Mathayo 11 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 11:1-30

Yesu Na Yohana Mbatizaji

(Luka 7:18-35)

111:1 Mt 7:28; 26:1Baada ya Yesu kumaliza kutoa maagizo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.

211:2 Mt 14:3Yohana aliposikia akiwa gerezani mambo ambayo Kristo11:2 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. alikuwa akiyafanya, aliwatuma wanafunzi wake 311:3 Za 118:26; Ebr 10:37ili wakamuulize, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”

4Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mnayosikia na kuyaona: 511:5 Lk 4:18-19; Isa 61:1-2Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema. 611:6 Mt 13:21; 26:31Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”

711:7 Mt 3:1-5Wale wanafunzi wa Yohana walipokuwa wanaondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo? 8Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari wako katika majumba ya wafalme. 911:9 Lk 1:76; 7:26Basi mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii. 1011:10 Mal 3:1; Lk 7:27Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa:

“ ‘Tazama nitamtuma mjumbe wangu mbele yako,

atakayetengeneza njia mbele yako.’

1111:11 Mt 13:17Amin, nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni ni mkuu kuliko Yohana. 1211:12 Lk 16:16; 13:24Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wanauteka. 1311:13 Lk 16:16Kwa maana manabii wote na Sheria walitabiri mpaka wakati wa Yohana. 1411:14 Mal 4:5; Yn 1:21Ikiwa mko tayari kukubali hilo, yeye ndiye yule Eliya ambaye manabii walikuwa wamesema angekuja. 1511:15 Lk 14:35; Ufu 2:7Yeye aliye na masikio, na asikie.

1611:16 Lk 7:31“Lakini kizazi hiki nikifananishe na nini? Kinafanana na watoto waliokaa sokoni wakiwaita wenzao na kuwaambia,

1711:17 Mit 29:9“ ‘Tuliwapigia filimbi,

lakini hamkucheza;

tuliwaimbia nyimbo za maombolezo,

lakini hamkuomboleza.’

1811:18 Mt 3:4; Lk 1:15Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali wala hanywi, nao wanasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’ 1911:19 Mt 9:11Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nao wanasema, ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.” ’ Lakini hekima huthibitishwa kuwa kweli kwa matendo yake.”

Onyo Kwa Miji Isiyotubu

(Luka 10:13-15)

2011:20 Lk 10:11Ndipo Yesu akaanza kushutumu miji ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu. 2111:21 Mk 8:22; Yn 1:44; Yoe 3:4; Mk 3:8; Yn 3:5-9“Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu. 2211:22 Mt 11:24; 10:15Lakini nawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi. 2311:23 Mt 4:13; Isa 14:13-15Nawe Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.11:23 Kuzimu ni Mahali pa wafu. Miujiza iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwepo hadi leo. 2411:24 Mt 10:15Lakini nakuambia kwamba, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ya hukumu kuliko wewe.”

Hakuna Amjuaye Baba Ila Mwana

(Luka 10:21-22)

2511:25 Lk 23:34; Yn 12:27-28; Mt 13:11; 1Kor 1:26-29Wakati huo Yesu alisema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo. 26Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.

2711:27 Mt 28:18; Yn 3:35; 10:15; 17:25-26“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: Hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.

Yesu Awaita Waliolemewa Na Mizigo

2811:28 Yn 7:37“Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 2911:29 Flp 2:5; 1Yn 2:6; Za 116:7; Yer 6:16Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. 3011:30 1Yn 5:3Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”

King James Version

Matthew 11:1-30

1And it came to pass, when Jesus had made an end of commanding his twelve disciples, he departed thence to teach and to preach in their cities. 2Now when John had heard in the prison the works of Christ, he sent two of his disciples, 3And said unto him, Art thou he that should come, or do we look for another? 4Jesus answered and said unto them, Go and shew John again those things which ye do hear and see: 5The blind receive their sight, and the lame walk, the lepers are cleansed, and the deaf hear, the dead are raised up, and the poor have the gospel preached to them. 6And blessed is he, whosoever shall not be offended in me.

7¶ And as they departed, Jesus began to say unto the multitudes concerning John, What went ye out into the wilderness to see? A reed shaken with the wind? 8But what went ye out for to see? A man clothed in soft raiment? behold, they that wear soft clothing are in kings’ houses. 9But what went ye out for to see? A prophet? yea, I say unto you, and more than a prophet. 10For this is he, of whom it is written, Behold, I send my messenger before thy face, which shall prepare thy way before thee. 11Verily I say unto you, Among them that are born of women there hath not risen a greater than John the Baptist: notwithstanding he that is least in the kingdom of heaven is greater than he. 12And from the days of John the Baptist until now the kingdom of heaven suffereth violence, and the violent take it by force. 13For all the prophets and the law prophesied until John. 14And if ye will receive it, this is Elias, which was for to come. 15He that hath ears to hear, let him hear.

16¶ But whereunto shall I liken this generation? It is like unto children sitting in the markets, and calling unto their fellows, 17And saying, We have piped unto you, and ye have not danced; we have mourned unto you, and ye have not lamented. 18For John came neither eating nor drinking, and they say, He hath a devil. 19The Son of man came eating and drinking, and they say, Behold a man gluttonous, and a winebibber, a friend of publicans and sinners. But wisdom is justified of her children.

20¶ Then began he to upbraid the cities wherein most of his mighty works were done, because they repented not: 21Woe unto thee, Chorazin! woe unto thee, Bethsaida! for if the mighty works, which were done in you, had been done in Tyre and Sidon, they would have repented long ago in sackcloth and ashes. 22But I say unto you, It shall be more tolerable for Tyre and Sidon at the day of judgment, than for you. 23And thou, Capernaum, which art exalted unto heaven, shalt be brought down to hell: for if the mighty works, which have been done in thee, had been done in Sodom, it would have remained until this day. 24But I say unto you, That it shall be more tolerable for the land of Sodom in the day of judgment, than for thee.

25¶ At that time Jesus answered and said, I thank thee, O Father, Lord of heaven and earth, because thou hast hid these things from the wise and prudent, and hast revealed them unto babes. 26Even so, Father: for so it seemed good in thy sight. 27All things are delivered unto me of my Father: and no man knoweth the Son, but the Father; neither knoweth any man the Father, save the Son, and he to whomsoever the Son will reveal him.

28¶ Come unto me, all ye that labour and are heavy laden, and I will give you rest. 29Take my yoke upon you, and learn of me; for I am meek and lowly in heart: and ye shall find rest unto your souls. 30For my yoke is easy, and my burden is light.