Mathayo 8 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 8:1-34

Yesu Amtakasa Mwenye Ukoma

(Marko 1:40-45; Luka 5:12-16)

1Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makutano makubwa ya watu yakamfuata. 28:2 Law 13:45; Lk 17:12; Mt 18:26; 20:22Mtu mmoja mwenye ukoma akaja na kupiga magoti mbele yake, akasema, “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”

3Yesu akanyoosha mkono wake akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Mara yule mtu akatakasika ukoma wake. 48:4 Mk 8:30; Lk 4:41; Law 14:2-32Kisha Yesu akamwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote. Lakini nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na utoe sadaka aliyoamuru Mose, ili kuwa ushuhuda kwao.”

Yesu Amponya Mtumishi Wa Jemadari

(Luka 7:1-10)

58:5 Lk 7:1; Yn 4:27Yesu alipoingia Kapernaumu, jemadari mmoja alimjia, kumwomba msaada, 68:6 Mt 4:24akisema, “Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani na amepooza, tena ana maumivu makali ya kutisha.”

7Yesu akamwambia, “Nitakuja na kumponya.”

88:8 Za 107:20Lakini yule jemadari akamwambia, “Bwana, mimi sistahili wewe kuingia chini ya dari yangu. Lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu atapona. 9Kwa kuwa mimi mwenyewe ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. Nikimwambia huyu, ‘Nenda,’ yeye huenda; na mwingine nikimwambia, ‘Njoo,’ yeye huja. Nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ yeye hufanya.”

108:10 Mt 15:28Yesu aliposikia maneno haya, alishangaa, akawaambia wale waliomfuata, “Amin, nawaambia, hata katika Israeli sijapata kuona yeyote mwenye imani kubwa namna hii. 118:11 Za 107:3; Mal 1:11; Lk 13:29Ninawaambia kwamba wengi watatoka mashariki na magharibi, nao wataketi karamuni pamoja na Abrahamu, Isaki na Yakobo katika Ufalme wa Mbinguni. 128:12 Mt 13:38; 25:30; Lk 13:28Lakini warithi wa Ufalme watatupwa katika giza la nje, ambako kutakuwako kilio na kusaga meno.”

138:13 Mt 9:22-29Kisha Yesu akamwambia yule jemadari, “Nenda na iwe kwako sawasawa na imani yako.” Naye yule mtumishi akapona saa ile ile.

Yesu Aponya Wengi

(Marko 1:29-34; Luka 4:38-41)

148:14 1Kor 9:5Yesu alipoingia nyumbani kwa Petro, alimkuta mama mkwe wa Petro amelala kitandani, akiwa ana homa. 158:15 Mk 1:29-34Akamgusa mkono wake na homa ikamwacha, naye akainuka na kuanza kumhudumia.

168:16 Mt 4:23-24Jioni ile, wakamletea watu wengi waliopagawa na pepo wachafu, naye akawatoa wale pepo wachafu kwa neno lake, na kuwaponya wagonjwa wote. 178:17 Isa 53:4; Mt 1:22Haya yalifanyika ili litimie lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba:

“Mwenyewe alitwaa udhaifu wetu

na alichukua magonjwa yetu.”

Gharama Ya Kumfuata Yesu

(Luka 9:57-62)

188:18 Mk 4:35; Lk 8:22Yesu alipoona makutano mengi wamemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake wavuke mpaka ngʼambo ya ziwa. 198:19 Lk 9:57, 58Kisha mwalimu mmoja wa sheria akamjia Yesu na kumwambia, “Mwalimu, nitakufuata kokote uendako.”

208:20 Dan 7:13; Mk 2:10Naye Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”

218:21 1Fal 19:20Mwanafunzi mwingine akamwambia, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”

228:22 Mt 4:19; Rum 6:13Lakini Yesu akamwambia, “Nifuate, uwaache wafu wawazike wafu wao.”

Yesu Atuliza Dhoruba

(Marko 4:35-41; Luka 8:22-25)

238:23 Za 4:8Naye alipoingia kwenye mashua, wanafunzi wake wakamfuata. 248:24 Mk 4:37; Lk 8:26Ghafula, kukainuka dhoruba kali baharini hata mashua ikaanza kufunikwa na mawimbi, lakini Yesu alikuwa amelala usingizi. 25Wanafunzi wake wakamwendea na kumwamsha, wakisema, “Bwana, tuokoe! Tunazama!”

268:26 Mt 6:30; Za 65:7; 89:9Naye Yesu akawaambia, “Kwa nini mnaogopa, enyi wa imani haba?” Kisha akaamka na kukemea dhoruba na mawimbi, nako kukawa shwari kabisa.

27Wale watu wakashangaa, wakisema, “Ni mtu wa namna gani huyu? Hata upepo na mawimbi vinamtii!”

Wawili Wenye Pepo Waponywa

(Marko 5:1-20; Luka 8:26-39)

288:28 Mt 4:24Walipofika ngʼambo katika nchi ya Wagerasi, watu wawili waliopagawa na pepo wachafu walitoka makaburini nao wakakutana naye. Watu hawa walikuwa wakali mno kiasi kwamba hakuna mtu aliyeweza kupita njia ile. 298:29 Lk 4:34; 2Pet 2:4Wakapiga kelele, “Una nini nasi, Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kututesa kabla ya wakati ulioamriwa?”

30Mbali kidogo kutoka pale walipokuwa, kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha. 31Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu, “Ukitutoa humu, turuhusu twende kwenye lile kundi la nguruwe.”

32Akawaambia, “Nendeni!” Hivyo wakatoka na kuwaingia wale nguruwe, nalo kundi lote likateremka gengeni kwa kasi, likaingia katika ziwa na kufa ndani ya maji. 33Wale watu waliokuwa wakiwachunga hao nguruwe wakakimbia wakaingia mjini, wakaeleza yote kuhusu yale yaliyowatokea wale waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu. 348:34 Lk 5:8; Mdo 16:39Kisha watu wote wa mji huo wakatoka kwenda kukutana na Yesu. Nao walipomwona wakamsihi aondoke kwenye nchi yao.

New International Reader’s Version

Matthew 8:1-34

Jesus Heals a Man Who Had a Skin Disease

1Jesus came down from the mountainside. Large crowds followed him. 2A man who had a skin disease came and got down on his knees in front of Jesus. He said, “Lord, if you are willing to make me ‘clean,’ you can do it.”

3Jesus reached out his hand and touched the man. “I am willing to do it,” he said. “Be ‘clean’!” Right away the man was healed of his skin disease. 4Then Jesus said to him, “Don’t tell anyone. Go and show yourself to the priest, and offer the gift Moses commanded. It will be a witness to everyone.”

A Roman Commander Has Faith

5When Jesus entered Capernaum, a Roman commander came to him. He asked Jesus for help. 6“Lord,” he said, “my servant lies at home and can’t move. He is suffering terribly.”

7Jesus said, “Shall I come and heal him?”

8The commander replied, “Lord, I am not good enough to have you come into my house. But just say the word, and my servant will be healed. 9I myself am a man under authority. And I have soldiers who obey my orders. I tell this one, ‘Go,’ and he goes. I tell that one, ‘Come,’ and he comes. I say to my slave, ‘Do this,’ and he does it.”

10When Jesus heard this, he was amazed. He said to those following him, “What I’m about to tell you is true. In Israel I have not found anyone whose faith is so strong. 11I say to you that many will come from the east and the west. They will take their places at the feast in the kingdom of heaven. They will sit with Abraham, Isaac and Jacob. 12But those who think they belong in the kingdom will be thrown outside, into the darkness. There they will weep and grind their teeth.”

13Then Jesus said to the Roman commander, “Go! It will be done just as you believed it would.” And his servant was healed at that moment.

Jesus Heals Many People

14When Jesus came into Peter’s house, he saw Peter’s mother-in-law. She was lying in bed. She had a fever. 15Jesus touched her hand, and the fever left her. She got up and began to serve him.

16When evening came, many people controlled by demons were brought to Jesus. He drove out the spirits with a word. He healed all who were sick. 17This happened so that what Isaiah the prophet had said would come true. He had said,

“He suffered the things we should have suffered.

He took on himself the sicknesses that should have been ours.” (Isaiah 53:4)

The Cost of Following Jesus

18Jesus saw the crowd around him. So he gave his disciples orders to go to the other side of the Sea of Galilee. 19Then a teacher of the law came to him. He said, “Teacher, I will follow you no matter where you go.”

20Jesus replied, “Foxes have dens. Birds have nests. But the Son of Man has no place to lay his head.”

21Another follower said to him, “Lord, first let me go and bury my father.”

22But Jesus told him, “Follow me. Let the dead bury their own dead.”

Jesus Calms the Storm

23Jesus got into a boat. His disciples followed him. 24Suddenly a terrible storm came up on the lake. The waves crashed over the boat. But Jesus was sleeping. 25The disciples went and woke him up. They said, “Lord! Save us! We’re going to drown!”

26He replied, “Your faith is so small! Why are you so afraid?” Then Jesus got up and ordered the winds and the waves to stop. It became completely calm.

27The disciples were amazed. They asked, “What kind of man is this? Even the winds and the waves obey him!”

Jesus Heals Two Men Controlled by Demons

28Jesus arrived at the other side of the lake in the area of the Gadarenes. Two men controlled by demons met him. They came from the tombs. The men were so wild that no one could pass that way. 29“Son of God, what do you want with us?” they shouted. “Have you come here to punish us before the time for us to be judged?”

30Not very far away, a large herd of pigs was feeding. 31The demons begged Jesus, “If you drive us out, send us into the herd of pigs.”

32Jesus said to them, “Go!” So the demons came out of the men and went into the pigs. The whole herd rushed down the steep bank. They ran into the lake and drowned in the water. 33Those who were tending the pigs ran off. They went into the town and reported all this. They told the people what had happened to the men who had been controlled by demons. 34Then the whole town went out to meet Jesus. When they saw him, they begged him to leave their area.