Luka 18 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 18:1-43

Mfano Wa Mjane Asiyekata Tamaa

118:1 Rum 1:10; Kol 4:2Kisha Yesu akawapa wanafunzi wake mfano ili kuwaonyesha kuwa yawapasa kuomba pasipo kukata tamaa. 2Akawaambia, “Katika mji mmoja alikuwepo hakimu ambaye hakumwogopa Mungu wala kumjali mtu. 318:3 Isa 1:17Katika mji huo alikuwako mjane mmoja ambaye alikuwa akija kwake mara kwa mara akimwomba, ‘Tafadhali nipatie haki kati yangu na adui yangu.’

4“Kwa muda mrefu yule hakimu alikataa. Lakini hatimaye akasema moyoni mwake, ‘Ijapokuwa simwogopi Mungu wala simjali mwanadamu, 518:5 Lk 11:8lakini kwa kuwa huyu mjane ananisumbuasumbua, nitahakikisha amepata haki yake ili asiendelee kunichosha kwa kunijia mara kwa mara!’ ”

618:6 Lk 7:13Bwana akasema, “Sikilizeni asemavyo huyu hakimu dhalimu. 718:7 Za 88:1; Ufu 6:10Je, Mungu hatawatendea haki wateule wake wanaomlilia usiku na mchana? Je, atakawia kuwasaidia? 818:8 Mt 8:20; 16:27Ninawaambia, atawapatia haki upesi. Lakini je, Mwana wa Adamu atakapokuja ataikuta imani duniani?”

Mfano Wa Farisayo Na Mtoza Ushuru

918:9 Lk 16:15; Isa 65:5Yesu akatoa mfano huu kwa wale waliojiamini kuwa wao ni wenye haki na kuwadharau wengine: 1018:10 Mdo 3:1“Watu wawili walikwenda Hekaluni kusali, mmoja wao alikuwa Farisayo na mwingine alikuwa mtoza ushuru. 1118:11 Za 135:2; Isa 1; 15; 58:2; Ufu 3:17Yule Farisayo, akasimama, akasali hivi na kuomba kwake mwenyewe: ‘Mungu, nakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wengine ambao ni wanyangʼanyi, wadhalimu, na wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru. 1218:12 Isa 58:3; Mt 9:14; Mal 3:8; Lk 11:42Mimi nafunga mara mbili kwa juma, na natoa sehemu ya kumi ya mapato yangu.’

1318:13 Isa 66:2; Lk 23:48; 5:32; 1Tim 1:15“Lakini yule mtoza ushuru akasimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua uso wake kutazama mbinguni, bali alijipigapiga kifuani na kusema: ‘Mungu, nihurumie, mimi mwenye dhambi.’

1418:14 Mt 23:12; Lk 14:11“Nawaambia, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amehesabiwa haki mbele za Mungu zaidi ya yule Farisayo. Kwa maana yeyote ajikwezaye atashushwa, na yeyote ajishushaye atakwezwa.”

Yesu Awabariki Watoto Wadogo

(Mathayo 19:13-15; Marko 10:13-16)

1518:15 Mt 19:13; Lk 10:13Pia, watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wachanga ili awaguse. Wanafunzi wake walipoona hivyo, wakawakemea. 1618:16 1Kor 14:20; 1Pet 2:2Lakini Yesu akawaita wale watoto waje kwake, akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa. 1718:17 Mt 11:25; 18:3Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”

Mtawala Tajiri

(Mathayo 19:16-30; Marko 10:17-31)

1818:18 Mt 19:16-29; Mk 10:17-3018:18 Lk 10:25Mtawala mmoja akamuuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”

19Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake. 2018:20 Kut 20:12-16; Rum 13:9Unazijua amri: ‘Usizini, usiue, usiibe, usishuhudie uongo, waheshimu baba yako na mama yako.’ ”

21Akajibu, “Amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”

2218:22 Mdo 2:45; Mt 6:20Yesu aliposikia haya, akamwambia, “Bado kuna jambo moja ulilopungukiwa. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”

23Aliposikia jambo hili, alisikitika sana kwa maana alikuwa mtu mwenye mali nyingi. 2418:24 Mit 11:28Yesu akamtazama, akasema, “Tazama jinsi ilivyo vigumu kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu! 25Hakika ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”

26Wale waliosikia haya wakauliza, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”

2718:27 Mt 19:26Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa wanadamu yanawezekana kwa Mungu.”

2818:28 Mt 4:19Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha vyote tulivyokuwa navyo tukakufuata!”

2918:29 Kum 33:9Yesu akajibu, “Amin, nawaambia, hakuna hata mtu aliyeacha nyumba yake, au mke, au ndugu, au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu 3018:30 Mt 12:32; 25:46ambaye hatapewa mara nyingi zaidi ya hivyo katika maisha haya, na hatimaye kupata uzima wa milele ujao.”

Yesu Atabiri Kifo Chake Mara Ya Tatu

(Mathayo 20:17-19; Marko 10:32-34)

3118:31 Lk 9:51; Za 22; Mt 8:20Yesu akawachukua wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na kila kitu kilichoandikwa na manabii kumhusu Mwana wa Adamu kitatimizwa. 3218:32 Lk 23:1; Mt 16:21; Mdo 2:23Kwa kuwa atatiwa mikononi mwa watu wasiomjua Mungu, nao watamdhihaki, watamtukana na kumtemea mate, watampiga mijeledi na kumuua. 3318:33 Mt 16:21Naye siku ya tatu atafufuka.”

3418:34 Mk 9:32; Lk 9:45Wanafunzi wake hawakuelewa mambo haya, kwa kuwa maana yake ilikuwa imefichika kwao, nao hawakujua Yesu alikuwa anazungumzia nini.

Yesu Amponya Kipofu Karibu Na Yeriko

(Mathayo 20:29-34; Marko 10:46-52)

3518:35 Lk 19:1-418:35 Mt 20:29-34; Mk 10:46-52Yesu alipokuwa anakaribia Yeriko, kipofu mmoja alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada. 36Kipofu huyo aliposikia umati wa watu ukipita, akauliza, “Kuna nini?” 3718:37 Mt 9:27; 17:15; Lk 18:13Wakamwambia, “Yesu wa Nazareti anapita.”

3818:38 Lk 18:39; Mt 9:27; 17:15; Lk 18:13Akapaza sauti, akasema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”

3918:39 Lk 18:38Wale waliokuwa wametangulia mbele wakamkemea, wakamwambia akae kimya. Lakini yeye akapaza sauti zaidi, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”

40Yesu akasimama, akawaamuru wamlete huyo mtu kwake. Alipokaribia, Yesu akamuuliza, 41“Unataka nikufanyie nini?”

Akajibu, “Bwana, nataka kuona.”

4218:42 Mt 9:22Yesu akamwambia, “Basi upate kuona. Imani yako imekuponya.” 4318:43 Mt 9:8; Lk 13:17Akapata kuona saa ile ile, akamfuata Yesu, huku akimsifu Mungu. Watu wote walipoona mambo hayo, nao wakamsifu Mungu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

路加福音 18:1-43

恆心禱告

1耶穌講了一個比喻來教導門徒要常常禱告,不要灰心。

2祂說:「某城有一位既不敬畏上帝也不尊重人的審判官。 3那城裡有一位寡婦常常來哀求這位審判官,說,『求你為我伸冤,懲辦我的對頭。』 4審判官總是充耳不聞,但後來心裡想,『雖然我不怕上帝,也不在乎人, 5可是這寡婦一直來煩我,還是替她伸冤好了,免得她再來煩我!』」

6主接著說:「你們聽,這不義的審判官尚且這麼說, 7難道上帝聽到祂揀選的人晝夜呼求,不替他們伸冤嗎?難道祂會一直耽延不理嗎? 8我告訴你們,祂必很快為他們伸冤。不過當人子來的時候,在世上找得到有信心的人嗎?」

兩種禱告

9耶穌對那些自以為義、藐視別人的人講了一個比喻: 10「有兩個人到聖殿裡禱告,一個是法利賽人,一個是稅吏。 11法利賽人站在那裡自言自語地禱告說,『上帝啊!我感謝你,因為我不像別人那樣勒索、不義、通姦,也不像這稅吏。 12我每週禁食兩次,奉獻全部收入的十分之一。』

13「但那稅吏卻遠遠地站著,連頭也不敢抬起來,捶著胸說,『上帝啊,求你憐憫我這個罪人!』

14「我告訴你們,二人回家後,被上帝算為義的是稅吏而不是法利賽人,因為自高的人必遭貶抑,謙卑的人必得尊榮。」

祝福孩子

15有許多人把嬰孩帶來要讓耶穌摸一摸他們,為他們祝福,門徒看見,就責備這些人。 16耶穌卻招呼他們過來,並對門徒說:「讓小孩子到我這裡來,不要阻止他們,因為上帝的國屬於這樣的人。 17我實在告訴你們,人若不像小孩子一樣接受上帝的國,絕不能進去。」

富豪求問永生

18一位官長問耶穌:「良善的老師,我該做什麼才能承受永生?」

19耶穌說:「你為什麼稱呼我『良善的老師』呢?只有上帝是良善的。 20你知道『不可通姦,不可殺人,不可偷盜,不可作偽證,要孝敬父母』這些誡命」。

21那人說:「我從小就遵行這些誡命。」

22耶穌聽了就對他說:「你還有一件事沒有做,就是變賣你所有的產業,分給窮人,你必有財寶存在天上,然後你還要來跟從我。」 23那人聽了,極其憂愁,因為他非常富有。

24耶穌見狀,就說;「有錢人進上帝的國真難啊! 25駱駝穿過針眼比有錢人進上帝的國還容易呢!」

26聽見的人就問:「這樣,誰能得救呢?」

27耶穌回答說:「對人而言,這不可能,但對上帝而言,凡事都可能。」

28彼得說:「你看!我們已經撇下一切來跟從你了。」

29耶穌說:「我實在告訴你們,任何人為了上帝的國而撇下房屋、妻子、弟兄、父母或兒女, 30今世必得百倍的獎賞,來世必得永生。」

再次預言受害和復活

31耶穌把十二使徒帶到一邊,對他們說:「你們要留意,我們現在前往耶路撒冷,先知書上有關人子的記載都要應驗, 32人子將被交在外族人的手裡,被他們嘲弄、虐待、吐唾沫、 33鞭打和殺害,但第三天祂必復活。」 34使徒卻一點也不明白,因為這番話的含意是隱藏的,他們聽不明白。

治癒耶利哥的瞎子

35耶穌快到耶利哥城的時候,有一個瞎子坐在路旁討飯。 36他聽見許多人經過,就詢問是怎麼回事。 37有人告訴他是拿撒勒人耶穌經過此地, 38他就高聲呼喊:「大衛的後裔耶穌啊,可憐我吧!」

39走在前面的人責備他,讓他安靜,但他反而叫得更大聲:「大衛的後裔啊,可憐我吧!」

40耶穌停下腳步,命人把他帶過來,然後問他: 41「你要我為你做什麼?」

他說:「主啊!我想能夠看見。」

42耶穌對他說:「你看見吧!你的信心救了你。」 43他立刻得見光明,並跟隨耶穌,一路讚美上帝。目睹這事的人也都讚美上帝。