Mathayo 6 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 6:1-34

Kuwapa Wahitaji

16:1 Mt 5:16; 23:5; Rum 12:8“Angalieni msitende wema wenu mbele ya watu ili wawaone. Kwa maana mkifanya hivyo, hamna thawabu kutoka kwa Baba yenu aliye mbinguni.

2“Hivyo mnapowapa wahitaji, msipige panda mbele yenu kama wafanyavyo wanafiki katika masinagogi na mitaani, ili wasifiwe na watu. Amin nawaambia wao wamekwisha kupokea thawabu yao. 36:3 Rum 12:8Lakini ninyi mtoapo sadaka, fanyeni kwa siri, hata mkono wako wa kushoto usijue mkono wako wa kuume unachofanya, 46:4 Mt 6:6, 18; Kol 3:23-24ili sadaka yako iwe ni siri. Ndipo Baba yako wa mbinguni, yeye aonaye sirini atakupa thawabu kwa wazi.

Kuhusu Maombi

(Luka 11:2-4)

56:5 Mk 11:25; Lk 18:10-14“Nanyi msalipo, msiwe kama wanafiki, maana wao hupenda kusali wakiwa wamesimama katika masinagogi na kando ya barabara ili waonekane na watu. Amin nawaambia, wao wamekwisha kupata thawabu yao. 66:6 1Fal 4:33Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Naye Baba yako aonaye sirini atakupa thawabu yako. 76:7 Mhu 5:2; 1Fal 18:26-29Nanyi mnaposali msiseme maneno kama wafanyavyo watu wasiomjua Mungu. Kwa maana wao hudhani kwamba watasikiwa kwa sababu ya wingi wa maneno yao. 86:8 Mt 6:32Msiwe kama wao, kwa sababu Baba yenu anajua kile mnachohitaji kabla hamjamwomba.

96:9 Lk 11:2-4; Yn 17:6“Hivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba:

“ ‘Baba yetu uliye mbinguni,

Jina lako litukuzwe.

10Ufalme wako uje.

Mapenzi yako yafanyike

hapa duniani kama huko mbinguni.

116:11 Mit 30:8Utupatie riziki yetu

ya kila siku.

126:12 Mt 18:21-35Utusamehe deni zetu,

kama sisi nasi tulivyokwisha

kuwasamehe wadeni wetu.

136:13 Yak 1:13; Mt 5:37Usitutie majaribuni,

bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu

[kwa kuwa Ufalme ni wako, na nguvu,

na utukufu, hata milele. Amen].’

146:14 Efe 4:32; Kol 3:13Kwa kuwa kama mkiwasamehe watu wengine wanapowakosea, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia. 156:15 Mk 11:25-26; Mt 18:35Lakini msipowasamehe watu wengine makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.

Kuhusu Kufunga

166:16 Isa 58:5-9; Zek 8:19“Mnapofunga, msiwe wenye huzuni kama wafanyavyo wanafiki. Maana wao hukunja nyuso zao ili kuwaonyesha wengine kwamba wamefunga. Amin, amin nawaambia wao wamekwisha kupata thawabu yao kamilifu. 176:17 Rut 3:3; Dan 10:3Lakini mnapofunga, jipakeni mafuta kichwani na kunawa nyuso zenu 186:18 Mt 6:4, 6ili kufunga kwenu kusionekane na watu wengine ila Baba yenu aketiye mahali pa siri; naye Baba yenu aonaye sirini atawapa thawabu yenu kwa wazi.

Akiba Ya Mbinguni

(Luka 12:33-34)

196:19 Mt 23:4; Lk 12:16-21; Yak 5:2-3“Msijiwekee hazina duniani, mahali ambapo nondo na kutu huharibu, nao wevi huvunja na kuiba. 206:20 1Tim 6:19; Mt 19:20; Lk 12:33-34; Kol 3:1-3Lakini jiwekeeni hazina mbinguni, mahali ambapo nondo na kutu haviharibu, wala wevi hawavunji na kuiba. 216:21 Lk 12:34Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo pia moyo wako utakapokuwa.

Jicho Ni Taa Ya Mwili

(Luka 11:34-36)

226:22 Lk 11:34-36“Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni nyofu, mwili wako wote utajaa nuru. 236:23 Mt 20:15Lakini kama jicho lako ni ovu, mwili wako wote utajawa na giza. Kwa hiyo basi, kama nuru iliyomo ndani yako ni giza, hilo ni giza kuu namna gani!

Mungu Na Mali

(Luka 16:13; 12:22-31)

246:24 Lk 16:9, 13“Hakuna mtu awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.6:24 Mali (au Utajiri) hapa inatoka neno Mamoni kwa Kiaramu au Mamona kwa Kiyunani.

Msiwe Na Wasiwasi

256:25 Flp 4:6; 1Pet 5:7“Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini au mtakunywa nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini. Je, maisha si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi? 266:26 Za 104:21; 136:25; Mt 10:29-31Waangalieni ndege wa angani; wao hawapandi wala hawavuni au kuweka ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani zaidi kuliko hao ndege? 276:27 Za 39:5Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?

28“Nanyi kwa nini mnajitaabisha kwa ajili ya mavazi? Fikirini maua ya shambani yameavyo. Hayafanyi kazi wala hayafumi. 296:29 1Fal 10:4-7Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua. 306:30 Mt 16:8; Lk 12:28Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo na kesho yanatupwa motoni, je, hatawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba? 31Kwa hiyo msiwe na wasiwasi, mkisema, ‘Tutakula nini?’ au ‘Tutakunywa nini?’ au ‘Tutavaa nini?’ 326:32 Mt 6:8Watu wasiomjua Mungu ndio wanaoshindania hayo, lakini Baba yenu wa mbinguni anafahamu kuwa mnahitaji haya yote. 336:33 Za 37:4, 25; Rum 14:17; Mk 10:29-30Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake, na haya yote atawapa pia. 34Kwa hiyo msiwe na wasiwasi kuhusu kesho, kwa sababu kesho itajitaabikia yenyewe. Yatosha kwa siku masumbufu yake.

Knijga O Kristu

Matej 6:1-34

O pomaganju onima koji su u potrebi

1“Pazite! Nemojte svoja dobra djela činiti javno da vam se drugi dive jer onda nećete primiti plaću od svojega nebeskog Oca.

2Zato kada daješ milodar, ne trubi pred sobom kao što to u sinagogama i na ulicama čine licemjeri da ih ljudi hvale. Zaista vam kažem, drugu nagradu osim te neće dobiti.6:2, 5 i 16 U grčkome: oni su već primili svoju plaću. 3Naprotiv, kada daješ milodar, neka tvoja ljevica ne zna što radi desnica. 4Udijeli svoj milodar potajno pa će te tvoj Otac, koji vidi i u tajnosti, nagraditi.”

O molitvi

(Mk 11:25; Lk 11:2-4)

5“I kada se molite, ne budite poput licemjera koji se vole moliti u sinagogama i po uličnim raskrižjima da ih ljudi vide. Zaista vam kažem, drugu nagradu osim te neće dobiti. 6Ti, naprotiv, kada se moliš, uđi nekamo gdje ćeš biti sam, zatvori za sobom vrata te se pomoli Ocu u tajnosti, a tvoj će te Otac, koji vidi u tajnosti, nagraditi. 7Kad se molite, ne nabrajajte isprazne riječi kao pogani, koji misle da će biti uslišani zbog svojega nabrajanja. 8Ne činite kao oni jer vaš Otac dobro zna što vam je potrebno i prije nego što ga zamolite. 9Zato se vi molite ovako:

‘Oče naš na nebu, neka se štuje tvoje sveto ime.

10Neka dođe tvoje kraljevstvo.

Neka se tvoja volja provodi

na zemlji kao i na nebu.

11Kruh naš svagdašnji daj nam danas

12i oprosti nam naše grijehe kao što i mi opraštamo onima koji griješe protiv nas.

13I ne dopusti da podlegnemo kušnji,

nego nas izbavi od Zloga.’6:13 U nekim rukopisima stoji još: Jer tvoji su kraljevstvo, sila i slava zauvijek. Amen.

14Jer ako oprostite ljudima njihove pogreške, i vaš će nebeski Otac vama oprostiti. 15Ali ne oprostite li vi drugima njihovih pogrešaka, ni vaš Otac neće vama oprostiti vaše grijehe.

O postu

16Kad postite, ne mrštite se kao licemjeri, koji izobliče lice kako bi ljudi opazili da poste. Zaista vam kažem, drugu nagradu osim te neće dobiti. 17Ali ti se, kada postiš, lijepo uredi 18da tvoj post ne zapaze ljudi, nego samo tvoj Otac koji je u tajnosti. I tvoj će ti Otac, koji vidi u tajnosti, uzvratiti.”

O novcu i imetku

(Lk 11:34-36; 12:33-34; 16:13)

19“Ne zgrćite sebi blago ovdje na zemlji, gdje ga mogu izgristi moljci ili može zahrđati, gdje lopovi provaljuju i kradu. 20Stječite sebi blago na nebu, gdje ga ne mogu izgristi moljci ni hrđa, gdje lopovi ne provaljuju i ne kradu. 21Jer gdje ti je blago, ondje će ti biti i srce.

22Oko je poput svjetiljke tijelu. Ne budete li odviše brinuli za materijalna dobra jasno ćete vidjeti u životu, 23ali ako za njih budete previše brinuli vid će vam biti zasjenjen i duboka će vam tama ispuniti život.

Ne može se služiti Bogu i bogatstvu

24Nitko ne može služiti dvojici gospodara. Ili će jednoga mrziti, a drugoga voljeti ili će jednome biti odan, a drugoga prezirati. Ne možete služiti i Bogu i bogatstvu.

Ne brinite se!

(Lk 12:22-31)

25Zato vam kažem: Ne brinite se tjeskobno kako ćete preživjeti, što ćete jesti ili piti, ni u što ćete obući svoje tijelo! Nije li život vredniji od hrane, a tijelo od odjeće? 26Pogledajte ptice nebeske! Niti siju, niti žanju, niti sabiru u žitnice jer ih hrani vaš nebeski Otac. A niste li vi mnogo vredniji od njih? 27Može li tko od vas sebi brigama produžiti život barem i za jedan dan?

28Zašto se onda brinuti za odjeću? Pogledajte samo poljske ljiljane! Niti se muče niti predu. 29A kažem vam da se ni kralj Salomon u svoj svojoj raskoši nije zaodjenuo kao jedan od njih. 30Pa ako Bog tako odijeva poljsku travu koja danas jest, a već se sutra baca u peć, zar se neće još i više brinuti za vas, malovjerni? 31Ne brinite se tjeskobno i ne govorite: ‘Što ćemo jesti?’, ‘Što ćemo piti?’ ili ‘U što ćemo se obući?’ 32jer tako čine nevjernici. Vaš nebeski Otac zna da vam je sve to potrebno. 33Stoga najprije tražite Božje kraljevstvo i njegovu pravednost, pa će vam se i to nadodati.

34Ne brinite se zato tjeskobno za sutra jer će ono donijeti nove brige. Današnja vam je muka dovoljna za danas.”