Mathayo 12 – NEN & SNC

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 12:1-50

Bwana Wa Sabato

(Marko 2:23-28; Luka 6:1-5)

112:1 Kum 23:25Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala. 212:2 Kut 20:10; Yn 9:6Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”

312:3 1Sam 21:1-6Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa? 412:4 Law 24:5-9Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao. 512:5 Hes 28:9-10; Yn 7:22-23Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia? 612:6 Mt 12:41-42Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa. 712:7 Hos 6:6; Mt 9:13Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia, 812:8 Mt 8:20kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”

Yesu Anamponya Mtu Aliyepooza Mkono

(Marko 3:1-6; Luka 6:6-11)

912:9 Mk 3:1; Lk 6:6Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao, 1012:10 Lk 14:3; Yn 9:6na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”

1112:11 Lk 15:5Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa? 1212:12 Mt 6:26; 10:31Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”

13Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine. 1412:14 Mwa 37:18; Yn 11:53Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.

Mtumishi Aliyechaguliwa Na Mungu

1512:15 Mt 4:23Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote, 1612:16 Mt 8:4akiwakataza wasiseme yeye ni nani. 1712:17 Isa 42:1-4; 41:9Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:

1812:18 Mt 3:7; Isa 42:1-4; 41:9“Tazama mtumishi wangu niliyemchagua,

mpendwa wangu, ninayependezwa naye.

Nitaweka Roho wangu juu yake,

naye atatangaza haki kwa mataifa.

19Hatagombana wala hatapiga kelele,

wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.

20Mwanzi uliopondeka hatauvunja,

na utambi unaofuka moshi hatauzima,

mpaka atakapoifanya haki ishinde.

2112:21 Isa 42:1-4Katika Jina lake mataifa

wataweka tumaini lao.”

Yesu Na Beelzebuli

(Marko 3:20-30; Luka 11:14-23)

2212:22 Mt 4:24; 9:32-33Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona. 2312:23 Mt 9:27Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”

2412:24 Mk 3:22; Mt 9:34Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli,12:24 Beelzebuli au Beelzebubu; pia 12:27. mkuu wa pepo wachafu.”

2512:25 Mt 9:4Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama. 2612:26 Mt 4:10Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama? 2712:27 Mdo 19:13Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu. 2812:28 1Yn 3:8; Mt 3:2Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.

2912:29 Isa 49:24-25; Lk 11:21-22“Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.

3012:30 Mk 9:40; Yn 11:52; Lk 11:23“Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya. 3112:31 Mk 3:28-29; Lk 12:10Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa. 3212:32 Tit 2:12; Efe 1:21; Ebr 6:5Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao.

Mti Na Matunda Yake

(Luka 6:43-45)

3312:33 Mt 7:16-17; Lk 6:43-44“Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake. 3412:34 Mt 3:7; 23:33; 15:18; Yn 8:43Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake. 3512:35 Lk 6:45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake. 36Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena. 37Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”

Ishara Ya Yona

(Marko 8:11-12; Luka 11:29-32)

3812:38 Yn 6:30; 1Kor 1:22Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”

3912:39 Yn 1:7; Mt 8:20; 16:21Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona. 4012:40 Yn 2:1, 2; 1:17; Mt 8:20; 16:21Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumi12:40 Nyangumi ni samaki mkubwa sana. kwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana. 4112:41 Yn 1:2; 3:15Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona. 4212:42 1Fal 10:2; 2Nya 9:1Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”

Mafundisho Kuhusu Pepo Mchafu

(Luka 11:24-26)

43“Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati. 44Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri. 4512:45 2Pet 2:20Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”

Mama Na Ndugu Zake Yesu

(Marko 3:31-35; Luka 8:19-21)

4612:46 Lk 11:24; Ay 1:7; 1Pet 5:8Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye. 47Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”

4812:48 Lk 2:49Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?” 49Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu! 5012:50 Mt 6:10; Yn 15:14Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”

Slovo na cestu

Matouš 12:1-50

Učedníci vymílají v sobotu obilí

1Jednou v sobotu, sváteční den židů, procházel Ježíš se svými učedníky obilným polem. Učedníci měli hlad, trhali klasy a jedli zrní. 2Farizejové to viděli a žalovali Ježíšovi: „Podívej se, tvoji žáci dělají, co je v sobotu zakázáno!“

3Ježíš na to: „Cožpak jste nečetli, co učinil král David, když on a jeho družina byli hladoví? 4Jak vešli do chrámu a jedli posvátné chleby, které směli jíst jen kněží? 5Nebo jste nečetli v Mojžíšově zákoně, že kněží v chrámu pracují v sobotu? Porušují sobotní klid, a přesto jsou bez hříchu. 6Ale říkám vám, že je tu někdo, kdo je víc než chrám. 7Kdybyste rozuměli biblickému slovu ‚Nejde mi o oběti, ale chci, abyste byli milosrdní!‘ pak byste nikoho neodsuzovali neprávem. 8Kristus je pánem i nad sobotou.“

Ježíš v sobotu uzdravuje muže s ochrnutou rukou

9Odtud šel do synagogy. 10Tam byl člověk s ochrnutou rukou. Farizejové hledali nějakou záminku, aby mohli Ježíše obžalovat, a proto se ho otázali: „Je dovoleno v sobotu uzdravovat?“ 11On jim na to řekl: „Kdyby někdo z vás měl jedinou ovci a ta by spadla v sobotu do rokle, nepodnikli byste vše, abyste ji vytáhli? 12Oč cennější je člověk! Proto je správné dělat dobro i v sobotu.“ 13Obrátil se k postiženému a řekl mu: „Natáhni ruku!“ On to udělal a byla zdravá jako ta druhá. 14Farizejové odešli a radili se, jak by Ježíše zneškodnili.

Velké zástupy následují Ježíše

15Ježíš to poznal a odešel odtud. Mnozí ho však následovali a on uzdravil všechny nemocné. 16Ale přikázal jim, aby o něm moc nemluvili. 17Tak se naplnilo Izajášovo proroctví:

18„To je můj služebník,

ten, pro kterého jsem se rozhodl,

můj milovaný, potěšení mé duše.

Dám mu svého Ducha a bude soudit národy.

19Nebude se přít, ani nikoho překřikovat,

nebude dělat hluk na ulicích,

20nalomené stéblo nedolomí,

doutnající knot neuhasí,

dokud všechno nenapraví.

21Stane se nadějí všech národů.“

Náboženští vůdcové obviňují Ježíše z posedlosti

22Pak přivedli k Ježíšovi slepého a němého člověka. Ježíš ho uzdravil, takže viděl a mluvil. 23Lidé užasli a říkali: „On je snad opravdu Boží král z rodu Davidova!“ 24Ale slyšeli to farizejové a namítali: „Vždyť neuzdravuje jinak než s pomocí temných sil!“

25Ježíš však poznal, co si myslí, a proto řekl: „Rozdělené království končí v ruinách a žádné město nebo domov vnitřně rozdvojené neobstojí. 26Tak nemůže satan vyhánět satana. Jak by pak obstálo jeho království? 27Já, podle vás, odstraňuji temnotu ve jménu duchovní tmy. I mezi vámi jsou lidé, kteří bojují proti temným silám. Zeptejte se jich, jakou mocí to činí. 28Jestliže já ovšem vyháním zlo v moci Božího Ducha, pak už k vám přišlo Boží království. 29Když chce někdo ukrást věci z domu silného člověka, musí ho nejdříve svázat, a pak si to může odnést. Tak i ze satanovy moci může vysvobodit jen ten, kdo je silnější než on.

30Kdo není se mnou, je proti mně, kdo se mnou neshromažďuje, rozhazuje.

31-32Co mluvíte proti mně, to vám může být odpuštěno. Ale pozor – nemluvte proti moci Ducha, který působí skrze mne. To vám Bůh nikdy neodpustí.

33Jaký strom vypěstujete, takové ponese ovoce. Dobrý dobré, planý plané. 34Vy podvodníci! Jak byste mohli mluvit dobré, když jste zlí? Čím srdce oplývá, tím ústa přetékají. 35Dobrý člověk rozdává z dobrého pokladu svého srdce a zlý člověk ze zlého. 36Počítejte s tím, že budete skládat účty z každého neupřímného slova. 37Vaše slova o vás rozhodnou: buď vás ospravedlní, nebo odsoudí.“

Náboženští vůdcové žádají, aby Ježíš učinil zázrak

38Potom žádali farizejové a učitelé zákona Ježíše, aby se prokázal nějakým zázrakem. 39On jim však odpověděl: „Vězíte v hříchu a zatvrzelosti, a proto vyžadujete další důkazy. Nedostanete je! 40Tak jako věříte, že byl Jonáš tři dny a tři noci v útrobách mořského živočicha, tak budete muset uvěřit, že Syn člověka třetí den vstane z hrobu.

41Lidé z Ninive vystoupí na soudu proti vám a usvědčí vás, protože oni vzali vážně Jonášovu zvěst. A k vám mluví ten, kdo je víc než Jonáš.

42Královna ze Sáby vystoupí na soudu jako další svědek proti vám. Neváhala přijet z daleké země, aby poznala Šalomounovu moudrost. A tady je někdo větší než Šalomoun.

43-45Když je z člověka vyhnán nečistý duch, hledá, kde jinde by se zabydlel. Ale nechce se snadno vzdát prvního hostitele. Když vidí, že srdce toho člověka je sice vyčištěné a upravené, ale zůstává prázdné, nastěhuje se tam zpět se sedmi společníky horšími, než je sám. Takový člověk je na tom potom hůř než předtím. To nebezpečí hrozí i vám.“

Ježíš říká, kdo tvoří jeho rodinu

46Ježíš ještě mluvil v přeplněném domě, když přišla jeho matka a bratři. Čekali venku, protože s ním chtěli mluvit. 47Když ho jeden z davu upozornil, že na něho čekají, 48řekl: „Kdo je má matka a moji bratři?“ 49Ukázal na své učedníky se slovy: „To je moje rodina. 50Každý, kdo poslouchá mého nebeského Otce, je můj bratr, sestra i matka!“