Luka 23 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 23:1-56

Yesu Apelekwa Kwa Pilato

(Mathayo 27:1-14; Marko 15:1-5; Yohana 18:28-38)

123:1 Mk 15:1; Yn 18:28Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato. 223:2 Lk 20:22; Yn 18:28Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo,23:2 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. mfalme.”

323:3 Mt 27:11; 1Tim 6:13Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”

Yesu akajibu, “Wewe wasema.”

423:4 1Tim 6:13; 2Kor 5:21Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”

523:5 Mk 1:14Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”

Yesu Apelekwa Kwa Herode

623:6 Lk 22:59Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?” 723:7 Mk 14:1; Lk 3:1Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.

823:8 Lk 9:9Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha. 923:9 Mk 14:61Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote. 10Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana. 1123:11 Mk 15:17-19; Yn 19:2-3Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato. 1223:12 Mdo 4:27Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.

Yesu Ahukumiwa Kifo

(Mathayo 27:15-26; Marko 15:6-15; Yohana 18:39–19:16)

1323:13 Mt 27:23; Mk 15:14; Yn 18:38Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu, 1423:14 Lk 23:1, 2, 4akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake. 15Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo. 1623:16 Mdo 16:37; 2Kor 11:23-24Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [ 1723:17 Mt 27:15; Mk 15:6; Yn 18:39Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]

1823:18 Mdo 3:13-14Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!” 19(Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)

20Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena. 21Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”

2223:22 Lk 23:18Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”

23Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda. 2423:24 Mt 27:26; Mk 15:15; Yn 19:17Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe. 25Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.

Kusulubiwa Kwa Yesu

(Mathayo 27:32-44; Marko 15:21-32; Yohana 19:17-27)

2623:26 Mt 27:32; Mk 15:21; Yn 19:17Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu. 2723:27 Lk 8:52Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea. 2823:28 Lk 19:41-44; 21:23-24Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu. 2923:29 Mt 24:19Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’ 3023:30 Hos 10:8; Ufu 6:16Ndipo

“ ‘wataiambia milima, “Tuangukieni!”

na vilima, “Tufunikeni!” ’

3123:31 Eze 20:47Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”

3223:32 Isa 53:12; Mt 27:38Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe. 33Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto. 3423:34 Mt 11:25; 5:44; Za 22:18Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.

3523:35 Za 22:17; Isa 42:1; Zek 12:10; Mt 27:39; Mk 15:29Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”

3623:36 Za 22:7; 69:21; Mt 27:48Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe, 3723:37 Lk 4:3, 9na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”

3823:38 Mt 2:2Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi.

Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.

3923:39 Mt 27:44; Mk 15:32Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”

40Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo? 4123:41 Lk 23:4Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”

4223:42 Mt 16; 27Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”

4323:43 1Kor 12:3-4; Ufu 2:7Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”23:43 Paradiso maana yake bustani nzuri, hapa ina maana mahali zinapokwenda roho za wacha Mungu, yaani watakatifu.

Kifo Cha Yesu

(Mathayo 27:45-56; Marko 15:33-41; Yohana 19:28-30)

4423:44 Amo 8:9Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa, 4523:45 Kut 26:31-33; Ebr 3:8; 10:19-20kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili. 4623:46 Mt 27:50; Za 31:5; 1Pet 2:23; Yn 19:30Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.

4723:47 Mt 9:8Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.” 4823:48 Lk 18:13Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao. 4923:49 Lk 8:2; Za 38:11Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.

Maziko Ya Yesu

(Mathayo 27:57-61; Marko 15:42-47; Yohana 19:38-42)

5023:50 Mt 27:59; Mk 15:46Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,23:50 Baraza la Wayahudi hapa ina maana ya Sanhedrin ambalo lilikuwa ndilo baraza la juu kabisa la utawala wa Kiyahudi, lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. 5123:51 Lk 2:25, 38lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa. 52Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. 53Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado. 5423:54 Mt 27:62Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.

5523:55 Lk 8:2; Mk 15:47Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa. 5623:56 Mk 16:1; Lk 24:1; Kut 12:16; 20:11Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.

Persian Contemporary Bible

لوقا 23:1-56

عيسی به مرگ محكوم می‌شود

1آنگاه اعضای شورا همگی برخاسته، عيسی را به حضور «پيلاطوس»، فرماندار رومی يهوديه بردند، 2و شكايات خود را عليه او عنوان كرده، گفتند: «اين شخص مردم را تحريک می‌كند كه به دولت روم ماليات ندهند، و ادعا می‌كند كه مسيح، يعنی پادشاه ماست.»

3پيلاطوس از عيسی پرسيد: «آيا تو مسيح، پادشاه يهود هستی؟»

عيسی جواب داد: «بلی، چنين است كه می‌گويی.»

4پيلاطوس رو به كاهنان اعظم و جماعت كرد و گفت: «خوب، اينكه جرم نيست!»

5ايشان پافشاری نموده، گفتند: «اما او در سراسر يهوديه، از جليل تا اورشليم، هر جا می‌رود، به ضد دولت روم آشوب بپا می‌كند.»

6پيلاطوس پرسيد: «مگر او اهل جليل است؟»

7وقتی از اين امر اطمينان حاصل كرد، دستور داد او را نزد هيروديس ببرند، زيرا ايالت جليل جزو قلمرو حكومت هيروديس بود. اتفاقاً هيروديس در آن روزها، به مناسبت عيد، در اورشليم به سر می‌برد. 8هيروديس از ديدن عيسی بسيار شاد شد، چون درباره او خيلی چيزها شنيده بود و اميدوار بود كه با چشم خود يكی از معجزات او را ببيند. 9او سؤالات گوناگونی از عيسی كرد، اما هيچ جوابی نشنيد.

10در اين ميان، كاهنان اعظم و ديگر علمای دين حاضر شدند و عيسی را به باد تهمت گرفتند. 11هيروديس و سربازانش نيز او را مسخره كرده، مورد اهانت قرار دادند، و لباسی شاهانه به او پوشاندند و نزد پيلاطوس باز فرستادند. 12همان روز پيلاطوس و هيروديس، دشمنی خود را كنار گذارده، با يكديگر صلح كردند.

13آنگاه پيلاطوس، كاهنان اعظم و سران يهود و مردم را فرا خواند 14و به ايشان گفت: «شما اين مرد را به اتهام شورش به ضد حكومت روم نزد من آورديد. من در حضور خودتان از او بازجويی كردم و متوجه شدم كه اتهامات شما عليه او بی‌اساس است. 15هيروديس نيز به همين نتيجه رسيد و به همين علت او را نزد ما پس فرستاد. اين مرد كاری نكرده است كه مجازاتش اعدام باشد. 16بنابراين، فقط دستور می‌دهم شلاقش بزنند، و بعد آزادش می‌كنم.» 17(طبق رسم، در هر عيد پِسَح يک زندانی آزاد می‌شد.)

18اما مردم يكصدا فرياد برآورده، گفتند: «اعدامش كن و ”باراباس“ را برای ما آزاد كن!» 19(باراباس به جرم شورش و خونريزی در اورشليم، زندانی شده بود.) 20پيلاطوس بار ديگر با مردم سخن گفت، چون می‌خواست عيسی را آزاد كند. 21اما ايشان بلندتر فرياد زدند: «مصلوبش كن! مصلوبش كن!»

22باز برای بار سوم پيلاطوس گفت: «چرا؟ مگر او مرتكب چه جنايتی شده است؟ من دليلی ندارم كه به مرگ محكومش كنم. دستور می‌دهم شلاقش بزنند و آزادش می‌كنم.» 23اما مردم با صدای بلند فرياد می‌زدند و با اصرار می‌خواستند كه او مصلوب شود؛ و سرانجام فريادهای ايشان غالب آمد، 24و پيلاطوس به درخواست ايشان، حكم اعدام عيسی را صادر كرد. 25سپس، باراباس را كه به علت شورش و خونريزی در حبس بود، آزاد كرد و عيسی را تحويل داد تا طبق تقاضای ايشان، اعدام شود.

مصلوب شدن عيسی

26سربازان رومی عيسی را بردند. هنگامی كه می‌رفتند، مردی به نام «شمعون قيروانی» را كه از مزرعه به شهر باز می‌گشت، مجبور كردند كه صليب عيسی را بردارد و به دنبال او ببرد. 27جمعيتی انبوه در پی او به راه افتادند و زنان بسياری نيز در ميان آنان برای او گريه و ماتم می‌كردند و به سينه خود می‌زدند.

28عيسی رو به اين زنان كرد و گفت: «ای دختران اورشليم، برای من گريه نكنيد؛ به حال خود و فرزندانتان گريه كنيد! 29چون روزهايی می‌آيد كه مردم خواهند گفت: خوشا به حال زنان بی‌اولاد؛ 30و آرزو خواهند كرد كه کوهها و تپه‌ها بر ايشان افتاده، پنهانشان كنند. 31زيرا اگر شخص بی‌گناهی مانند من، اين گونه مجازات شود، مجازات افراد خطاكار و گناهكار، همچون نسل شما، چه خواهد بود؟!»

32‏-33دو جنايتكار را بردند تا با او اعدام كنند. نام محل اعدام، «كاسهٔ سر» بود. در آنجا هر سه را به صليب ميخكوب كردند، عيسی در وسط و آن دو جنايتكار در دو طرف او. 34در چنين حالی، عيسی فرمود: «ای پدر، اين مردم را ببخش، زيرا كه نمی‌دانند چه می‌كنند.»

سربازان رومی لباسهای عيسی را به حكم قرعه ميان خود تقسيم كردند. 35مردم ايستاده بودند و تماشا می‌كردند. سران قوم نيز ايستاده، به او می‌خنديدند و مسخره‌كنان می‌گفتند: «برای ديگران معجزات زيادی انجام داد؛ حال اگر واقعاً مسيح و برگزيده خداست، خود را نجات دهد!»

36سربازان نيز او را مسخره نموده، شراب ترشيده خود را به او تعارف می‌كردند، 37و می‌گفتند: «اگر تو پادشاه يهود هستی، خود را نجات بده!» 38بالای سر او، بر صليب، تخته‌ای كه تقصيرنامهٔ او بود، كوبيدند. روی آن به زبانهای يونانی، رومی و عبری نوشته شده بود: «اينست پادشاه يهود!»

39يكی از آن دو جنايتكار كه در كنار عيسی مصلوب شده بود، به طعنه به او گفت: «اگر تو مسيح هستی، چرا خودت و ما را نجات نمی‌دهی؟»

40‏-41اما آن ديگری، او را سرزنش كرد و گفت: «حتی در حال مرگ هم از خدا نمی‌ترسی؟ ما حقمان است كه بميريم، چون گناهكاريم. اما از اين شخص، يک خطا هم سر نزده است.» 42سپس رو به عيسی كرد و گفت: «ای عيسی، وقتی ملكوت خود را آغاز كردی، مرا هم به یاد آور!»

43عيسی جواب داد: «خاطرجمع باش كه تو همين امروز با من در بهشت خواهی بود!»

مرگ عيسی

44به هنگام ظهر، برای مدت سه ساعت، تاريكی همه جا را فرا گرفت، 45و نور خورشيد از تابيدن باز ايستاد. آنگاه پرده ضخيمی كه در جايگاه مقدس خانه خدا آويزان بود، دو تكه شد.

46سپس عيسی با صدايی بلند گفت: «ای پدر، روح خود را به دستهای تو می‌سپارم.» اين را گفت و جان سپرد.

47افسر رومی كه مأمور اجرای حكم بود، وقتی اين صحنه را ديد خدا را ستايش كرد و گفت: «اين مرد حقيقتاً بی‌گناه بود!»

48كسانی كه برای تماشا گرد آمده بودند، وقتی اين اتفاقات را ديدند، اندوهگين و سينه‌زنان، به خانه‌های خود بازگشتند. 49در اين ميان، دوستان عيسی و زنانی كه از جليل به دنبال او آمده بودند، دورتر ايستاده، اين وقايع را می‌نگريستند.

تدفين جسد عيسی

50‏-52آنگاه شخصی به نام يوسف، اهل رامهٔ يهوديه، نزد پيلاطوس رفت و اجازه خواست كه جسد عيسی را دفن كند. يوسف مردی خداشناس بود و انتظار آمدن مسيح را می‌كشيد. در ضمن، او يكی از اعضای شورای عالی يهود بود، اما با تصميمات و اقدام ساير اعضای شورا موافق نبود. 53او پس از كسب اجازه، جسد عيسی را از بالای صليب پايين آورد، آن را در كفن پيچيد و در قبر تازه‌ای گذاشت كه قبلاً كسی در آن گذاشته نشده بود. اين قبر كه شبيه يک غار كوچک بود، در دامنه تپه‌ای در داخل يک صخره، تراشيده شده بود. 54تمام كار كفن و دفن، همان عصر جمعه انجام شد. يهوديان كارهای روز تعطيل شنبه را عصر روز جمعه تدارک می‌ديدند.

55زنانی كه از جليل به دنبال عيسی آمده بودند، همراه يوسف رفتند و محل قبر را ديدند و مشاهده كردند كه جسد عيسی چگونه در آن گذاشته شد. 56سپس به خانه بازگشتند و دارو و عطريات تهيه كردند كه به رسم آن زمان، به جسد بمالند تا زود فاسد نشود. اما وقتی دارو آماده شد، ديگر روز شنبه فرا رسيده بود. پس مطابق قانون مذهبی يهود، در آن روز به استراحت پرداختند.