Mhubiri 6 – NEN & NVI-PT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 6:1-12

1Nimeona ubaya mwingine chini ya jua, nao unalemea sana wanadamu: 26:2 Kum 8:7-10; Za 17:14; Amu 18:10; Mhu 5:13-19Mungu humpa mwanadamu utajiri, mali na heshima, hivyo hakukosa chochote moyo wake unachokitamani. Lakini Mungu hamwezeshi kuvifurahia, badala yake mgeni ndiye anayevifurahia. Hili ni ubatili, ni ubaya unaosikitisha.

36:3 Ay 3:3, 16; Es 7:10; Mhu 4:3Mtu anaweza kuwa na watoto mia moja naye akaishi miaka mingi, lakini haidhuru kuwa ataishi muda mrefu kiasi gani, kama hawezi kufurahia mafanikio yake na kwamba hapati mazishi ya heshima, ninasema afadhali mtoto aliyezaliwa akiwa amekufa kuliko yeye. 4Kuzaliwa kwake hakuna maana, huondokea gizani na gizani jina lake hufunikwa. 5Ingawa hakuwahi kuliona jua wala kujua kitu chochote, yeye ana pumziko zaidi kuliko mtu huyo, 66:6 Mhu 2:16Hata kama huyo mtu ataishi miaka elfu mara mbili na zaidi, lakini akashindwa kufurahia mafanikio yake, je, wote hawaendi sehemu moja?

76:7 Mit 16:26; 27:20; 1Tim 6:6-8Juhudi zote za binadamu ni kwa ajili ya kinywa chake,

hata hivyo hamu yake kamwe haitoshelezwi.

86:8 Mhu 2:15Mtu mwenye hekima ana faida gani

zaidi ya mpumbavu?

Mtu maskini anapata faida gani

kwa kujua jinsi ya kujistahi

mbele ya watu wengine?

9Ni bora kile ambacho jicho linakiona

kuliko hamu isiyotoshelezwa.

Hili nalo ni ubatili,

ni kukimbiza upepo.

106:10 Ay 9:32; Isa 45:9; Mhu 3:15Lolote lililopo limekwisha kupewa jina,

naye mwanadamu alivyo ameshajulikana;

hakuna mtu awezaye kushindana

na mwenye nguvu kuliko yeye.

11Maneno yanavyokuwa mengi,

ndivyo yanavyokosa maana,

Je, hilo linamfaidia vipi yeyote?

126:12 Yak 4:14; Ay 10:20; 20:8; 14:2; 1Nya 29:15; Za 39:6Kwa maana ni nani anayejua lililo jema kwa ajili ya maisha ya mwanadamu, katika siku chache na za ubatili anazopita kama kivuli? Ni nani awezaye kumwambia yatakayotokea chini ya jua baada ya yeye kuondoka?

Nova Versão Internacional

Eclesiastes 6:1-12

1Vi ainda outro mal debaixo do sol, que pesa bastante sobre a humanidade: 2Deus dá riquezas, bens e honra ao homem, de modo que não lhe falta nada que os seus olhos desejam; mas Deus não lhe permite desfrutar tais coisas, e outro as desfruta em seu lugar. Isso não faz sentido; é um mal terrível.

3Um homem pode ter cem filhos e viver muitos anos. No entanto, se não desfrutar as coisas boas da vida, digo que uma criança que nasce morta e nem ao menos recebe um enterro digno tem melhor sorte que ele. 4Ela nasce em vão e parte em trevas, e nas trevas o seu nome fica escondido. 5Embora jamais tenha visto o sol ou conhecido qualquer coisa, ela tem mais descanso do que tal homem. 6Pois, de que lhe valeria viver dois mil anos, sem desfrutar a sua prosperidade? Afinal, não vão todos para o mesmo lugar?

7Todo o esforço do homem é feito para a sua boca;

contudo, o seu apetite jamais se satisfaz.

8Que vantagem tem o sábio em relação ao tolo?

Que vantagem tem o pobre

em saber como se portar diante dos outros?

9Melhor é contentar-se com o que os olhos veem

do que sonhar com o que se deseja.

Isso também não faz sentido;

é correr atrás do vento.

10Tudo o que existe já recebeu nome,

e já se sabe o que o homem é;

não se pode lutar contra alguém mais forte.

11Quanto mais palavras,

mais tolices6.11 Ou menos sentido; ou ainda mais frustração,

e sem nenhum proveito.

12Na verdade, quem sabe o que é bom para o homem, nos poucos dias de sua vida vazia, em que ele passa como uma sombra? Quem poderá contar-lhe o que acontecerá debaixo do sol depois que ele partir?