Malaki 2 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Malaki 2:1-17

Onyo Kwa Makuhani

1“Sasa onyo hili ni kwa ajili yenu, enyi makuhani. 22:2 Kum 28:15Kama hamtasikiliza, na kama hamtaki kuielekeza mioyo yenu kuheshimu Jina langu, nitatuma laana juu yenu, nami nitalaani baraka zenu. Naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamkuielekeza mioyo yenu kuniheshimu mimi,” Asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

3“Kwa sababu yenu nitawakatilia mbali wazao wenu. Nitazipaka nyuso zenu mavi, mavi ya dhabihu zenu. Nanyi mtafukuzwa pamoja nazo mtoke mbele zangu. 4Nanyi mtajua kuwa nimewapelekea onyo hili ili kwamba Agano langu na Lawi lipate kuendelea,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. 52:5 Hes 25:12; Kum 33:8“Agano langu lilikuwa pamoja naye, agano la uhai na amani, nami nilimpa yote, ili aniche na kuniheshimu, naye akaniheshimu na kusimama akilicha Jina langu. 62:6 Dan 12:3; Lk 1:16-17; Yak 5:20Fundisho la kweli lilikuwa kinywani mwake, wala hakuna uongo wowote uliopatikana katika midomo yake. Alitembea nami katika amani na unyofu, naye akawageuza wengi kutoka dhambini.

72:7 Kum 17:9; Isa 42:19; Hag 1:13; Gal 4:14“Kwa maana yapasa midomo ya kuhani kuhifadhi maarifa. Tena kutoka kinywani mwake watu wangepaswa kutafuta mafundisho, kwa sababu yeye ni mjumbe wa Bwana Mwenye Nguvu Zote. 82:8 1Sam 2:17Lakini mmegeuka mkaiacha njia, na kwa mafundisho yenu mmesababisha wengi kujikwaa. Mmevunja agano na Lawi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. 9“Kwa hiyo nimewasababisha ninyi kudharauliwa na kufedheheshwa mbele ya watu wote, kwa sababu hamkufuata njia zangu, bali mmeonyesha upendeleo katika mambo ya sheria.”

Yuda Si Mwaminifu

102:10 Isa 51:2; Mt 3:9; 1Kor 8:6; Ebr 12:9; Za 100:3Je, sote hatuna Baba mmoja? Hatukuumbwa na Mungu mmoja? Kwa nini basi tunalinajisi Agano la baba zetu kwa kukosa uaminifu kila mmoja kwa mwenzake?

112:11 Neh 13:23Yuda amevunja uaminifu. Jambo la kuchukiza limetendeka katika Israeli na katika Yerusalemu: Yuda amepanajisi mahali patakatifu apendapo Bwana, kwa kuoa binti wa mungu mgeni. 12Kwa maana kwa mtu yeyote atendaye jambo hili, Bwana na amkatilie mbali kutoka hema za Yakobo, hata kama huwa anamletea Bwana Mwenye Nguvu Zote sadaka.

132:13 Yer 11:11; 14:12; Za 39:12; 66:18; Isa 58:2Kitu kingine mnachokifanya: Mnaifurikisha madhabahu ya Bwana kwa machozi. Mnalia na kuugua kwa sababu yeye haziangalii tena sadaka zenu wala hazikubali kwa furaha kutoka mikononi mwenu. 142:14 Mwa 21:30; 24:22; Mit 5:18; Ebr 13:4Mnauliza, “Kwa nini?” Ni kwa sababu Bwana ni shahidi kati yako na mke wa ujana wako, kwa sababu umevunja uaminifu naye, ingawa yeye ni mwenzako, mke wa agano lako la ndoa.

152:15 Mwa 2:24; Mt 19:4-6; Kum 14:2; 4:15; 1Kor 7:14; 7:10; Isa 54:6; Ebr 13:4Je, Bwana hakuwafanya wao kuwa mmoja? Katika mwili na katika roho wao ni wa Mungu. Kwa nini wawe mmoja? Kwa sababu Mungu alikuwa akitafuta mzao mwenye kumcha Mungu. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, mtu asivunje uaminifu kwa mke wa ujana wake.

162:16 Kum 24:1; Mt 5:31-32; 19:4-9; Isa 58:4; Mk 10:4-5; Mwa 6:11; 34:25; Mit 4:17; Za 51:10“Ninachukia kuachana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli, “pia nachukia mtu anayejivika jeuri kama vazi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, wala msije mkavunja uaminifu.

Siku Ya Hukumu

172:17 Isa 1:14; Eze 18:25; Za 5:4; Ay 8:3; Mwa 18:25Mmemchosha Bwana kwa maneno yenu.

Nanyi mnauliza, “Tumemchosha kwa namna gani?”

Mmemchosha kwa kusema, “Wote watendao mabaya ni wema machoni pa Bwana, naye anapendezwa nao” au “Mungu wa haki yuko wapi?”

New International Version

Malachi 2:1-17

Additional Warning to the Priests

1“And now, you priests, this warning is for you. 2If you do not listen, and if you do not resolve to honor my name,” says the Lord Almighty, “I will send a curse on you, and I will curse your blessings. Yes, I have already cursed them, because you have not resolved to honor me.

3“Because of you I will rebuke your descendants2:3 Or will blight your grain; I will smear on your faces the dung from your festival sacrifices, and you will be carried off with it. 4And you will know that I have sent you this warning so that my covenant with Levi may continue,” says the Lord Almighty. 5“My covenant was with him, a covenant of life and peace, and I gave them to him; this called for reverence and he revered me and stood in awe of my name. 6True instruction was in his mouth and nothing false was found on his lips. He walked with me in peace and uprightness, and turned many from sin.

7“For the lips of a priest ought to preserve knowledge, because he is the messenger of the Lord Almighty and people seek instruction from his mouth. 8But you have turned from the way and by your teaching have caused many to stumble; you have violated the covenant with Levi,” says the Lord Almighty. 9“So I have caused you to be despised and humiliated before all the people, because you have not followed my ways but have shown partiality in matters of the law.”

Breaking Covenant Through Divorce

10Do we not all have one Father2:10 Or father? Did not one God create us? Why do we profane the covenant of our ancestors by being unfaithful to one another?

11Judah has been unfaithful. A detestable thing has been committed in Israel and in Jerusalem: Judah has desecrated the sanctuary the Lord loves by marrying women who worship a foreign god. 12As for the man who does this, whoever he may be, may the Lord remove him from the tents of Jacob2:12 Or 12 May the Lord remove from the tents of Jacob anyone who gives testimony in behalf of the man who does this—even though he brings an offering to the Lord Almighty.

13Another thing you do: You flood the Lord’s altar with tears. You weep and wail because he no longer looks with favor on your offerings or accepts them with pleasure from your hands. 14You ask, “Why?” It is because the Lord is the witness between you and the wife of your youth. You have been unfaithful to her, though she is your partner, the wife of your marriage covenant.

15Has not the one God made you? You belong to him in body and spirit. And what does the one God seek? Godly offspring.2:15 The meaning of the Hebrew for the first part of this verse is uncertain. So be on your guard, and do not be unfaithful to the wife of your youth.

16“The man who hates and divorces his wife,” says the Lord, the God of Israel, “does violence to the one he should protect,”2:16 Or “I hate divorce,” says the Lord, the God of Israel, “because the man who divorces his wife covers his garment with violence,” says the Lord Almighty.

So be on your guard, and do not be unfaithful.

Breaking Covenant Through Injustice

17You have wearied the Lord with your words.

“How have we wearied him?” you ask.

By saying, “All who do evil are good in the eyes of the Lord, and he is pleased with them” or “Where is the God of justice?”