Mhubiri 2 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mhubiri 2:1-26

Anasa Ni Ubatili

12:1 Za 10:6; Lk 12:19; Mhu 7:4; 8:15Nikafikiri moyoni mwangu, “Haya basi, nitakujaribu kwa anasa nione ni lipi lililo jema.” Lakini hilo nalo likaonekana ni ubatili. 22:2 Mit 14:13; Isa 22:12-13; Mhu 7:6Nikasema, “Kicheko nacho ni upumbavu. Nayo matokeo ya anasa ni nini?” 32:3 Amu 9:13; Rut 3:3; Amo 6:3-6; Mhu 3:12-13; 5:18; 8:15Nikajaribu kujifurahisha kwa mvinyo na kukumbatia upumbavu, huku bado akili yangu inaniongoza kwa hekima. Nilitaka kuona ni lipi bora watu wafanye kwa siku chache wanazoishi chini ya mbingu.

42:4 1Fal 7:1-12; Wim 8:11; 2Nya 2:1Nikafanya miradi mikubwa: Nikajijengea majumba na kulima mashamba ya mizabibu. 5Nikatengeneza bustani na viwanja vya starehe nikaotesha huko kila aina ya miti ya matunda. 6Nikajenga mabwawa ya kukusanya maji ya kunyweshea hii miti iliyokuwa inastawi vizuri. 7Nikanunua watumwa wa kiume na wa kike na watumwa wengine walizaliwa nyumbani mwangu. Pia nilikuwa na makundi ya ngʼombe, kondoo na mbuzi kuliko mtu yeyote aliyewahi kuishi Yerusalemu kabla yangu. 82:8 1Fal 9:28; 10:10-21; 2Sam 19:35; Amu 3:15Nikajikusanyia fedha na dhahabu, hazina za wafalme na za majimbo. Nikajipatia waimbaji wanaume na wanawake, nazo nyumba za masuria: vitu ambavyo moyo wa mwanadamu hufurahia. 92:9 1Nya 29:25; Mhu 1:12-16Nikawa maarufu sana kuliko mtu mwingine yeyote aliyepata kuishi Yerusalemu kabla yangu. Katika haya yote bado nikawa nina hekima.

10Sikujinyima kitu chochote ambacho macho yangu yalikitamani,

hakuna anasa ambayo niliunyima moyo wangu.

Moyo wangu ulifurahia kazi zangu zote,

hii ilikuwa thawabu ya kazi zangu zote.

11Hata hivyo nilipokuja kuangalia yote ambayo

mikono yangu ilikuwa imefanya

na yale niliyotaabika kukamilisha,

kila kitu kilikuwa ni ubatili, ni kukimbiza upepo;

hapakuwa na faida yoyote chini ya jua.

Hekima Na Upumbavu Ni Ubatili

12Kisha nikageuza mawazo yangu kufikiria hekima,

wazimu na upumbavu.

Ni nini zaidi mtu anayetawala baada ya mfalme

anachoweza kufanya ambacho hakijafanywa?

132:13 Mhu 7:11-12, 19; 9:18Nikaona kuwa hekima ni bora kuliko upumbavu,

kama vile nuru ilivyo bora kuliko giza.

142:14 Za 49:10; Mit 17:24; Mhu 8:1; 3:19; 7:2; 9:3, 11-12Mtu mwenye hekima ana macho katika kichwa chake,

lakini mpumbavu anatembea gizani;

lakini nikaja kuona kwamba

wote wawili hatima yao inafanana.

152:15 Mhu 6:8Kisha nikafikiri moyoni mwangu,

“Hatima ya mpumbavu itanipata mimi pia.

Nitafaidi nini basi kwa kuwa na hekima?”

Nikasema moyoni mwangu,

“Hili nalo ni ubatili.”

162:16 Za 49:10; 112:6; Mhu 1:11Kwa maana kwa mtu mwenye hekima,

kama ilivyo kwa mpumbavu,

hatakumbukwa kwa muda mrefu,

katika siku zijazo wote watasahaulika.

Kama vile ilivyo kwa mpumbavu,

mtu mwenye hekima pia lazima atakufa!

Kutaabika Ni Ubatili

17Kwa hiyo nikachukia maisha, kwa sababu kazi inayofanyika chini ya jua ilikuwa masikitiko kwangu. Yote hayo ni ubatili, ni kukimbiza upepo. 182:18 Za 39:6; 49:10; 1Fal 12:13Nikachukia kila kitu nilichokuwa nimetaabikia chini ya jua, kwa sababu ni lazima nimwachie yule ajaye baada yangu. 19Nani ajuaye kama atakuwa ni mtu mwenye hekima au mpumbavu? Lakini hata hivyo yeye ndiye atakayetawala kazi zote ambazo nimemiminia juhudi na ustadi chini ya jua. Hili nalo ni ubatili. 20Kwa hiyo moyo wangu ukaanza kukata tamaa juu ya kazi yangu yote niliyoifanya kwa taabu chini ya jua. 21Kwa kuwa mtu anaweza kufanya kazi yake kwa hekima, maarifa na ustadi, kisha analazimika kuacha vyote alivyo navyo kwa mtu mwingine ambaye hajavifanyia kazi. Hili nalo pia ni ubatili tena ni balaa kubwa. 222:22 Mhu 3:9; 1:3Mtu atapata nini kwa taabu yote na kuhangaika kwa bidii katika kazi anayotaabikia chini ya jua? 232:23 Ay 5:7; 7:2; 14:1; Mhu 1:18; Mwa 3:17Siku zake zote kazi yake ni maumivu na masikitiko, hata usiku akili yake haipati mapumziko. Hili nalo pia ni ubatili.

242:24 1Kor 15:32; Mhu 3:12-13, 22; 7:7-10; 8:15; 5:17-19; 9:7-10; 11:7-10; Ay 2:10Hakuna kitu bora anachoweza kufanya mtu zaidi ya kula na kunywa na kuridhika katika kazi yake. Hili nalo pia, ninaona, latokana na mkono wa Mungu, 25kwa sababu pasipo yeye, ni nani awezaye kula na kufurahi? 262:26 Ay 27:17; 9:4; Mit 13:22Kwa yule mtu anayempendeza Mungu, Mungu humpa hekima, maarifa na furaha, bali kwa mwenye dhambi Mungu humpa kazi ya kukusanya na kuhifadhi utajiri ili Mungu ampe yule anayempenda. Hili nalo pia ni ubatili, ni kukimbiza upepo.

Japanese Contemporary Bible

伝道者の書 2:1-26

2

楽しみはむなしい

1-2それで私は、「愉快に生きよう。思う存分楽しむのだ」と思いました。ところが、こうした生き方も実にむなしいことがわかりました。一日中笑っているのは愚かなことです。それが何の得になるのでしょう。

3いろいろ試してみてから、私は知恵を探求し続ける一方で、酒を飲んで元気になろうと思いました。次に、もう一度考えを変えて、愚かな者になりきることにしました。多くの人が経験する幸福を味わってみようと思ったのです。

4-6今度は、大規模な事業に乗り出して、仕事からくる充実感を得ようとしました。邸宅を建て、ぶどう園、庭園、公園、それに果樹園まで造り、良い作物を実らせるために貯水池まで造ってみたのです。

7-8次に、男女の奴隷を買いました。私の家で生まれた奴隷たちもいます。ほかに家畜の群れも飼ってみましたが、その数は以前のどの王よりも多かったのです。さらに、多くの州や国から、税金として金銀をかき集めました。また文化的な活動として、混声コーラス・グループやオーケストラを組織しました。そのうえ私には、大ぜいの美しいそばめがいたのです。

9こうして、歴代のエルサレムの王もしなかったような、あらゆることをやってみました。両眼をしっかり見開いて、これらのものの価値を見極めようとしたのです。 10欲しいものは何でも手に入れ、したい放題の楽しみをしてみました。つらい仕事にも大きな喜びがあることを知りました。この喜びこそ、実に、あらゆる労働に共通した報酬なのです。

知恵と愚かさはむなしい

11しかし、してきたことを振り返ってみると、どれもこれも役に立たないことばかりで、風を追うようなものでした。これこそ価値があると言えるものなど、どこにもありませんでした。

12そこで、知恵と無知の価値を比較してみることにしました。おそらくだれでも、同じ結論に達するでしょう。 13-14それは、こういうことです。光が闇にまさっているように、知恵は無知よりはるかに価値があります。賢い人は先々を正しく判断しますが、愚かな人は先のことがわかりません。ところが私は、知恵のある人にも知恵の足りない人にも共通点があることに気づきました。 15知恵の足りない人が死ぬように、いずれこの私も死ぬということです。それなら、知恵をつけたところで、いったい何の益があるというのでしょう。私は、知恵をつけることでさえむなしいものだと悟ったのです。 16賢い人も愚かな人も死ぬのです。時がたてば、両者とも、すっかり忘れられてしまいます。 17私はここまでわかると、生きているのがいやになりました。人生は不条理きわまりないからです。何もかもむなしく、風を追うようなものです。

労苦はむなしい

18一生懸命に築き上げたものが他者のものになると思うと、いやになってきます。 19そればかりか、跡取り息子が愚か者か賢い者か、だれにわかるでしょう。それでも、私の財産はすべて、息子のものになるのです。なんと気分がめいることではありませんか。

20-23こうして、満足感を与えてくれると考えていた労苦も愚かしく思われ、見切りをつけました。生涯をかけて知恵や知識や技術を追求しても、せっかく手に入れたものを全部、何もしなかった者に譲るはめになるのです。そんな者が、私が努力して得たものを受け継ぐのです。むなしいだけでなく、不公平です。どれほど必死に働いても何の役にも立ちません。あるものといえば、悲しみと悩みに押しつぶされそうな、心の休まらない日々と眠れない夜です。全くむなしい話ではありませんか。

24-26そこで私は、食べたり飲んだりすることと、労働を楽しむこと以外に生きがいはない、と判断しました。しかも、このような楽しみさえ神の御手から来るとわかったのです。というのも、神の世話にならなければ、だれも食べたり楽しんだりすることはできないからです。神は、お心にかなった者に知恵、知識、喜びを与えます。ところが神は、罪人が金持ちになると、その財産を取り上げ、お心にかなった者に分け与えるのです。ここにも、風を追うようなむなしさの一例があります。