Mhubiri 5 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 5:1-20

Simama Katika Kicho Cha Mungu

15:1 Za 89:7; Kut 3:5; Hos 6:6Linda hatua zako uendapo katika nyumba ya Mungu. Karibia usikilize kuliko kutoa dhabihu ya wapumbavu, ambao hawajui kuwa wanafanya kosa.

25:2 Amu 11:35; Ay 6:24; Mit 10:19; 20:25Usiwe mwepesi kuzungumza,

usiwe na haraka katika moyo wako

kuzungumza lolote mbele za Mungu.

Mungu yuko mbinguni

nawe uko duniani,

kwa hiyo maneno yako

na yawe machache.

35:3 Ay 20:8; Mhu 10:14Kama vile ndoto huja

wakati kuna shughuli nyingi,

ndivyo yalivyo mazungumzo ya mpumbavu

wakati kuna maneno mengi.

45:4 Mwa 28:20; Kum 23:21; Hes 30:2; Za 76:11; 119:60; Amu 11:35Wakati unapomwekea Mungu nadhiri, usikawie kuitimiza. Yeye hafurahii wapumbavu; timiza nadhiri yako. 55:5 Yon 2:9; Mdo 5:4; Hes 30:2-4Ni afadhali usiweke nadhiri kuliko kuiweka na usiitimize. 6Usiruhusu kinywa chako kukuingiza dhambini. Tena usijitetee mbele ya huyo mjumbe wa hekaluni, ukisema, “Niliweka nadhiri kwa makosa.” Kwa nini Mungu akasirike kwa ajili ya yale unayosema na kuiharibu kazi ya mikono yako? 75:7 Kum 10:12; Mhu 3:14; 12:13Kuota ndoto kwingi na maneno mengi ni ubatili. Kwa hiyo simama katika kicho cha Mungu.

Utajiri Ni Ubatili

85:8 Mhu 3:16; 4:1; Za 12:5Kama ukiona maskini wanaonewa katika nchi, hukumu na haki vikipotoshwa, usishangazwe na mambo hayo, kwa maana afisa mmoja anaangaliwa na aliye juu yake zaidi na juu ya hao wawili kuna wengine walio juu zaidi yao. 9Mafanikio ya nchi ni kwa ajili ya wote, hata mfalme mwenyewe hufaidi kutoka mashambani.

10Yeyote apendaye fedha kamwe

hatosheki na fedha;

yeyote apendaye utajiri kamwe

hatosheki na kipato chake.

Hili nalo pia ni ubatili.

11Mali ikiongezeka, ndivyo walaji

wanavyoongezeka.

Hii nayo inamfaidia nini mwenye mali

isipokuwa ni kushibisha macho yake?

125:12 Ay 20:20Usingizi wa kibarua ni mtamu,

awe amekula kidogo au kingi,

lakini wingi wa mali

humnyima tajiri usingizi.

135:13 Mhu 6:1-2Nimeshaona uovu mzito chini ya jua:

Utajiri uliolimbikizwa kwa kujinyima

na kuleta madhara kwa mwenye mali,

14au utajiri uliopotea kwa bahati mbaya,

hivyo kwamba wakati akiwa na mwana

hakuna chochote kilichobaki kwa ajili yake.

155:15 Za 49:17; 1Tim 6:7; Ay 1:21; Mhu 1:3Mtu hutoka tumboni mwa mama yake uchi,

naye jinsi alivyokuja vivyo hivyo huondoka.

Hachukui chochote kutokana na kazi yake

ambacho anaweza kukibeba mkononi mwake.

165:16 Mit 11:29; Mhu 1:3Hili nalo ni baya la kusikitisha:

Kama vile mtu ajavyo, vivyo hivyo huondoka,

naye anapata faida gani,

maadamu hutaabika kwa ajili ya upepo?

17Siku zake zote hula gizani,

pamoja na fadhaa kubwa,

mateso na hasira.

185:18 Mhu 2:3, 10, 14, 24Ndipo nikatambua kwamba ni vyema na sahihi kwa mtu kula na kunywa na kutosheka katika kazi yake ngumu chini ya jua katika siku chache za maisha yake Mungu alizompa, kwa maana hili ndilo fungu lake. 195:19 1Nya 29:12; 2Nya 1:12; Ay 31:2; Mhu 2:24; 6:2Zaidi ya yote, Mungu anapompa mtu yeyote utajiri na milki, humwezesha kuvifurahia, kukubali fungu lake na kuwa na furaha katika kazi yake, hii ni karama ya Mungu. 205:20 Kum 12:7, 18; Kut 23:25Mara chache mtu huzifikiri siku za maisha yake, kwa sababu Mungu humfanya ashikwe na furaha ya moyoni.

La Bible du Semeur

Ecclésiaste 5:1-19

1Ne te presse pas d’ouvrir la bouche et ne te laisse pas entraîner par ton cœur à formuler hâtivement une parole en présence de Dieu, car Dieu est au ciel, et toi tu es sur la terre. Que tes propos soient donc peu nombreux. 2En effet, de même que les rêves naissent de la multitude des occupations, de même un flot abondant de paroles engendre des propos inconsidérés.

3Si tu as fait un vœu à Dieu, accomplis-le sans tarder5.3 Pour les règles régissant les vœux, voir Dt 23.22-24 ; 1 S 1.11, 24-28., car les insensés déplaisent à Dieu. Ce que tu as promis, tiens-le. 4Il vaut mieux ne pas faire de vœu qu’en faire et ne pas s’en acquitter.

5Ne laisse pas tes paroles te charger d’une faute et ne va pas dire au représentant de Dieu5.5 C’est-à-dire le prêtre chargé de présenter à Dieu les vœux des fidèles (Ml 2.7). : « Mon vœu était une erreur. » Pourquoi irriter Dieu par tes paroles et faire échouer tes entreprises ? 6C’est pourquoi, là où il y a abondance de rêves et multiplication de paroles légères5.6 Autre traduction : Car beaucoup de vaines rêveries aboutissent à beaucoup de paroles en l’air., crains plutôt Dieu.

La hiérarchie oppressive

7Si tu vois dans une région que les pauvres sont opprimés, que la justice et le droit sont bafoués, ne t’étonne pas trop de la chose, car chaque dirigeant dépend du pouvoir5.7 L’hébreu peut signifier deux choses : soit que le dirigeant subordonné est couvert par son supérieur, soit qu’il est soumis aux pressions exercées par son supérieur. d’un supérieur, et au-dessus d’eux, il y a encore des supérieurs hiérarchiques. 8Mais malgré tout, ceci demeure dans l’intérêt du pays : qu’au profit de l’agriculture, on se soumette au roi5.8 Autres traductions : qu’il y ait un roi au service de l’agriculture ; ou bien : le roi est lui aussi dépendant de l’agriculture..

Sur la richesse

9Qui aime l’argent n’en aura jamais assez, et qui se complaît dans l’abondance ne sera jamais satisfait de ses revenus. Cela encore est dérisoire.

10Plus on possède de biens, plus se multiplient les profiteurs. Et quel avantage en tire leur possesseur si ce n’est le spectacle que lui offrent ces gens ?

11Doux est le sommeil du travailleur, qu’il ait peu ou beaucoup à manger, mais l’abondance du riche l’empêche de dormir.

12J’ai vu sous le soleil une terrible calamité : il arrive que les richesses conservées par un homme fassent son malheur. 13Qu’elles viennent à se perdre à cause de quelque mauvaise affaire, et il ne lui en reste rien lorsqu’il met un fils au monde. 14Il est sorti nu du sein de sa mère, et il partira comme il est venu, sans emporter dans ses mains une miette du fruit de son labeur. 15Qu’il reparte comme il était venu est aussi une terrible calamité. Quel avantage a-t-il donc à trimer ainsi pour du vent ? 16Sa vie durant, ses jours s’écoulent bien sombres, pleins de chagrins, de souffrances et d’amertume.

Conclusion : Jouis de la vie que Dieu te donne

17Voici ce que j’ai considéré comme bon pour ma part : il est approprié pour l’homme de manger, de boire et de goûter au bonheur au milieu de tout le labeur qui lui donne tant de peine sous le soleil, pendant les jours que Dieu lui donne à vivre ; c’est là sa part. 18En effet, si Dieu donne à un homme des richesses et des biens, et s’il lui accorde la possibilité d’en profiter, d’en retirer sa part et de trouver de la joie au milieu de son labeur, c’est un don de Dieu. 19Ainsi cet homme ne s’appesantit pas sur sa vie5.19 Autre traduction : ne réfléchit pas à la brièveté de sa vie. puisque Dieu le tient occupé à la joie5.19 D’après les versions anciennes. D’autres comprennent : Dieu lui répond par la joie. qui remplit son cœur.