Marko 7 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 7:1-37

Kilicho Safi Na Kilicho Najisi

(Mathayo 15:1-20)

17:1 Mt 15:1Mafarisayo na baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu wakakusanyika mbele ya Yesu. 27:2 Mdo 11:8; Rum 14:14Wakawaona baadhi ya wanafunzi wake wakila chakula kwa mikono iliyo najisi, yaani, bila kunawa kama ilivyotakiwa na sheria ya dini ya Wayahudi. 37:3 Mk 7:5-13; Lk 11:38-39(Kwa kuwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali chakula pasipo kunawa kwa kufuata desturi za wazee wao. 47:4 Mt 23:25Wanapotoka sokoni hawawezi kula pasipo kunawa. Pia kuna desturi nyingine nyingi wanazofuata kama vile jinsi ya kuosha vikombe, vyungu na vyombo vya shaba.)

57:5 Gal 1:14; Kol 2:8Kwa hiyo wale Mafarisayo na walimu wa sheria wakamuuliza Yesu, “Mbona wanafunzi wako hawafuati desturi za wazee, na badala yake wanakula kwa mikono najisi?”

67:6 Isa 29:13; Mt 15:8Yesu akawajibu, “Nabii Isaya alisema ukweli alipotabiri juu yenu, ninyi wanafiki. Kama ilivyoandikwa:

“ ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao,

lakini mioyo yao iko mbali nami.

77:7 Isa 29:13Huniabudu bure,

nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’

87:8 Mk 7:3Ninyi mmeziacha amri za Mungu na kushika desturi za watu.”

97:9 Mk 7:3Naye akawaambia, “Ninyi mnayo njia nzuri ya kukataa amri za Mungu ili mpate kuyashika mapokeo yenu! 107:10 Kut 20:21; Kum 5:16; Kut 21:17; Law 20:9Kwa mfano, Mose alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’ 117:11 Mt 23:16-18Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia ni Korbani’ (yaani kimewekwa wakfu kwa Mungu), 12basi hawajibiki tena kumsaidia baba yake au mama yake. 137:13 Ebr 4:12; Mk 7:3Kwa njia hiyo ninyi mnabatilisha neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyojiwekea. Nanyi mnafanya mambo mengi ya aina hiyo.”

147:14 Mt 15:10Yesu akaita tena ule umati wa watu, akawaambia, “Nisikilizeni, kila mmoja wenu na mwelewe jambo hili. 157:15 Mdo 10:14, 15Hakuna kitu kinachomwingia mtu kimtiacho unajisi, lakini kile kimtokacho ndicho kimtiacho unajisi. [ 167:16 Mt 11:15Kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia na asikie.]”

177:17 Mk 9:28Akiisha kuuacha ule umati wa watu na kuingia ndani, wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano ule. 18Akawajibu, “Je, hata nanyi hamwelewi? Je, hamfahamu kwamba kitu kimwingiacho mtu hakimtii unajisi? 197:19 Kol 2:16; 1Tim 4:3-5; Mdo 10:15Mtu akila kitu hakiingii moyoni mwake bali tumboni, na baadaye hutolewa nje ya mwili wake.” (Kwa kusema hivi, Yesu alivihalalisha vyakula vyote kuwa ni “safi.”)

20Akaendelea kusema, “Kile kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. 217:21 Mwa 6:5; 8:21; Mt 15:21-28Kwa maana kutoka ndani ya moyo wa mtu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji, uzinzi, 227:22 Mt 20:15tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, matukano, kiburi na upumbavu. 23Maovu haya yote hutoka ndani ya mtu, nayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi.”

Imani Ya Mwanamke Msirofoinike

(Mathayo 15:21-28)

247:24 Mt 21:21Ndipo Yesu akaondoka hapo akaenda sehemu za Tiro. Akaingia katika nyumba moja, naye hakutaka mtu yeyote ajue kwamba yuko humo. Lakini hakuweza kujificha. 257:25 Mt 4:24Mara mwanamke mmoja, ambaye binti yake mdogo alikuwa na pepo mchafu, akaja na kumpigia magoti miguuni pake. 26Basi huyo mwanamke alikuwa Myunani, aliyezaliwa Foinike ya Siria.7:26 Kulikuwa na Foinike ya Siria (ndio Shamu) na Foinike ya Libya. Akamsihi Yesu amtoe binti yake huyo pepo mchafu.

27Yesu akamwambia, “Waache watoto washibe kwanza, kwa maana si vyema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”

28Lakini yule mwanamke akamjibu, “Bwana, hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya chakula cha watoto.”

29Ndipo Yesu akamjibu, “Kwa sababu ya jibu lako, nenda zako nyumbani; yule pepo mchafu amemtoka binti yako.”

30Akaenda zake nyumbani akamkuta binti yake amelala kitandani, yule pepo mchafu akiwa amemtoka.

Yesu Amponya Mtu Aliyekuwa Kiziwi Na Bubu

317:31 Mt 11:21; 4:18-25; Mk 5:20Kisha Yesu akaondoka sehemu za Tiro, akapita katikati ya Sidoni, hadi Bahari ya Galilaya na kuingia eneo la Dekapoli. 327:32 Mt 9:32; Lk 11:14; Mk 5:23Huko, watu wakamletea Yesu mtu mmoja kiziwi, ambaye pia alikuwa na kigugumizi, wakamwomba aweke mkono wake juu ya huyo mtu na amponye.

337:33 Mk 8:23Baadaye Yesu akampeleka yule kiziwi kando mbali na watu, Yesu akatia vidole vyake masikioni mwa yule mtu. Kisha akatema mate na kuugusa ulimi wa yule mtu. 347:34 Mk 6:41; Yn 11:41; Mk 8:12Ndipo Yesu akatazama mbinguni, akavuta hewa ndani kwa nguvu akamwambia, “Efatha!” (yaani, “Funguka!”) 357:35 Isa 35:5-6Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukaachiliwa, akaanza kuongea sawasawa.

367:36 Mt 8:4Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote habari hizi. Lakini kadiri alivyowazuia, ndivyo walivyozidi kutangaza kwa bidii. 377:37 Isa 35:5Walistaajabu mno. Wakasema, “Amefanya mambo yote vizuri mno! Amewawezesha viziwi wasikie na bubu waseme!”

King James Version

Mark 7:1-37

1Then came together unto him the Pharisees, and certain of the scribes, which came from Jerusalem. 2And when they saw some of his disciples eat bread with defiled, that is to say, with unwashen, hands, they found fault. 3For the Pharisees, and all the Jews, except they wash their hands oft, eat not, holding the tradition of the elders. 4And when they come from the market, except they wash, they eat not. And many other things there be, which they have received to hold, as the washing of cups, and pots, brasen vessels, and of tables. 5Then the Pharisees and scribes asked him, Why walk not thy disciples according to the tradition of the elders, but eat bread with unwashen hands? 6He answered and said unto them, Well hath Esaias prophesied of you hypocrites, as it is written, This people honoureth me with their lips, but their heart is far from me. 7Howbeit in vain do they worship me, teaching for doctrines the commandments of men. 8For laying aside the commandment of God, ye hold the tradition of men, as the washing of pots and cups: and many other such like things ye do. 9And he said unto them, Full well ye reject the commandment of God, that ye may keep your own tradition. 10For Moses said, Honour thy father and thy mother; and, Whoso curseth father or mother, let him die the death: 11But ye say, If a man shall say to his father or mother, It is Corban, that is to say, a gift, by whatsoever thou mightest be profited by me; he shall be free. 12And ye suffer him no more to do ought for his father or his mother; 13Making the word of God of none effect through your tradition, which ye have delivered: and many such like things do ye.

14¶ And when he had called all the people unto him, he said unto them, Hearken unto me every one of you, and understand: 15There is nothing from without a man, that entering into him can defile him: but the things which come out of him, those are they that defile the man. 16If any man have ears to hear, let him hear. 17And when he was entered into the house from the people, his disciples asked him concerning the parable. 18And he saith unto them, Are ye so without understanding also? Do ye not perceive, that whatsoever thing from without entereth into the man, it cannot defile him; 19Because it entereth not into his heart, but into the belly, and goeth out into the draught, purging all meats? 20And he said, That which cometh out of the man, that defileth the man. 21For from within, out of the heart of men, proceed evil thoughts, adulteries, fornications, murders, 22Thefts, covetousness, wickedness, deceit, lasciviousness, an evil eye, blasphemy, pride, foolishness: 23All these evil things come from within, and defile the man.

24¶ And from thence he arose, and went into the borders of Tyre and Sidon, and entered into an house, and would have no man know it: but he could not be hid. 25For a certain woman, whose young daughter had an unclean spirit, heard of him, and came and fell at his feet: 26The woman was a Greek, a Syrophenician by nation; and she besought him that he would cast forth the devil out of her daughter. 27But Jesus said unto her, Let the children first be filled: for it is not meet to take the children’s bread, and to cast it unto the dogs. 28And she answered and said unto him, Yes, Lord: yet the dogs under the table eat of the children’s crumbs. 29And he said unto her, For this saying go thy way; the devil is gone out of thy daughter. 30And when she was come to her house, she found the devil gone out, and her daughter laid upon the bed.

31¶ And again, departing from the coasts of Tyre and Sidon, he came unto the sea of Galilee, through the midst of the coasts of Decapolis. 32And they bring unto him one that was deaf, and had an impediment in his speech; and they beseech him to put his hand upon him. 33And he took him aside from the multitude, and put his fingers into his ears, and he spit, and touched his tongue; 34And looking up to heaven, he sighed, and saith unto him, Ephphatha, that is, Be opened. 35And straightway his ears were opened, and the string of his tongue was loosed, and he spake plain. 36And he charged them that they should tell no man: but the more he charged them, so much the more a great deal they published it; 37And were beyond measure astonished, saying, He hath done all things well: he maketh both the deaf to hear, and the dumb to speak.