Luka 4 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 4:1-44

Yesu Ajaribiwa Na Shetani

(Mathayo 4:1-11; Marko 1:12-13)

14:1 Lk 1:15-45; 3:3-21; Eze 37:1; Lk 2:27Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani, 24:2 Kut 34:28; 1Fal 19:8mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.

34:3 Mt 4:3Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”

44:4 Kum 8:3Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’ ”

54:5 Mt 24:14Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja. 64:6 Yn 14:30Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka. 7Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”

84:8 Kum 6:3Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’ ”

94:9 Mt 4:5Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa, 104:10 Za 91:11, 12kwa maana imeandikwa:

“ ‘Atakuagizia malaika zake

ili wakulinde;

114:11 Za 91:12nao watakuchukua mikononi mwao,

usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’ ”

124:12 Kum 6:12Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ”

134:13 Ebr 4:15; Yn 14:30Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.

Mwanzo Wa Huduma Ya Galilaya

(Mathayo 4:12-17; Marko 1:14-15)

144:14 Mt 4:12; 9:26Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando. 154:15 Mt 4:23Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.

Yesu Akataliwa Nazareti

(Mathayo 13:53-58; Marko 6:1-6)

164:16 Mt 2:23; 13:54Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome, 174:17 Isa 61:1, 2; 58:6naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:

184:18 Yn 3:34“Roho wa Bwana yu juu yangu,

kwa sababu amenitia mafuta

kuwahubiria maskini habari njema.

Amenituma kuwatangazia wafungwa

kufunguliwa kwao,

na vipofu kupata kuona tena,

kuwaweka huru wanaoonewa,

19na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”

204:20 Mt 26:55Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 214:21 Mt 1:22Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”

224:22 Yn 6:42; 7:15Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”

234:23 Mt 2:23; Mk 1:21-28; 2:1-12Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’ ”

244:24 Mt 13:57; Yn 4:44Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe. 254:25 1Fal 18:1; Ufu 11:6Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima. 264:26 1Fal 17:8-16; Mt 11:21Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni. 274:27 2Fal 5:1-14Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”4:27 Shamu hapa inamaanisha Syria.

28Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana. 294:29 Hes 15:35; Ebr 13:12Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali. 304:30 Yn 8:59; 10:39Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.

Yesu Atoa Pepo Mchafu

(Marko 1:21-28)

314:31 Mt 4:13Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha. 324:32 Mt 7:28-29Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.

334:33 Mk 1:23Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema, 344:34 Mt 8:28-29; Mk 1:24; Yak 2:19“Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”

354:35 Mt 8:26; Lk 8:24Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru. 364:36 Mt 7:28-29; 10:1Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!” 374:37 Mt 9:26Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.

Yesu Awaponya Wengi

(Mathayo 8:14-17; Marko 1:29-34)

384:38 Mt 8:14; Mk 1:29Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie. 394:39 Lk 4:35, 41Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.

404:40 Mk 5:23; Mt 4:23Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya. 414:41 Mt 4:3; 8:4Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.4:41 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta.

424:42 Mk 1:35Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke. 434:43 Mt 3:2Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.” 444:44 Mt 4:23Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.

New International Reader’s Version

Luke 4:1-44

Jesus Is Tempted in the Desert

1Jesus, full of the Holy Spirit, left the Jordan River. The Spirit led him into the desert. 2There the devil tempted him for 40 days. Jesus ate nothing during that time. At the end of the 40 days, he was hungry.

3The devil said to him, “If you are the Son of God, tell this stone to become bread.”

4Jesus answered, “It is written, ‘Man must not live only on bread.’ ” (Deuteronomy 8:3)

5Then the devil led Jesus up to a high place. In an instant, he showed Jesus all the kingdoms of the world. 6He said to Jesus, “I will give you all their authority and glory. It has been given to me, and I can give it to anyone I want to. 7If you worship me, it will all be yours.”

8Jesus answered, “It is written, ‘Worship the Lord your God. He is the only one you should serve.’ ” (Deuteronomy 6:13)

9Then the devil led Jesus to Jerusalem. He had Jesus stand on the highest point of the temple. “If you are the Son of God,” he said, “throw yourself down from here. 10It is written,

“ ‘The Lord will command his angels to take good care of you.

11They will lift you up in their hands.

Then you won’t trip over a stone.’ ” (Psalm 91:11,12)

12Jesus answered, “Scripture says, ‘Do not test the Lord your God.’ ” (Deuteronomy 6:16)

13When the devil finished all this tempting, he left Jesus until a better time.

Jesus Is Not Accepted in Nazareth

14Jesus returned to Galilee in the power of the Holy Spirit. News about him spread through the whole countryside. 15He was teaching in their synagogues, and everyone praised him.

16Jesus went to Nazareth, where he had been brought up. On the Sabbath day he went into the synagogue as he usually did. He stood up to read. 17And the scroll of Isaiah the prophet was handed to him. Jesus unrolled it and found the right place. There it is written,

18“The Spirit of the Lord is on me.

He has anointed me

to announce the good news to poor people.

He has sent me to announce freedom for prisoners.

He has sent me so that the blind will see again.

He wants me to set free those who are treated badly.

19And he has sent me to announce the year when he will set his people free.” (Isaiah 61:1,2)

20Then Jesus rolled up the scroll. He gave it back to the attendant and sat down. The eyes of everyone in the synagogue were staring at him. 21He began by saying to them, “Today this passage of Scripture is coming true as you listen.”

22Everyone said good things about him. They were amazed at the gracious words they heard from his lips. “Isn’t this Joseph’s son?” they asked.

23Jesus said, “Here is a saying you will certainly apply to me. ‘Doctor, heal yourself!’ And you will tell me this. ‘Do the things here in your hometown that we heard you did in Capernaum.’ ”

24“What I’m about to tell you is true,” he continued. “A prophet is not accepted in his hometown. 25I tell you for sure that there were many widows in Israel in the days of Elijah. And there had been no rain for three and a half years. There wasn’t enough food to eat anywhere in the land. 26But Elijah was not sent to any of those widows. Instead, he was sent to a widow in Zarephath near Sidon. 27And there were many in Israel who had skin diseases in the days of Elisha the prophet. But not one of them was healed except Naaman the Syrian.”

28All the people in the synagogue were very angry when they heard that. 29They got up and ran Jesus out of town. They took him to the edge of the hill on which the town was built. They planned to throw him off the cliff. 30But Jesus walked right through the crowd and went on his way.

Jesus Drives Out an Evil Spirit

31Then Jesus went to Capernaum, a town in Galilee. On the Sabbath day he taught the people. 32They were amazed at his teaching, because his words had authority.

33In the synagogue there was a man controlled by a demon, an evil spirit. He cried out at the top of his voice. 34“Go away!” he said. “What do you want with us, Jesus of Nazareth? Have you come to destroy us? I know who you are. You are the Holy One of God!”

35“Be quiet!” Jesus said firmly. “Come out of him!” Then the demon threw the man down in front of everybody. And it came out without hurting him.

36All the people were amazed. They said to each other, “What he says is amazing! With authority and power he gives orders to evil spirits. And they come out!” 37The news about Jesus spread throughout the whole area.

Jesus Heals Many People

38Jesus left the synagogue and went to the home of Simon. At that time, Simon’s mother-in-law was suffering from a high fever. So they asked Jesus to help her. 39He bent over her and commanded the fever to leave, and it left her. She got up right away and began to serve them.

40At sunset, people brought to Jesus all who were sick. He placed his hands on each one and healed them. 41Also, demons came out of many people. The demons shouted, “You are the Son of God!” But he commanded them to be quiet. He would not allow them to speak, because they knew he was the Messiah.

42At dawn, Jesus went out to a place where he could be by himself. The people went to look for him. When they found him, they tried to keep him from leaving them. 43But he said, “I must announce the good news of God’s kingdom to the other towns also. That is why I was sent.” 44And he kept on preaching in the synagogues of Judea.