Matendo 22 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 22:1-30

Ushuhuda Wa Paulo Kwa Wayahudi Wa Yerusalemu

122:1 Mdo 7:2“Ndugu zangu na baba zangu, sikilizeni utetezi wangu.”

222:2 Mdo 21:40Waliposikia akisema kwa lugha ya Kiebrania, wakanyamaza kimya kabisa.

Ndipo Paulo akasema, 322:3 Mdo 9:11; Lk 10:39; Mdo 5:34; 26:5; 21:20“Mimi ni Myahudi, niliyezaliwa Tarso huko Kilikia, lakini nimelelewa katika mji huu. Miguuni mwa Gamalieli, nilifundishwa kikamilifu katika sheria ya baba zetu, na nikawa mwenye juhudi kwa ajili ya Mungu kama kila mmoja wenu alivyo leo. 422:4 Mdo 8:3Niliwatesa watu wa Njia hii hadi kufa, nikiwakamata waume kwa wake na kuwatupa gerezani, 522:5 Lk 22:66; Rum 7:1; Mdo 9:2kama kuhani mkuu na baraza zima la wazee wanavyoweza kushuhudia kunihusu. Hata nilipokea barua kutoka kwao kwenda kwa ndugu wale wa Dameski, nami nikaenda huko ili kuwaleta watu hawa Yerusalemu kama wafungwa ili waadhibiwe.

Paulo Aeleza Juu Ya Kuokoka Kwake

(Matendo 9:1-19; 26:12-18)

622:6 Mdo 9:3“Nilipokuwa njiani kuelekea Dameski, yapata saa sita mchana, ghafula nuru kubwa kutoka mbinguni ikanimulika kotekote. 7Nikaanguka chini, nikasikia sauti ikiniambia, ‘Sauli, Sauli! Mbona unanitesa?’

822:8 Mk 1:24“Nikajibu, ‘Wewe ni nani Bwana?’

“Naye akaniambia, ‘Mimi ni Yesu wa Nazareti unayemtesa.’ 922:9 Mdo 26:13; 9:7Basi wale watu waliokuwa pamoja nami waliiona ile nuru, lakini hawakuisikia sauti ya yule aliyekuwa akisema nami.

1022:10 Mdo 16:30“Nikauliza, ‘Nifanye nini Bwana?’

“Naye Bwana akaniambia, ‘Inuka uingie Dameski, huko utaambiwa yote yakupasayo kufanya.’ 1122:11 Mdo 9:8Kwa kuwa nilikuwa siwezi kuona kwa ajili ya mngʼao wa ile nuru, wenzangu wakanishika mkono wakaniongoza kuingia Dameski.

1222:12 Mdo 9:17; 19:22“Mtu mmoja mcha Mungu, jina lake Anania, alikuja kuniona. Alizishika sana sheria zetu, na aliheshimiwa sana na Wayahudi waliokuwa wakiishi huko Dameski. 13Akasimama karibu nami, akasema, ‘Ndugu Sauli, pata kuona tena!’ Saa ile ile nikapata kuona tena, nami nikaweza kumwona.

1422:14 Mdo 3:13; 1Kor 9:1; 15:8; Mdo 7:52“Akasema, ‘Mungu wa baba zetu amekuchagua wewe ili ujue mapenzi yake, umwone yeye Aliye Mwenye Haki na upate kusikia maneno kutoka kinywani mwake. 1522:15 Mdo 23:11; 26:16Kwa kuwa utakuwa shahidi wake kwa watu kuhusu kile ulichokiona na kukisikia. 1622:16 Mdo 2:38; Za 51:2; Rum 10:13Sasa basi, mbona unakawia? Inuka, ukabatizwe na dhambi zako zikasafishwe, ukiliita Jina lake.’

Paulo Atumwa Kwa Watu Wa Mataifa

1722:17 Mdo 9:26; 10:10“Baada ya kurudi Yerusalemu, nilipokuwa ninaomba Hekaluni, nilipitiwa na usingizi wa ghafula 1822:18 Mdo 22:14; Mt 10:14nikamwona Bwana akiniambia, ‘Harakisha utoke Yerusalemu upesi, maana hawataukubali ushuhuda wako kunihusu mimi.’

1922:19 Mdo 8:3; Mt 10:17“Nami nikasema, ‘Bwana, wao wenyewe wanajua jinsi nilivyokwenda kwenye kila sinagogi ili kuwatupa gerezani na kuwapiga wale waliokuamini. 2022:20 Mdo 7:57-60; 8:1Wakati damu ya shahidi wako Stefano ilipomwagwa, mimi mwenyewe nilikuwa nimesimama kando, nikikubaliana na kitendo hicho na kutunza mavazi ya wale waliomuua.’

2122:21 Mdo 9:15; 13:46“Ndipo Bwana akaniambia, ‘Nenda, kwa maana nitakutuma mbali, kwa watu wa Mataifa.’ ”

Paulo Na Jemadari Wa Kirumi

2222:22 Mdo 21:36Ule umati wa watu wakamsikiliza Paulo mpaka aliposema neno hilo, ndipo wakapaza sauti zao na kupiga kelele wakisema, “Mwondoeni duniani, hafai kuishi!”

2322:23 Mdo 7:58; 2Sam 16:13Walipokuwa wakipiga kelele na kutoa mavazi yao huku wakirusha mavumbi juu hewani, 2422:24 Mdo 21:34yule jemadari akaamuru Paulo aingizwe kwenye ngome. Akaelekeza kwamba achapwe viboko na aulizwe ili kujua kwa nini watu walikuwa wanampigia kelele namna hiyo. 2522:25 Mdo 16:37Lakini walipokwisha kumfunga kwa kamba za ngozi ili wamchape viboko, Paulo akamwambia kiongozi wa askari aliyekuwa amesimama pale karibu naye, “Je, ni halali kwenu kwa mujibu wa sheria kumchapa mtu ambaye ni raiya wa Rumi hata kabla hajapatikana na hatia?”

26Yule kiongozi aliposikia maneno haya, alimwendea yule jemadari na kumwambia, “Unataka kufanya nini? Kwa maana huyu mtu ni raiya wa Rumi.”

27Yule jemadari akaja akamuuliza Paulo, “Niambie, wewe ni raiya wa Rumi?”

Paulo akajibu, “Naam, hakika ndiyo.”

28Ndipo yule jemadari akasema, “Mimi ilinigharimu kiasi kikubwa cha fedha kupata uraia wangu.”

Paulo akasema “Lakini mimi ni raiya wa Rumi kwa kuzaliwa.”

2922:29 Mdo 16:38Mara wale waliokuwa wanataka kumhoji wakajiondoa haraka, naye yule jemadari akaingiwa na hofu alipotambua ya kuwa amemfunga Paulo, ambaye ni raia wa Rumi, kwa minyororo.

Paulo Apelekwa Mbele Ya Baraza

3022:30 Mdo 23:28; 21:33; Mt 5:22Kesho yake, kwa kuwa yule jemadari alitaka kujua hakika kwa nini Paulo alikuwa anashutumiwa na Wayahudi, alimfungua, na akawaagiza viongozi wa makuhani na baraza lote likutane. Kisha akamleta Paulo, akamsimamisha mbele yao.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

使徒行傳 22:1-30

1「各位父老兄弟,請聽我解釋!」 2在場的人聽見保羅講的是希伯來話,更加安靜了。保羅說: 3「我是猶太人,生於基利迦大數,在耶路撒冷長大,曾在迦瑪列門下嚴格地按著我們祖先的律法接受教育,像你們今日一樣熱心事奉上帝。 4我曾經把信奉這道的男女信徒抓進監獄,迫害他們,置他們於死地。 5大祭司和眾長老都可以為我作證。我還拿著他們寫給大馬士革猶太人的信去拘捕那裡的信徒,押回耶路撒冷受刑。

6「當我快到大馬士革的時候,大約中午時分,突然從天上有一道強光四面照著我。 7我就仆倒在地,聽見有聲音對我說,『掃羅掃羅!你為什麼迫害我?』 8我回答說,『主啊,你是誰?』他說,『我就是你迫害的拿撒勒人耶穌!』 9我的同伴雖然也看見那道強光,卻聽不懂那位說話者的聲音。 10接著我又問,『主啊!我該怎麼辦?』主說,『起來,到大馬士革去,那裡會有人將指派給你的事告訴你。』

11「那道耀眼的光照得我雙眼失明,於是同行的人拉著我的手,帶我進了大馬士革12那裡有一個嚴守律法的虔誠人名叫亞拿尼亞,深受當地所有猶太人的尊敬。 13他來探望我,站在我身邊說,『掃羅弟兄,重見光明吧!』就在那一刻,我抬頭看見了他。 14他又說,『我們祖先的上帝揀選了你,要你明白祂的旨意,又讓你親自看見那位公義者、聽到祂的聲音。 15因為你將作祂的見證人,把所見所聞告訴萬民。 16現在你還等什麼呢?起來求告祂的名,接受洗禮,洗淨你的罪。』

17「後來,我回到耶路撒冷,在聖殿裡禱告的時候,進入異象, 18看見主對我說,『趕快離開耶路撒冷,因為這裡的人不會接受你為我做的見證。』 19我說,『主啊!他們都知道我從前搜遍各會堂,逮捕、毒打信你的人。 20當你的見證人司提凡為你流血殉道時,我自己也站在旁邊贊同殺他的人,還替他們保管衣服。』 21主卻對我說,『去吧!我要差遣你到遙遠的外族人那裡。』」

因羅馬公民身分而免刑

22眾人一聽到這裡,就高喊:「從世上除掉這樣的人!他不配活著!」 23百姓咆哮著脫掉外衣,揚起塵土。 24千夫長下令把保羅押回營房,預備鞭打拷問他,要查出眾人向他咆哮的緣由。 25他們把保羅綁起來正要鞭打,保羅問旁邊的百夫長:「未經定罪就拷打羅馬公民合法嗎?」

26百夫長一聽,立刻去稟告千夫長說:「你看該怎麼辦?這人是羅馬公民。」

27千夫長就來問保羅:「告訴我,你是羅馬公民嗎?」

保羅說:「是的。」

28千夫長說:「我花了很多錢才當上羅馬公民!」

保羅說:「我生來就是。」

29那些準備拷問保羅的士兵立刻退下了。千夫長也害怕起來,因為發現保羅羅馬公民,他卻下令捆綁了保羅

保羅在公會申辯

30第二天,千夫長想知道保羅猶太人指控的真相,就為保羅鬆了綁,並召聚了祭司長和全公會的人,然後將保羅帶來,讓他站在眾人面前。