Mathayo 23 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 23:1-39

Yesu Awashutumu Walimu Wa Sheria Na Mafarisayo

(Marko 12:38-40; Luka 11:39-52; 20:45-47)

123:1 Mk 12:38-40Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake: 223:2 Ezr 7:6, 25; Neh 8:4“Walimu wa sheria na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Mose, 323:3 Mal 2:7, 8hivyo inawapasa kuwatii na kufanya kila kitu wanachowaambia. Lakini msifuate yale wanayotenda, kwa sababu hawatendi yale wanayohubiri. 423:4 Mdo 15:10; Gal 6:13Wao hufunga mizigo mikubwa na kuiweka mabegani mwa watu, lakini wao wenyewe hawako radhi hata kuinua kidole ili kuisogeza.

523:5 Mt 6:1-5, 16; Kut 13:6-9; Hes 15:38; Kum 22:12“Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao. 623:6 Lk 14:7; 20:46Wanapenda kukalia viti vya heshima katika karamu, na vile viti maalum sana katika masinagogi. 723:7 Mk 9:5; Yn 20:16Hupenda kusalimiwa masokoni na kutaka watu wawaite ‘Rabi.’23:7 Rabi maana yake Bwana, Mwalimu.

823:8 Yak 3:1; 2Kor 1:24; 1Pet 5:3“Lakini ninyi msiitwe ‘Rabi,’ kwa sababu mnaye Bwana mmoja na ninyi nyote ni ndugu. 923:9 Mal 1:6; Mt 9:6Nanyi msimwite mtu yeyote ‘Baba,’ hapa duniani, kwa maana mnaye Baba mmoja, naye yuko mbinguni. 10Wala msiitwe ‘Mwalimu,’ kwa maana mnaye mwalimu mmoja tu, ndiye Kristo.23:10 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. 1123:11 Mt 20:26; Mk 9:35Yeye aliye mkuu kuliko ninyi nyote miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu. 1223:12 Za 18:27; Lk 1:52Kwa kuwa yeyote anayejikweza atashushwa, na yeyote anayejinyenyekeza atakwezwa.

1323:13 Mt 23:25-29; Lk 11:52“Lakini ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Kwa maana mnawafungia watu milango ya Ufalme wa Mbinguni. Ninyi wenyewe hamuingii humo, nao wale wanaotaka kuingia mnawazuia. [ 1423:14 Mk 12:40; Lk 20:47; 2Tim 3:6; Tit 1:11Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Mnakula katika nyumba za wajane, nanyi kwa kujifanya kuwa wema, mnasali sala ndefu. Kwa hiyo hukumu yenu itakuwa kuu zaidi.]

1523:15 Mdo 6:5; 13:43; Mt 5:22“Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Ninyi mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja mwongofu, lakini baada ya kumpata, mnamfanya mwana wa jehanamu mara mbili kuliko ninyi!

1623:16 Isa 9; 16; Mt 15:14; 5:33-35“Ole wenu, viongozi vipofu! Ninyi mwasema, ‘Mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini mtu akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, amefungwa kwa kiapo chake.’ 1723:17 Kut 30:29Ninyi vipofu wapumbavu! Ni kipi kilicho kikuu zaidi: ni ile dhahabu, au ni lile Hekalu linaloifanya hiyo dhahabu kuwa takatifu? 18Pia mnasema, ‘Mtu akiapa kwa madhabahu, si kitu; lakini mtu akiapa kwa sadaka iliyo juu ya madhabahu, amefungwa kwa kiapo chake’ 1923:19 Kut 29:37Ninyi vipofu! Ni kipi kikuu zaidi: ni sadaka, au ni madhabahu yanayoifanya hiyo sadaka kuwa takatifu? 20Kwa hiyo, mtu aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hayo madhabahu na vitu vyote vilivyo juu yake. 2123:21 1Fal 8:13; Za 26:8Naye mtu aapaye kwa Hekalu, huapa kwa hilo Hekalu na kwa huyo akaaye ndani yake. 2223:22 Za 11:4; Mt 5:34Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa yeye aketiye juu ya kiti hicho.

2323:23 Law 27:30; Mik 6:8; Lk 11:42“Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnatoa zaka ya mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu zaidi ya sheria, yaani haki, huruma na uaminifu. Iliwapasa kufanya haya makuu ya sheria bila kupuuza hayo matoleo. 2423:24 Mt 23:16Ninyi viongozi vipofu, mnachuja kiroboto lakini mnameza ngamia!

2523:25 Mk 7:4; Lk 11:39“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnasafisha kikombe na sahani kwa nje, lakini ndani mmejaa unyangʼanyi na kutokuwa na kiasi. 2623:26 Tit 1:15; Yn 9:40Ewe Farisayo kipofu! Safisha ndani ya kikombe na sahani kwanza, ndipo nje itakuwa safi pia.

2723:27 Lk 11:44; Mdo 23:3“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo yanapendeza kwa nje, lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila aina ya uchafu. 2823:28 Lk 16:15Vivyo hivyo, kwa nje ninyi mnaonekana kwa watu kuwa wenye haki, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.

2923:29 Lk 11:47-48“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki. 30Nanyi mwasema, ‘Kama tungaliishi wakati wa baba zetu, tusingalikuwa tumeshiriki katika kumwaga damu ya manabii!’ 3123:31 Mt 5:12; Mdo 7:51-52Hivyo mnajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii. 3223:32 1The 2:16; Eze 20:4Haya basi, kijazeni kipimo cha dhambi ya baba zenu!

3323:33 Mt 3:7; 12:34; 5:22“Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanamu? 3423:34 2Nya 36:15-16; Lk 11:49; Mt 10:17; 10:23Kwa sababu hii, tazameni, natuma kwenu manabii na wenye hekima na walimu. Baadhi yao mtawaua na kuwasulubisha, na wengine wao mtawapiga mijeledi katika masinagogi yenu na kuwafuatia kutoka mji mmoja hadi mji mwingine. 3523:35 Mwa 4:8; Ebr 11:4; 2Nya 24:21Hivyo ile damu ya wenye haki wote iliyomwagwa hapa duniani, tangu damu ya Abeli, ambaye alikuwa hana hatia, hadi damu ya Zekaria mwana wa Barakia, mliyemuua kati ya patakatifu na madhabahu, itawajia juu yenu. 3623:36 Mt 24:34; Lk 11:50-51Amin, nawaambia, haya yote yatakuja juu ya kizazi hiki.

Yesu Aililia Yerusalemu

(Luka 13:34-35)

3723:37 2Nya 24:21; Mt 5:12“Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka! 3823:38 1Fal 9:7-8; Yer 22:5Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa. 3923:39 Za 118:26; Mt 21:9Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena tangu sasa mpaka mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana.’ ”

King James Version

Matthew 23:1-39

1Then spake Jesus to the multitude, and to his disciples, 2Saying, The scribes and the Pharisees sit in Moses’ seat: 3All therefore whatsoever they bid you observe, that observe and do; but do not ye after their works: for they say, and do not. 4For they bind heavy burdens and grievous to be borne, and lay them on men’s shoulders; but they themselves will not move them with one of their fingers. 5But all their works they do for to be seen of men: they make broad their phylacteries, and enlarge the borders of their garments, 6And love the uppermost rooms at feasts, and the chief seats in the synagogues, 7And greetings in the markets, and to be called of men, Rabbi, Rabbi. 8But be not ye called Rabbi: for one is your Master, even Christ; and all ye are brethren. 9And call no man your father upon the earth: for one is your Father, which is in heaven. 10Neither be ye called masters: for one is your Master, even Christ. 11But he that is greatest among you shall be your servant. 12And whosoever shall exalt himself shall be abased; and he that shall humble himself shall be exalted.

13¶ But woe unto you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye shut up the kingdom of heaven against men: for ye neither go in yourselves, neither suffer ye them that are entering to go in. 14Woe unto you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye devour widows’ houses, and for a pretence make long prayer: therefore ye shall receive the greater damnation. 15Woe unto you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye compass sea and land to make one proselyte, and when he is made, ye make him twofold more the child of hell than yourselves. 16Woe unto you, ye blind guides, which say, Whosoever shall swear by the temple, it is nothing; but whosoever shall swear by the gold of the temple, he is a debtor! 17Ye fools and blind: for whether is greater, the gold, or the temple that sanctifieth the gold? 18And, Whosoever shall swear by the altar, it is nothing; but whosoever sweareth by the gift that is upon it, he is guilty. 19Ye fools and blind: for whether is greater, the gift, or the altar that sanctifieth the gift? 20Whoso therefore shall swear by the altar, sweareth by it, and by all things thereon. 21And whoso shall swear by the temple, sweareth by it, and by him that dwelleth therein. 22And he that shall swear by heaven, sweareth by the throne of God, and by him that sitteth thereon. 23Woe unto you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye pay tithe of mint and anise and cummin, and have omitted the weightier matters of the law, judgment, mercy, and faith: these ought ye to have done, and not to leave the other undone. 24Ye blind guides, which strain at a gnat, and swallow a camel. 25Woe unto you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye make clean the outside of the cup and of the platter, but within they are full of extortion and excess. 26Thou blind Pharisee, cleanse first that which is within the cup and platter, that the outside of them may be clean also. 27Woe unto you, scribes and Pharisees, hypocrites! for ye are like unto whited sepulchres, which indeed appear beautiful outward, but are within full of dead men’s bones, and of all uncleanness. 28Even so ye also outwardly appear righteous unto men, but within ye are full of hypocrisy and iniquity. 29Woe unto you, scribes and Pharisees, hypocrites! because ye build the tombs of the prophets, and garnish the sepulchres of the righteous, 30And say, If we had been in the days of our fathers, we would not have been partakers with them in the blood of the prophets. 31Wherefore ye be witnesses unto yourselves, that ye are the children of them which killed the prophets. 32Fill ye up then the measure of your fathers. 33Ye serpents, ye generation of vipers, how can ye escape the damnation of hell?

34¶ Wherefore, behold, I send unto you prophets, and wise men, and scribes: and some of them ye shall kill and crucify; and some of them shall ye scourge in your synagogues, and persecute them from city to city: 35That upon you may come all the righteous blood shed upon the earth, from the blood of righteous Abel unto the blood of Zacharias son of Barachias, whom ye slew between the temple and the altar. 36Verily I say unto you, All these things shall come upon this generation. 37O Jerusalem, Jerusalem, thou that killest the prophets, and stonest them which are sent unto thee, how often would I have gathered thy children together, even as a hen gathereth her chickens under her wings, and ye would not! 38Behold, your house is left unto you desolate. 39For I say unto you, Ye shall not see me henceforth, till ye shall say, Blessed is he that cometh in the name of the Lord.