Luka 5 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 5:1-39

Kuitwa Kwa Wanafunzi Wa Kwanza

(Mathayo 4:18-22; Marko 1:16-20)

15:1 Mk 4:14; Ebr 4:12Siku moja Yesu alipokuwa amesimama karibu na Ziwa la Genesareti,5:1 Yaani Bahari ya Galilaya. watu wengi wakiwa wanasongana kumzunguka ili wapate kusikia neno la Mungu, 2akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, zikiwa zimeachwa hapo na wavuvi waliokuwa wanaosha nyavu zao. 35:3 Mt 13:2Akaingia katika mojawapo ya hizo mashua ambayo ilikuwa ya Simoni, akamwomba aisogeze ndani ya maji kidogo kutoka ufuoni. Kisha akaketi na kufundisha watu akiwa mle ndani ya mashua.

45:4 Yn 21:6Alipomaliza kunena, akamwambia Simoni, “Sasa peleka mashua hadi kilindini kisha mshushe nyavu zenu mkavue samaki.”

55:5 Lk 9:33, 49; 17:13; Yn 21:3Simoni akamjibu, “Bwana, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha na hatukuvua chochote. Lakini, kwa neno lako nitazishusha nyavu.”

65:6 Yn 21:11Nao walipozishusha nyavu zao, wakavua samaki wengi sana, nyavu zao zikajaa zikaanza kukatika. 7Wakawaashiria wavuvi wenzao kwenye ile mashua nyingine ili waje kuwasaidia. Wakaja, wakajaza mashua zote mbili samaki hata zikaanza kuzama.

85:8 Mwa 18:27; Ay 42:6Simoni Petro alipoona haya yaliyotukia, alianguka miguuni mwa Yesu na kumwambia, “Bwana, ondoka kwangu. Mimi ni mtu mwenye dhambi!” 9Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wameshangazwa sana na wingi wa samaki waliokuwa wamepata. 105:10 Mt 14:27Vivyo hivyo wenzake Simoni, yaani Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walishangazwa pia.

Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.” 115:11 Mt 4:11Hivyo wakasogeza mashua zao mpaka ufuoni mwa bahari, wakaacha kila kitu na kumfuata.

Yesu Amtakasa Mtu Mwenye Ukoma

(Mathayo 8:1-4; Marko 1:40-45)

125:12 Mt 8:12Ikawa siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamjia. Alipomwona Yesu, alianguka chini mpaka uso wake ukagusa ardhi, akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.”

13Yesu akanyoosha mkono wake, akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Na mara ukoma wake ukatakasika.

145:14 Mt 8:4Yesu akamwagiza akisema, “Usimwambie mtu yeyote, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”

155:15 Mt 9:26Lakini habari zake Yesu zikazidi sana kuenea kotekote kuliko wakati mwingine wowote. Makutano makubwa ya watu yalikuwa yakikusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. 165:16 Mt 14:23Lakini mara kwa mara Yesu alijitenga nao ili kwenda mahali pa faragha kuomba.

Yesu Amponya Mtu Mwenye Kupooza

(Mathayo 9:1-8; Marko 2:1-12)

175:17 Mt 15:1; Lk 2:46; Mk 5:30; Lk 6:19Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na walimu wa sheria, waliokuwa wametoka kila kijiji cha Galilaya na kutoka Uyahudi na Yerusalemu, walikuwa wameketi huko. Nao uweza wa Bwana ulikuwa juu yake kuponya wagonjwa. 185:18 Mt 9:2; Mk 2:8Wakaja watu wamembeba mgonjwa aliyepooza kwenye mkeka. Wakajaribu kumwingiza ndani ili wamweke mbele ya Yesu. 19Walipokuwa hawawezi kufanya hivyo kwa sababu ya umati wa watu, wakapanda juu ya paa, wakaondoa baadhi ya matofali, wakamteremsha yule mgonjwa kwa mkeka wake hadi katikati ya ule umati pale mbele ya Yesu.

205:20 Lk 7:48-49Yesu alipoiona imani yao, akamwambia yule mgonjwa, “Rafiki, dhambi zako zimesamehewa.”

215:21 Isa 43:25; Lk 7:49; Yn 5:12Mafarisayo na wale walimu wa sheria wakaanza kuuliza, “Ni nani mtu huyu anayesema maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”

22Yesu akijua mawazo yao akawauliza, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu? 23Je, ni lipi lililo rahisi zaidi, kumwambia, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’? 245:24 Mt 8:20Lakini ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Akamwambia yule aliyepooza, “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.” 25Mara yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama mbele yao wote, akachukua mkeka wake, akaenda zake nyumbani, huku akimtukuza Mungu. 265:26 Mt 9:8Kila mmoja akashangaa na kumtukuza Mungu. Wakajawa na hofu ya Mungu, wakasema, “Leo tumeona mambo ya ajabu.”

Yesu Amwita Lawi

(Mathayo 9:9-13; Marko 2:13-17)

275:27 Mt 4:19Baada ya haya, Yesu alitoka na kumwona mtoza ushuru mmoja jina lake Lawi akiwa amekaa forodhani, mahali pake pa kutoza ushuru. Akamwambia, “Nifuate.” 285:28 Lk 5:11; Mt 4:19Naye Lawi akaacha kila kitu, akaondoka, akamfuata.

295:29 Lk 15:1Kisha Lawi akamfanyia Yesu karamu kubwa nyumbani kwake, nao umati mkubwa wa watoza ushuru na watu wengine walikuwa wakila pamoja nao. 305:30 Mdo 23:9; Mt 9:11Lakini Mafarisayo na walimu wa sheria waliokuwa wa dhehebu lao wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu, wakisema, “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”

31Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa. 325:32 Yn 3:17Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.”

Yesu Aulizwa Kuhusu Kufunga

(Mathayo 9:14-17; Marko 2:18-22)

335:33 Lk 7:18; Yn 1:35; 3:25-26; Mt 14:17; Mk 2:18-22Wakamwambia Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo mara kwa mara hufunga na kuomba, lakini wanafunzi wako wanaendelea kula na kunywa.”

345:34 Yn 3:29; Mt 14:17; Mk 2:18-22Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwafanya wageni wa bwana arusi kufunga wakati yuko pamoja nao? 355:35 Lk 9:22; 7:22; Mt 14:17; Mk 2:18-22Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.”

365:36 Mt 14:17; Mk 2:18-22; Mt 9:16, 17; Mk 2:21, 22Yesu akawapa mfano huu, akawaambia: “Hakuna mtu achanaye kiraka kutoka kwenye nguo mpya na kukishonea kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, atakuwa amechana nguo mpya, na kile kiraka hakitalingana na ile nguo iliyochakaa. 375:37 Mt 14:17; Mk 2:18-22Hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo yote itamwagika. 385:38 Mt 14:17; Mk 2:18-22Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya. 395:39 Mt 14:17; Mk 2:18-22Wala hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai ya zamani, bali husema, ‘Ile ya zamani ni nzuri zaidi.’ ”

Knijga O Kristu

Luka 5:1-39

Prvi učenici

(Mt 4:18-22; Mk 1:16-20; Iv 1:40-42)

1Dok je jednom stajao na obali Genezaretskoga jezera5:1 Galilejskog jezera, Galilejskog mora. a mnoštvo je nagrnulo k njemu da sluša Božju riječ, 2Isus ugleda dvije lađice koje su ribari ostavili uz obalu jer su ispirali mreže. 3Uđe u jednu od njih te zamoli Šimuna, kojemu je pripadala, da ju malo odgurne od obale. Zatim sjedne i počne iz lađice poučavati narod.

4Kad je završio s govorom, reče Šimunu: “Izvezi natrag na pučinu, pa bacite mreže za lov!” 5“Gospodine,” reče mu Šimun, “cijelu smo noć teško radili i ništa nismo uhvatili, ali kad ti tako kažeš, bacit ću mreže.” 6Kad su ih bacili, u njih se uhvati toliko riba da su se razdirale. 7Ribari stanu mahati svojim drugovima u drugoj lađici da im priskoče u pomoć. Oni dođu, pa napune obje lađice ribom tako da su gotovo tonule.

8Kad je to vidio Šimun Petar, padne na koljena pred Isusom i reče mu: “Gospodine, udalji se od mene jer sam odviše grešan da bih ti bio blizu!” 9Silna lovina riba zaprepastila je njega i sve koji su bili s njime, 10pa tako i Šimunove drugove Jakova i Ivana, Zebedejeve sinove.

Isus odgovori Šimunu: “Ne boj se! Od sada ćeš loviti ljude!” 11Oni izvuku lađice na kopno, a zatim sve ostave i pođu za njim.

Isus iscjeljuje gubavca

(Mt 8:2-4; Mk 1:40-44)

12U nekome mjestu gdje je Isus boravio pojavi se iznenada pred njim čovjek pun gube. Čim spazi Isusa, baci se pred njega ničice, licem prema zemlji, i zamoli ga: “Gospodine, ako hoćeš, možeš me iscijeliti!”

13Isus ispruži ruku i dotakne ga. “Hoću!” reče. “Budi čist!” I guba odmah nestane. 14Isus mu zapovjedi: “Nikome o tomu ne govori, već idi ravno svećeniku te sa sobom ponesi žrtveni dar prema Mojsijevu zakonu kao javno svjedočanstvo svojeg ozdravljenja.”

15Ali glas o Isusu pronosio se sve dalje, pa je golemo mnoštvo naroda nahrupilo da ga sluša i da ozdravi od bolesti. 16A on je odlazio moliti se na samotna mjesta.

Isus iscjeljuje uzetog čovjeka

(Mt 9:1-8; Mk 2:3-12)

17Jednoga dana dok je Isus poučavao, ondje su sjedili farizeji i pismoznanci koji su došli iz svih galilejskih i judejskih sela i iz Jeruzalema, a njega je sila Gospodnja poticala da iscjeljuje. 18Neki ljudi donijeli su uzetog čovjeka na nosilima. Htjeli su ga unijeti unutra i položiti pred Isusa, 19ali nisu se kroz mnoštvo uspjeli probiti do njega. Zato se popnu na krov, načine otvor među crepovima te ga s nosilima spuste među mnoštvo pred Isusa.

20Kad Isus vidje njihovu vjeru, reče bolesniku: “Čovječe, oprošteni su ti grijesi!”

21Pismoznanci i farizeji nato počnu umovati: “Tko je ovaj da tako huli? Tko može opraštati grijehe osim jedinoga Boga!”

22Isus prozre njihovo umovanje, pa ih upita: “Zašto to smatrate hulom? 23Što je lakše reći: ‘Grijesi su ti oprošteni’ ili ‘Ustani i idi’? 24Dokazat ću vam da ja, Sin Čovječji, imam vlast na zemlji opraštati grijehe.” Okrene se zatim prema uzetome i reče: “Zapovijedam ti: ustani, uzmi nosila i idi kući!”

25Čovjek smjesta ustane te naočigled svih uzme nosila i ode slaveći Boga. 26Nato sve obuzme zanos, pa su slavili Boga i silno prestrašeni govorili: “Ovo što smo danas vidjeli je čudesno!”

Isus poziva Levija

(Mt 9:9-13; Mk 2:14-17)

27Izlazeći nakon toga, Isus ugleda ubirača poreza5:27 Ubirači poreza bili su u to doba omraženi u narodu zbog suradnje s okupatorskim vlastima i zbog toga što su iznuđivali novac od siromašnoga puka. imenom Levi kako sjedi u svojemu uredu te ga pozove: “Pođi za mnom!” 28Levi nato ustane, ostavi sve te pođe za njim.

29Poslije Levi u svojemu domu priredi veliku gozbu u čast Isusu. S njima je za stolom sjedilo mnogo ubirača poreza i drugih uzvanika. 30A farizeji i pismoznanci negodovali su i govorili učenicima: “Zašto jedete i pijete s ubiračima poreza i drugim grešnicima?”

31Isus im odgovori: “Ne treba liječnik zdravima, nego bolesnima. 32Nisam došao zvati pravednike na obraćenje, već grešnike.”

Rasprava o postu

(Mt 9:14-17; Mk 2:18-22)

33Oni mu nato prigovore: “Ivanovi i farizejski učenici često poste i mole se, a tvoji jedu i piju!”

34Isus im odgovori: “Zar možete siliti svatove da poste dok je mladoženja s njima? 35Ali doći će dani kada će im ugrabiti mladoženju. Tada će postiti.”

36Zatim im Isus to objasni prispodobom: “Nitko neće rupu na starome odijelu zakrpati tkaninom koju je otparao s novoga jer bi tako poderao i novo odijelo, a starome odijelu krpa s novoga ionako ne bi pristajala. 37I nitko ne ulijeva novo vino u stare mjehove jer bi se od njega raspuknuli. Tako bi se i vino prolilo i mjehovi uništili. 38Zato novo vino mora se ulijevati u nove mješine. 39I nitko pijući staro vino ne poželi piti novo. ‘Staro je bolje’, kažu.”