Mika 3 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mika 3:1-12

Viongozi Na Manabii Wakemewa

13:1 Yer 5:5Kisha nikasema,

“Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo,

enyi watawala wa nyumba ya Israeli.

Je, hampaswi kujua hukumu,

23:2 Za 53:4; Eze 22:27ninyi mnaochukia mema

na kupenda maovu;

ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi

na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;

33:3 Za 14:4; Sef 3:3; Ay 24:14; Eze 11:7; 24:4-5; 34:4ninyi mnaokula nyama ya watu wangu,

mnaowachuna ngozi

na kuvunja mifupa yao vipande vipande;

mnaowakatakata kama nyama

ya kuwekwa kwenye sufuria

na kama nyama

ya kuwekwa kwenye chungu?”

43:4 Kum 1:45; 31:17; 1Sam 8:18; Yer 11:11; Isa 58:4; Mit 1:28; Ay 15:31; Eze 8:18Kisha watamlilia Bwana,

lakini hatawajibu.

Wakati huo atawaficha uso wake

kwa sababu ya uovu waliotenda.

53:5 Isa 3:12; 9:16; 53:6; 56:10; Mt 7:15; Yer 4:10Hili ndilo asemalo Bwana:

“Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu,

mtu akiwalisha,

wanatangaza ‘amani’;

kama hakufanya hivyo,

wanaandaa kupigana vita dhidi yake.

63:6 Isa 8:19-22; 29:10; Eze 7:26; 12:24Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono,

na giza, msiweze kubashiri.

Jua litawachwea manabii hao,

nao mchana utakuwa giza kwao.

73:7 Yer 6:15; Mik 7:16; Isa 44:25; Es 6:12; Za 74:9; Amu 8:11; Law 13:45; Eze 20:3Waonaji wataaibika

na waaguzi watafedheheka.

Wote watafunika nyuso zao

kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”

83:8 1Kor 2:1, 4; Isa 58:1; 57:12; 61:2Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu,

nimejazwa Roho wa Bwana,

haki na uweza,

kumtangazia Yakobo kosa lake,

na Israeli dhambi yake.

93:9 Isa 58:1-2; 1:23Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo,

enyi watawala wa nyumba ya Israeli,

mnaodharau haki

na kupotosha kila lililo sawa;

103:10 Yer 22:13, 17; Isa 59:7; Mik 7:2; Hab 2:12; Nah 3:1; Eze 22:27mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu

na Yerusalemu kwa uovu.

113:11 Kut 23:8; Law 19:15; Mal 2:9; Eze 22:12; Mik 7:3; Yer 6:13; 1Tim 1:11; 1Sam 4:5-6; Eze 13:19; 34:2; Isa 1:23; 10:20; 56:11; Yer 6:13; 7:4; Mao 4:13; Hos 4:8, 18Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa,

na makuhani wake wanafundisha kwa malipo,

nao manabii wake wanatabiri kwa fedha.

Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema,

“Je, Bwana si yumo miongoni mwetu?

Hakuna maafa yatakayotupata.”

123:12 2Fal 25:9; Isa 6:11; Mik 1:6; Za 79:1; Yer 52:13; 22:6; Mao 5:18; Eze 5:14Kwa hiyo kwa sababu yenu,

Sayuni italimwa kama shamba,

Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto,

na kilima cha Hekalu

kitakuwa kichuguu

kilichofunikwa na vichaka.

Hoffnung für Alle

Micha 3:1-12

Gottes Urteil über die führenden Männer und falschen Propheten

1Ich, Micha, sagte: Hört her, ihr führenden Männer Israels, ihr Nachkommen von Jakob! Eigentlich solltet ihr doch das Recht kennen. 2-3Aber ihr hasst das Gute und liebt das Böse. Ihr geht mit meinem Volk um wie mit Schlachtvieh, dem man die Haut abzieht, das Fleisch herunterschneidet und die Knochen zerhackt. Dann werft ihr alles zusammen in einen Topf und lasst es euch schmecken! 4Doch es kommt der Tag, da werdet ihr zum Herrn um Hilfe schreien, aber er wird euch nicht mehr anhören. Er will nichts mehr mit euch zu tun haben wegen all eurer Verbrechen.

5Auch für eure Propheten hat der Herr eine Botschaft! Glück und Frieden sagen sie denen voraus, die ihnen zu essen geben. Doch wer ihnen keine Geschenke gibt, dem drohen sie mit Gottes Strafgericht. Weil sie das Volk in die Irre führen, kündigt Gott ihnen an: 6»Finsterste Nacht wird über euch hereinbrechen, so dass ihr nicht mehr in die Zukunft schauen könnt und vergeblich auf Visionen wartet. Die Sonne wird nicht mehr für euch scheinen, selbst am helllichten Tag tappt ihr im Dunkeln. 7Mit eurer Wahrsagerei und euren Prophezeiungen ist es dann endgültig vorbei, ihr müsst euch in Grund und Boden schämen! Denn ich antworte nicht mehr, wenn ihr mich befragt. Ihr könnt nur noch vor Trauer euer Gesicht verhüllen.«

8Mich aber hat der Herr mit seinem Geist erfüllt. Er gibt mir die Kraft und den Mut, für das Recht einzutreten und den Israeliten ihre Vergehen vorzuwerfen. Ich nenne ihre Sünden beim Namen.

9Hört her, ihr führenden Männer Israels, ihr Nachkommen von Jakob! Ihr verabscheut das Recht und setzt euch bedenkenlos darüber hinweg. 10Ihr baut Jerusalem aus und geht dabei über Leichen, eure Häuser sind auf Unrecht gegründet. 11Die Richter sind bestechlich, die Priester lassen sich für jeden Rat gut bezahlen, und auch die Propheten schlagen Geld aus ihrer Wahrsagerei. Doch alle berufen sich auf den Herrn und behaupten: »Der Herr ist mitten unter uns, es kann uns nichts passieren!«

12Darum wird der Berg Zion zu einem umgepflügten Acker werden, die Stadt Jerusalem zu einem Trümmerhaufen, und auf dem Tempelberg wird das Gestrüpp wuchern! Ihr seid schuld daran, dass dies alles so kommt!