Matendo 28 – NEN & HHH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 28:1-31

Paulo Kisiwani Malta

128:1 Mdo 16:10; 27:26, 39Baada ya kufika nchi kavu salama, ndipo tukafahamu kwamba jina la kile kisiwa ni Malta. 228:2 Mdo 27:3; 2Kor 11:27Wenyeji wa kile kisiwa wakatufanyia ukarimu usio wa kawaida. Waliwasha moto na kutukaribisha sisi sote kwa sababu mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa na baridi. 3Paulo alikuwa amekusanya mzigo wa kuni na alipokuwa anaweka kwenye moto kwa ajili ya joto, nyoka mwenye sumu akatoka humo na kujisokotea mkononi mwake. 428:4 Mk 16:18; Lk 13:2, 4Wale wenyeji wa kile kisiwa walipomwona yule nyoka akiningʼinia mkononi mwa Paulo, wakaambiana, “Huyu mtu lazima awe ni muuaji, ingawa ameokoka kutoka baharini, haki haijamwacha aishi.” 528:5 Lk 10:19Lakini Paulo akamkungʼutia yule nyoka ndani ya moto wala yeye hakupata madhara yoyote. 628:6 Mdo 14:11Watu walikuwa wanangoja avimbe au aanguke ghafula na kufa. Lakini baada ya kungoja kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna chochote kisicho cha kawaida kilichomtokea, wakabadili mawazo yao na kuanza kusema kwamba yeye ni mungu.

7Basi karibu na sehemu ile, palikuwa na shamba kubwa la mtu mmoja kiongozi wa kile kisiwa, aliyeitwa Publio. Alitupokea na akatuhudumia kwa ukarimu mkubwa kwa muda wa siku tatu. 828:8 Yak 5:14, 15; Mdo 9:40Baba yake Publio alikuwa mgonjwa kitandani, akiwa anaumwa homa na kuhara damu. Paulo akaingia ndani ili kumwona na baada ya maombi, akaweka mikono juu yake na kumponya. 9Jambo hili lilipotukia, watu wote wa kisiwa kile waliokuwa wagonjwa wakaja, nao wakaponywa. 1028:10 Mt 15:6; 1Tim 5:17; Za 15:4Wakatupa heshima nyingi, nasi tulipokuwa tayari kusafiri kwa njia ya bahari, wakapakia melini vitu vyote tulivyokuwa tunavihitaji.

Paulo Awasili Rumi

1128:11 Mdo 27:6Miezi mitatu baadaye tukaanza safari kwa meli iliyokuwa imetia nanga kwenye kisiwa hicho kwa ajili ya majira ya baridi. Hii ilikuwa meli ya Iskanderia yenye alama ya miungu pacha waitwao Kasta na Poluksi. 12Kituo chetu cha kwanza kilikuwa Sirakusa na tukakaa huko siku tatu. 13Kisha tukangʼoa nanga, tukafika Regio. Siku iliyofuata, upepo mkali wa kusi ukavuma, na siku ya pili yake tukafika Puteoli. 1428:14 Mdo 1:16Huko tukawakuta ndugu, nasi tukakaribishwa tukae nao kwa siku saba. Hivyo tukaendelea na safari mpaka Rumi. 1528:15 Mdo 1:16Ndugu wa huko Rumi waliposikia habari zetu, walikuja mpaka Soko la Apio na mahali paitwapo Mikahawa Mitatu kutulaki. Paulo alipowaona, alimshukuru Mungu akatiwa moyo. 1628:16 Mdo 24:23; 27:3Tulipofika Rumi, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake akiwa na askari wa kumlinda.

Paulo Ahubiri Rumi Chini Ya Ulinzi

1728:17 Mdo 25:2; 22:5; 25:8; 6:14Siku tatu baadaye Paulo akawaita pamoja viongozi wa Kiyahudi. Walipokwisha kukusanyika akawaambia, “Ndugu zangu, ingawa sikufanya jambo lolote dhidi ya watu wetu au dhidi ya desturi za baba zetu, lakini nilikamatwa huko Yerusalemu nikakabidhiwa kwa Warumi. 1828:18 Mdo 22:24; 26:31, 32; 23:9Wao walipokwisha kunihoji, wakataka kuniachia huru kwa sababu hawakuona kosa lolote nililolifanya linalostahili adhabu ya kifo. 1928:19 Mdo 25:11; 26:32Lakini Wayahudi walipopinga uamuzi huo, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisari, ingawa sikuwa na lalamiko lolote juu ya taifa langu. 2028:20 Mdo 26:6, 7; 21:33Basi hii ndiyo sababu nimewatumania, ili niseme nanyi. Kwa kuwa ni kwa ajili ya tumaini la Israeli nimefungwa kwa minyororo.”

2128:21 Mdo 22:5Wakamjibu, “Hatujapokea barua zozote kutoka Uyahudi zinazokuhusu, wala hapana ndugu yeyote aliyekuja hapa ambaye ametoa taarifa au kuzungumza jambo lolote baya juu yako. 2228:22 Mdo 24:5, 14Lakini tungependa kusikia kutoka kwako unalofikiri kwa sababu tunajua kwamba kila mahali watu wanazungumza mabaya kuhusu jamii hii.”

2328:23 Mt 3:2; Mdo 19:8; 17:3; 8:35Baada ya kupanga siku ya kuonana naye, watu wengi wakaja kuanzia asubuhi hadi jioni akawaeleza na kutangaza kuhusu Ufalme wa Mungu akijaribu kuwahadithia juu ya Yesu kutoka Sheria ya Mose na kutoka Manabii. 2428:24 Mdo 14:4Baadhi wakasadiki yale aliyosema, lakini wengine hawakuamini. 25Hivyo hawakukubaliana, nao walipokuwa wanaondoka, Paulo akatoa kauli moja zaidi: “Roho Mtakatifu alinena kweli na baba zenu aliposema mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba:

2628:26 Isa 6:9; Yer 5:21; Eze 12:2; Mt 13:14, 15; Mk 4:12; Lk 8:10; Yn 12:40; Rum 11:8“ ‘Nenda kwa watu hawa na useme,

“Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa;

na pia mtatazama, lakini hamtaona.”

2728:27 Za 119:70; Isa 6:9, 10Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu;

hawasikii kwa masikio yao,

na wamefumba macho yao.

Wasije wakaona kwa macho yao,

na wakasikiliza kwa masikio yao,

wakaelewa kwa mioyo yao,

na kugeuka nami nikawaponya.’

2828:28 Lk 2:30; Mdo 13:46“Basi na ijulikane kwenu kwamba, huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, nao watasikiliza.” [ 29Naye akiisha kusema maneno haya, Wayahudi wakaondoka wakiwa na hoja nyingi miongoni mwao.]

30Kwa miaka miwili mizima Paulo alikaa huko kwa nyumba aliyokuwa amepanga. Akawakaribisha wote waliokwenda kumwona. 3128:31 Mdo 4:29; Mt 4:23; Mdo 4:29; 28:23; Mt 4:23; Mdo 4:23; 4:23; 4:31; Efe 6:19Akahubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri wote na bila kizuizi chochote.

Habrit Hakhadasha/Haderekh

מעשי השליחים 28:1-31

1עד מהרה גילינו שאנו על האי מלטה. 2תושבי המקום נהגו בנו בטוב־לב ראוי לציון, והבעירו מדורה כדי לחמם אותנו בקור העז ובגשם הסוחף.

3פולוס קושש ענפים וזרדים יבשים, והשליך אותם אל תוך המדורה. לפתע זינק על זרועו נחש ארסי שביקש מפלט מהחום. 4כשראו אנשי האי את הנחש התלוי על זרועו, אמרו זה לזה: ”הוא בטח רוצח! הוא אמנם ניצל מן הים, אולם הצדק לא יניח לו לחיות!“

5אך פולוס ניער את הנחש אל תוך האש, והוא עצמו כלל לא נפגע. 6האנשים הביטו בו בדריכות וציפו לראות את גופו מתנפח או נופל מת. אולם לאחר שחיכו זמן רב ולא קרה דבר, שינו את דעתם והחליטו שפולוס הוא ודאי אל!

7אחוזתו של פובליוס, מושל האי, הייתה בקרבת החוף. הוא הזמין אותנו לביתו ואירח אותנו שלושה ימים. 8באותה עת היה אביו של פובליוס חולה מאוד – הייתה לו דיזנטריה והוא קדח מחום. פולוס הלך לחדרו של החולה, התפלל בעדו, סמך את ידיו עליו, והאיש נרפא. 9לאחר מכן באו שאר חולי האי אל פולוס, וגם הם נרפאו. 10התושבים היו אסירי תודה והציפו אותנו במתנות הוקרה. כאשר הגיע מועד הפלגתנו, הם מילאו את האונייה באוכל ובציוד.

11שלושה חודשים לאחר שעלתה ספינתנו על שירטון עלינו על אונייה אחרת והמשכנו בדרכנו. הפעם הפלגנו באונייה ”התאומים“, שבאה מאלכסנדריה ועגנה באי מלטה במשך החורף. 12תחנתנו הראשונה הייתה סירקוז, שם נשארנו שלושה ימים. 13מסירקוז הפלגנו לרגיום. כעבור יום החלה לנשוב רוח דרומית, וביום השני הגענו לפוטיולי. 14בפוטיולי פגשנו לבסוף מאמינים. הם הפצירו בנו להישאר איתם שבוע ימים, ומשם הפלגנו לרומא.

15כאשר שמעו האחים ברומא על דבר בואנו, נסעו מרחק רב מחוץ לעירם כדי לקבל את פנינו. חלקם חיכו לנו בכיכר אפיוס (כשישים ושמונה ק״מ מרומא), וחלקם הצטרפו אלינו ב”שלושת הפונדקים“ (כ־חמישים וחמישה ק״מ מרומא). כשפולוס ראה אותם הוא התעודד מאוד והודה לה׳.

16בהגיעם לרומא הורשה פולוס לגור בכל מקום שרצה, אם כי תמיד נלווה אליו חייל. 17כעבור שלושה ימים כינס פולוס את מנהיגי היהודים המקומיים, ואמר להם: ”היהודים בירושלים אסרו אותי ומסרו אותי לידי הממשל הרומאי, למרות שלא פגעתי באיש ולא עברתי על חוקי אבותינו. 18הרומאים ערכו לי משפט ורצו לשחרר אותי, מכיוון שלא מצאו כל סיבה לדון אותי למוות, כפי שדרשו היהודים. 19אולם מאחר שהיהודים מחו נגד ההחלטה, מצאתי לנחוץ לערער לפני הקיסר, למרות שלא רציתי לתבוע את עמי. 20ביקשתי מכם לבוא הנה היום כדי שנכיר זה את זה, וכדי שאוכל לומר לכם שאני אסור באזיקים אלה רק משום שאני מאמין שהמשיח כבר בא!“

21”לא שמענו עליך שום דבר רע.“ ענו מנהיגי היהודים. ”לא קיבלנו מכתבים מיהודה, ולא שמענו דיווחים מפי הבאים לכאן מירושלים. 22אולם אנחנו רוצים לשמוע במה אתה מאמין, כי הדבר היחיד שאנו יודעים על המשיחיים האלה הוא שבכל מקום מתנגדים לכת הזאת.“

23הם קבעו מועד לפגישתם הבאה, ובאותו יום התאסף קהל רב ליד ביתו של פולוס. הוא סיפר להם על מלכות האלוהים, ולימד אותם על אודות ישוע מתוך כתבי־הקודש – מהתורה ומהנביאים. הוא החל ללמד אותם בבוקר, ולא הפסיק עד הערב.

24אחדים האמינו לדבריו, ואחרים לא האמינו. 25לאחר שהתווכחו בינם לבין עצמם, הם עזבו את המקום כשדבריו של פולוס מהדהדים באוזניהם: ”רוח הקודש צדק כששם דברים אלה בפי ישעיהו הנביא:28‏.25 כח 25 ישעיהו ו 9‏-10

26’לך ואמרת לעם הזה:

שמעו שמוע ואל תבינו,

וראו ראו ואל תדעו;

27השמן לב העם הזה

ואזניו הכבד ועיניו השע,

פן יראה בעיניו ובאזניו ישמע,

ולבבו יבין ושב ורפא לו‘.

28‏-29משום כך אני רוצה שתדעו כי ישועה זאת מוצעת גם לגויים, והם ישמעו.“

30במשך השנתיים הבאות התגורר פולוס בבית ששכר לעצמו, וקיבל בברכה את כל מי שבא לבקרו. 31הוא בישר באומץ את דבר מלכות האלוהים, לימד על אודות האדון ישוע המשיח, ואיש לא ניסה להפריע לו.