Matendo 20 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 20:1-38

Paulo Apita Makedonia Na Uyunani

120:1 Mdo 11:26; 16:9Baada ya zile ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi pamoja akawatia moyo, akawaaga, akaanza safari kwenda Makedonia. 2Alipita katika sehemu zile, akinena na watu maneno mengi ya kuwatia moyo. Ndipo hatimaye akawasili Uyunani, 320:3 2Kor 11:26; 1The 2:15-16; Mdo 16:9ambako alikaa kwa muda wa miezi mitatu. Alipokuwa anakaribia kuanza safari kwa njia ya bahari kwenda Shamu, kwa sababu Wayahudi walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yake, aliamua kurudi kupitia njia ya Makedonia. 420:4 Mdo 19:29; 17:19-29; 16:1; Efe 6:21; 2Tim 4:12; Mdo 21:29; 2Tim 4:20Paulo alikuwa amefuatana na Sopatro mwana wa Piro, Mberoya, Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonike na Gayo, mtu wa Derbe, Timotheo pamoja na Tikiko na Trofimo kutoka sehemu ya Asia. 520:5 Mdo 16:10; 16:8Hawa watu walitutangulia wakaenda kutungojea Troa. 620:6 Mdo 16:2; 18:8Lakini sisi tukasafiri kwa njia ya bahari kwa siku tano kutoka Filipi baada ya siku za Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, nasi tukaungana na wengine huko Troa, ambako tulikaa kwa siku saba.

Eutiko Afufuliwa Huko Troa

720:7 1Kor 16:2; Ufu 1:10Siku ya kwanza ya juma tulikutana pamoja kwa ajili ya kumega mkate. Paulo akaongea na watu, naye kwa kuwa alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliendelea kuongea mpaka usiku wa manane. 820:8 Mdo 1:13Kwenye chumba cha ghorofani walimokuwa wamekutania kulikuwa na taa nyingi. 9Kijana mmoja jina lake Eutiko, alikuwa amekaa dirishani, wakati Paulo alipokuwa akihubiri kwa muda mrefu, alipatwa na usingizi mzito, akaanguka kutoka ghorofa ya tatu, wakamwinua akiwa amekufa. 1020:10 1Fal 17:21; 2Fal 4:34; Mt 9:23; 24Paulo akashuka chini, akajitupa juu yake na kumkumbatia, akasema, “Msishtuke, uzima wake bado umo ndani yake.” 1120:11 Mdo 20:7; Mt 14:19Kisha Paulo akapanda tena ghorofani, akamega mkate na kula. Baada ya kuongea mpaka mapambazuko, akaondoka. 12Watu wakamrudisha yule kijana nyumbani akiwa hai nao wakafarijika sana.

Paulo Awaaga Wazee Wa Efeso

13Tukatangulia melini tukasafiri mpaka Aso ambako tungempakia Paulo. Alikuwa amepanga hivyo kwa maana alitaka kufika kwa miguu. 14Alipotukuta huko Aso, tulimpakia melini, tukasafiri wote mpaka Mitilene. 1520:15 2Tim 4:20Kutoka huko tuliendelea kwa njia ya bahari, na kesho yake tukafika mahali panapokabili Kio. Siku iliyofuata tukavuka kwenda Samo, na kesho yake tukawasili Mileto. 1620:16 Mdo 18:19; 19:21; 2:1; 1Kor 16:8Paulo alikuwa ameamua tusipitie Efeso ili asitumie muda mwingi huko sehemu za Asia, kwa sababu alikuwa anatamani kama ikiwezekana kufika Yerusalemu kabla ya siku ya Pentekoste.

1720:17 Mdo 11:30Paulo akiwa Mileto, alituma mjumbe kwenda Efeso kuwaita wazee wa kanisa waje wakutane naye. 1820:18 Mdo 18:19, 21; 19:1-4Walipofika akawaambia, “Ninyi wenyewe mnajua jinsi nilivyoishi katikati yenu muda wote tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia. 19Nilimtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi nikivumilia taabu na mapingamizi yaliyonipata kutokana na hila za Wayahudi. 2020:20 Za 40:10Mnajua kwamba sikusita kuhubiri jambo lolote ambalo lingekuwa la kuwafaa ninyi, lakini nilifundisha hadharani na nyumba kwa nyumba. 2120:21 Mdo 18:5; 2:38; Efe 1:15; Kol 2:5Nimewashuhudia Wayahudi na Wayunani kwamba inawapasa kumgeukia Mungu kwa kutubu dhambi na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.

2220:22 Mdo 19:21“Nami sasa nimesukumwa na Roho, ninakwenda Yerusalemu wala sijui ni nini kitakachonipata huko. 2320:23 Mdo 21:4; 9:16Ila ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu amenionya kuwa vifungo na mateso vinaningoja. 2420:24 Mdo 21:13; 2Kor 4:1; Gal 1:1; Tit 1:3Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani kwangu, kama kuyamaliza mashindano na kukamilisha ile kazi Bwana Yesu aliyonipa, yaani, kazi ya kuishuhudia Injili ya neema ya Mungu.

2520:25 Mt 4:23; Mdo 20:38; Rum 15:23“Nami sasa najua ya kuwa hakuna hata mmoja miongoni mwenu ambaye nimemhubiria Ufalme wa Mungu katika kwenda kwangu huku na huko, atakayeniona uso tena. 2620:26 Mdo 18:6Kwa hiyo nawatangazia leo, sina hatia ya damu ya mtu awaye yote. 27Kwa kuwa sikusita kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu. 2820:28 1Pet 5:2Jilindeni nafsi zenu na mlilinde lile kundi lote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi wake. Lichungeni kanisa lake Mungu alilolinunua kwa damu yake mwenyewe. 2920:29 Mt 7:15Najua kwamba baada yangu kuondoka, mbwa mwitu wakali watakuja katikati yenu ambao hawatalihurumia kundi. 3020:30 Mdo 11:26Hata kutoka miongoni mwenu watainuka watu na kuupotosha ukweli ili wawavute wanafunzi wawafuate. 3120:31 Mdo 19:10Hivyo jilindeni! Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuacha kamwe kuwaonya kila mmoja kwa machozi usiku na mchana.

3220:32 Mdo 14:23; Mt 25:34; Ebr 9:15; Mdo 26:18“Sasa nawakabidhi kwa Mungu na kwa neno la neema yake, linaloweza kuwajenga na kuwapa ninyi urithi miongoni mwa wote ambao wametakaswa. 3320:33 1Sam 12:3; 1The 2:5Sikutamani fedha wala dhahabu wala vazi la mtu yeyote. 3420:34 Mdo 18:3Ninyi wenyewe mnajua kwamba mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami. 3520:35 Rum 15:1; 1Kor 9:12; 2Kor 11:9, 12; 12:13; Efe 4:28; 1The 4:11; 2The 3:8Katika kila jambo nimewaonyesha kwamba kwa njia hii ya kufanya kazi kwa bidii imetupasa kuwasaidia wadhaifu, mkikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe jinsi alivyosema, ‘Ni heri kutoa kuliko kupokea.’ ”

3620:36 Lk 22:41; Mdo 9:40Paulo alipomaliza kusema haya akapiga magoti pamoja nao wote akaomba. 3720:37 Lk 15:20Wote wakalia, wakamkumbatia Paulo na kumbusu, 38Kilichowahuzunisha zaidi ni kwa sababu ya yale maneno aliyosema kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Wakaenda naye mpaka kwenye meli.

King James Version

Acts 20:1-38

1And after the uproar was ceased, Paul called unto him the disciples, and embraced them, and departed for to go into Macedonia. 2And when he had gone over those parts, and had given them much exhortation, he came into Greece, 3And there abode three months. And when the Jews laid wait for him, as he was about to sail into Syria, he purposed to return through Macedonia. 4And there accompanied him into Asia Sopater of Berea; and of the Thessalonians, Aristarchus and Secundus; and Gaius of Derbe, and Timotheus; and of Asia, Tychicus and Trophimus. 5These going before tarried for us at Troas. 6And we sailed away from Philippi after the days of unleavened bread, and came unto them to Troas in five days; where we abode seven days. 7And upon the first day of the week, when the disciples came together to break bread, Paul preached unto them, ready to depart on the morrow; and continued his speech until midnight. 8And there were many lights in the upper chamber, where they were gathered together. 9And there sat in a window a certain young man named Eutychus, being fallen into a deep sleep: and as Paul was long preaching, he sunk down with sleep, and fell down from the third loft, and was taken up dead. 10And Paul went down, and fell on him, and embracing him said, Trouble not yourselves; for his life is in him. 11When he therefore was come up again, and had broken bread, and eaten, and talked a long while, even till break of day, so he departed. 12And they brought the young man alive, and were not a little comforted.

13¶ And we went before to ship, and sailed unto Assos, there intending to take in Paul: for so had he appointed, minding himself to go afoot. 14And when he met with us at Assos, we took him in, and came to Mitylene. 15And we sailed thence, and came the next day over against Chios; and the next day we arrived at Samos, and tarried at Trogyllium; and the next day we came to Miletus. 16For Paul had determined to sail by Ephesus, because he would not spend the time in Asia: for he hasted, if it were possible for him, to be at Jerusalem the day of Pentecost.

17¶ And from Miletus he sent to Ephesus, and called the elders of the church. 18And when they were come to him, he said unto them, Ye know, from the first day that I came into Asia, after what manner I have been with you at all seasons, 19Serving the Lord with all humility of mind, and with many tears, and temptations, which befell me by the lying in wait of the Jews: 20And how I kept back nothing that was profitable unto you, but have shewed you, and have taught you publickly, and from house to house, 21Testifying both to the Jews, and also to the Greeks, repentance toward God, and faith toward our Lord Jesus Christ. 22And now, behold, I go bound in the spirit unto Jerusalem, not knowing the things that shall befall me there: 23Save that the Holy Ghost witnesseth in every city, saying that bonds and afflictions abide me. 24But none of these things move me, neither count I my life dear unto myself, so that I might finish my course with joy, and the ministry, which I have received of the Lord Jesus, to testify the gospel of the grace of God. 25And now, behold, I know that ye all, among whom I have gone preaching the kingdom of God, shall see my face no more. 26Wherefore I take you to record this day, that I am pure from the blood of all men. 27For I have not shunned to declare unto you all the counsel of God.

28¶ Take heed therefore unto yourselves, and to all the flock, over the which the Holy Ghost hath made you overseers, to feed the church of God, which he hath purchased with his own blood. 29For I know this, that after my departing shall grievous wolves enter in among you, not sparing the flock. 30Also of your own selves shall men arise, speaking perverse things, to draw away disciples after them. 31Therefore watch, and remember, that by the space of three years I ceased not to warn every one night and day with tears. 32And now, brethren, I commend you to God, and to the word of his grace, which is able to build you up, and to give you an inheritance among all them which are sanctified. 33I have coveted no man’s silver, or gold, or apparel. 34Yea, ye yourselves know, that these hands have ministered unto my necessities, and to them that were with me. 35I have shewed you all things, how that so labouring ye ought to support the weak, and to remember the words of the Lord Jesus, how he said, It is more blessed to give than to receive.

36¶ And when he had thus spoken, he kneeled down, and prayed with them all. 37And they all wept sore, and fell on Paul’s neck, and kissed him, 38Sorrowing most of all for the words which he spake, that they should see his face no more. And they accompanied him unto the ship.