Mhubiri 7 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 7:1-29

Hekima

17:1 Ufu 14:13; Wim 1:3; Mit 22:1; Ay 10:18Afadhali sifa nzuri kuliko manukato safi,

nayo siku ya kufa kuliko ya kuzaliwa.

27:2 Za 90:12; Mit 11:19; Mhu 2:14Afadhali kwenda kwenye nyumba ya msiba

kuliko kwenda kwenye nyumba ya karamu,

kwa kuwa kifo ni hatima ya kila mwanadamu,

imewapasa walio hai kuliweka hili mioyoni mwao.

37:3 2Kor 7:10; Mit 14:13Huzuni ni afadhali kuliko kicheko,

kwa sababu uso wenye huzuni wafaa kwa moyo.

47:4 Mhu 2:1; Yer 16:8Moyo wa wenye hekima uko katika nyumba ya msiba,

lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya anasa.

57:5 Za 141:5; Mit 13:18; 15:31-32Afadhali kusikia karipio la mtu mwenye hekima,

kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.

67:6 Za 58:9; Mhu 2:2; Mit 14:13Kama ilivyo kuvunjika kwa miiba chini ya sufuria,

ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu.

Hili nalo pia ni ubatili.

77:7 Kut 18:21; 23:8; Kum 16:19Dhuluma humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu,

nayo rushwa huuharibu moyo.

87:8 Mit 14:29; Gal 5:22Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake,

uvumilivu ni bora kuliko kiburi.

97:9 Mit 16:32; 14:17, 29; Mt 5:22Usiwe mwepesi kukasirika rohoni mwako,

kwa kuwa hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.

10Usiseme, “Kwa nini siku za kale zilikuwa bora kuliko siku hizi?”

Kwa maana si hekima kuuliza maswali kama hayo.

117:11 Mit 8:10-11; Mhu 2:13; 11:7Hekima, kama ulivyo urithi, ni kitu chema

na huwafaidia wale walionalo jua.

12Hekima ni ulinzi kama fedha ilivyo ulinzi,

lakini faida ya maarifa ni hii:

kwamba hekima huhifadhi maisha ya aliye nayo.

137:13 Isa 14:27; Mhu 2:24; 1:15Tafakari kile Mungu alichokitenda:

Nani awezaye kunyoosha

kile ambacho yeye amekipinda?

147:14 Ay 1:21; Mhu 2:24Nyakati zikiwa nzuri, ufurahi,

lakini nyakati zikiwa mbaya, tafakari:

Mungu amefanya hiyo moja,

naam, sanjari7:14 Sanjari hapa maana yake mwandamano wa vitu, wanyama au watu. na hiyo nyingine.

Kwa hiyo, mwanadamu hawezi kugundua

kitu chochote kuhusu maisha yake ya baadaye.

157:15 Mhu 8:14; Yer 12:1; Ay 21:7; 7:7Katika maisha haya yangu ya ubatili nimeshaona haya mawili:

mtu mwadilifu akiangamia katika uadilifu wake,

naye mtu mwovu akiishi maisha marefu katika uovu wake.

16Usiwe mwenye haki kupita kiasi,

wala usiwe na hekima kupita kiasi:

kwa nini kujiangamiza mwenyewe?

177:17 Ay 15:32; Za 55:23Usiwe mwovu kupita kiasi,

wala usiwe mpumbavu:

kwa nini kufa kabla ya wakati wako?

187:18 Mhu 3:14Ni vyema kushika hilo moja

na wala usiache hilo jingine likupite.

Mtu amchaye Mungu ataepuka huko kupita kiasi.7:18 Au: atafuata hayo yote mawili.

197:19 Mhu 2:13; 9:13-18; Mit 8:14Hekima humfanya yeye aliye nayo kuwa na uwezo zaidi

kuliko watawala kumi katika mji.

207:20 1Fal 8:46; Rum 3:12, 23; Gal 3:22; Za 14:3; Mit 20:9; Ay 4:17Hakuna mtu mwenye haki duniani

ambaye hufanya mambo ya haki

na kamwe asitende dhambi.

217:21 Mit 30:10Usitie maanani kila neno linalosemwa na watu,

la sivyo, waweza kumsikia

mtumishi wako akikulaani:

22kwa kuwa unafahamu moyoni mwako

kwamba wewe mwenyewe mara nyingi

umewalaani wengine.

237:23 Mhu 1:17; Rum 1:22Yote haya niliyajaribu kwa hekima, nikasema,

“Nimeamua kuwa na hekima”:

lakini hii ilikuwa nje ya uwezo wangu.

247:24 Ay 28:12; 11:12; Isa 55:8-9Vyovyote hekima ilivyo,

hekima iko mbali sana na imejificha,

ni nani awezaye kuigundua?

257:25 Ay 28:3; Mhu 1:17Nikageuza fikira zangu ili kuelewa,

kuchunguza na kuitafuta hekima

na kusudi la mambo,

na ili kuelewa ujinga wa uovu,

na wazimu wa upumbavu.

267:26 Kut 10:7; Amu 14:15; Mit 7:23; 22:14; 2:16-19; 5:3-5Nimeona jambo lililo chungu kuliko mauti,

mwanamke ambaye ni mtego,

ambaye moyo wake ni wavu wa kutegea

na mikono yake ni minyororo.

Mtu ampendezaye Mungu atamkwepa,

bali mwenye dhambi atanaswa naye.

27Mhubiri anasema, “Tazama, hili ndilo nililogundua:

“Nimegundua kitu kimoja baada ya kingine nilipokuwa katika kusudi la mambo:

287:28 1Fal 11:3ningali natafiti

lakini sipati:

nilimpata mwanaume mmoja mnyofu miongoni mwa elfu,

lakini hakuna mwanamke mmoja mnyofu miongoni mwao.

29Hili ndilo peke yake nililolipata:

Mungu amemuumba mwanadamu mnyofu,

lakini mwanadamu amebuni mambo mengi.”

Japanese Contemporary Bible

伝道者の書 7:1-29

7

知恵について

1良い評判を得ることは、

最高級の香水より値打ちがあり、

死ぬ日は生まれた日より大切である。

2宴会に顔を出すより、

葬式に列席するほうがよい。

やがて死ぬわけだから、

生きているうちに死について考えるのは良いことだ。

3悲しみは笑いにまさっている。

悲しみは、私たちの心から

不純物を取り除く効果があるからだ。

4知恵ある者は死についてじっくり考えるが、

愚か者はどうしたら今

愉快に過ごせるかだけを考える。

5愚か者からちやほやされるより、

知恵ある者に痛烈な批評を受けるほうが良い。

6愚か者のお世辞は、火にくべた紙切れのように、

何の役にも立たない。

そんなものに心を動かすのは、

なんとむなしいことか。

7知恵ある者も、わいろによって愚かな者になる。

わいろは人の判断力を麻痺させるからだ。

8終わりは初めにまさっている。

忍耐は高慢にまさっている。

9短気を起こしてはならない。

短気は愚か者の特徴だからだ。

10過ぎ去った昔の栄光に未練を残してはいけない。

ほんとうに昔が今より良かったか、わからないからだ。

11知恵ある者になることは、金持ちになるのと同じくらい

いや、それ以上の価値がある。

12知恵からでも金銭からでも、

利益を上げることができる。

しかし賢くなることのほうが、

多くの利点がある。

13神のすることに目を留め、それに従いなさい。神が決めたことを変えることなどできません。 14順境のときには、できるだけ楽しみなさい。逆境が訪れたら、神は与えると同時に取り上げる方だと知りなさい。こうしてすべての人が、この世ではあらゆるものがむなしいと悟るのです。

15-17私は、このむなしい人生のすべてを見てきました。正しい人が若死にし、悪人がたいそう長生きすることもあるのです。だから、正しすぎたり、知恵がありすぎたりして、自滅してはいけません。かといって、悪人になりすぎるのも、愚か者になるのも考えものです。自分の時が来る前に死んではいけません。 18任せられた仕事は、どんなことがあっても手放してはいけません。神を敬っているなら、必ず神からの祝福を期待できるのです。

19知恵ある者は、町の十人の有力者の力を合わせたより力があります。 20この世界には、いつも品行方正で一度も罪を犯さない人など一人もいません。

21-22人の言うことをすべて気にしてはいけません。時として使用人からのろわれるかもしれません。あなたも、何度も人をのろったはずです。

23私は知恵ある者になろうと、できるだけのことをしてみました。「知恵ある者になりたい」と人前で言ってみましたが、知恵ある者になることはできませんでした。 24知恵は遠いかなたにあって、探し出すのはきわめて困難です。 25私は知恵と道理を見つけようと、あらゆる所を探しました。また、悪行が愚かで、愚かさがどれほどばかげたことであるか悟ろうとしました。

26悪い女は死よりも大きな苦痛を与えます。神に喜ばれる者は恵みによって彼女から逃れますが、罪を犯す者は彼女のしかけた罠にかかってしまいます。

27-28そこで、「私の結論はこうだ」と伝道者は言います。私はあらゆる方面から調べてみて、次のことを確信するようになりました。私が話を聞いた男の千人に一人は、確かに知恵がある人物です。しかし女には、知恵のある者は一人もいませんでした。 29さらに、次のことも知りました。神は人を正しい者に造ったのに、人々は堕落の道に向かって行ったということです。