Mathayo 27 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 27:1-66

Yesu Aletwa Mbele Ya Pilato

(Marko 15:1; Luka 23:1-2; Yohana 18:28-32)

127:1 Mk 15:1; Lk 22:66Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri pamoja dhidi ya Yesu ili kumuua. 227:2 Mt 20:19; Mdo 3:13; 1Tim 6:13Wakamfunga, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato, ambaye alikuwa mtawala wa Kirumi.

Yuda Ajinyonga

(Matendo 1:18-19)

327:3 Mt 10:4; 26:14-15Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti Yesu, alipoona kuwa Yesu amehukumiwa, akajuta na akarudisha vile vipande thelathini vya fedha alivyopewa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu. 427:4 Mt 27:24Akasema, “Nimetenda dhambi, kwa maana nimeisaliti damu isiyo na hatia.”

Wakamjibu, “Hilo latuhusu nini sisi? Ni shauri yako.”

527:5 Lk 1:9, 21; Mdo 1:18-19Basi Yuda akavitupa vile vipande vya fedha ndani ya Hekalu akaondoka akaenda kujinyonga.

627:6 Mk 12:41Wale viongozi wa makuhani wakazichukua zile fedha wakasema, “Si halali kuchanganya fedha hizi na sadaka kwa sababu hizi ni fedha zenye damu.” 7Kwa hiyo baada ya kushauriana, waliamua kuzitumia kununulia shamba la mfinyanzi, liwe mahali pa kuzikia wageni. 827:8 Mdo 1:19Hii ndiyo sababu lile shamba likaitwa Shamba la Damu hadi leo. 927:9 Mt 1:22Ndipo likatimia lile lililonenwa na nabii Yeremia, kwamba, “Walichukua vile vipande thelathini vya fedha, thamani aliyopangiwa na watu wa Israeli, 1027:10 Zek 11:12-13; Yer 32:6-9wakanunulia shamba la mfinyanzi, kama vile Bwana alivyoniagiza.”

Yesu Mbele Ya Pilato

(Marko 15:2-15; Luka 23:3-25; Yohana 18:33–19:16)

1127:11 Mt 2:2Wakati huo Yesu akiwa amesimama mbele ya mtawala, mtawala akamuuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”

Yesu akasema, “Wewe wasema hivyo.”

1227:12 Mk 14:61; Yn 19:9Lakini viongozi wa makuhani na wazee walipomshtaki, hakujibu neno. 1327:13 Mt 26:62Ndipo Pilato akamuuliza, “Je, husikii ni mambo mangapi wanayokushtaki nayo?” 1427:14 Mk 14:61Lakini Yesu hakumjibu hata kwa shtaka moja, kiasi kwamba mtawala alishangaa sana.

1527:15 Yn 18:39Basi ilikuwa ni desturi ya mtawala kumfungua mfungwa mmoja aliyechaguliwa na umati wa watu wakati wa sikukuu. 16Wakati huo alikuwepo mfungwa mmoja mwenye sifa mbaya, aliyeitwa Baraba. 1727:17 Mt 1:16Hivyo umati wa watu walipokusanyika, Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie nani, Baraba au Yesu yeye aitwaye Kristo?” 1827:18 Yn 11:47, 48; 12:19Kwa kuwa alitambua Yesu alikuwa amekabidhiwa kwake kwa ajili ya wivu.

1927:19 Yn 19:13; Mt 27:24; Hes 12:6Pilato akiwa ameketi kwenye kiti cha hukumu, mkewe akampelekea ujumbe huu: “Usiwe na jambo lolote juu ya mtu huyu asiye na hatia, kwa kuwa leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”

2027:20 Mdo 3:14Lakini viongozi wa makuhani na wazee wakaushawishi ule umati wa watu kwamba waombe Baraba afunguliwe, naye Yesu auawe.

21Mtawala akawauliza tena, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka niwafungulie?”

Wakajibu, “Baraba.”

2227:22 Mt 1:16Pilato akawaambia, “Basi nifanye nini na huyu Yesu aitwaye Kristo?”

Wakajibu wote, “Msulubishe!”

23Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?”

Lakini wao wakazidi kupiga kelele, wakisema, “Msulubishe!”

2427:24 Mt 26:5; Za 26:6; Kum 21:6-8Pilato alipoona kwamba hawezi kufanya lolote, lakini badala yake ghasia zilikuwa zinaanza, akachukua maji, akanawa mikono yake mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Sina hatia juu ya damu ya mtu huyu, hili ni jukumu lenu!”

2527:25 Yos 2:19; Mdo 5:28Watu wote wakajibu, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”

2627:26 Isa 53:5; Yn 19:1Basi akawafungulia Baraba. Lakini baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.

Askari Wamdhihaki Yesu

(Marko 15:16-20; Yohana 19:2-3)

2727:27 Yn 18:28-33; 19:9Kisha askari wa mtawala wakampeleka Yesu kwenye Praitorio27:27 Praitorio maana yake ni makao makuu ya mtawala, jumba la kifalme lililokuwa linakaliwa na Pontio Pilato huko Yerusalemu, palipokuwa na kiti cha hukumu. na wakakusanya kikosi kizima cha askari kumzunguka. 2827:28 Yn 19:2Wakamvua nguo zake na kumvika vazi la rangi nyekundu, kisha 2927:29 Isa 53:3; Yn 19:2-3wakasokota taji ya miiba, wakaiweka kichwani pake. Wakamwekea fimbo katika mkono wake wa kuume, na wakapiga magoti mbele zake na kumdhihaki, wakisema, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!” 3027:30 Mt 16:21; 26:27; 27:31; Isa 53:7Wakamtemea mate, wakachukua ile fimbo wakampiga kichwani tena na tena. 3127:31 Mk 15:20-41; Lk 23:26Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakampeleka ili wakamsulubishe.

Yesu Asulubishwa

(Marko 15:21-32; Luka 23:26-43; Yohana 19:17-27)

3227:32 Ebr 13:12; Mdo 11:20; Mk 15:21; Lk 23:26Walipokuwa wakienda, wakakutana na mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba. 3327:33 Yn 19:17Wakafika mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa). 3427:34 Mt 27:18; Za 69:21Hapo wakampa Yesu divai iliyochanganywa na nyongo ili anywe; lakini alipoionja, akakataa kuinywa. 3527:35 Za 22:18Walipokwisha kumsulubisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura. [Hili lilifanyika ili litimie lile neno lililonenwa na nabii, “Waligawa nguo zangu miongoni mwao na vazi langu wakalipigia kura.”] 3627:36 Mt 27:54Kisha wakaketi, wakamchunga. 3727:37 Mk 15:26; Lk 23:38; Yn 19:19Juu ya kichwa chake, kwenye msalaba, wakaandika shtaka lake hivi: Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi. 3827:38 Isa 53:12Wanyangʼanyi wawili walisulubiwa pamoja naye, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto. 3927:39 Za 109:25; Mao 2:15Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao 4027:40 Mt 26:61; Yn 2:19; Mt 4:3-6na kusema, “Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe mwenyewe basi! Kama wewe ni Mwana wa Mungu, shuka kutoka msalabani.”

41Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wakamdhihaki wakisema, 4227:42 Yn 1:49; 12:13; 3:15“Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe! Yeye ni Mfalme wa Israeli! Ashuke sasa kutoka msalabani, nasi tutamwamini. 4327:43 Za 22:8Anamwamini Mungu, basi Mungu na amwokoe sasa kama anamtaka, kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’ ” 4427:44 Mk 15:32; Lk 23:39Hata wale wanyangʼanyi waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana vivyo hivyo.

Kifo Cha Yesu

(Marko 15:33-41; Luka 23:44-49; Yohana 19:28-30)

4527:45 Amo 8:9Tangu saa sita hadi saa tisa giza liliifunika nchi yote. 4627:46 Za 22:1Ilipofika saa tisa, Yesu akapaza sauti akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)

47Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama pale waliposikia hayo, wakasema, “Anamwita Eliya.”

4827:48 Mt 27:34; Za 69:21Ghafula mmoja wao akaenda mbio na kuleta sifongo, akaichovya kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe. 49Wengine wakasema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”

5027:50 Yn 19:30Yesu alipolia tena kwa sauti kuu, akaitoa roho yake.

5127:51 Kut 26:31-33; Ebr 10:19Wakati huo huo pazia la Hekalu likachanika vipande viwili, kuanzia juu hadi chini. Dunia ikatetemeka na miamba ikapasuka. 52Makaburi yakafunguka na miili ya watakatifu waliokuwa wamekufa ikafufuliwa. 5327:53 Mt 4:5Wakatoka makaburini, na baada ya Yesu kufufuka, waliingia kwenye Mji Mtakatifu na kuwatokea watu wengi.

5427:54 Mt 4:3; 17:5Basi yule jemadari na wale waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu walipoona lile tetemeko na yale yote yaliyokuwa yametukia, waliogopa, wakasema, “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”

5527:55 Lk 8:2-3Walikuwako wanawake huko wakiangalia kwa mbali. Hawa walikuwa wamemfuata Yesu tangu Galilaya ili kushughulikia mahitaji yake. 5627:56 Lk 24:10; Yn 19:25Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo na Yosefu, na mama yao wana wa Zebedayo.

Maziko Ya Yesu

(Marko 15:42-47; Luka 23:50-56; Yohana 19:38-42)

5727:57 Kut 34:25; Mk 15:42; Lk 23:50; Yn 19:38Ilipofika jioni, alifika mtu mmoja tajiri kutoka Arimathaya aitwaye Yosefu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu. 58Akamwendea Pilato ili kumwomba mwili wa Yesu. Pilato akaamuru apewe. 59Yosefu akauchukua mwili wa Yesu, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, 6027:60 Mk 16:4; Mdo 13:29na kuuweka katika kaburi lake mwenyewe jipya, alilokuwa amelichonga kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa katika ingilio la kaburi, akaenda zake. 61Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwepo mahali pale, wakiwa wameketi mkabala na kaburi.

Walinzi Pale Kaburini

62Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalizi ya Sabato, viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakamwendea Pilato 6327:63 Mt 16:21na kusema, “Bwana, tumekumbuka kwamba yule mdanganyifu wakati alikuwa bado hai alisema, ‘Baada ya siku tatu nitafufuka.’ 6427:64 Mt 28:13Kwa hiyo uamuru kaburi lilindwe kwa uthabiti mpaka baada ya siku tatu. La sivyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kuuiba mwili wake na kuwaambia watu kwamba amefufuliwa kutoka kwa wafu. Udanganyifu huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”

6527:65 Mt 28:11Pilato akawaambia, “Ninyi mnao askari walinzi. Nendeni, liwekeeni ulinzi kadri mwezavyo.” 6627:66 Dan 6:7; Mt 28:2; 28:11Kwa hiyo wakaenda na walinzi ili kulilinda kaburi kwa uthabiti, wakatia muhuri kwenye lile jiwe na kuweka ulinzi.

New International Reader’s Version

Matthew 27:1-66

Judas Hangs Himself

1It was early in the morning. All the chief priests and the elders of the people planned how to put Jesus to death. 2So they tied him up and led him away. Then they handed him over to Pilate, who was the governor.

3Judas, who had handed him over, saw that Jesus had been sentenced to die. He felt deep shame and sadness for what he had done. So he returned the 30 silver coins to the chief priests and the elders. 4“I have sinned,” he said. “I handed over a man who is not guilty.”

“What do we care?” they replied. “That’s your problem.”

5So Judas threw the money into the temple and left. Then he went away and hanged himself.

6The chief priests picked up the coins. They said, “It’s against the law to put this money into the temple fund. It is blood money. It has paid for a man’s death.” 7So they decided to use the money to buy a potter’s field. People from other countries would be buried there. 8That is why it has been called the Field of Blood to this day. 9Then the words spoken by Jeremiah the prophet came true. He had said, “They took the 30 silver coins. That price was set for him by the people of Israel. 10They used the coins to buy a potter’s field, just as the Lord commanded me.” (Zechariah 11:12,13; Jeremiah 19:1–13; 32:6–9)

Jesus Is Brought to Pilate

11Jesus was standing in front of the governor. The governor asked him, “Are you the king of the Jews?”

“Yes. You have said so,” Jesus replied.

12But when the chief priests and the elders brought charges against him, he did not answer. 13Then Pilate asked him, “Don’t you hear the charges they are bringing against you?” 14But Jesus made no reply, not even to a single charge. The governor was really amazed.

15It was the governor’s practice at the Passover Feast to let one prisoner go free. The people could choose the one they wanted. 16At that time they had a well-known prisoner named Jesus Barabbas. 17So when the crowd gathered, Pilate asked them, “Which one do you want me to set free? Jesus Barabbas? Or Jesus who is called the Messiah?” 18Pilate knew that the leaders wanted to get their own way. He knew this was why they had handed Jesus over to him.

19While Pilate was sitting on the judge’s seat, his wife sent him a message. It said, “Don’t have anything to do with that man. He is not guilty. I have suffered a great deal in a dream today because of him.”

20But the chief priests and the elders talked the crowd into asking for Barabbas and having Jesus put to death.

21“Which of the two do you want me to set free?” asked the governor.

“Barabbas,” they answered.

22“Then what should I do with Jesus who is called the Messiah?” Pilate asked.

They all answered, “Crucify him!”

23“Why? What wrong has he done?” asked Pilate.

But they shouted even louder, “Crucify him!”

24Pilate saw that he wasn’t getting anywhere. Instead, the crowd was starting to get angry. So he took water and washed his hands in front of them. “I am not guilty of this man’s death,” he said. “You are accountable for that!”

25All the people answered, “Put the blame for his death on us and our children!”

26Pilate let Barabbas go free. But he had Jesus whipped. Then he handed him over to be nailed to a cross.

The Soldiers Make Fun of Jesus

27The governor’s soldiers took Jesus into the palace, which was called the Praetorium. All the rest of the soldiers gathered around him. 28They took off his clothes and put a purple robe on him. 29Then they twisted thorns together to make a crown. They placed it on his head. They put a stick in his right hand. Then they fell on their knees in front of him and made fun of him. “We honor you, king of the Jews!” they said. 30They spit on him. They hit him on the head with the stick again and again. 31After they had made fun of him, they took off the robe. They put his own clothes back on him. Then they led him away to nail him to a cross.

Jesus Is Nailed to a Cross

32On their way out of the city, they met a man from Cyrene. His name was Simon. They forced him to carry the cross. 33They came to a place called Golgotha. The word Golgotha means the Place of the Skull. 34There they mixed wine with bitter spices and gave it to Jesus to drink. After tasting it, he refused to drink it. 35When they had nailed him to the cross, they divided up his clothes by casting lots. 36They sat down and kept watch over him there. 37Above his head they placed the written charge against him. It read,

This is Jesus, the King of the Jews.

38Two rebels against Rome were crucified with him. One was on his right and one was on his left. 39Those who passed by shouted at Jesus and made fun of him. They shook their heads 40and said, “So you are going to destroy the temple and build it again in three days? Then save yourself! Come down from the cross, if you are the Son of God!” 41In the same way the chief priests, the teachers of the law and the elders made fun of him. 42“He saved others,” they said. “But he can’t save himself! He’s the king of Israel! Let him come down now from the cross! Then we will believe in him. 43He trusts in God. Let God rescue him now if he wants him. He’s the one who said, ‘I am the Son of God.’ ” 44In the same way the rebels who were being crucified with Jesus also made fun of him.

Jesus Dies

45From noon until three o’clock, the whole land was covered with darkness. 46About three o’clock, Jesus cried out in a loud voice. He said, “Eli, Eli, lema sabachthani?” This means “My God, my God, why have you deserted me?” (Psalm 22:1)

47Some of those standing there heard Jesus cry out. They said, “He’s calling for Elijah.”

48Right away one of them ran and got a sponge. He filled it with wine vinegar and put it on a stick. He offered it to Jesus to drink. 49The rest said, “Leave him alone. Let’s see if Elijah comes to save him.”

50After Jesus cried out again in a loud voice, he died.

51At that moment the temple curtain was torn in two from top to bottom. The earth shook. The rocks split. 52Tombs broke open. The bodies of many holy people who had died were raised to life. 53They came out of the tombs. After Jesus was raised from the dead, they went into the holy city. There they appeared to many people.

54The Roman commander and those guarding Jesus saw the earthquake and all that had happened. They were terrified. They exclaimed, “He was surely the Son of God!”

55Not very far away, many women were watching. They had followed Jesus from Galilee to take care of his needs. 56Mary Magdalene was among them. Mary, the mother of James and Joseph, was also there. So was the mother of Zebedee’s sons.

Jesus Is Buried

57As evening approached, a rich man came from the town of Arimathea. His name was Joseph. He had become a follower of Jesus. 58He went to Pilate and asked for Jesus’ body. Pilate ordered that it be given to him. 59Joseph took the body and wrapped it in a clean linen cloth. 60He placed it in his own new tomb that he had cut out of the rock. He rolled a big stone in front of the entrance to the tomb. Then he went away. 61Mary Magdalene and the other Mary were sitting there across from the tomb.

The Guards at the Tomb

62The next day was the day after Preparation Day. The chief priests and the Pharisees went to Pilate. 63“Sir,” they said, “we remember something that liar said while he was still alive. He claimed, ‘After three days I will rise again.’ 64So give the order to make the tomb secure until the third day. If you don’t, his disciples might come and steal the body. Then they will tell the people that Jesus has been raised from the dead. This last lie will be worse than the first.”

65“Take some guards with you,” Pilate answered. “Go. Make the tomb as secure as you can.” 66So they went and made the tomb secure. They put a royal seal on the stone and placed some guards on duty.