Kutoka 26 – NEN & TCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 26:1-37

Maskani Ya Mungu

(Kutoka 36:8-38)

126:1 Kut 29:42; 40:2; Law 8:10; Hes 1:50; Yos 22:19-20; 2Sam 7:2; 1Fal 1:30; Mdo 7:44; Ebr 8:2-5; 13:10; Ufu 21:3; Kut 25:18“Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo. 2Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane,26:2 Dhiraa 28 ni sawa na mita 13. na upana wa dhiraa nne26:2 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. 326:3 1Kor 12:4-12Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano. 426:4 Efe 4:13; Kol 2:2, 19Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho. 5Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane. 6Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.

726:7 Kut 36:14“Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani. 8Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini,26:8 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. na upana wa dhiraa nne. 9Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani. 10Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine. 11Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja. 12Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema. 13Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika. 1426:14 Kut 36:19; Hes 3:25; 4:25Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.26:14 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili.

15“Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani. 16Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi26:16 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. na upana wa dhiraa moja na nusu, 17zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii. 18Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani, 1926:19 Kut 38:27kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi. 20Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini 21na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili. 22Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani, 23na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali. 24Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana. 25Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.

2626:26 Kut 36:31; Rum 15:1; Gal 6:2“Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani, 27matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani. 28Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine. 29Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.

3026:30 Kut 40:2; 25:9; Hes 9:15; Ebr 8:5; Mdo 7:44; Ebr 8:5“Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.

3126:31 Hes 4:5; 2Nya 3:14; Mt 27:51; Lk 23:45; Ebr 9:3; Kut 25:18; 36:35; Law 16:2; Kut 25:18; 36:35“Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia. 32Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha. 3326:33 Kut 27:21; 35:12; 40:2-3, 21; Law 16:2; Hes 3:31; 4:5; 2Nya 3:14; Law 16:2, 16; 1Fal 6:16; 7:50; 8:6; 2Nya 3:8; 5:7; Eze 41:5; Ebr 9:2-3Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu. 3426:34 Kut 25:21; 30:6; 37:6; Law 16:2; Ebr 9:5Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu. 3526:35 Kut 25:23; Ebr 9:2; Kut 25:31Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.

3626:36 Kut 35:15; 40:5; 28; Za 45:14; Eze 16:10; 26:16; 27:7“Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. 3726:37 Kut 38:1Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.

Tagalog Contemporary Bible

Exodus 26:1-37

Ang Toldang Sambahan

(Exo. 36:8-38)

1“Magpagawa ka ng Toldang Sambahan. Ito ang mga gagamitin sa paggawa nito: sampung piraso ng pinong telang linen na may lanang kulay asul, ube at pula. At paburdahan ito ng kerubin sa mahuhusay na mambuburda. 2Kailangang magkakasukat ang bawat tela na may habang 42 talampakan at may lapad na anim na talampakan. 3Pagdugtong-dugtungin ninyo ito ng tiglilima. 4At pagawan mo ng parang singsing na telang asul ang bawat gilid ng pinagdugtong na mga tela, 5at tig-50 na parang singsing na tela sa bawat dulo at kailangan magkatapat sa isaʼt isa. 6Magpagawa ka ng 50 kawit na ginto para mapagkabit ang parang mga singsing na tela sa dalawang pinagsamang tela. Sa pamamagitan nito, magagawa ang Toldang Sambahan.

7“Pagawan mo ng talukbong ang Tolda. Labing-isang pirasong tela na gawa sa balahibo ng kambing ang gagamitin sa paggawa nito. 8Kailangang may haba na 45 talampakan ang bawat tela at anim na talampakan ang lapad. 9Pagdugtong-dugtungin mo ang limang tela at ganoon din ang gawin sa natirang anim. Ang ikaanim naman ay tutupiin at ilalagay sa harap ng tolda. 10Palagyan mo rin ito ng 50 parang singsing na tela ang bawat gilid ng pinagdugtong na mga tela, 11at ikabit dito ang 50 tansong kawit. 12Ilaylay mo sa likod ng Tolda ang kalahati ng sobrang tela, 13at ilaylay din sa bawat gilid ang isaʼt kalahating talampakan ng tela na sobra sa pangtalukbong ng Tolda. 14Ang ibabaw ng talukbong ng Tolda ay papatungan ng balat ng lalaking tupa na kinulayan ng pula, at papatungan din ng magandang klase ng balat.26:14 magandang klase ng balat: Maaaring ang ibig sabihin, balat ng “dolphin.”

15“Dapat ang balangkas ng Tolda ay tablang akasya. 16Ang haba ng bawat tabla ay 15 talampakan at ang lapad ay dalawang talampakan. 17Ang bawat tabla ay nilagyan ng dalawang mitsa26:17 mitsa: sa Ingles, “tenon.” para maidugtong ito sa isa pang tabla. Ganito ang ginawa nila sa bawat tabla. 18Ang 20 sa mga tablang ito ay gagamitin sa pagtatayo ng Tolda sa timog na bahagi. 19Ang mga tablang ito ay isinuksok sa 40 pundasyong pilak – dalawang pundasyon sa bawat tabla. 20Ang hilagang bahagi ng Tolda ay gagamitan din ng 20 tabla, 21at isinuksok din sa 40 pundasyong pilak – dalawang pundasyon sa bawat tabla. 22Ang bandang kanlurang bahagi naman ng Tolda ay ginamitan nila ng anim na tabla, 23at dalawang tabla sa mga gilid nito. 24Pagdugtungin ang mga tabla sa mga sulok mula sa ilalim hanggang sa itaas. Kailangang ganito rin ang gawin sa dalawang tabla sa mga gilid. 25Kaya may walong tabla sa bahaging ito ng Tolda, at nakasuksok ito sa 16 na pundasyong pilak – dalawang pundasyon sa bawat tabla.

26“Magpagawa ka rin ng mga akasyang biga – lima para sa bahaging hilaga ng Tolda, 27lima rin sa bahaging timog, at lima pa rin sa bahaging kanluran sa likod ng Tolda. 28Ang biga sa gitna ng balangkas ay manggagaling sa dulo ng Tolda papunta sa kabilang dulo. 29Pabalutan ng ginto ang mga tabla at palagyan ng mga argolyang26:29 argolya: Tingnan ang “footnote” sa 25:12. Ganito rin sa 27:4. ginto na pagsusuotan ng mga biga, pabalutan din ng ginto ang mga biga.

30“Kailangang ipatayo mo ang Toldang Sambahan ayon sa planong sinabi ko sa iyo rito sa bundok.

31“Magpagawa ka rin ng kurtina na gawa sa pinong telang linen na may lanang kulay asul, ube at pula. At paburdahan mo ito ng kerubin. 32Ipakabit ito sa mga kawit na ginto sa apat na haliging akasya na nababalutan ng ginto. Ang apat na haliging ito ay nakasuksok sa apat na pundasyong pilak. 33Kapag nakabit na ang kurtina sa mga kawit, ilagay sa likod nito ang Kahon ng Kasunduan. Ang kurtina ang maghihiwalay sa Banal na Lugar at sa Pinakabanal na Lugar. 34Ang Kahon ng Kasunduan ay dapat ilagay sa Pinakabanal na Lugar at dapat may takip ito. 35Ilagay ang mesa sa labas ng Pinakabanal na Lugar, sa hilagang bahagi ng Tolda, at sa bandang timog, ilagay sa tapat ng mesa ang lalagyan ng ilaw.

36“Magpagawa ka ng isa pang kurtina para sa pintuan ng Toldang Sambahan. Pinong telang linen rin ito na binurdahan gamit ang lanang kulay asul, ube at pula. At napakaganda ng pagkakaburda nito. 37Pagkatapos, ipakabit ito sa mga kawit na ginto sa limang haliging akasya na nababalutan ng ginto. Ang limang haliging ito ay nakasuksok sa limang pundasyong tanso.