Kutoka 8 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 8:1-32

18:1 Kut 3:12; 4:23; 5:1; 9:1Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu. 28:2 Za 78:45; 105:30; Ufu 16:13Kama ukikataa kuwaruhusu kuondoka, basi nitaipiga nchi yako yote kwa kuwaletea vyura. 38:3 Kut 10:6; 12:34Mto Naili utafurika vyura. Watakuja kwenye jumba lako la kifalme na katika chumba chako cha kulala na kitandani mwako, katika nyumba za maafisa wako na kwa watu wako, vyura hao wataingia katika meko yenu na kwenye vyombo vya kukandia unga. 4Vyura watapanda juu yako, juu ya watu wako na maafisa wako wote.’ ”

58:5 Kut 4:2, 17; 7:9-23; 10:13, 21-22; 14:27Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha mkono wako ukiwa na ile fimbo yako juu ya vijito, mifereji na madimbwi, fanya vyura waje juu ya nchi ya Misri.’ ”

68:6 Za 78:45; 105:30Ndipo Aroni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, nao vyura wakatokea na kuifunika nchi. 78:7 Kut 7:11; Mt 24:24Lakini waganga wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao, nao pia wakafanya vyura kuja juu ya nchi ya Misri.

88:8 Kut 9:28; 10:8, 17; Hes 21:7; 1Sam 12:19; 1Fal 13:6; Yer 42:2; Mdo 8:24Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kusema, “Mwombeni Bwana awaondoe vyura kutoka kwangu na kwa watu wangu, nami nitawaachia watu wenu waende kumtolea Bwana dhabihu.”

98:9 Kut 9:5Mose akamwambia Farao, “Ninakupa heshima ya kuamua ni wakati gani wa kukuombea wewe, maafisa wako na watu wako ili kwamba vyura watoke kwenu na kwenye nyumba zenu. Isipokuwa wale walio katika Mto Naili.”

108:10 Kut 9:14; 15:11; Kum 3:24; 4:35; 33:26; 2Sam 7:22; 1Fal 8:23; 1Nya 17:20; 2Nya 6:14; Za 71:19; 86:8; 89:6; Isa 40:18; 42:8; 46:9; Yer 49:19; Mik 7:18Farao akasema, “Kesho.”

Mose akamjibu, “Itakuwa kama unavyosema, ili upate kujua kwamba hakuna yeyote kama Bwana Mungu wetu. 11Vyura wataondoka kwako na katika nyumba zako, kwa maafisa wako na kwa watu wako, ila watabakia katika Mto Naili tu.”

12Baada ya Mose na Aroni kuondoka kwa Farao, Mose akamlilia Bwana kuhusu vyura aliokuwa amewaleta kwa Farao. 138:13 Yak 5:16-18Naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Vyura wakafia ndani ya nyumba, viwanjani na mashambani. 14Wakayakusanya malundo, nchi nzima ikanuka. 158:15 Mhu 8:11; Kut 7:14Lakini Farao alipoona pametokea nafuu, akaushupaza moyo wake na hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.

Pigo La Tatu: Viroboto

168:16 Kut 4:2Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Nyoosha fimbo yako uyapige mavumbi ya ardhi,’ nayo nchi yote ya Misri mavumbi yatakuwa viroboto.” 178:17 Za 105:31Wakafanya hivyo, Aroni aliponyoosha mkono wake wenye fimbo na kuyapiga mavumbi ya nchi, viroboto wakawajia watu na wanyama. Mavumbi yote katika nchi ya Misri yakawa viroboto. 188:18 Kut 7:11; 9:11; Dan 5:8Lakini waganga walipojaribu kutengeneza viroboto kwa siri ya uganga wao, hawakuweza. Nao viroboto walikuwa juu ya watu na wanyama.

198:19 Kut 7:5, 13-15; 10:7; 12:33; 31:18; 1Sam 6:9; Neh 9:6; Za 8:3; 33:6; Lk 11:20Waganga wale wakamwambia Farao, “Hiki ni kidole cha Mungu.” Lakini moyo wa Farao ukawa mgumu naye hakuwasikiliza, kama vile Bwana alivyosema.

Pigo La Nne: Mainzi

208:20 Kut 7:15; 9:13; 3:18Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi na usimame mbele ya Farao wakati anapokwenda mtoni nawe umwambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu. 21Kama hutawaachia watu wangu waondoke nitakupelekea makundi ya mainzi juu yako, kwa maafisa wako, kwa watu wako na kwenye nyumba zenu. Nyumba za Wamisri zitajazwa mainzi, hata na ardhi yote ya Misri.

228:22 Mwa 45:10; Kut 7:5; 9:4-6, 26, 29; 10:23; 11:7; 12:13; 19:5; Kum 4:20; 7:6; 14:2; 26:18; 1Fal 8:36; Ay 36:11; Za 33:12; 135:4; Mal 3:17“ ‘Lakini siku ile nitafanya kitu tofauti katika nchi ya Gosheni, ambapo watu wangu wanaishi, hapatakuwepo na makundi ya mainzi, ili mpate kujua kwamba Mimi, Bwana, niko katika nchi hii. 238:23 Kut 9:4-6; 10:23; 11:7; 12:23-27Nitaweka tofauti kati ya watu wangu na watu wenu. Ishara hii ya ajabu itatokea kesho.’ ”

248:24 Za 78:45; 105:31Naye Bwana akafanya hivyo. Makundi makubwa ya mainzi yalimiminika katika jumba la kifalme la Farao na katika nyumba za maafisa wake, pia nchi yote ya Misri ikaharibiwa na mainzi.

258:25 Kut 9:27; 10:16; 12:31Ndipo Farao akamwita Mose na Aroni na kuwaambia, “Nendeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu katika nchi hii.”

268:26 Mwa 43:32Lakini Mose akamwambia, “Hilo halitakuwa sawa. Dhabihu tutakazomtolea Bwana Mungu wetu zitakuwa chukizo kwa Wamisri. Kama tukitoa dhabihu ambazo ni chukizo mbele yao, je, hawatatupiga mawe? 278:27 Mwa 30:36; Kut 3:18Ni lazima twende mwendo wa siku tatu mpaka tufike jangwani ili tumtolee Bwana Mungu wetu dhabihu, kama alivyotuagiza.”

288:28 Yer 37:3; Mdo 8:24Farao akamwambia, “Nitawaruhusu mwende kumtolea Bwana Mungu wenu dhabihu huko jangwani, lakini hamna ruhusa kwenda mbali sana. Sasa mniombee.”

298:29 Kut 9:30; 10:11; Isa 26:10Mose akajibu, “Mara tu nitakapoondoka, nitamwomba Bwana na kesho mainzi yataondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake. Hakikisha tu kwamba Farao hatatenda kwa udanganyifu tena kwa kutokuwaachia watu waende kumtolea Bwana dhabihu.”

308:30 Kut 9:33; 10:18Ndipo Mose akamwacha Farao na kumwomba Bwana, 31naye Bwana akafanya lile Mose alilomwomba. Mainzi yakaondoka kwa Farao, kwa maafisa wake na kwa watu wake, wala hakuna hata inzi aliyebakia. 328:32 Kut 7:14Lakini wakati huu pia Farao akaushupaza moyo wake, wala hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

出埃及记 8:1-32

蛙灾

1耶和华对摩西说:“你进宫去告诉法老,‘耶和华说,让以色列百姓离开,好事奉我。 2如果你不听从,我就使青蛙来毁坏你的国土。 3尼罗河将充满青蛙,它们要跳到你的宫里、卧室和床铺上,你的臣仆和百姓家里,你的炉灶和揉面盆里。 4青蛙还会跳到你和你的百姓及众臣仆身上。’”

5耶和华对摩西说:“你叫亚伦埃及各地的江河、溪流和池塘伸杖,使青蛙遍布埃及全境。” 6亚伦伸杖,青蛙就遍布了埃及全境。 7巫师也行邪术如法炮制,叫青蛙上来。 8法老召摩西亚伦进宫,对他们说:“你们快求耶和华,使这些青蛙离开我们,我便让百姓去献祭给耶和华。” 9摩西对法老说:“好吧,你要我在什么时候为你以及你的臣仆和百姓祷告,叫这些青蛙离开你和你的宫殿,只留在河里呢?” 10法老说:“明天。”摩西说:“就照你说的,这样你就知道没有神明能比得上我们的上帝耶和华。 11明天青蛙会离开你、你的宫殿、你的臣仆和百姓,只留在河里。” 12摩西亚伦离开法老后,摩西就为法老所受的蛙灾一事向耶和华呼求。 13耶和华答应了摩西的祈求。凡在房屋内、院子里和田野中的青蛙都死了。 14百姓把青蛙的尸体堆积起来,埃及全境都充满了死青蛙的腐臭气味。 15法老看见灾难已经过去,便又硬着心,不肯听从摩西亚伦的话,正如耶和华所言。

虱灾

16耶和华对摩西说:“你吩咐亚伦用杖击打地上的尘土,使埃及境内的尘土变成虱子。” 17他们就照上帝的吩咐去做,亚伦伸杖击打地上的尘土,虱子就跑到人和牲畜身上,全埃及的尘土都变成了虱子。 18巫师们也试图用邪术变出虱子来,却无法成功。埃及的百姓和牲畜身上长满了虱子。 19巫师们对法老说:“这是上帝的作为。”法老的心却仍然刚硬,不肯答应摩西亚伦的要求,正如耶和华所言。

苍蝇之灾

20耶和华对摩西说:“明天清早,你趁法老去河边时去见他,告诉他,‘耶和华说,放我的子民走,他们好事奉我, 21不然,我就叫无数的苍蝇飞到你、你的臣仆和百姓身上,进到你们各自的家中,使埃及遍地布满苍蝇。 22但那天,我子民居住的歌珊却丝毫不会受搅扰,这样你就知道我耶和华主宰天下。 23我要把我的子民跟你的百姓分开,明天我必行这神迹。’” 24耶和华果然这样行。密密麻麻的苍蝇飞进法老的王宫和他臣仆的家里,埃及全国都受到苍蝇的毁坏。 25法老召见摩西亚伦,对他们说:“你们可以去献祭给你们的上帝,不过要在我的境内举行。” 26摩西说:“这怎么行?我们用来献祭的东西,是埃及人最憎恶的。如果我们在埃及境内举行这样的仪式,他们一定会拿石头打死我们。 27我们要照我们上帝耶和华的吩咐离开这里,走三天的路程到旷野去献祭给祂。” 28法老说:“好,我让你们去旷野献祭给你们的上帝耶和华,只是不要走得太远。现在为我祈求吧。” 29摩西说:“我离开这里就去祈求耶和华,使苍蝇明天就离开你及你的臣仆和百姓,但这次你不可再食言,阻止以色列人去向耶和华献祭。” 30摩西说完以后,便离开王宫,去祈求耶和华。 31耶和华就照摩西的祈求,使成群的苍蝇离开法老及其臣仆和百姓,一只也没有留下。 32这一次,法老又硬着心,不肯让百姓离开埃及