Matendo 21 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 21:1-40

Paulo Aenda Yerusalemu

121:1 Mdo 16:10Tulipokwisha kujitenga nao, tukaanza safari kwa njia ya bahari moja kwa moja mpaka Kosi. Siku ya pili yake tukafika Rodo na kutoka huko tukaenda Patara. 221:2 Mdo 11:19Hapo tukapata meli iliyokuwa inavuka kwenda Foinike tukapanda tukasafiri nayo. 321:3 Lk 2:2Tulipokiona kisiwa cha Kipro, tukakizunguka tukakiacha upande wetu wa kushoto, tukasafiri mpaka Shamu, tukatia nanga katika bandari ya Tiro ambapo meli yetu ilikuwa ipakue shehena yake. 421:4 Mdo 11:26; 20:23Baada ya kuwatafuta wanafunzi wa huko, tukakaa nao kwa siku saba. Wale wanafunzi wakiongozwa na Roho wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu. 521:5 Mdo 20:36Lakini muda wetu ulipokwisha, tukaondoka tukaendelea na safari yetu. Wale wanafunzi pamoja na wake zao na watoto wakatusindikiza hadi nje ya mji. Wote tukapiga magoti pale pwani tukaomba. 621:6 Yn 1:11Baada ya kuagana, tukapanda melini, nao wakarudi majumbani mwao.

721:7 Mdo 12:20; 1:16Tukaendelea na safari yetu toka Tiro tukafika Tolemai, tukawasalimu ndugu wa huko, tukakaa nao kwa siku moja. 821:8 Efe 4:11; 2Tim 4:5; Mdo 6:5; 8:26, 40Siku iliyofuata tukaondoka, tukafika Kaisaria. Huko tukaenda nyumbani kwa mwinjilisti mmoja jina lake Filipo, aliyekuwa mmoja wa wale Saba, tukakaa kwake. 921:9 Yoe 2:28; Mdo 2:17; Kut 15:20Filipo alikuwa na binti wanne mabikira waliokuwa wanatoa unabii.

1021:10 Mdo 11:28Baada ya kukaa kwa siku kadhaa, akateremka nabii mmoja kutoka Uyahudi jina lake Agabo. 1121:11 Isa 20:2, 4Alipotufikia akachukua mshipi wa Paulo akajifunga, akautumia kufunga mikono na miguu yake mwenyewe akasema, “Roho Mtakatifu anasema: ‘Hivi ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga mwenye mshipi huu na kumkabidhi kwa watu wa Mataifa.’ ”

12Tuliposikia maneno haya sisi na ndugu wengine tukamsihi Paulo asiende Yerusalemu. 1321:13 Mdo 20:24Lakini Paulo akajibu, “Kwa nini mnalia na kunivunja moyo? Mimi niko tayari si kufungwa tu, bali hata kufa huko Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.” 1421:14 Mt 6:10; 26:42; Lk 11:2; 22:42; Rum 1:18Alipokuwa hashawishiki, tukaacha kumsihi, tukasema, “Mapenzi ya Bwana na yatendeke.”

1521:15 Mdo 19:21Baada ya haya, tukajiandaa, tukaondoka kwenda Yerusalemu. 1621:16 Mdo 8:40Baadhi ya wanafunzi kutoka Kaisaria wakafuatana nasi na kutupeleka nyumbani kwa Mnasoni, ambaye tungekaa kwake. Yeye alikuwa mtu wa Kipro, mmoja wa wanafunzi wa zamani.

Kukamatwa Kwa Paulo, Na Safari Yake Kwenda Rumi

(21:17–28:31)

Paulo Awasili Yerusalemu

1721:17 Mdo 15:4Tulipofika Yerusalemu ndugu wakatukaribisha kwa furaha. 1821:18 Mdo 15; 13; 11:30Kesho yake Paulo pamoja na wengine wetu tulikwenda kumwona Yakobo, na wazee wote walikuwepo. 1921:19 Mdo 14:27; 1:17Baada ya kuwasalimu, Paulo akatoa taarifa kamili ya mambo yote ambayo Mungu alikuwa amefanya miongoni mwa watu wa Mataifa kupitia huduma yake.

2021:20 Gal 1:14; Flp 3:6Baada ya kusikia mambo haya wakamwadhimisha Mungu. Ndipo wakamwambia Paulo, “Ndugu, unaona kulivyo na maelfu ya Wayahudi walioamini, nao wote wana juhudi kwa ajili ya sheria. 2121:21 Mdo 15:19-21; 1Kor 7:18, 19; Mdo 6:14Lakini wameambiwa habari zako kwamba unafundisha Wayahudi wote waishio miongoni mwa watu wa Mataifa kumkataa Mose, na kwamba unawaambia wasiwatahiri watoto wao wala kufuata desturi zetu. 22Sasa tufanyeje? Bila shaka watasikia kwamba umekuja Yerusalemu. 2321:23 Mdo 18:18Kwa hiyo fanya lile tunalokuambia. Tunao watu wanne hapa ambao wameweka nadhiri. 2421:24 Mdo 24:18; 18:18Jiunge na watu hawa, mfanye utaratibu wa ibada ya kujitakasa pamoja nao, na ulipe gharama ili wanyoe nywele zao. Kwa njia hii kila mtu atafahamu ya kuwa mambo waliyosikia si ya kweli na kwamba wewe unaishika sheria. 2521:25 Mdo 15:20-29Lakini kuhusu wale watu wa Mataifa walioamini, tumewaandikia uamuzi wetu: kwamba wajitenge na vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, au kula nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati.”

2621:26 Hes 6:13, 20; Mdo 24:18Ndipo kesho yake Paulo akawachukua wale watu na akajitakasa pamoja nao. Akaingia ndani ya hekalu ili atoe taarifa ya tarehe ambayo siku zao za utakaso zingemalizika na sadaka ingetolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.

Paulo Akamatwa

2721:27 Yer 26:8; 1The 2:16Zile siku saba zilipokaribia kumalizika, baadhi ya Wayahudi kutoka sehemu za Asia waliokuwa wamemwona Paulo ndani ya Hekalu, wakachochea umati wote wa watu, nao wakamkamata. 2821:28 Mt 24; 15; Mdo 6:13Wakapiga kelele wakisema, “Waisraeli wenzetu, tusaidieni! Huyu ndiye yule mtu anayefundisha kila mtu na kila mahali, kinyume na watu wetu, sheria zetu na hata Hekalu hili. Zaidi ya hayo amewaleta Wayunani ndani ya Hekalu na kupanajisi mahali hapa patakatifu.” 2921:29 Mdo 20:4; 18:19(Walikuwa wamemwona Trofimo, mwenyeji wa Efeso, akiwa mjini pamoja na Paulo wakadhani kuwa Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.)

3021:30 Mdo 26:26; 16:19Mji wote ukataharuki, watu wakaja wakikimbia kutoka pande zote wakamkamata Paulo, wakamburuta kutoka Hekaluni. Milango ya Hekalu ikafungwa. 31Walipokuwa wakitaka kumuua, habari zikamfikia jemadari wa jeshi la askari wa Kirumi kwamba mji wa Yerusalemu wote ulikuwa katika machafuko. 3221:32 Mdo 23:27Mara yule jemadari akachukua maafisa wengine wa jeshi pamoja na askari wakakimbilia kwenye ile ghasia, wale watu waliokuwa wakifanya ghasia walipomwona yule jemadari na askari wakija, wakaacha kumpiga Paulo.

3321:33 Mdo 12:6; Efe 6:20; 2Tim 2:9Yule jemadari akaja, akamkamata Paulo akaamuru afungwe kwa minyororo miwili. Akauliza yeye ni nani, na alikuwa amefanya nini. 3421:34 Mdo 19:32; 22:24Baadhi ya watu katika ule umati wakapiga kelele, hawa wakisema hili na wengine lile. Yule jemadari alipoona kuwa hawezi kupata hakika ya habari kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo apelekwe katika ngome ya jeshi. 3521:35 Mdo 21:40Paulo alipofika penye ngazi, ilibidi askari wambebe juu juu kwa sababu fujo za ule umati wa watu zilikuwa kubwa. 3621:36 Lk 23:18; Yn 19:15Umati wa watu ulikuwa ukifuata ukiendelea kupiga kelele ukisema, “Mwondoe huyu!”

Paulo Anajitetea

3721:37 Mdo 21:34Mara tu Paulo alipokaribia kuingizwa kwenye ngome ya jeshi, akamwambia yule jemadari, “Je, naweza kukuambia jambo moja?”

Yule jemadari akamjibu, “Je, unajua Kiyunani? 3821:38 Mt 24:26; Mdo 5:36Je, wewe si yule Mmisri ambaye siku hizi za karibuni alianzisha uasi akaongoza kundi la magaidi 4,000 wenye silaha jangwani?”

3921:39 Mdo 9:11; 23:3Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso, huko Kilikia, raiya wa mji maarufu. Tafadhali niruhusu nizungumze na hawa watu.”

4021:40 Mdo 12:17; Yn 5:2Akiisha kupata ruhusa ya yule jemadari, Paulo akasimama penye ngazi akawapungia watu mkono ili wanyamaze. Wote waliponyamaza kimya, Paulo akazungumza nao kwa lugha ya Kiebrania, akasema:

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

使徒行传 21:1-40

保罗前往耶路撒冷

1我们和众人道别之后,乘船直接驶往哥士,第二天到达罗底,从那里前往帕大喇2帕大喇遇到一艘开往腓尼基的船,就上了船。 3塞浦路斯遥遥在望,船从该岛的南面绕过,一直驶向叙利亚。因为船要在泰尔卸货,我们就在那里上了岸, 4找到当地的门徒后,便和他们同住了七天。他们受圣灵的感动力劝保罗不要去耶路撒冷5时间到了,我们继续前行,众门徒和他们的妻子儿女送我们出城。大家跪在岸边祷告之后,彼此道别。 6我们上了船,众人也回家去了。

7我们从泰尔乘船抵达多利买,上岸探访那里的弟兄姊妹,和他们住了一天。 8第二天我们离开那里,来到凯撒利亚,住在传道人腓利家里。他是当初选出的七位执事之一。 9腓利有四个未出嫁的女儿,都能说预言。 10过了几天,一个名叫亚迦布的先知从犹太下来。 11他到了我们这里,拿保罗的腰带绑住自己的手脚,说:“圣灵说,‘耶路撒冷犹太人也要这样捆绑这腰带的主人,把他交给外族人。’”

12听到这话,我们和当地的信徒都苦劝保罗不要去耶路撒冷13保罗说:“你们为什么这样哭泣,令我心碎呢?我为主耶稣的名甘愿受捆绑,甚至死在耶路撒冷。”

14我们知道再劝也无济于事,只好对他说:“愿主的旨意成就。”

15过了几天,我们收拾行装启程上耶路撒冷16有几个凯撒利亚的门徒和我们一起去,并带我们到一个信主已久的塞浦路斯拿孙家里住宿。

保罗会见雅各和众长老

17我们抵达耶路撒冷后,受到弟兄姊妹的热烈欢迎。 18第二天,保罗和我们去见雅各,众长老都在那里。 19保罗向大家问安之后,便一一述说上帝如何借着他传福音给外族人。 20大家听了,都同声赞美上帝,又对保罗说:“弟兄,你知道数以万计的犹太人信了主,他们都严守律法。 21他们听见有人说你教导住在外族人中的犹太人背弃摩西的律法,不替孩子行割礼,也不遵守犹太人的规矩。 22他们一定会听到你来这里的消息,这该怎么办? 23请你听我们的建议,这里有四位向上帝许过愿的弟兄, 24你和他们一起去行洁净礼,并由你替他们付费,让他们可以剃头,好叫众人知道你严守律法,循规蹈矩,关于你的传闻都是假的。 25至于那些外族信徒,我们已经写信吩咐他们,不可吃祭过偶像的食物,不可吃血和勒死的牲畜,不可淫乱。”

保罗被捕

26于是,保罗和四位弟兄第二天行了洁净礼,然后上圣殿报告他们洁净期满的日子,好在期满后让祭司为他们每个人献祭物。 27当七日的洁净期将满的时候,有些从亚细亚来的犹太人发现保罗在圣殿里,就煽动众人去抓他。 28他们高喊:“以色列人快来帮忙!就是这人到处教唆人反对我们的民族、律法和圣殿。他还带希腊人进圣殿,玷污这圣地。” 29这是因为他们在城里见过一个名叫特罗非摩以弗所人和保罗在一起,以为保罗一定把他带进圣殿了。

30消息一传开,全城轰动。众人冲进圣殿把保罗拉出来,随即关上殿门。 31正当他们要杀保罗的时候,有人把耶路撒冷发生骚乱的消息报告给罗马军营的千夫长, 32千夫长马上带着军兵和几个百夫长赶来了。众人一见千夫长和军队,便停止殴打保罗33千夫长上前拿住保罗,命人用两条铁链把他锁起来,问他是什么人、做了什么事。 34人群中有人这样喊,有人那样喊,情形混乱不堪,千夫长无法辨明真相,便命人将保罗带回军营。 35保罗刚走上台阶,众人便凶猛地拥挤过来,士兵们只好把他举起来抬着走。 36众人挤在后面喊着说:“杀掉他!”

保罗的申辩

37士兵们抬着保罗来到军营门口,保罗问千夫长:“我可以和你讲几句话吗?”千夫长说:“你也懂希腊话吗? 38不久前煽动叛乱、带着四千暴徒逃到旷野去的那个埃及人是你吗?” 39保罗说:“我是犹太人,来自基利迦大数,并非无名小城的人。请准许我向百姓讲几句话。” 40千夫长答应了,保罗就站在台阶上向众人挥手示意,他们都安静下来,保罗希伯来话对他们说: