Kutoka 26 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 26:1-37

Maskani Ya Mungu

(Kutoka 36:8-38)

126:1 Kut 29:42; 40:2; Law 8:10; Hes 1:50; Yos 22:19-20; 2Sam 7:2; 1Fal 1:30; Mdo 7:44; Ebr 8:2-5; 13:10; Ufu 21:3; Kut 25:18“Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo. 2Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane,26:2 Dhiraa 28 ni sawa na mita 13. na upana wa dhiraa nne26:2 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. 326:3 1Kor 12:4-12Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano. 426:4 Efe 4:13; Kol 2:2, 19Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho. 5Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane. 6Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.

726:7 Kut 36:14“Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani. 8Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini,26:8 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. na upana wa dhiraa nne. 9Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani. 10Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine. 11Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja. 12Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema. 13Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika. 1426:14 Kut 36:19; Hes 3:25; 4:25Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.26:14 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili.

15“Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani. 16Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi26:16 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. na upana wa dhiraa moja na nusu, 17zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii. 18Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani, 1926:19 Kut 38:27kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi. 20Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini 21na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili. 22Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani, 23na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali. 24Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana. 25Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.

2626:26 Kut 36:31; Rum 15:1; Gal 6:2“Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani, 27matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani. 28Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine. 29Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.

3026:30 Kut 40:2; 25:9; Hes 9:15; Ebr 8:5; Mdo 7:44; Ebr 8:5“Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.

3126:31 Hes 4:5; 2Nya 3:14; Mt 27:51; Lk 23:45; Ebr 9:3; Kut 25:18; 36:35; Law 16:2; Kut 25:18; 36:35“Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia. 32Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha. 3326:33 Kut 27:21; 35:12; 40:2-3, 21; Law 16:2; Hes 3:31; 4:5; 2Nya 3:14; Law 16:2, 16; 1Fal 6:16; 7:50; 8:6; 2Nya 3:8; 5:7; Eze 41:5; Ebr 9:2-3Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu. 3426:34 Kut 25:21; 30:6; 37:6; Law 16:2; Ebr 9:5Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu. 3526:35 Kut 25:23; Ebr 9:2; Kut 25:31Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.

3626:36 Kut 35:15; 40:5; 28; Za 45:14; Eze 16:10; 26:16; 27:7“Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. 3726:37 Kut 38:1Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.

Korean Living Bible

출애굽기 26:1-37

성막

1“너는 가늘게 꼰 베실과 청색, 자색, 홍색 실로 곱게 짠 열 폭의 천에 그룹 천사 모양을 정교하게 수놓아 성막을 만들어라.

2각 폭의 크기는 똑같이 길이 12.6미터, 너비 1.8미터로 하고

3다섯 폭씩 서로 연결하여 두 쪽의 큰 폭을 만들어라.

4-5그리고 두 개의 그 큰 폭 한쪽 가에 각각 50개의 청색 고를 달고

6금갈고리 50개를 만들어 그 갈고리를 양쪽 청색 고에 꿰어 하나의 성막으로 연결하여라.

7“그런 다음 너는 염소털로 만든 열한 폭의 천으로 성막 덮개를 만들어라.

8각 폭을 길이 13.5미터, 너비 1.8미터로 하여 열한 폭의 크기를 모두 똑같게 하고

9다섯 폭을 서로 이어 하나의 큰 폭이 되게 하며 나머지 여섯 폭도 그렇게 하고 그 여섯째 폭은 반을 접어서 그 절반을 성막 앞에 늘어뜨려 놓아라.

10그리고 두 개의 그 큰 폭 한쪽 가에 각각 50개의 고를 달고

11놋갈고리 50개를 만들어 그 갈고리로 양쪽 고에 꿰어 하나로 연결하여라.

12또 반으로 접은 나머지 절반은 성막 뒤로 늘어뜨리고

13전체 너비가 앞의 성막보다 90센티미터가 더 넓은 이 덮개를 양쪽으로 각각 45센티미터씩 늘어뜨려 성막이 완전히 덮이게 하라.

14“그런 다음 너는 붉게 물들인 숫양의 가죽으로 그 위에 덮을 또 다른 덮개를 만들고 또 26:14 또는 ‘해달’바닷소의 가죽으로 제일 윗덮개를 만들어라.

15“너는 아카시아나무로 성막 널빤지를 만들어 세워라.

16널빤지 한 장의 크기는 길이 4.5미터, 너비 68센티미터로 하고

17각 널빤지마다 두 촉을 만들어 널빤지끼리 서로 연결하라. 모든 널빤지를 다 이런 식으로 해야 한다.

18너는 널빤지 20개를 서로 연결하여 성막 남쪽 벽을 만들고

19은받침 40개를 만들어 널빤지 하나에 두 개씩 받쳐라. 그것은 널빤지 밑에 두 촉을 만들고 은받침에 각각 홈통을 만들어 서로 끼우도록 해야 한다.

20성막 북쪽에도 널빤지 20개를 만들어 연결하고

21은받침 40개를 만들어 널빤지 하나에 두 개씩 받쳐라.

22그리고 성막 뒤인 서쪽에는 널빤지 여섯 개를 만들어 세우고

23성막 뒤 두 모퉁이에는 널빤지 둘을 만들어 세워라. 이 모퉁이 널빤지는

24아래에서부터 위까지 26:24 또는 ‘두 겹 두께로 하여’옆면과 겹쳐 세워 한 고리에 연결되게 해야 한다.

25이렇게 되면 성막 뒷편의 널빤지는 모두 여덟 개가 되며 은받침은 널빤지 하나에 두 개씩 모두 열여섯 개가 될 것이다.

26-27“그리고 너는 아카시아나무로 가로대 를 만들어 성막의 양쪽 옆면과 뒷면에 각각 다섯 개씩 끼워라.

28널빤지 가운데 끼울 중간 가로대는 성막 이쪽 끝에서 저쪽 끝까지 미치게 해야 한다.

29또 성막 널빤지와 가로대를 금으로 싸고 가로대를 꿸 금고리도 만들어라.

30너는 내가 산에서 보여 준 설계대로 성막을 세워야 한다.

31“너는 청색, 자색, 홍색 실과 가늘게 꼰 베실로 휘장을 만들어 그 위에 그룹 천사를 정교하게 수놓아라.

32그리고 아카시아나무로 네 기둥을 만들어 금으로 싸서 네 개의 은받침 위에 세우고

33금갈고리로 휘장을 거기에 달아라. 그런 다음 법궤를 그 휘장 안에 들여놓아라. 그 휘장이 성소와 지성소를 갈라 놓을 것이다.

34그리고 너는 지성소 안의 법궤 위에 속죄소가 될 궤 뚜껑을 올려놓고

35그 휘장 바깥 북쪽에는 상을 놓고 그 맞은편인 남쪽에는 등대를 놓아라.

36“너는 청색, 자색, 홍색 실과 가늘게 꼰 베실로 수를 놓아 짜서 성막 출입구 휘장을 만들어라.

37그리고 아카시아나무로 기둥 다섯 개를 만들어 금으로 싸고 그 휘장을 걸 갈고리도 금으로 만들며 그 기둥을 받칠 다섯 개의 기둥 받침은 놋으로 만들어라.”