Luka 24 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 24:1-53

Kufufuka Kwa Yesu

(Mathayo 28:1-10; Marko 16:1-8; Yohana 20:1-10)

124:1 Lk 23:56; Mt 28:1; Mk 16; 1; Yn 20:2Mnamo siku ya kwanza ya juma, alfajiri na mapema, wale wanawake walichukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa, wakaenda kaburini. 224:2 Mt 24:2; Mk 16:5Wakakuta lile jiwe limevingirishwa kutoka kwenye kaburi, 324:3 Lk 24:23; Mk 16:5lakini walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu. 424:4 Yn 20:12; Mdo 1:10Walipokuwa wanashangaa juu ya jambo hili, ghafula watu wawili waliokuwa wamevaa mavazi yanayongʼaa kama umeme wakasimama karibu nao. 5Wale wanawake, wakiwa na hofu, wakainamisha nyuso zao mpaka chini. Lakini wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu? 624:6 Mt 17:22-23; Mk 9:30-31Hayuko hapa; amefufuka! Kumbukeni alivyowaambia alipokuwa bado yuko pamoja nanyi huko Galilaya kwamba: 724:7 Mt 8:20; 16:21‘Ilikuwa lazima Mwana wa Adamu atiwe mikononi mwa watu wenye dhambi na waovu ili asulubiwe, na siku ya tatu afufuke.’ ” 824:8 Yn 2:22Ndipo wakayakumbuka maneno ya Yesu.

924:9 Mt 28:8; Mk 16:10Waliporudi kutoka huko kaburini, wakawaeleza wale wanafunzi kumi na mmoja pamoja na wengine wote mambo haya yote. 1024:10 Lk 8:1-3; Mk 6:30Basi Maria Magdalene, Yoana, na Maria mama yake Yakobo, pamoja na wanawake wengine waliofuatana nao ndio waliwaelezea mitume habari hizi. 1124:11 Mk 16:11Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi. 1224:12 Yn 20:3-7; 20:10Hata hivyo, Petro akainuka na kukimbia kwenda kule kaburini. Alipoinama kuchungulia, akaona vile vitambaa vya kitani, ila hakuona kitu kingine. Naye akaenda zake akijiuliza nini kilichotokea.

Njiani Kwenda Emau

(Marko 16:12-13)

1324:13 Mk 16:12Ikawa siku iyo hiyo, wanafunzi wawili wa Yesu walikuwa njiani wakienda kijiji kilichoitwa Emau, yapata maili saba24:13 Maili saba ni kama kilomita 11.2. kutoka Yerusalemu. 14Walikuwa wakizungumza wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotukia. 1524:15 Mt 18:20Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akaja akatembea pamoja nao, 1624:16 Yn 20:14; 21:4lakini macho yao yakazuiliwa ili wasimtambue.

17Akawauliza, “Ni mambo gani haya mnayozungumza wakati mnatembea?”

Wakasimama, nyuso zao zikionyesha huzuni. 1824:18 Yn 19:25Mmoja wao, aliyeitwa Kleopa, akamuuliza, “Je, wewe ndiye peke yako mgeni huku Yerusalemu ambaye hufahamu mambo yaliyotukia humo siku hizi?”

1924:19 Mk 1:24Akawauliza, “Mambo gani?”

Wakamjibu, “Mambo ya Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii, mwenye uwezo mkuu katika maneno yake na matendo yake, mbele za Mungu na mbele ya wanadamu wote. 2024:20 Lk 23:13Viongozi wa makuhani na viongozi wetu walimtoa ahukumiwe kufa, nao wakamsulubisha. 2124:21 Lk 1:68; 2:38; Mt 16:21Lakini tulikuwa tumetegemea kwamba yeye ndiye angelikomboa Israeli. Zaidi ya hayo, leo ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee. 2224:22 Mt 28:8; Mk 16:10; Lk 24:9, 10; Yn 20:18Isitoshe, baadhi ya wanawake katika kundi letu wametushtusha. Walikwenda kaburini leo alfajiri, 23lakini hawakuukuta mwili wake. Walirudi wakasema wameona maono ya malaika ambao waliwaambia kwamba Yesu yu hai. 2424:24 Lk 24:12; Yn 20:3-19Kisha baadhi ya wenzetu walikwenda kaburini wakalikuta kama vile wale wanawake walivyokuwa wamesema, lakini yeye hawakumwona.”

25Yesu akawaambia, “Ninyi ni wajinga kiasi gani, nanyi ni wazito mioyoni mwenu kuamini mambo yote yaliyonenwa na manabii! 2624:26 Ebr 2:10; 1Pet 1:11Je, haikumpasa Kristo24:26 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. kuteswa kwa njia hiyo na kisha aingie katika utukufu wake?” 2724:27 Mwa 3:15; Hes 2:19; Mk 7:20; Mal 3:1; Yn 1:45Naye akianzia na Sheria ya Mose na Manabii wote, akawafafanulia jinsi Maandiko yalivyosema kumhusu yeye.

2824:28 Mwa 32:26; 42:7; Mk 6:49Nao walipokaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, Yesu akawa kama anaendelea mbele. 2924:29 Mwa 19:3; Mdo 16:15Lakini wao wakamsihi sana akae nao, wakisema, “Kaa hapa nasi, kwa maana sasa ni jioni na usiku unaingia.” Basi akaingia ndani kukaa nao.

3024:30 Mt 14:19Alipokuwa mezani pamoja nao, akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akaanza kuwagawia. 3124:31 Za 39:3; Lk 24:16Ndipo macho yao yakafumbuliwa, nao wakamtambua, naye akatoweka machoni pao. Hawakumwona tena. 3224:32 Za 39:3; Lk 24:27, 28Wakaulizana wao kwa wao, “Je, mioyo yetu haikuwakawaka kwa furaha ndani yetu alipokuwa anazungumza nasi njiani na kutufafanulia Maandiko?”

33Wakaondoka mara, wakarudi Yerusalemu. Wakawakuta wale wanafunzi kumi na mmoja na wale waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika 3424:34 1Kor 15:5wakisema, “Ni kweli! Bwana amefufuka, naye amemtokea Simoni.” 3524:35 Lk 24:30, 31Kisha wale wanafunzi wawili wakaeleza yaliyotukia njiani na jinsi walivyomtambua Yesu alipoumega mkate.

Yesu Awatokea Wanafunzi Wake

(Mathayo 28:16-20; Marko 16:14-18; Yohana 20:19-23; Matendo 1:6-8)

3624:36 Yn 20:19, 21, 26; 14:27Walipokuwa bado wanazungumza hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”

3724:37 Mk 6:49Wakashtuka na kuogopa wakidhani kwamba wameona mzuka. 38Lakini Yesu akawauliza, “Kwa nini mnaogopa? Kwa nini mna shaka mioyoni mwenu? 3924:39 Yn 20:27; 1Yn 1:1Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”

40Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake. 4124:41 Mwa 45:26; Yn 21:5Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”

42Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa, 4324:43 Mdo 10:40naye akakichukua na kukila mbele yao.

4424:44 Lk 24:26; Mt 1:22; 16:21; Za 110Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”

4524:45 Mdo 16:14Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko. 4624:46 Lk 24:26; Isa 50:6; 53:2Akawaambia, “Haya ndiyo yaliyoandikwa: Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu. 4724:47 Mdo 10:43; 13:38; Mt 28:19; Mk 13:10Toba na msamaha wa dhambi zitatangaziwa mataifa yote kupitia jina lake kuanzia Yerusalemu. 4824:48 Yn 15:27; 1Pet 5:1Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.

Kuahidiwa Kwa Roho Mtakatifu

4924:49 Yn 14:16; Mdo 1:4“Tazama nitawatumia ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini hadi mtakapovikwa uwezo utokao juu.”

Kupaa Kwa Yesu Mbinguni

(Marko 16:19-20; Matendo 1:9-11)

5024:50 Mt 21:11Akiisha kuwaongoza mpaka kwenye viunga vya Bethania, akainua mikono yake juu na kuwabariki. 5124:51 2Fal 2:11Alipokuwa anawabariki, akawaacha, akachukuliwa mbinguni. 5224:52 Mt 28:9, 17Kisha wakamwabudu na kurudi Yerusalemu wakiwa wamejawa na furaha kuu. 5324:53 Mdo 2:46Nao wakadumu ndani ya Hekalu wakimtukuza Mungu. Amen.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

路加福音 24:1-53

耶穌死裡復活

1週日黎明時分,幾位婦女帶著預備好的香料來到墳前, 2發現墓口的大石頭已經滾到旁邊, 3便進去,卻沒有看見主耶穌的遺體。 4正在猜疑之間,突然有兩個衣服發光的人站在旁邊, 5她們嚇得俯伏在地。那兩個人對她們說:「你們為什麼在死人中找活人呢? 6祂不在這裡,已經復活了!記住祂在加利利對你們說的話, 7『人子必須被交在罪人的手中,被釘在十字架上,在第三天復活。』」

8她們想起耶穌的話來, 9便離開墓地回去把事情的經過告訴十一個使徒和其他人。 10這些婦女就是抹大拉瑪麗亞約亞娜雅各的母親瑪麗亞及其他人。

11大家聽了都不相信,認為是無稽之談。 12彼得卻起身跑到墓地,屈身往墓裡張望,只見細麻布在那裡,他便離開了,對發生的事大惑不解。

耶穌的顯現

13同一天,有兩個門徒前往離耶路撒冷十一公里的以馬忤斯村, 14一路談論著最近發生的一切事。 15正談論的時候,耶穌走過來和他們同行。 16可是,他們認不出耶穌。

17耶穌問他們:「你們一路上在談論什麼?」

他們停下腳步,滿面愁容, 18其中一個叫革流巴的說:「難道在耶路撒冷作客的人中,只有你不知道近日發生的大事嗎?」

19耶穌問:「什麼事?」

他們說:「就是拿撒勒人耶穌的事。祂本來是個先知,在上帝和百姓面前言談舉止充滿力量。 20我們的祭司長和官長卻把祂押去判了死刑,釘在十字架上。

21「我們一直希望祂就是要拯救以色列的那位。還有,今天是事發後的第三天, 22我們當中有幾位婦女一早到耶穌的墳墓, 23發現耶穌的遺體不見了,回來說天使曾向她們顯現並告訴她們耶穌已經復活了。

24「後來我們有幾個人親自去墳墓察看,果然像她們所說的,耶穌的遺體不見了。」

25耶穌對他們說:「無知的人啊!為什麼遲遲不肯相信先知的話呢? 26基督豈不是要先這樣受害,然後進入祂的榮耀嗎?」

27耶穌接著從摩西和眾先知的記載開始,把有關自己的經文都向他們講解明白。

28快到以馬忤斯村時,耶穌好像還要繼續前行。 29他們極力挽留祂,說:「天快黑了,時候不早了,跟我們一同住宿吧。」耶穌就和他們一起進村住下。

30吃飯的時候,耶穌拿起餅來,祝謝後,掰開遞給他們。 31忽然他們眼睛明亮了,認出是耶穌。耶穌很快從他們眼前消失了。

32二人彼此議論說:「一路上祂和我們說話、為我們解釋聖經的時候,我們心裡不是很火熱嗎?」 33二人馬上趕回耶路撒冷,看到十一位使徒及其同伴正聚在一起談論: 34「主真的復活了,祂向西門顯現了。」

35二人也把路上發生的事以及掰餅時認出主的經過述說了一遍。

36正說的時候,耶穌出現在他們中間,說:「願你們平安!」 37他們又驚又怕,以為是看見了鬼魂。

38耶穌說:「你們為什麼憂心忡忡?為什麼心存疑惑呢? 39你們看我的手和腳,就知道真的是我。來摸摸看,鬼魂沒有骨和肉,你們看!我有。」 40說完,便伸出手和腳給他們看。

41門徒又驚又喜,半信半疑。耶穌問:「你們這裡有吃的嗎?」 42他們便給祂一片烤魚, 43祂接過魚來在他們面前吃了。

44耶穌對他們說:「我跟你們在一起的時候曾經說過,摩西的律法書、先知的書以及詩篇裡有關我的記載都要應驗。」 45於是,耶穌開啟了他們的心竅,使他們明白這些經文, 46又對他們說:「聖經上說,基督必受害,然後在第三天從死裡復活, 47人們要奉祂的名傳揚悔改、赦罪的福音,從耶路撒冷一直傳遍萬國。

48「你們是這些事的見證人, 49我要把我父所應許的賜給你們。不過,你們要留在城裡,直到你們得到天上來的能力。」

耶穌升天

50耶穌帶著門徒來到伯大尼附近,舉起雙手為他們祝福。 51正祝福的時候,祂就離開了他們,被接到天上去了。 52門徒都敬拜祂,然後歡歡喜喜地回到耶路撒冷53他們常在聖殿裡讚美上帝。