Luka 3 – NEN & NSP

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 3:1-38

Yohana Mbatizaji Aanza Kuhubiri

(Mathayo 3:1-12; Marko 1:1-8; Yohana 1:19-28)

13:1 Mt 27:2Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene, 23:2 Yn 18:13; Mdo 4:6; Mt 3:1nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani. 33:3 Mk 3:16; Mal 1:4Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi. 43:4 Isa 40:3-5; Mt 3:3; Mk 1:3; Yn 1:23Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:

“Sauti ya mtu aliaye nyikani,

‘Itengenezeni njia ya Bwana,

yanyoosheni mapito yake.

5Kila bonde litajazwa,

kila mlima na kilima vitashushwa.

Njia zilizopinda zitanyooshwa,

na zilizoparuza zitasawazishwa.

63:6 Za 98:2; Lk 2:30Nao watu wote watauona

wokovu wa Mungu.’ ”

73:7 Mt 12:34; 23:33; Rum 1:18Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja? 83:8 Isa 51:7; Gal 3:7Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya. 93:9 Mt 3:10Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”

103:10 Mdo 2:37; 16:30Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”

113:11 Isa 58:7; Eze 18:7Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”

123:12 Lk 7:29Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”

133:13 Lk 19:8Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”

143:14 Law 19:11Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?”

Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”

153:15 Mt 3:1; Yn 1:19-20; Mdo 13:25Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.3:15 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. 163:16 Mk 1:4; Yn 1:26, 33; Mdo 11:16Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji.3:16 Tafsiri nyingine zinasema ndani ya maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto. 173:17 Isa 30:24; Mt 13:30; 25:41Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.” 18Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.

193:19 Mt 14:1Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya, 203:20 Mt 14:3-4Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.

Kubatizwa Kwa Bwana Yesu

(Mathayo 3:13-17; Marko 1:9-11)

213:21 Mt 14:23; Mk 1:35Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka. 223:22 Isa 42:1; Yn 1:32-33; Mt 3:17Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”

Ukoo Wa Bwana Yesu

(Mathayo 1:1-17)

233:23 Mt 4:17; Lk 1:27Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu,

Yosefu alikuwa mwana wa Eli,

24Eli alikuwa mwana wa Mathati,

Mathati alikuwa mwana wa Lawi,

Lawi alikuwa mwana wa Melki,

Melki alikuwa mwana wa Yanai,

Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,

25Yosefu alikuwa mwana wa Matathia,

Matathia alikuwa mwana wa Amosi,

Amosi alikuwa mwana wa Nahumu,

Nahumu alikuwa mwana wa Esli,

Esli alikuwa mwana wa Nagai,

26Nagai alikuwa mwana wa Maathi,

Maathi alikuwa mwana wa Matathia,

Matathia alikuwa mwana wa Semeini,

Semeini alikuwa mwana wa Yoseki,

Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,

273:27 Mt 1:12; 1Nya 3:17Yoda alikuwa mwana wa Yoanani,

Yoanani alikuwa mwana wa Resa,

Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli,

Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli,

Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,

28Neri alikuwa mwana wa Melki,

Melki alikuwa mwana wa Adi,

Adi alikuwa mwana wa Kosamu,

Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu,

Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,

29Eri alikuwa mwana wa Yoshua,

Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri,

Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu,

Yorimu alikuwa mwana wa Mathati,

Mathati alikuwa mwana wa Lawi,

30Lawi alikuwa mwana wa Simeoni,

Simeoni alikuwa mwana wa Yuda,

Yuda alikuwa mwana wa Yosefu,

Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu,

Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu,

Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,

313:31 2Sam 5:14; 1Nya 3:5Melea alikuwa mwana wa Mena,

Mena alikuwa mwana wa Matatha,

Matatha alikuwa mwana wa Nathani,

Nathani alikuwa mwana wa Daudi,

323:32 Rut 4:22; 1Nya 2:10Daudi alikuwa mwana wa Yese,

Yese alikuwa mwana wa Obedi,

Obedi alikuwa mwana wa Boazi,

Boazi alikuwa mwana wa Salmoni,

Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,

333:33 Rut 4:18-22; 1Nya 2:10Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu,

Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu,

Aramu alikuwa mwana wa Hesroni,

Hesroni alikuwa mwana wa Peresi,

Peresi alikuwa mwana wa Yuda,

343:34 Mwa 11:24-26Yuda alikuwa mwana wa Yakobo,

Yakobo alikuwa mwana wa Isaki,

Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu,

Abrahamu alikuwa mwana wa Tera,

Tera alikuwa mwana wa Nahori,

35Nahori alikuwa mwana wa Serugi,

Serugi alikuwa mwana wa Reu,

Reu alikuwa mwana wa Pelegi,

Pelegi alikuwa mwana wa Eberi,

Eberi alikuwa mwana wa Sala,

363:36 Mwa 5:28-32; 11:12Sala alikuwa mwana wa Kenani,

Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi,

Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu,

Shemu alikuwa mwana wa Noa,

Noa alikuwa mwana wa Lameki,

373:37 Mwa 5:12-25Lameki alikuwa mwana wa Methusela,

Methusela alikuwa mwana wa Enoki,

Enoki alikuwa mwana wa Yaredi,

Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli,

Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,

383:38 Mwa 5:19Kenani alikuwa mwana wa Enoshi,

Enoshi alikuwa mwana wa Sethi,

Sethi alikuwa mwana wa Adamu,

Adamu alikuwa mwana wa Mungu.

New Serbian Translation

Лука 3:1-38

Проповедање Јована Крститеља

1Била је петнаеста година владавине цара Тиверија. Тада је Понтије Пилат управљао Јудејом, Ирод је владао Галилејом, а његов брат Филип Итурејом и Трахонитидом, док је Лисанија управљао Авилином. 2Првосвештеници су били Ана и Кајафа. У то време је Бог позвао Јована, Захаријиног сина, који је био у пустињи. 3Јован је прошао целу област око реке Јордан проповедајући покајање и крштење ради опроштења греха.

4Овако је, наиме, написано у Књизи пророка Исаије:

„Глас једног пустињом одзвања:

’Пут Господњи приправите;

друмове за њега поравнајте.

5Свака ће се долина испунити,

спустиће се свака гора и брежуљак;

што је стрмо, постаће равно,

што је неравно, постаће глатко,

6и сваки човек ће видети спасење Божије.’“

7Много народа је долазило к Јовану да их крсти, али он им је говорио: „Породе змијски, ко вам је рекао да бежите пред надолазећим гневом Божијим? 8Него, донесите плодове који доказују покајање. И не говорите у себи: ’Аврахам је наш отац!’, јер вам кажем да Бог може и од овог камења да подигне децу Аврахаму. 9Већ је секира спремна да у корену посече дрвета, јер свако дрво које не рађа добар род, одсеца се и баца у ватру.“

10Народ га је питао: „Шта онда да чинимо?“

11Јован им одговори: „Ко има две кошуље, нека да једну ономе ко нема и ко има храну нека чини слично.“

12Дошли су и порезници да се крсте, па су и они упитали Јована: „Учитељу, шта ми да чинимо?“

13Јован им рече: „Не узимајте више од онога што је прописано.“

14И војници га упитају: „А шта да чинимо ми?“ Јован им одговори: „Не изнуђујте новац ни од кога и никога лажно не оптужујте, него будите задовољни својом платом.“

15У народу се пробудила нада, па су се сви питали о Јовану: „Да није он Христос?“

16Јован им свима одговори: „Ја вас крштавам водом, али после мене долази неко ко је моћнији од мене. Ја нисам достојан да одрешим ремење на његовој обући. Он ће вас крстити Светим Духом и огњем. 17У његовој руци је лопата да овеје своје гумно и да сабере жито у своју житницу, а плеву ће спалити неугасивим огњем.“ 18Јован је и на много других начина подстицао народ и навештавао Радосну вест.

19А Јован је јавно прекоревао и тетрарха Ирода, због тога што је овај живео са Иродијадом, женом свога брата, и због свих злодела која је починио. 20На све то, Ирод је додао још једно злодело: бацио је Јована у тамницу.

Исусово крштење

21Пошто се крстио сав народ, крстио се и Исус. Док се молио, отворе се небеса, 22те Дух Свети сиђе на њега у облику голуба. Тада се зачуо глас са неба: „Ти си Син мој вољени, ти си ми сва радост!“

Исусови преци

23Исус је имао око тридесет година када је почео да делује. Свет је мислио да је он био Јосифов син,

а потомак: Илијев,

24Мататов,

Левијев,

Мелхијев,

Јанејев,

Јосифов,

25Мататијин,

Амосов,

Наумов,

Еслијев,

Нангејев,

26Ма̂тов,

Мататијин,

Симеинов,

Јосихов,

Јодин,

27Јохананов,

Рисин,

Зоровавељов,

Салатилов,

Ниријев,

28Мелхијев,

Адијев,

Косамов,

Елмадамов,

Иров,

29Исусов,

Елиезеров,

Јоримов,

Мататов,

Левијев,

30Симеунов,

Јудин,

Јосифов,

Јонамов,

Елиакимов,

31Мелејин,

Менин,

Мататин,

Натанов,

Давидов,

32Јесејев,

Овидов,

Возов,

Салин,

Насонов,

33Аминадавов,

Админов,

Арнијев,

Есронов,

Фаресов,

Јудин,

34Јаковљев,

Исаков,

Аврахамов,

Тарин,

Нахоров,

35Серухов,

Рагавов,

Фалеков,

Еверов,

Салин,

36Каинамов,

Арфаксадов,

Симов,

Нојев,

Ламехов,

37Матусалин,

Енохов,

Јаредов,

Малалеилов,

Каинамов,

38Еносов,

Ситов,

Адамов,

Божији.