Kutoka 12 – NEN & NVI-PT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 12:1-51

Pasaka

1Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri, 212:2 Kut 13:4; 23:15; 34:18; 40:2; Kum 16:1; Kut 12:18“Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu. 312:3 Mk 14:12; 1Kor 5:7Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba. 4Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu. 512:5 Kut 29:1; Law 1:3; 3:1; 4:3; 22:18-21; 23:12; Hes 6:14; 15:8; 28:3; Kum 15:21; 17:1; Ebr 9:14; 1Pet 1:19Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi. 612:6 Law 23:5; Hes 9:1-11; Yos 5:10; 2Nya 30:2; Kut 16:12; Kum 16:4-6Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni. 712:7 Eze 9:6Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao. 812:8 Kut 16:19; 23:18; 34:25; Law 7:15; Hes 9:11; Kut 13:3; Kum 16:3-7; 2Nya 35:13; 1Kor 5:8Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu. 912:9 Kut 29:13-22; Law 3:3Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani. 1012:10 Kut 13:7; 29:34; Law 22:30; Kum 16:4Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto. 1112:11 Kum 16:3; Isa 48:20; 52:11; Law 23:5; Hes 9:2-4; 28:16; Kum 16:1; Yos 5:10; 2Fal 23:21-23; 2Nya 30:1; Ezr 6:19; Isa 31:5; Eze 45:21Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.

1212:12 Amo 5:17; Isa 10:33; 31:8; 37:36; Kut 4:23; 13:15; 15:11; 18:11; Hes 33:4; 2Nya 2:5; Za 95:3; 97:9; 135:5; Isa 19:1; Kut 11:4; Yer 43:12; 44:8; Kut 6:2“Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana. 1312:13 Ebr 11:28; Kut 8:23Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.

1412:14 Kut 13:9; 23:14; 32:5; 13:5, 10; 27:21; Law 3:17; 10:9; 16:29; 23:14; 24; 3; Hes 18:23“Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu. 1512:15 Kut 13:6-7; 23:15; 34:18; Law 23:6; Hes 28:17; Kum 16:3; 1Kor 5:7; Mwa 17:14; Hes 9:13Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli. 1612:16 Hes 29:35Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.

1712:17 Kut 23:15; 34:18; Kum 16:16; 2Nya 8:13; 30:21; Ezr 6:22; Mt 26:17; Lk 22:1; Mdo 12:3; Kut 6:6, 26; 13:3; Law 19:36; 3:17“Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu. 1812:18 Law 23:5-8; Hes 28:16-25Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja. 1912:19 Mwa 17:14; Hes 9:14; 15:14; 35:15; Kum 1:16; Yos 8:33Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa. 2012:20 Law 3:17; Hes 35:29; Eze 6:6; Kut 13:6Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”

2112:21 Mk 14:12-16; Kut 12:11Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka. 2212:22 Law 14:4-6; Hes 19:18; Za 51:7; Ebr 11:28; Kut 12:7Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi. 2312:23 Isa 19:22; Ufu 7:3; Mwa 16:7; Isa 37:36; Kut 12:7, 13; Yer 6:26; 48:8; 1Kor 10:10; Ebr 11:28Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.

24“Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu. 2512:25 Mwa 15:14; Kut 3:17Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii. 2612:26 Kut 10:2; 13:8; Yos 4:6Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’ 2712:27 Kut 8:23; 12:11; Mwa 24:26; Kut 4:31Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’ ” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu. 28Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.

2912:29 Kut 11:4; Mwa 19:13; Kut 4:23; 9:6; Za 78:51Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia. 3012:30 Kut 11:6Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.

Kutoka

3112:31 Kut 8:8Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba. 3212:32 Kut 10:9, 26; Mwa 27:34Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”

3312:33 Kut 6:1; 1Sam 6:6; Mwa 20:3; Kut 8:19; Za 105:38Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!” 34Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao. 3512:35 Kut 3:22; Mwa 24:53Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo. 3612:36 Mwa 39:21; Kut 3:22Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.

3712:37 Mwa 47:11; Kut 13:20; Hes 33:3-5; Mwa 12:2; Kut 38:26; Hes 1:46; 2:32; 11:13-21; 26:51Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto. 3812:38 Hes 11:4; Yos 8:35Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe. 3912:39 Kut 3:20; 6:1; 11:1Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.

4012:40 Mwa 15:13; Mdo 7:6; Gal 3:17Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430. 4112:41 Kut 6:26; 3:10; 12:17Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri. 4212:42 Kut 13:10; Law 3:17; Hes 9:3; Kum 16:1, 6Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.

Masharti Kwa Ajili Ya Pasaka

4312:43 Hes 9:14; 15:14; 2Nya 6:32-33; Isa 14:1; 56:3-6; 60:10; Kut 12:11Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka:

“Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka. 4412:44 Mwa 17:12-13Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri, 4512:45 Law 22:10lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.

4612:46 Hes 9:12; Za 22:14; 34:20; Mit 17:22; Yn 19:36“Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote. 47Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.

4812:48 Law 19:18, 34; 24:22; Hes 9:14; 10:32; Eze 44:7“Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila. 4912:49 Law 24:22; Hes 15:15-16, 29; Kum 1; 16Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”

50Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni. 5112:51 Kut 3:10; 6:6, 26; 12:41Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.

Nova Versão Internacional

Êxodo 12:1-51

A Páscoa

1O Senhor disse a Moisés e a Arão, no Egito: 2“Este deverá ser o primeiro mês do ano para vocês. 3Digam a toda a comunidade de Israel que no décimo dia deste mês todo homem deverá separar um cordeiro ou um cabrito, para a sua família, um para cada casa. 4Se uma família for pequena demais para um animal inteiro, deve dividi-lo com seu vizinho mais próximo, conforme o número de pessoas e conforme o que cada um puder comer. 5O animal escolhido será macho de um ano, sem defeito, e pode ser cordeiro ou cabrito. 6Guardem-no até o décimo quarto dia do mês, quando toda a comunidade de Israel irá sacrificá-lo, ao pôr do sol. 7Passem, então, um pouco do sangue nas laterais e nas vigas superiores das portas das casas nas quais vocês comerão o animal. 8Naquela mesma noite comerão a carne assada no fogo, com ervas amargas e pão sem fermento. 9Não comam a carne crua, nem cozida em água, mas assada no fogo: cabeça, pernas e vísceras. 10Não deixem sobrar nada até pela manhã; caso isso aconteça, queimem o que restar. 11Ao comerem, estejam prontos para sair: cinto no lugar, sandálias nos pés e cajado na mão. Comam apressadamente. Esta é a Páscoa do Senhor.

12“Naquela mesma noite passarei pelo Egito e matarei todos os primogênitos, tanto dos homens como dos animais, e executarei juízo sobre todos os deuses do Egito. Eu sou o Senhor! 13O sangue será um sinal para indicar as casas em que vocês estiverem; quando eu vir o sangue, passarei adiante. A praga de destruição não os atingirá quando eu ferir o Egito.

14“Este dia será um memorial que vocês e todos os seus descendentes celebrarão como festa ao Senhor. Celebrem-no como decreto perpétuo. 15Durante sete dias comam pão sem fermento. No primeiro dia tirem de casa o fermento, porque quem comer qualquer coisa fermentada, do primeiro ao sétimo dia, será eliminado de Israel. 16Convoquem uma reunião santa no primeiro dia e outra no sétimo. Não façam nenhum trabalho nesses dias, exceto o da preparação da comida para todos. É só o que poderão fazer.

17“Celebrem a festa dos pães sem fermento, porque foi nesse mesmo dia que eu tirei os exércitos de vocês do Egito. Celebrem esse dia como decreto perpétuo por todas as suas gerações. 18No primeiro mês comam pão sem fermento, desde o entardecer do décimo quarto dia até o entardecer do vigésimo primeiro. 19Durante sete dias vocês não deverão ter fermento em casa. Quem comer qualquer coisa fermentada será eliminado da comunidade de Israel, seja estrangeiro, seja natural da terra. 20Não comam nada fermentado. Onde quer que morarem, comam apenas pão sem fermento”.

A Décima Praga: A Morte dos Primogênitos

21Então Moisés convocou todas as autoridades de Israel e lhes disse: “Escolham um cordeiro ou um cabrito para cada família. Sacrifiquem-no para celebrar a Páscoa! 22Molhem um feixe de hissopo no sangue que estiver na bacia e passem o sangue na viga superior e nas laterais das portas. Nenhum de vocês poderá sair de casa até o amanhecer. 23Quando o Senhor passar pela terra para matar os egípcios, verá o sangue na viga superior e nas laterais da porta e passará sobre aquela porta, e não permitirá que o destruidor entre na casa de vocês para matá-los.

24“Obedeçam a essas instruções como decreto perpétuo para vocês e para os seus descendentes. 25Quando entrarem na terra que o Senhor prometeu dar a vocês, celebrem essa cerimônia. 26Quando os seus filhos perguntarem: ‘O que significa esta cerimônia?’, 27respondam-lhes: É o sacrifício da Páscoa ao Senhor, que passou sobre as casas dos israelitas no Egito e poupou nossas casas quando matou os egípcios”. Então o povo curvou-se em adoração. 28Depois os israelitas se retiraram e fizeram conforme o Senhor tinha ordenado a Moisés e a Arão.

29Então, à meia-noite, o Senhor matou todos os primogênitos do Egito, desde o filho mais velho do faraó, herdeiro do trono, até o filho mais velho do prisioneiro que estava no calabouço, e também todas as primeiras crias do gado. 30No meio da noite o faraó, todos os seus conselheiros e todos os egípcios se levantaram. E houve grande pranto no Egito, pois não havia casa que não tivesse um morto.

O Êxodo

31Naquela mesma noite o faraó mandou chamar Moisés e Arão e lhes disse: “Saiam imediatamente do meio do meu povo, vocês e os israelitas! Vão prestar culto ao Senhor, como vocês pediram. 32Levem os seus rebanhos, como tinham dito, e abençoem a mim também”.

33Os egípcios pressionavam o povo para que se apressasse em sair do país, dizendo: “Todos nós morreremos!” 34Então o povo tomou a massa de pão ainda sem fermento e a carregou nos ombros, nas amassadeiras embrulhadas em suas roupas. 35Os israelitas obedeceram à ordem de Moisés e pediram aos egípcios objetos de prata e de ouro, bem como roupas. 36O Senhor concedeu ao povo uma disposição favorável da parte dos egípcios, de modo que lhes davam o que pediam; assim eles despojaram os egípcios.

37Os israelitas foram de Ramessés até Sucote. Havia cerca de seiscentos mil homens a pé, além de mulheres e crianças. 38Grande multidão de estrangeiros de todo tipo seguiu com eles, além de grandes rebanhos, tanto de bois como de ovelhas e cabras. 39Com a massa que haviam levado do Egito, fizeram pães sem fermento. A massa não tinha fermentado, pois eles foram expulsos do Egito e não tiveram tempo de preparar comida.

40Ora, o período que os israelitas viveram no Egito12.40 O Pentateuco Samaritano e a Septuaginta dizem no Egito e em Canaã. foi de quatrocentos e trinta anos. 41No dia em que se completaram os quatrocentos e trinta anos, todos os exércitos do Senhor saíram do Egito. 42Assim como o Senhor passou em vigília aquela noite para tirar do Egito os israelitas, estes também devem passar em vigília essa mesma noite, para honrar o Senhor, por todas as suas gerações.

As Leis sobre a Participação na Páscoa

43Disse o Senhor a Moisés e a Arão: “Estas são as leis da Páscoa: Nenhum estrangeiro poderá comê-la. 44O escravo comprado poderá comer da Páscoa, depois de circuncidado, 45mas o residente temporário e o trabalhador contratado dela não comerão.

46“Vocês a comerão numa só casa; não levem nenhum pedaço de carne para fora da casa nem quebrem nenhum dos ossos. 47Toda a comunidade de Israel terá que celebrar a Páscoa.

48“Qualquer estrangeiro residente entre vocês que quiser celebrar a Páscoa do Senhor terá que circuncidar todos os do sexo masculino da sua família; então poderá participar como o natural da terra. Nenhum incircunciso poderá participar. 49A mesma lei se aplicará ao natural da terra e ao estrangeiro residente”.

50Todos os israelitas fizeram como o Senhor tinha ordenado a Moisés e a Arão. 51No mesmo dia o Senhor tirou os israelitas do Egito, organizados segundo as suas divisões.