Mathayo 2 – NEN & SNC

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 2:1-23

Wataalamu Wa Nyota Wafika Kumwona Mtoto Yesu

12:1 Lk 2:4, 6; Mwa 10:30; 25:6; 1Fal 4:30Baada ya Yesu kuzaliwa katika mji wa Bethlehemu huko Uyahudi, wakati wa utawala wa Mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu 22:2 Yer 23:5; Yn 1:49; Hes 24:17wakiuliza, “Yuko wapi huyo aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tumeona nyota yake ikitokea mashariki, nasi tumekuja kumwabudu.”

3Mfalme Herode aliposikia jambo hili aliingiwa na hofu sana pamoja na watu wote wa Yerusalemu. 42:4 2Nya 36:14; 34:13; Mal 2:7Herode akawaita pamoja viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, akawauliza ni mahali gani ambapo Kristo2:4 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. angezaliwa. 52:5 Yn 7:42; Mik 5:2Nao wakamwambia, “Katika Bethlehemu ya Uyahudi, kwa maana hivyo ndivyo ilivyoandikwa na nabii:

62:6 Mik 5:2; 2Sam 5:2; Yn 7:42; Ufu 2:27“ ‘Nawe, Bethlehemu, katika nchi ya Yuda,

wewe si mdogo miongoni

mwa watawala wa Yuda;

kwa maana kutoka kwako atakuja mtawala

atakayekuwa mchungaji

wa watu wangu Israeli.’ ”

7Ndipo Herode akawaita wale wataalamu wa nyota kwa siri na kutaka kujua kutoka kwao uhakika kamili wa wakati ile nyota ilionekana. 8Kisha akawatuma waende Bethlehemu akiwaambia, “Nendeni mkamtafute kwa bidii huyo mtoto. Nanyi mara mtakapomwona, mniletee habari ili na mimi niweze kwenda kumwabudu.”

9Baada ya kumsikia mfalme, wale wataalamu wa nyota wakaenda zao, nayo ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, nao wakaifuata mpaka iliposimama mahali pale alipokuwa mtoto. 10Walipoiona ile nyota wakajawa na furaha kubwa mno. 112:11 Isa 60:3; Za 72:10Walipoingia ndani ya ile nyumba, wakamwona mtoto pamoja na Maria mama yake, wakamsujudu na kumwabudu yule mtoto Yesu. Ndipo wakafungua hazina zao, wakamtolea zawadi za dhahabu, uvumba na manemane. 122:12 Ebr 11:7; Mt 2:13; 2:19; 2:22; 27:19Nao wakiisha kuonywa katika ndoto wasirudi kwa Herode, wakarudi kwenda katika nchi yao kwa njia nyingine.

Yosefu, Maria Na Mtoto Yesu Wakimbilia Misri

132:13 Mdo 5:19; Mt 27:19Walipokwisha kwenda zao, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto akamwambia, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapowaambia, kwa maana Herode anataka kumtafuta huyu mtoto ili amuue.”

14Kisha Yosefu akaondoka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake wakati wa usiku, nao wakaenda Misri 152:15 Hes 11:1; Kut 4:22-23ambako walikaa mpaka Herode alipofariki. Hili lilifanyika ili litimie lile lililonenwa na Bwana kwa kinywa cha nabii kusema: “Nilimwita mwanangu kutoka Misri.”

16Herode alipongʼamua kwamba wale wataalamu wa nyota wamemshinda kwa akili, alikasirika sana, naye akatoa amri ya kuwaua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili kurudi chini katika mji wa Bethlehemu na sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda alioambiwa na wale wataalamu wa nyota. 172:17 Yer 31:15; Mt 2:17, 23; 1:2Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia.

182:18 Mwa 35:19“Sauti ilisikika huko Rama,

maombolezo na kilio kikubwa,

Raheli akilia kwa ajili ya wanawe,

akikataa kufarijiwa,

kwa sababu hawako tena.”

Kurudi Kutoka Misri

192:19 Mt 27:19Baada ya Herode kufa, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto huko Misri 20na kusema, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mwende, mrudi katika nchi ya Israeli kwa sababu wale waliokuwa wanatafuta uhai wa mtoto wamekufa.”

21Basi Yosefu, akaondoka akamchukua mtoto na mama yake wakaenda mpaka nchi ya Israeli. 222:22 Mt 27:19; Lk 2:39Lakini aliposikia kwamba Arkelao alikuwa anatawala huko Uyahudi mahali pa Herode baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye akiisha kuonywa katika ndoto, akaenda zake sehemu za Galilaya, 232:23 Lk 1:26; Isa 11:1; Yn 1:46akaenda akaishi katika mji ulioitwa Nazareti. Hivyo likawa limetimia neno lililonenwa na manabii, “Ataitwa Mnazarayo.”

Slovo na cestu

Matouš 2:1-23

Příchod učenců z východní země

1Ježíš se narodil v Betlémě v Judsku za vlády krále Heroda. V té době přijeli do Jeruzaléma učenci z východní země a vyptávali se: 2„Kde je ten židovský král, který se právě narodil? Viděli jsme na východě jeho hvězdu a přišli jsme se mu poklonit.“

3Tato novina velmi znepokojila krále Heroda, a nejen jeho, ale i všechny obyvatele Jeruzaléma. 4Král svolal všechny přední kněze a učitele zákona a ptal se jich, kde se má narodit Kristus. 5Oni mu odpověděli: „V Betlémě v Judsku. Prorok to předpověděl:

6‚Betléme, nejsi poslední v Judsku,

z tebe vyjde vévoda,

který se bude starat o můj lid

jako pastýř o ovce.‘ “

7Herodes si učence z východu tajně pozval a podrobně se jich vyptával, kdy se ta hvězda objevila. Poslal je do Betléma a pověřil je úkolem: 8„Jděte a důkladně zjistěte vše o tom dítěti, a až je najdete, přijďte mi to oznámit; půjdu se mu také poklonit.“

9Učenci krále vyslechli a vydali se na cestu.

A hle! Hvězda, kterou viděli na východě, jim ukazovala cestu až k místu, kde bylo dítě. 10Měli z toho nevýslovnou radost. 11Vešli do domu a našli tam dítě s jeho matkou Marií. Padli před ním na kolena, klaněli se mu a dali mu vzácné dary – zlato, kadidlo a drahocenný olej. 12Ve snu je však Bůh varoval, aby se nevraceli k Herodovi. Zvolili tedy jinou zpáteční cestu.

Útěk do Egypta

13Po odchodu učenců měl Josef sen, ve kterém mu anděl přikázal: „Vstaň, vezmi dítě a jeho matku a uteč s nimi do Egypta; tam zůstaň, dokud ti neřeknu. Herodes bude totiž pátrat po dítěti, aby je připravil o život.“ 14Josef hned v noci vstal, vzal dítě i matku a vydal se s nimi do Egypta. 15Tam byli až do smrti krále Heroda. Splnila se tím Boží předpověď vyslovená prorokem: „Z Egypta jsem povolal svého syna.“

16Když Herodes poznal, že ho východní učenci zklamali, velmi se rozhněval a dal pobít v Betlémě a okolí všechny chlapce do stáří dvou let. Tento věk odhadl podle výpovědi učenců. 17Tehdy se vyplnilo Jeremjášovo proroctví:

18„Slyším nářek,

pláč a bědování.

To matka oplakává své syny

a nedá se utěšit,

protože jsou mrtví.“

Návrat do Nazaretu

19Když Herodes zemřel, znovu se ukázal Josefovi ve snu anděl 20a vybídl ho: „Vezmi dítě i jeho matku a vrať se do izraelské země, protože už zemřeli ti, kteří usilovali o život dítěte.“ 21Josef poslechl a vrátili se. 22Velmi se však zalekl, když se dověděl, že Herodovým nástupcem v Judsku je jeho syn Archelaos. Ve snu dostal od Boha další pokyn, aby šel do Galileje. 23Usídlil se v Nazaretu a tím se splnila další proroctví o Mesiáši, že totiž bude nazýván Nazaretský.