Marko 16 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 16:1-20

Kufufuka Kwa Yesu

(Mathayo 28:1-8; Luka 24:1-12; Yohana 20:1-10)

116:1 Lk 24:9; Yn 19:39-40Sabato ilipomalizika, Maria Magdalene, Maria mama yake Yakobo, na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu. 216:2 Lk 24:1; Yn 20:1Asubuhi na mapema, siku ya kwanza ya juma, mara tu baada ya kuchomoza jua, walikwenda kaburini. 316:3 Mk 15:46Njiani wakawa wanaulizana wao kwa wao, “Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe kutoka kwenye ingilio la kaburi?”

4Lakini walipotazama, wakaona lile jiwe, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha kuvingirishwa kutoka pale penye ingilio la kaburi. 516:5 Lk 24:3-4Walipokuwa wakiingia mle kaburini, wakamwona kijana mmoja aliyevaa joho jeupe akiwa ameketi upande wa kuume, nao wakastaajabu.

616:6 Mk 1:24Yule malaika akawaambia, “Msistaajabu. Mnamtafuta Yesu, Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa. Tazameni mahali walipomlaza. 716:7 Yn 21:1-23; Mk 14:28Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake pamoja na Petro, kwamba, ‘Anawatangulia kwenda Galilaya. Huko ndiko mtamwona, kama alivyowaambia.’ ”

816:8 Mt 28:8; Lk 24:9Hivyo wakatoka, wakakimbia kutoka mle kaburini wakiwa na hofu kuu na mshangao. Nao hawakumwambia mtu yeyote neno lolote, kwa sababu waliogopa.

Yesu Anamtokea Maria Magdalene

(Mathayo 28:9-10; Yohana 20:11-18)

916:9 Mk 15:4-7Yesu alipofufuka alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma alimtokea kwanza Maria Magdalene, yule ambaye alikuwa amemtoa pepo wachafu saba. 1016:10 Lk 24:10; Yn 20:18Maria akaenda, naye akawaambia wale waliokuwa wamefuatana na Yesu, waliokuwa wanaomboleza na kulia. 1116:11 Mk 16:13, 14; Lk 24:11Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Maria alikuwa amemwona, hawakusadiki.

Yesu Awatokea Wanafunzi Wawili

(Luka 24:13-35)

1216:12 Lk 24:13-32Baadaye Yesu akawatokea wawili miongoni mwa wanafunzi wake walipokuwa wakienda shambani akiwa katika sura nyingine. 13Nao wakarudi na kuwaambia wenzao. Lakini hawakuwasadiki wao pia.

Yesu Awaagiza Wale Wanafunzi Kumi Na Mmoja

(Mathayo 28:16-20; Luka 24:36-49; Yohana 20:19-23; Matendo 1:6-8)

1416:14 Lk 24:36-43Baadaye Yesu akawatokea wale wanafunzi kumi na mmoja walipokuwa wakila chakula. Akawakemea kwa kutoamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao kwa kutosadiki wale waliomwona baada yake kufufuka.

1516:15 Mt 28:18-20; Mdo 1:8Akawaambia, “Enendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. 1616:16 Mdo 16:31; Yn 12:48Yeyote aaminiye na kubatizwa ataokoka. Lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa. 1716:17 Lk 10:17; 1Kor 13:1; 14:2-39Nazo ishara hizi zitafuatana na wanaoamini: Kwa Jina langu watatoa pepo wachafu; watasema kwa lugha mpya; 1816:18 Lk 10:19; Mdo 28:3-5; 6:6watashika nyoka kwa mikono yao; na hata wakinywa kitu chochote cha kuua, hakitawadhuru kamwe; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”

[Yesu Apaa Kwenda Mbinguni

(Luka 24:50-53; Matendo 1:9-11)

1916:19 Lk 24:50-51; Yn 6:6; Mdo 1:19; 1Tim 3:16; Za 110:1; Mt 26:64; Mdo 2:33; 5:31; Rum 8:34; Kol 3:1; Ebr 1:3; 12:2Baada ya Bwana Yesu kusema nao, alichukuliwa juu mbinguni na kuketi mkono wa kuume wa Mungu. 2016:20 Yn 4:48Kisha wanafunzi wake wakatoka, wakahubiri kila mahali, naye Bwana akatenda kazi pamoja nao na kulithibitisha neno lake kwa ishara zilizofuatana nalo.]

O Livro

Marcos 16:1-20

A ressurreição

(Mt 28.1-8; Lc 24.1-12; Jo 20.1-18)

1Quando terminou o sábado, Maria Madalena, Salomé e Maria, mãe de Tiago, foram comprar perfumes para pôr no corpo de Jesus. 2No domingo de manhã, ao nascer do sol, elas foram ao túmulo. 3Pelo caminho, interrogavam-se como poderiam afastar a enorme pedra da entrada. 4Mas quando chegaram, viram que a pedra, muito pesada, já tinha sido removida e que a entrada estava aberta. 5Entraram no túmulo e viram, sentado do lado direito, um jovem vestido de branco e assustaram-se. 6Então ele disse-lhes: “Não fiquem atemorizadas. É Jesus, o nazareno que foi crucificado, que procuram? Não está aqui, ressuscitou! 7Vejam, era aqui que o seu corpo se encontrava. Vão e deem este recado aos seus discípulos, incluindo Pedro: ‘Jesus vai adiante de vocês para a Galileia e ali o verão, tal como vos disse antes de morrer.’ ” 8Trémulas e confusas, demasiado amedrontadas para falar, as mulheres saíram do túmulo em fuga. E não disseram nada uma à outra, porque estavam assustadas.

9Na madrugada de domingo Jesus ressuscitou e a primeira pessoa que o viu foi Maria Madalena, de quem tinha expulsado sete demónios. 10Ela veio ter com os discípulos que estavam tristes e chorosos. 11E anunciou-lhes que tinha visto Jesus que se encontrava vivo. Mas eles não acreditaram.

12Naquele dia, mais tarde, Jesus apareceu de outra forma a dois deles que iam de Jerusalém para os campos. 13Estes voltaram correndo para Jerusalém, para dar a notícia aos outros, mas ninguém acreditou neles. 14Mais tarde, Jesus apareceu aos onze discípulos, quando estavam a comer juntos, e censurou-os pela sua incredulidade, pela sua dureza de coração em acreditar nos testemunhos daqueles que o tinham visto depois de ter ressuscitado dentre os mortos.

15Então disse-lhes: “Vão por todo o mundo e preguem a boa nova a todos e em toda a parte. 16Quem crer e for batizado será salvo, mas quem não quiser crer será condenado. 17E darei a quem crer os seguintes sinais: em meu nome expulsará demónios e falará novas línguas. 18Poderá até pegar em serpentes e se beber alguma coisa venenosa não lhe fará mal. Poderá colocar as mãos sobre os doentes e curá-los.”

19Quando acabou de falar-lhes, Jesus foi levado para o céu e sentou-se à direita de Deus. 20Os discípulos foram pregando por toda a parte e o Senhor estava com eles, comprovando o que diziam com os sinais que acompanhavam a sua mensagem.