Amo 5:15; Mik 2:12; Isa 44:4; Za 110:3; 133:3Mabaki ya Yakobo yatakuwa

katikati ya mataifa mengi

kama umande kutoka kwa Bwana,

kama manyunyu juu ya majani,

ambayo hayamngoji mtu

wala kukawia kwa mwanadamu.

85:8 Mwa 49:9; Mik 4:13; Zek 10:5; Isa 5:29; Za 50:22; Hos 5:14Mabaki ya Yakobo yatakuwa miongoni mwa mataifa,

katikati ya mataifa mengi,

kama simba miongoni mwa wanyama wa msituni,

kama mwana simba miongoni

mwa makundi ya kondoo,

ambaye anaumiza vibaya na kuwararua

kila anapopita katikati yao,

wala hakuna awezaye kuokoa.

95:9 Za 10:12Mkono wako utainuliwa juu kwa ushindi juu ya watesi wako,

nao adui zako wote wataangamizwa.

105:10 Kut 15:4, 19; Hos 14:3; Hag 2:22; Zek 9:10“Katika siku ile,” asema Bwana,

“nitaangamiza farasi zenu katikati yenu

na kubomoa magari yenu ya vita.

115:11 Kum 29:23; Isa 6:11; Mao 2:2; Hos 10:14; Amo 5:9Nitaiangamiza miji ya nchi yenu

na kuziangusha chini ngome zenu zote.

125:12 Kum 18:10-12; Isa 8:19; 2:9Nitaangamiza uchawi wenu

na hamtapiga tena ramli.

135:13 Nah 1:14; Hos 2:10; Isa 2:8; 2:18; Eze 6:9; Zek 13:2Nitaangamiza vinyago vyenu vya kuchonga

na mawe yenu ya ibada yatoke katikati yenu;

hamtasujudia tena

kazi ya mikono yenu.

145:14 Kut 34:13; Amu 3:7; 2Fal 17:10Nitangʼoa nguzo za Ashera katikati yenu

na kubomoa miji yenu.

155:15 Isa 65:12Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu

juu ya mataifa ambayo hayajanitii.”

King James Version

Micah 5:1-15

1Now gather thyself in troops, O daughter of troops: he hath laid siege against us: they shall smite the judge of Israel with a rod upon the cheek. 2But thou, Beth-lehem Ephratah, though thou be little among the thousands of Judah, yet out of thee shall he come forth unto me that is to be ruler in Israel; whose goings forth have been from of old, from everlasting.5.2 everlasting: Heb. the days of eternity 3Therefore will he give them up, until the time that she which travaileth hath brought forth: then the remnant of his brethren shall return unto the children of Israel.

4¶ And he shall stand and feed in the strength of the LORD, in the majesty of the name of the LORD his God; and they shall abide: for now shall he be great unto the ends of the earth.5.4 feed: or, rule 5And this man shall be the peace, when the Assyrian shall come into our land: and when he shall tread in our palaces, then shall we raise against him seven shepherds, and eight principal men.5.5 principal: Heb. princes of 6And they shall waste the land of Assyria with the sword, and the land of Nimrod in the entrances thereof: thus shall he deliver us from the Assyrian, when he cometh into our land, and when he treadeth within our borders.5.6 waste: Heb. eat up5.6 in the…: or, with her own naked swords

7And the remnant of Jacob shall be in the midst of many people as a dew from the LORD, as the showers upon the grass, that tarrieth not for man, nor waiteth for the sons of men.

8¶ And the remnant of Jacob shall be among the Gentiles in the midst of many people as a lion among the beasts of the forest, as a young lion among the flocks of sheep: who, if he go through, both treadeth down, and teareth in pieces, and none can deliver.5.8 sheep: or, goats 9Thine hand shall be lifted up upon thine adversaries, and all thine enemies shall be cut off. 10And it shall come to pass in that day, saith the LORD, that I will cut off thy horses out of the midst of thee, and I will destroy thy chariots: 11And I will cut off the cities of thy land, and throw down all thy strong holds: 12And I will cut off witchcrafts out of thine hand; and thou shalt have no more soothsayers: 13Thy graven images also will I cut off, and thy standing images out of the midst of thee; and thou shalt no more worship the work of thine hands.5.13 standing…: or, statues 14And I will pluck up thy groves out of the midst of thee: so will I destroy thy cities.5.14 cities: or, enemies 15And I will execute vengeance in anger and fury upon the heathen, such as they have not heard.