Luka 10 – NEN & SZ-PL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 10:1-42

Yesu Awatuma Wale Sabini Na Wawili

110:1 Lk 7:13; 9:1-2, 51-52; Mk 6:7; Mt 10:1Baada ya hayo, Bwana akawachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawili wawili katika kila mji na kila sehemu aliyokusudia kwenda baadaye. 210:2 Mt 9:37-38; Yn 4:35Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno. 310:3 Mt 10:16Haya! nendeni. Ninawatuma kama wana-kondoo katikati ya mbwa mwitu. 410:4 Lk 9:3-5; 2Fal 4:29Msichukue mkoba, wala mfuko, wala viatu, na msimsalimu mtu yeyote njiani.

510:5 Mt 4:12“Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza semeni, ‘Amani iwe kwenu.’ 6Kama kuna mtu wa amani humo, basi amani yenu itakuwa juu yake. La sivyo, itawarudia. 710:7 Mt 10:10; 1Kor 9:14Kaeni katika nyumba hiyo, mkila na kunywa kile watakachowapa, kwa sababu kila mtendakazi anastahili malipo yake. Msihamehame kutoka nyumba hadi nyumba.

810:8 1Kor 10:27“Mkienda katika mji na watu wake wakawakaribisha, kuleni chochote kiwekwacho mbele yenu, 910:9 Mt 3:2; 10:7waponyeni wagonjwa waliomo na waambieni: ‘Ufalme wa Mungu umekaribia.’ 10Lakini mkiingia katika mji, nao hawakuwakaribisha, tokeni mwende katika barabara zake mkaseme: 1110:11 Mt 10:14; Mk 6:11‘Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu, tunayakungʼuta dhidi yenu. Lakini mjue kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.’ 1210:12 Mt 10:15; 11:24Ninawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ile kuliko mji ule.

Onyo Kwa Miji Isiyotubu

(Mathayo 11:20-24)

1310:13 Lk 6:24-26; Ufu 11:3“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani, kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu. 14Lakini itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi. 1510:15 Mt 4:13; Mwa 11:4; Kum 1:28; Isa 14:13; Yer 51:53Nawe, Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu.”

1610:16 Mt 10:40; Yn 13:20“Yeye awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi; naye awakataaye ninyi amenikataa mimi. Lakini yeye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.”

1710:17 Mk 16:17Wale sabini na wawili wakarudi kwa furaha, na kusema, “Bwana, hata pepo wachafu wanatutii kwa jina lako.”

1810:18 Mt 4:10; Isa 14:12; Ufu 9:1Yesu akawaambia, “Nilimwona Shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme wa radi. 1910:19 Mk 16:18; Mdo 28:3-5Tazama nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na juu ya nguvu zote za adui; wala hakuna kitu chochote kitakachowadhuru. 2010:20 Dan 12:1; Flp 4:3Basi, msifurahi kwa kuwa pepo wachafu wanawatii, bali furahini kwa kuwa majina yenu yameandikwa mbinguni.”

Yesu Anashangilia

(Mathayo 11:25-27; 13:16-17)

2110:21 1Kor 1:26-29Wakati huo Yesu akashangilia katika Roho Mtakatifu, akasema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo. Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.

2210:22 Mt 28:18; Yn 1:18“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu. Hakuna mtu amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ni nani ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.”

2310:23 Mt 13:16, 17 Basi Yesu akawageukia wanafunzi wake akanena nao faraghani, akawaambia, “Heri macho yanayoona yale mambo mnayoyaona. 2410:24 1Pet 1:10-12Kwa maana nawaambia, manabii wengi na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.”

Mfano Wa Msamaria Mwema

2510:25 Mt 19:16; Lk 18:18Wakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Yesu, akamuuliza, “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”

26Yesu akamjibu, “Imeandikwaje katika Sheria? Kwani unasoma nini humo?”

2710:27 Kum 6:5; Law 19:18; Mt 5:43Akajibu, “ ‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote’; tena, ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’ ”

2810:28 Law 18; 5; Rum 7:10Yesu akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”

2910:29 Lk 16:15Lakini yule mtaalamu wa sheria, akitaka kujionyesha kuwa mwenye haki, akamuuliza Yesu, “Jirani yangu ni nani?”

30Yesu akamjibu akasema, “Mtu mmoja alikuwa akiteremka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko, naye akaangukia mikononi mwa wanyangʼanyi. Wakampiga, wakaondoka, wakamwacha akiwa karibu kufa. 3110:31 Law 21:1-3Kuhani mmoja alikuwa akipitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani. 32Vivyo hivyo, Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine, akamwacha hapo barabarani 3310:33 Mt 10:5Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri alipomwona, alimhurumia. 34Akaenda alipokuwa na akasafisha majeraha yake kwa divai na mafuta, kisha akayafunga. Ndipo akampandisha kwenye punda wake, akampeleka mpaka kwenye nyumba ya wageni na kumtunza. 35Kesho yake, yule Msamaria akachukua dinari mbili10:35 Dinari mbili ni sawa na mshahara wa kibarua wa siku mbili. akampa yule mwenye nyumba ya wageni na kusema, ‘Mtunze, nami nirudipo nitakulipa gharama yoyote ya ziada uliyotumia kwa ajili yake.’

36“Ni yupi basi miongoni mwa hawa watatu wewe unadhani ni jirani yake yule mtu aliyeangukia mikononi mwa wanyangʼanyi?”

37Yule mtaalamu wa sheria akajibu, “Ni yule aliyemhurumia.”

Ndipo Yesu akamwambia, “Nenda, ukafanye vivyo hivyo.”

Yesu Awatembelea Martha Na Maria

3810:38 Yn 11:1; 12:2-3Ikawa Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakienda Yerusalemu, akaingia kwenye kijiji kimoja ambapo mwanamke mmoja aliyeitwa Martha alimkaribisha nyumbani kwake. 3910:39 Lk 8:35Martha alikuwa na mdogo wake aliyeitwa Maria, ambaye aliketi chini miguuni mwa Bwana akisikiliza yale aliyokuwa akisema. 4010:40 Mk 4:38Lakini Martha alikuwa akihangaika na maandalizi yote yaliyokuwa yafanyike. Martha akaja kwa Yesu na kumuuliza, “Bwana, hujali kwamba ndugu yangu ameniachia kazi zote mwenyewe? Basi mwambie anisaidie.”

4110:41 Mt 6:25-34; Lk 12:11, 22Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, mbona unasumbuka na kuhangaika na mengi? 4210:42 Za 27:4Lakini kunahitajika kitu kimoja tu. Maria amechagua kile kilicho bora, wala hakuna mtu atakayemwondolea.”

Słowo Życia

Łukasza 10:1-42

Jezus posyła siedemdziesięciu

1Potem Pan wybrał siedemdziesięciu uczniów i wysłał ich po dwóch do miast i wiosek, które zamierzał odwiedzić. 2—Żniwo jest wielkie—mówił im—a tak mało pracujących! Proście więc gospodarza, aby posłał więcej pracowników na żniwa. 3Idźcie! Posyłam was jak owce między wilki. 4Nie bierzcie ze sobą pieniędzy ani torby podróżnej, ani nawet zapasowego obuwia. Wędrując, nie traćcie ani chwili, nawet na tradycyjne przywitanie się z napotkanymi ludźmi. 5Gdy odwiedzicie jakiś dom, życzcie wszystkim pokoju. 6Jeśli to pobożni ludzie, odpowiedzą wam tym samym. Jeśli nie—pokój pozostanie z wami. 7Nie zmieniajcie miejsca pobytu, ale pozostańcie w jednym domu aż do opuszczenia tej miejscowości. Jedzcie tam i pijcie bez skrępowania, gdyż jako robotnicy macie prawo do zapłaty. 8W jakimkolwiek mieście was przyjmą, korzystajcie z ich gościnności. 9Uzdrawiajcie chorych i mówcie: „Nadchodzi królestwo Boże!”. 10Lecz jeśli gdzieś nie zostaniecie przyjęci, stańcie na rynku i powiedzcie: 11„Nawet kurz waszego miasta strząsamy z naszych stóp. Wiedzcie, że odrzucacie królestwo Boże, które było tak blisko was”. 12Mówię wam, że w dniu sądu grzesznym mieszkańcom Sodomy i Gomory będzie lżej niż temu miastu.

13Następnie Jezus dodał:

—Marny wasz los, Korozain i Betsaido! Gdyby cuda, których u was dokonałem, wydarzyły się wśród grzesznych mieszkańców Tyru i Sydonu, już dawno by się opamiętali, siedząc w worze pokutnym i popiele. 14Wiedzcie, że w dniu sądu mieszkańcom Tyru i Sydonu będzie łatwiej niż wam! 15A ty, Kafarnaum? Chcesz być wywyższone aż do nieba? Upadniesz aż do piekła!

16Potem powiedział do uczniów:

—Kto was słucha, Mnie słucha. A kto się od was odwraca, odrzuca także Mnie, a tym samym Ojca, który Mnie posłał.

17Po pewnym czasie powróciło siedemdziesięciu uczniów i z radością oznajmiło:

—Panie, ze względu na Ciebie nawet złe duchy były nam posłuszne!

18—Tak, widziałem szatana spadającego z nieba z szybkością błyskawicy!—rzekł Jezus. 19—Dałem wam władzę nad wszelką jego mocą, abyście mogli chodzić po wężach i skorpionach, nie doznając żadnej krzywdy. 20Nie fascynujcie się jednak tym, że złe duchy są wam posłuszne. Cieszcie się raczej z tego, że wasze imiona wpisane są do księgi obywateli nieba.

21Następnie, napełniony radością Ducha Świętego, Jezus powiedział:

—Uwielbiam Cię, Ojcze, Panie nieba i ziemi! Ty ukryłeś swoją prawdę przed mędrcami i znawcami, a objawiłeś ją prostym ludziom. Tego właśnie pragnąłeś!

22—Ojciec powierzył Mi całą prawdę—wyjaśniał Jezus zebranym. —Nikt nie zna Mnie, Syna, tylko mój Ojciec. I nikt nie zna mojego Ojca, tylko Ja, Syn oraz ten, komu zechcę Go objawić.

23Jakiś czas później, gdy byli już sami, rzekł do uczniów:

—Bóg was ogromnie wyróżnił, pozwalając wam to wszystko widzieć. 24W przeszłości wielu proroków i władców pragnęło zobaczyć i usłyszeć to, co wy, ale nie mogli.

Przypowieść o Samarytaninie

25Pewien przywódca religijny przyszedł do Jezusa i zadał Mu podchwytliwe pytanie:

—Nauczycielu, co mam czynić, aby otrzymać życie wieczne?

26—Co na ten temat mówi Prawo Mojżesza? Co w nim czytasz?—zapytał Jezus.

27—„Kochaj twojego Pana i Boga całym sercem, całą duszą, z całych swoich sił oraz całym umysłem, a bliźnich kochaj tak, jak kochasz samego siebie!”—odpowiedział.

28—Dobrze powiedziałeś—odrzekł Jezus. —Tak postępuj, a będziesz żył wiecznie!

29—A kto jest moim bliźnim?—zapytał rozmówca, chcąc się usprawiedliwić.

30Wtedy Jezus opowiedział mu następującą historię:

—Pewnego człowieka, idącego z Jerozolimy do Jerycha, napadli bandyci. Zdarli z niego odzież, pobili, okradli i bliskiego śmierci zostawili przy drodze. 31Przypadkiem przechodził tamtędy kapłan. Zauważył biedaka, lecz przeszedł na drugą stronę drogi i ominął go. 32Tak samo postąpił lewita, dozorca świątyni—po prostu minął go. 33Przejeżdżał też tamtędy człowiek z pogardzanej przez wszystkich Samarii. Podszedł do rannego, popatrzył i zrobiło mu się go żal. 34Obmył jego rany winem i oliwą, przewiązał je, a potem posadził rannego na swojego osła i przewiózł go do zajazdu, gdzie dalej się nim zajmował. 35Następnego dnia wręczył gospodarzowi sporą sumę pieniędzy i poprosił: „Zaopiekuj się nim, a jeśli wydasz więcej—pokryję to w drodze powrotnej”.

36Kończąc opowieść, Jezus zwrócił się do rozmówcy:

—Który z tych trzech, twoim zdaniem, okazał się bliźnim napadniętego przez bandytów?

37—Ten, który mu pomógł.

—Więc i ty postępuj podobnie—odpowiedział Jezus.

W domu Marty i Marii

38Kontynuując podróż do Jerozolimy, Jezus zatrzymał się w pewnej wiosce. Skorzystał z zaproszenia niejakiej Marty. 39Jej siostra, Maria, usiadła u stóp Jezusa i słuchała Go. 40Marta zaś była bardzo zajęta przygotowaniem posiłku. W końcu podeszła do Niego i zapytała:

—Czy nie razi Cię to, Panie, że moja siostra siedzi bezczynnie, podczas gdy ja mam tyle pracy? Powiedz jej, żeby mi pomogła!

41—Droga Marto, zabiegasz o tak wiele rzeczy—rzekł do niej 42—a przecież tak naprawdę liczy się tylko jedno. To właśnie wybrała Maria i nie zostanie jej to odebrane.