Marko 1 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 1:1-45

Mahubiri Ya Yohana Mbatizaji

(Mathayo 3:1-12; Luka 3:1-8; Yohana 1:19-28)

11:1 Mt 4:3Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

21:2 Mal 3:1; Lk 7:27Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:

“Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako,

atakayetengeneza njia mbele yako”:

31:3 Isa 40:3; Yn 1:23“sauti ya mtu aliaye nyikani.

‘Itengenezeni njia ya Bwana,

yanyoosheni mapito yake.’ ”

41:4 Yn 1:26, 33; Mt 3:1; Mdo 11:16; Lk 1:7Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi. 51:5 Mt 3:5Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani. 61:6 Law 11:22; Mt 3:4Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu. 71:7 Mdo 13:25; Yn 1:27; Mdo 13:25Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake. 81:8 Yoe 2:28; Yn 1:33Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”

Ubatizo Wa Yesu

(Mathayo 3:13-17; Luka 3:21-22)

91:9 Mt 2:23; Lk 3:21Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani. 101:10 Yn 1:32Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua. 111:11 Mt 3:17; Mk 9:7; Za 2:7; Isa 42:1Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”

Majaribu Ya Yesu

(Mathayo 4:1-11; Luka 4:1-13)

121:12 Mt 4:1; Lk 4:1Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani, 131:13 Mt 4:10; Ebr 4:15naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.

Yesu Aanza Kuhubiri

141:14 Mt 4:12; 4:23; 4:12; 4:23; Lk 4:14, 15Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu, 151:15 Rum 5:6; Gal 4:4; Mdo 20:21akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”

Yesu Awaita Wanafunzi Wanne

(Mathayo 4:12-22; Luka 4:14-15; 5:1-11)

161:16 Mt 4:18; Lk 5:4Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi. 171:17 Mt 13:47Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.” 181:18 Mt 19:27; Lk 5:11; Mt 4:19Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.

191:19 Mt 4:21Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao. 20Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.

Yesu Amtoa Pepo Mchafu

(Luka 4:31-37)

211:21 Mk 1:39; Mt 4:23Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha. 221:22 Mt 7:28-29Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria. 231:23 Lk 4:33Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, 241:24 Mt 8:29; Yn 1:45-46; Mdo 4:10; Za 16:10; 1Yn 2:20naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”

251:25 Mk 1:34Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” 261:26 Mk 9:20Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.

271:27 Mk 10:24, 32Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!” 281:28 Mk 9:26Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.

Yesu Amponya Mama Mkwe Wa Simoni

(Mathayo 8:14-15; Luka 4:38-39)

291:29 Mt 8:14; Lk 4:38Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea. 30Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake. 311:31 Lk 7:14Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.

Yesu Aponya Wengi

(Mathayo 8:16-17; Luka 4:40-41)

321:32 Mt 4:24Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu. 33Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo. 341:34 Mt 4:23; Mk 3:12; Mdo 16:17-18Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.

Yesu Aenda Galilaya

(Luka 4:42-44)

351:35 Lk 3:21Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba. 361:36 Lk 4:43-44Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta, 37nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”

381:38 Isa 61:1Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.” 391:39 Mt 4:23-24Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.

Yesu Amtakasa Mwenye Ukoma

(Mathayo 8:1-4; Luka 5:12-16)

401:40 Mk 10:17Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”

41Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!” 42Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika. 431:43 Mk 3:12; 7:36Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake 441:44 Mt 8:4; Law 13:49; 14:1-32akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.” 451:45 Lk 5:15-16, 17; Yn 6:2Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.

King James Version

Mark 1:1-45

1The beginning of the gospel of Jesus Christ, the Son of God; 2As it is written in the prophets, Behold, I send my messenger before thy face, which shall prepare thy way before thee. 3The voice of one crying in the wilderness, Prepare ye the way of the Lord, make his paths straight. 4John did baptize in the wilderness, and preach the baptism of repentance for the remission of sins. 5And there went out unto him all the land of Judæa, and they of Jerusalem, and were all baptized of him in the river of Jordan, confessing their sins. 6And John was clothed with camel’s hair, and with a girdle of a skin about his loins; and he did eat locusts and wild honey; 7And preached, saying, There cometh one mightier than I after me, the latchet of whose shoes I am not worthy to stoop down and unloose. 8I indeed have baptized you with water: but he shall baptize you with the Holy Ghost. 9And it came to pass in those days, that Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptized of John in Jordan. 10And straightway coming up out of the water, he saw the heavens opened, and the Spirit like a dove descending upon him: 11And there came a voice from heaven, saying, Thou art my beloved Son, in whom I am well pleased. 12And immediately the Spirit driveth him into the wilderness. 13And he was there in the wilderness forty days, tempted of Satan; and was with the wild beasts; and the angels ministered unto him. 14Now after that John was put in prison, Jesus came into Galilee, preaching the gospel of the kingdom of God, 15And saying, The time is fulfilled, and the kingdom of God is at hand: repent ye, and believe the gospel. 16Now as he walked by the sea of Galilee, he saw Simon and Andrew his brother casting a net into the sea: for they were fishers. 17And Jesus said unto them, Come ye after me, and I will make you to become fishers of men. 18And straightway they forsook their nets, and followed him. 19And when he had gone a little further thence, he saw James the son of Zebedee, and John his brother, who also were in the ship mending their nets. 20And straightway he called them: and they left their father Zebedee in the ship with the hired servants, and went after him. 21And they went into Capernaum; and straightway on the sabbath day he entered into the synagogue, and taught. 22And they were astonished at his doctrine: for he taught them as one that had authority, and not as the scribes. 23And there was in their synagogue a man with an unclean spirit; and he cried out, 24Saying, Let us alone; what have we to do with thee, thou Jesus of Nazareth? art thou come to destroy us? I know thee who thou art, the Holy One of God. 25And Jesus rebuked him, saying, Hold thy peace, and come out of him. 26And when the unclean spirit had torn him, and cried with a loud voice, he came out of him. 27And they were all amazed, insomuch that they questioned among themselves, saying, What thing is this? what new doctrine is this? for with authority commandeth he even the unclean spirits, and they do obey him. 28And immediately his fame spread abroad throughout all the region round about Galilee. 29And forthwith, when they were come out of the synagogue, they entered into the house of Simon and Andrew, with James and John. 30But Simon’s wife’s mother lay sick of a fever, and anon they tell him of her. 31And he came and took her by the hand, and lifted her up; and immediately the fever left her, and she ministered unto them. 32And at even, when the sun did set, they brought unto him all that were diseased, and them that were possessed with devils. 33And all the city was gathered together at the door. 34And he healed many that were sick of divers diseases, and cast out many devils; and suffered not the devils to speak, because they knew him. 35And in the morning, rising up a great while before day, he went out, and departed into a solitary place, and there prayed. 36And Simon and they that were with him followed after him. 37And when they had found him, they said unto him, All men seek for thee. 38And he said unto them, Let us go into the next towns, that I may preach there also: for therefore came I forth. 39And he preached in their synagogues throughout all Galilee, and cast out devils. 40And there came a leper to him, beseeching him, and kneeling down to him, and saying unto him, If thou wilt, thou canst make me clean. 41And Jesus, moved with compassion, put forth his hand, and touched him, and saith unto him, I will; be thou clean. 42And as soon as he had spoken, immediately the leprosy departed from him, and he was cleansed. 43And he straitly charged him, and forthwith sent him away; 44And saith unto him, See thou say nothing to any man: but go thy way, shew thyself to the priest, and offer for thy cleansing those things which Moses commanded, for a testimony unto them. 45But he went out, and began to publish it much, and to blaze abroad the matter, insomuch that Jesus could no more openly enter into the city, but was without in desert places: and they came to him from every quarter.