Luka 1 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 1:1-80

1Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu, 21:2 Mk 1:1; Mdo 1:21-22; 2Pet 1:16; 1Yn 1:1; Mk 4:14kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana, 31:3 Mdo 11:4; 24:3; 26:25; 1:1mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo, 41:4 Yn 20:31; Mdo 2:42ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.

Kuzaliwa Kwa Yohana Mbatizaji Kwatabiriwa

51:5 1Nya 24:10; Mt 2:1Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni. 61:6 Kum 5:33; Lk 2:25Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama. 7Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.

81:8 1Nya 24:19; 2Nya 8:14Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu, 91:9 2Nya 29:11; Za 141:2alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba. 101:10 Law 16:17Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.

111:11 Mdo 5:19; Kut 30:1-10Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria. 121:12 Amu 6:22-23; 13:22Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu. 131:13 Mt 14:27; 3:1; Lk 1:60-63Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana. 141:14 Lk 1:58Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake. 151:15 Law 10:9; Lk 7:33; Yer 1:5; Gal 1:15Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake. 161:16 Mal 4:5, 6Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao. 171:17 Mt 11:14; Mal 4:4-6Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”

181:18 Mwa 17:17Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”

191:19 Mt 18:10; Lk 1:26Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema. 201:20 Kut 4:11; Eze 3:26Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”

21Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni. 221:22 Lk 1:62Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.

231:23 2Fal 11:5Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake. 24Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.

251:25 Mwa 30:23; Isa 4:1Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”

Kuzaliwa Kwa Yesu Kwatabiriwa

261:26 Lk 1:62; Mt 2:23Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti, 271:27 Mt 1:16-20; Lk 2:4kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria. 281:28 Amu 5:24Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”

291:29 Lk 1:12Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?” 301:30 Mt 14:27Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu. 311:31 Isa 7:14; Mt 1:21-25Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu. 321:32 Mk 5:7Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake. 331:33 Mt 28:18; 2Sam 7:16; Ebr 1:8Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

34Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”

351:35 Mt 1:18; 4:3; Mk 1:24Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu. 361:36 Lk 1:24Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa. 371:37 Mt 19:26; Mwa 18:14; Zek 8:6; Mt 18:26; Mk 10:27; Rum 4:21Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”

38Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.

Maria Aenda Kumtembelea Elizabeti

391:39 Lk 1:65; Yos 21:9, 10, 11Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi. 40Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti. 411:41 Lk 1:15; Mwa 25; 22Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu, 421:42 Amu 5:24akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa. 431:43 Yn 13:13Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu? 44Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha. 451:45 Lk 1:20; 11:28Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”

Wimbo Wa Maria Wa Sifa

461:46 Za 34:2-3Naye Maria akasema:

“Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,

471:47 Za 18:46; 1Tim 4:10nayo roho yangu inamfurahia

Mungu Mwokozi wangu,

481:48 Za 138:5; Lk 11:27kwa kuwa ameangalia kwa fadhili

unyonge wa mtumishi wake.

Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,

491:49 Za 71:19; 111:9kwa maana yeye Mwenye Nguvu

amenitendea mambo ya ajabu:

jina lake ni takatifu.

501:50 Kut 20:6; Za 103:17Rehema zake huwaendea wale wamchao,

kutoka kizazi hadi kizazi.

511:51 Za 98:1; Isa 40:10Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake;

amewatawanya wale wenye kiburi

ndani ya mioyo yao.

521:52 Mt 23:12; 1Sam 2:6; Ay 5:11; Za 11:3, 6Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi,

lakini amewainua wanyenyekevu.

531:53 Za 107:9; 1Sam 3:5Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri,

bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.

541:54 Za 98:3Amemsaidia mtumishi wake Israeli,

kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu

551:55 Za 132:11; Gal 3:16Abrahamu na uzao wake milele,

kama alivyowaahidi baba zetu.”

56Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.

Kuzaliwa Kwa Yohana Mbatizaji

57Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume. 581:58 Lk 1:14Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.

591:59 Law 12:3; Flp 3:5Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake. 601:60 Lk 1:13, 63; Mt 3:1Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”

61Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”

621:62 Lk 1:22Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani. 631:63 Lk 1:13, 60; Mt 3:1Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.” 641:64 Lk 1:20; Eze 24:27Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu. 65Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote. 661:66 Mwa 39:2; Mdo 11:21Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.

Unabii Wa Zekaria

671:67 Yoe 2:28Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:

681:68 Mwa 24:27; 1Fal 8:15; Za 111:9; Lk 7:16“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli,

kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.

691:69 2Sam 22:23; Za 132:17Naye ametusimamishia pembe1:69 Pembe hapa inamaanisha nguvu. ya wokovu

katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,

701:70 Yer 23:3; Za 132:17kama alivyonena kwa vinywa vya manabii

wake watakatifu tangu zamani,

711:71 Za 106:10kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu,

na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:

721:72 Mik 7:20; Za 106:45; Eze 16:60ili kuonyesha rehema kwa baba zetu

na kukumbuka Agano lake takatifu,

731:73 Mwa 22:16-18kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:

741:74 Ebr 9:14kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu,

tupate kumtumikia yeye pasipo hofu

751:75 Efe 4:24katika utakatifu na haki mbele zake,

siku zetu zote.

761:76 Mt 11:9; Mk 5:7; Mal 3:1; Mt 3:3“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana;

kwa kuwa utamtangulia Bwana

na kuandaa njia kwa ajili yake,

771:77 Yer 31:34; Mt 1:21kuwajulisha watu wake juu ya wokovu

utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,

781:78 Mal 4:2kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu,

nuru itokayo juu itatuzukia

791:79 Za 107:14; Mdo 26:18ili kuwaangazia wale waishio gizani

na katika uvuli wa mauti,

kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”

801:80 Lk 2:40, 52Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.

Persian Contemporary Bible

لوقا 1:1-80

1عاليجناب تِئوفيلوس:

بسياری كوشيده‌اند شرح زندگی عيسی مسيح را به نگارش درآورند؛ 2‏-3و برای انجام اين كار، از مطالبی استفاده كرده‌اند كه از طريق شاگردان او و شاهدان عينی وقايع، در دسترس ما قرار گرفته است. اما از آنجا كه من خود، اين مطالب را از آغاز تا پايان، با دقت بررسی و مطالعه كرده‌ام، چنين صلاح ديدم كه ماجرا را به طور كامل و به ترتيب برايتان بنويسم، 4تا از درستی تعليمی كه يافته‌ايد، اطمينان حاصل كنيد.

مژدهٔ تولد يحيای تعميددهنده

5ماجرا را از كاهنی يهودی آغاز می‌كنم، با نام زكريا، كه در زمان هيروديس، پادشاه يهوديه، زندگی می‌كرد. او عضو دسته‌ای از خدمهٔ خانهٔ خدا بود كه ابيا نام داشت. همسرش اليزابت نيز مانند خود او از قبيلهٔ كاهنان يهود و از نسل هارون برادر موسی بود. 6زكريا و اليزابت هر دو در نظر خدا بسيار درستكار بودند و با جان و دل تمام احكام الهی را بجا می‌آوردند. 7اما آنها فرزندی نداشتند، زيرا اليزابت نازا بود؛ از اين گذشته، هر دو بسيار سالخورده بودند.

8‏-9يكبار كه دستهٔ ابيا در خانهٔ خدا خدمت می‌كرد، و زكريا نيز به انجام وظايف كاهنی خود مشغول بود، به حكم قرعه نوبت به او رسيد كه به جايگاه مقدس خانهٔ خدا داخل شود و در آنجا بخور بسوزاند. 10به هنگام سوزاندن بخور، جمعيت انبوهی در صحن خانهٔ خدا مشغول عبادت بودند. 11‏-12ناگهان فرشته‌ای بر زكريا ظاهر شد و در طرف راست قربانگاه بخور ايستاد. زكريا از ديدن فرشته مبهوت و هراسان شد.

13فرشته به او گفت: «ای زكريا، نترس! چون آمده‌ام به تو خبر دهم كه خدا دعايت را شنيده است، و همسرت اليزابت برايت پسری به دنیا خواهد آورد كه نامش را يحيی خواهی گذارد. 14اين پسر باعث شادی و سُرور شما خواهد شد، و بسياری نيز از تولدش شادی خواهند نمود. 15زيرا او يكی از مردان بزرگ خدا خواهد شد. او هرگز نبايد شراب و مشروبات سُكرآور بنوشد، چون حتی پيش از تولد، از روح‌القدس پر خواهد بود! 16بسياری از بنی‌اسرائيل توسط او به سوی خداوند، خدای خود بازگشت خواهند نمود. 17او خدمت خود را با همان روح و قدرت الياس، آن نبی قديم انجام خواهد داد. او پيشاپيش مسيح خواهد آمد تا مردم را برای ظهور او آماده كند، دلهای پدران را به پسران نزديک سازد و به افراد سركش بياموزد كه همچون اجداد خويش خداوند را دوست داشته و مردم خداترسی باشند.»

18زكريا به فرشته گفت: «ولی اين غيرممكن است، چون من پير شده‌ام و همسرم نيز سالخورده است!»

19فرشته در جواب گفت: «من جبرائيل هستم كه در حضور خدا می‌ايستم و اوست كه مرا فرستاده تا اين خبر خوش را به تو دهم. 20اما حال كه سخنان مرا باور نكردی، قدرت تكلم را از دست خواهی داد و تا زمانی كه كودک به دنیا بيايد يارای سخن گفتن نخواهی داشت؛ زيرا آنچه گفتم، در زمان مقرر واقع خواهد شد.»

21در اين ميان، مردم در صحن خانهٔ خدا منتظر زكريا بودند و از اينكه او در بيرون آمدن از جايگاه مقدس اين همه تأخير می‌كرد، در حيرت بودند. 22سرانجام وقتی بيرون آمد و نتوانست با ايشان سخن گويد، از اشارات او پی بردند كه در جايگاه مقدس خانهٔ خدا رؤيايی ديده است.

23زكريا پس از پايان دوره خدمتش، به خانهٔ خود بازگشت. 24طولی نكشيد كه همسرش اليزابت باردار شد. او برای مدت پنج ماه گوشه‌نشينی اختيار كرد و می‌گفت: 25«سرانجام خداوند بر من نظر لطف انداخت و كاری كرد كه ديگر در ميان مردم شرمگين نباشم!»

مژدهٔ تولد عيسی

26در ششمين ماه بارداری اليزابت، خدا فرشته خود جبرائيل را به ناصره، يكی از شهرهای استان جليل فرستاد، 27تا وحی او را به دختری به نام مريم برساند. مريم نامزدی داشت به نام يوسف، از نسل داوود پادشاه.

28جبرائيل به مريم ظاهر شد و گفت: «سلام بر تو ای دختری كه مورد لطف پروردگار قرار گرفته‌ای! خداوند با توست!»

29مريم سخت پريشان و متحير شد، چون نمی‌توانست بفهمد منظور فرشته از اين سخنان چيست.

30فرشته به او گفت: «ای مريم، نترس! زيرا خدا بر تو نظر لطف انداخته است! 31تو بزودی باردار شده، پسری به دنیا خواهی آورد و نامش را عيسی خواهی نهاد. 32او مردی بزرگ خواهد بود و پسر خدا ناميده خواهد شد و خداوند تخت سلطنت جدش داوود را به او واگذار خواهد كرد 33تا برای هميشه بر قوم اسرائيل سلطنت كند. سلطنت او هرگز پايان نخواهد يافت!»

34مريم از فرشته پرسيد: «اما چگونه چنين چيزی امكان دارد؟ دست هيچ مردی هرگز به من نرسيده است!»

35فرشته جواب داد: «روح‌القدس بر تو نازل خواهد شد و قدرت خدا بر تو سايه خواهد افكند. از اين رو آن نوزاد مقدس بوده، فرزند خدا خوانده خواهد شد. 36بدان كه خويشاوند تو اليزابت نيز شش ماه پيش در سن پيری باردار شده و بزودی پسری به دنیا خواهد آورد؛ بلی، همان كسی كه همه او را نازا می‌خواندند. 37زيرا برای خدا هيچ كاری محال نيست!»

38مريم گفت: «من خدمتگزار خداوند هستم و هر چه او بخواهد، با كمال ميل انجام می‌دهم. از خدا می‌خواهم كه هر چه گفتی، همان بشود.» آنگاه فرشته ناپديد شد.

مريم از اليزابت ديدار می‌کند

39‏-40پس از چند روز، مريم تدارک سفر ديد و شتابان نزد اليزابت رفت، كه با همسرش زكريا، در يكی از شهرهای واقع در منطقه كوهستان يهوديه زندگی می‌كرد. مريم وارد خانه شد و سلام كرد. 41به محض اينكه صدای سلام مريم به گوش اليزابت رسيد، بچه در رحم او به حركت درآمد. اليزابت از روح‌القدس پر شد 42و با صدای بلند به مريم گفت: «خدا تو را بيش از همهٔ زنان ديگر مورد لطف خود قرار داده است! فرزندت نيز سرچشمهٔ بركات برای انسانها خواهد بود. 43چه افتخار بزرگی است برای من، كه مادر خداوندم به ديدنم بيايد! 44وقتی وارد شدی و به من سلام كردی، به محض اينكه صدايت را شنيدم، بچه از شادی در رَحِمِ من به حركت درآمد! 45خوشا به حال تو، زيرا ايمان آوردی كه هر چه خدا به تو گفته است، به انجام خواهد رسيد!»

سرود شکرگزاری مريم

46مريم گفت: «خداوند را با تمام وجود ستايش می‌كنم، 47و روح من، به سبب نجات‌دهنده‌ام خدا، شاد و مسرور می‌گردد! 48چون او منِ ناچيز را مورد عنايت قرار داده است. از اين پس، همهٔ نسلها مرا خوشبخت خواهند خواند، 49زيرا خدای قادر و قدوس در حق من كارهای بس بزرگ كرده است.

50«لطف و رحمت او، نسل اندر نسل شامل حال آنانی می‌شود كه از او می‌ترسند. 51او دست خود را با قدرت دراز كرده و متكبران را همراه نقشه‌هايشان پراكنده ساخته است. 52سلاطين را از تخت به زير كشيده و فروتنان را سربلند كرده است. 53گرسنگان را با نعمتهای خود سير كرده، اما ثروتمندان را تهی دست روانه نموده است. 54او رحمت خود را كه به اجداد ما وعده داده بود، به ياد آورده و به ياری قوم خود، اسرائيل، آمده است. 55بلی، او وعدهٔ ابدی خود را كه به ابراهيم و فرزندان او داده بود، به ياد آورده است.»

56مريم حدود سه ماه نزد اليزابت ماند. سپس به خانه خود بازگشت.

تولد يحيای تعميددهنده

57سرانجام، انتظار اليزابت پايان يافت و زمان وضع حملش فرا رسيد و پسری به دنیا آورد. 58وقتی كه همسايگان و بستگان او از اين خبر آگاهی يافتند و ديدند كه خداوند چه لطف بزرگی در حق او نموده است، نزد او آمده، در شادی‌اش شريک شدند.

59چون نوزاد هشت روزه شد، تمام بستگان و دوستان برای مراسم ختنه گرد آمدند و قصد داشتند نام پدرش، زكريا را بر او بگذارند. 60اما اليزابت نپذيرفت و گفت: «نام او يحيی خواهد بود.»

61گفتند: «اما در خانواده تو، كسی به اين نام نبوده است.»

62پس با اشاره، از پدر نوزاد پرسيدند كه نام او را چه بگذارند.

63زكريا با اشاره، تخته‌ای خواست و در برابر چشمان حيرت‌زدهٔ همه نوشت: «نامش يحيی است!» 64در همان لحظه زبانش باز شد و قدرت سخن گفتن را باز يافت و به شكرگزاری خدا پرداخت. 65همسايگان با ديدن تمام اين وقايع بسيار متعجب شدند، و خبر اين ماجرا در سراسر كوهستان يهوديه پخش شد. 66هر كه اين خبر را می‌شنيد، به فكر فرو می‌رفت و از خود می‌پرسيد: «اين بچه، در آينده چه خواهد شد؟» زيرا همه می‌ديدند كه او مورد توجه خداوند قرار دارد.

نبوت زکريا

67آنگاه پدرش زكريا، از روح‌القدس پر شد و چنين نبوت كرد:

68«خداوند، خدای اسرائيل را سپاس باد، زيرا به ياری قوم خود شتافته و ايشان را رهايی بخشيده است. 69او بزودی برای ما نجات دهنده‌ای قدرتمند از نسل داوود خواهد فرستاد؛ 70چنانكه از گذشته‌های دور، از زبان انبيای مقدس خود وعده می‌داد 71كه شخصی را خواهد فرستاد تا ما را از چنگ دشمنانمان و از دست همه آنانی كه از ما نفرت دارند، رهايی بخشد.

72‏-73«خداوند نسبت به نياكان ما، رحيم و مهربان بوده است. بلی، او عهد و پيمان مقدسی را كه با ابراهيم بست، از ياد نبرده 74و اين افتخار را نصيب ما كرده كه از دست دشمنانمان رهايی يابيم و بدون ترس و واهمه از آنان، او را عبادت نماييم 75و تمام روزهای عمر خود را در حضور او با پاكی و عدالت بگذرانيم.

76«و تو ای فرزند، نبی خدای تعالی ناميده خواهی شد، زيرا پيشاپيش خداوند حركت خواهی كرد تا راه او را آماده نمايی، 77و قوم او را آگاه سازی كه با آمرزش گناهانشان نجات خواهند يافت. 78‏-79اينها، همه به سبب رحمت و شفقت بی‌پايان خدای ماست. بزودی سپيده صبح از افق آسمان بر ما طلوع خواهد كرد تا بر كسانی كه در تاريكی و سايه مرگ ساكن هستند، بتابد و همهٔ ما را به سوی آرامش و صفا هدايت نمايد.»

80آن كودک رشد كرد و صاحب روحی توانا شد. او در بيابانها به سر می‌برد؛ تا روزی فرا رسيد كه می‌بايست خدمت خود را در ميان قوم اسرائيل آغاز كند.