Kutoka 35 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 35:1-35

Masharti Ya Sabato

135:1 Kut 34:32Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye: 235:2 Law 23:3; Mwa 2:3; Kut 34:21; Kum 5:13-14; Kut 31:14, 15; Hes 15:32; Lk 13:14Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe. 335:3 Kut 16:23Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”

Vifaa Kwa Ajili Ya Maskani Ya Mungu

(Kutoka 25:1-9)

435:4 Kut 25:1, 2Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru: 535:5 Kut 25:2; 2Kor 9:7Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba; 6nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi; 7ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo;35:7 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. mbao za mshita; 835:8 Kut 25:6mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri; 9vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.

1035:10 Kut 31:6; 39:43; 1Fal 7:14; Isa 28:26“Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru: 1135:11 Kut 26:1-37; 36:8-38; Mdo 7:44, 45; Ebr 8:2, 5; 9:2-11; Ufu 21:3Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako; 1235:12 Kut 25:10-22; 37:1-9; 26:33Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia; 1335:13 Kut 25:23-30; 37:10-16meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho; 1435:14 Kut 25:31kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga; 1535:15 Kut 30:1-6; 37:26-28; 30:34-38; 26:36; 1Sam 2:28; 1Nya 23:13; 2Nya 29:11; Lk 1:9madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani; 1635:16 Kut 27:1-8; 38:1-7; 30:18madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake; 1735:17 Kut 27:9; 38:9-20pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua; 1835:18 Kut 27:19; 38:20vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake; 1935:19 Kut 28:2; 31:10; 39:1mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”

20Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose, 2135:21 Kut 25:2; 36:2; 1Nya 28:2, 9; 29:9; Ezr 7:27; 2Kor 8:12; 9:7na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu. 22Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana. 2335:23 Kut 39:1; 1Nya 29:8Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta. 24Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta. 2535:25 Kut 28:3; 31:6; 36:1; 2Fal 23:7; Mit 31:19-24Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi. 2635:26 Kut 25:2; 1Nya 29:6-8Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi. 27Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani. 2835:28 Kut 25:6Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri. 2935:29 Kut 25:2-7; 36:3; 2Fal 12:4Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.

Bezaleli Na Oholiabu

(Kutoka 31:1-11)

30Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, 3135:31 2Nya 2:7, 14naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi, 32ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba, 33kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza. 3435:34 Kut 31:6; 2Nya 2:14Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine. 3535:35 Kut 31:3, 6; 36:1, 2; 1Fal 7:14; 1Nya 2:14; Isa 28:26; Yak 1:5Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.

La Bible du Semeur

Exode 35:1-35

Le tabernacle

Le jour du sabbat

1Moïse réunit toute l’assemblée des Israélites et leur dit : Voici ce que l’Eternel a ordonné de faire : 2Vous ferez votre ouvrage pendant six jours, mais le septième jour sera pour vous un jour de repos complet, consacré à l’Eternel. Quiconque fera un travail ce jour-là sera mis à mort35.2 Voir Ex 20.8-11 ; 23.12 ; 31.12-17 ; 34.21 ; Lv 23.3 ; Dt 5.12-14.. 3Vous n’allumerez de feu dans aucune de vos habitations le jour du sabbat.

Instructions sur les offrandes pour le tabernacle

4Moïse dit à toute l’assemblée des Israélites : Voici ce que l’Eternel a commandé35.4 Pour les v. 4-29, voir 25.1-7. : 5Prélevez parmi vous une contribution pour l’Eternel. Toute personne qui le souhaite dans son cœur apportera à l’Eternel une contribution en bronze, en argent ou en or, 6ou des fils de pourpre violette ou écarlate, de rouge éclatant, du fin lin et du poil de chèvre, 7des peaux de béliers teintes en rouge, des peaux de dauphins et du bois d’acacia, 8de l’huile pour le chandelier et des aromates pour l’huile d’onction et le parfum aromatique, 9des pierres d’onyx et d’autres pierres à enchâsser pour l’éphod et pour le pectoral.

Les instructions sur les artisans du tabernacle

10Tous les gens habiles parmi vous, qu’ils viennent et exécutent tout ce que l’Eternel a prescrit : 11le tabernacle, sa tente et sa couverture, ses agrafes, ses cadres, ses traverses, ses piliers et ses socles, 12le coffre sacré avec ses barres et le propitiatoire, le voile de séparation, 13la table, ses barres et tous ses accessoires, ainsi que les pains destinés à être exposés devant l’Eternel, 14le chandelier, ses ustensiles, ses lampes et l’huile d’éclairage, 15l’autel des parfums et ses barres, l’huile d’onction sainte, le parfum aromatique et le rideau pour l’entrée de la Demeure, 16l’autel des holocaustes, sa grille de bronze, ses barres et tous ses accessoires, la cuve et son socle, 17les tentures du parvis, ses piliers, ses socles et le rideau pour l’entrée du parvis, 18les piquets du tabernacle, ceux du parvis et leurs cordages, 19les vêtements de cérémonie pour faire le service dans le sanctuaire, les vêtements sacrés pour le prêtre Aaron, et ceux de ses fils pour l’exercice du sacerdoce.

Le peuple apporte ses offrandes

20Puis la communauté des Israélites se retira de la présence de Moïse. 21Alors tous ceux dont le cœur les y disposait et qui en avaient la volonté vinrent apporter à l’Eternel leur contribution en vue de la construction de la tente de la Rencontre, de tout l’ouvrage qui s’y rapporte et de la confection des vêtements sacrés. 22Tous ceux qui le souhaitaient de tout leur cœur, les hommes autant que les femmes, vinrent apporter des pendentifs, des boucles, des anneaux, des bracelets et toutes sortes d’ornements en or, et ils les offrirent à l’Eternel avec le geste de présentation. 23Tous ceux qui avaient chez eux des fils de pourpre violette ou écarlate, de rouge éclatant, du fin lin, du poil de chèvre, des peaux de béliers teintes en rouge et des peaux de dauphins les apportèrent. 24Tous ceux qui avaient mis de côté une offrande en argent et en bronze l’apportèrent à l’Eternel. Tous ceux qui avaient chez eux du bois d’acacia l’apportèrent pour tout l’ouvrage à réaliser. 25Toutes les femmes habiles filèrent le lin de leurs mains et apportèrent des fils de pourpre violette et écarlate, de rouge éclatant et du fin lin. 26Toutes les femmes habiles qui le désiraient de tout cœur filèrent les poils de chèvre. 27Les chefs du peuple apportèrent les pierres d’onyx et les pierres à enchâsser pour l’éphod et le pectoral, 28les aromates et l’huile pour le chandelier, pour l’huile d’onction et pour le parfum aromatique. 29Tous les Israélites, hommes et femmes, que leur cœur poussait à apporter quelque chose pour les ouvrages que l’Eternel avait ordonné d’exécuter par l’intermédiaire de Moïse, apportèrent leurs offrandes volontaires à l’Eternel.

Les artisans du tabernacle

30Moïse dit aux Israélites : Voyez, l’Eternel a désigné Betsaléel, fils d’Ouri, descendant de Hour, de la tribu de Juda35.30 Pour les v. 30 à 36.7, voir 31.1-11.. 31Il l’a rempli de l’Esprit de Dieu qui lui confère de l’habileté, de l’intelligence et de la compétence pour exécuter toutes sortes d’ouvrages, 32pour concevoir des projets, pour travailler l’or, l’argent et le bronze, 33pour tailler des pierres à enchâsser, pour sculpter le bois et pour réaliser toutes sortes d’ouvrages. 34Il lui a aussi accordé, de même qu’à Oholiab, fils d’Ahisamak de la tribu de Dan, le don d’enseigner sa technique à d’autres. 35Il les a doués d’habileté pour exécuter toutes sortes de travaux de graveur et de concepteur, pour broder la pourpre violette, le rouge éclatant et le fin lin, pour réaliser des travaux de toutes sortes et concevoir des projets.