Mhubiri 3 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 3:1-22

Kila Jambo Lina Wakati Wake

13:1 Mhu 8:6Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo,

nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:

23:2 Mwa 47:29; Isa 28:24; 38:1wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa,

wakati wa kupanda na wakati wa kungʼoa yaliyopandwa,

33:3 Kum 5:17wakati wa kuua na wakati wa kuponya,

wakati wa kubomoa,

na wakati wa kujenga,

43:4 Kut 15:20; 2Sam 6:16wakati wa kulia na wakati wa kucheka,

wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,

5wakati wa kutawanya mawe na wakati wa kukusanya mawe,

wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia,

6wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza,

wakati wa kuweka na wakati wa kutupa,

73:7 Amo 5:13; Es 4:14wakati wa kurarua na wakati wa kushona,

wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza,

8wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia,

wakati wa vita na wakati wa amani.

9Mfanyakazi anapata faida gani kutokana na taabu yake? 103:10 Mhu 1:13Nimeona mzigo Mungu alioweka juu ya wanadamu. 113:11 Kum 32:4; Mhu 8:17; Ay 11:7; 28:23; Rum 11:33Amefanya kila kitu kiwe kizuri kwa wakati wake. Pia ameiweka hiyo milele katika mioyo ya wanadamu, wala hawawezi kutambua kwa kina yale ambayo Mungu amefanya tangu mwanzo hadi mwisho. 12Ninajua kwamba hakuna kitu bora kwa wanadamu kuliko kuwa na furaha na kutenda mema wakati wanapoishi. 133:13 Za 34:12; Kum 12:7, 18; Mhu 2:3, 24; 5:19Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote. 143:14 Ay 23:15; Yak 1:17; Mhu 5:7; 7:18; 8:12-13Ninajua kwamba kila kitu anachokifanya Mungu kitadumu milele, hakuna kinachoweza kuongezwa au kupunguzwa. Mungu hufanya hivyo ili watu wamche yeye.

153:15 Mhu 6:10; 1:9Chochote kilichopo kilishakuwepo,

na kitakachokuwepo kimekwishakuwepo kabla;

naye Mungu huyaita yale yaliyopita yarudi tena.

16Pia nikaona kitu kingine tena chini ya jua:

Mahali pa kutolea hukumu,

uovu ulikuwepo,

mahali pa kupatia haki,

uovu ulikuwepo.

173:17 Ay 34:11; 19:29; Mt 16:27; Mhu 11:9; 12:14Nikafikiri moyoni mwangu,

“Mungu atawaleta hukumuni

wote wawili wenye haki na waovu,

kwa maana kutakuwako na wakati kwa ajili ya kila jambo,

wakati kwa ajili ya kila tendo.”

183:18 Za 73:22Pia nikafikiri, “Kuhusu wanadamu, Mungu huwajaribu ili wajione kwamba wao ni kama wanyama. 193:19 Mhu 2:14; Za 49:12Hatima ya mwanadamu ni kama ile ya wanyama; wote wana mwisho unaofanana: Jinsi anavyokufa mnyama, ndivyo anavyokufa mwanadamu. Wote wana pumzi inayofanana; mwanadamu hana cha zaidi kuliko mnyama. Kila kitu ni ubatili. 203:20 Mwa 2:7; 3:19-20; Ay 34:10Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi. 213:21 Mhu 12:7Ni nani ajuaye kama roho ya mtu huenda juu na roho ya mnyama hushuka chini ardhini?”

223:22 Mhu 2:10, 24; 5:18; Ay 31:2Kwa hiyo nikaona kwamba hakuna kitu kilicho bora zaidi kwa mwanadamu kuliko kuifurahia kazi yake, kwa sababu hilo ndilo fungu lake. Kwa maana ni nani awezaye kumrudisha ili aje kuona kile kitakachotendeka baada yake?

King James Version

Ecclesiastes 3:1-22

1To every thing there is a season, and a time to every purpose under the heaven: 2A time to be born, and a time to die; a time to plant, and a time to pluck up that which is planted;3.2 to be…: Heb. to bear 3A time to kill, and a time to heal; a time to break down, and a time to build up; 4A time to weep, and a time to laugh; a time to mourn, and a time to dance; 5A time to cast away stones, and a time to gather stones together; a time to embrace, and a time to refrain from embracing;3.5 to refrain from: Heb. to be far from 6A time to get, and a time to lose; a time to keep, and a time to cast away;3.6 get: or, seek 7A time to rend, and a time to sew; a time to keep silence, and a time to speak; 8A time to love, and a time to hate; a time of war, and a time of peace. 9What profit hath he that worketh in that wherein he laboureth? 10I have seen the travail, which God hath given to the sons of men to be exercised in it.

11He hath made every thing beautiful in his time: also he hath set the world in their heart, so that no man can find out the work that God maketh from the beginning to the end. 12I know that there is no good in them, but for a man to rejoice, and to do good in his life. 13And also that every man should eat and drink, and enjoy the good of all his labour, it is the gift of God. 14I know that, whatsoever God doeth, it shall be for ever: nothing can be put to it, nor any thing taken from it: and God doeth it, that men should fear before him. 15That which hath been is now; and that which is to be hath already been; and God requireth that which is past.3.15 that which is past: Heb. that which is driven away

16¶ And moreover I saw under the sun the place of judgment, that wickedness was there; and the place of righteousness, that iniquity was there. 17I said in mine heart, God shall judge the righteous and the wicked: for there is a time there for every purpose and for every work. 18I said in mine heart concerning the estate of the sons of men, that God might manifest them, and that they might see that they themselves are beasts.3.18 that God…: or, that they might clear God, and see, etc 19For that which befalleth the sons of men befalleth beasts; even one thing befalleth them: as the one dieth, so dieth the other; yea, they have all one breath; so that a man hath no preeminence above a beast: for all is vanity. 20All go unto one place; all are of the dust, and all turn to dust again. 21Who knoweth the spirit of man that goeth upward, and the spirit of the beast that goeth downward to the earth?3.21 of man: Heb. of the sons of man3.21 goeth upward: Heb. is ascending, etc 22Wherefore I perceive that there is nothing better, than that a man should rejoice in his own works; for that is his portion: for who shall bring him to see what shall be after him?