Kutoka 1 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 1:1-22

Waisraeli Waonewa

11:1 Mwa 46:8Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake: 2Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda; 3Isakari, Zabuloni na Benyamini; 41:4 Mwa 35:22-26; Hes 1:20-43Dani na Naftali, Gadi na Asheri. 51:5 Mwa 46:26Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.

61:6 Mwa 50:26; Mdo 7:15Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa, 71:7 Mwa 12:2; Kum 7:13; Eze 16:7lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.

81:8 Yer 43:11; 46:2Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri. 91:9 Mwa 26:16Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi. 101:10 Mwa 15:13; Kut 3:7; 18:11; Za 64:2; 71:10; 83:3; 105:24-25; Isa 53:3; Mdo 7:17-19Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”

111:11 Kut 3:7; 5:4, 10-14; 6:6-7; 2:11; Mwa 15:13; 47:11; Yos 9:27; Isa 60:10; 1Fal 9:19, 21; 1Nya 22:2; 2Nya 8:4Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao. 12Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli, 131:13 Mwa 15:13-14; Kut 5:21; 16:3; Law 25:43-53; Kum 4:20; 26:6; 1Fal 8:15; Za 129:1; Isa 30:6; 48:10; Yer 11:4kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili. 141:14 Kum 26:6; Ezr 9:9; Isa 14:3; Mwa 11:3; Kut 2:23; 3:9; Hes 20:15; Mdo 7:19; 1Sam 10:11; 2Sam 13:4Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.

151:15 Mwa 35:17Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua, 16“Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.” 171:17 Mit 16:6; 1Sam 22:17; Dan 3:16-18; Mdo 4:18-20; 5:29Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi. 18Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”

191:19 Law 19:11; Yos 2:4-6; 1Sam 19:14; 2Sam 17:20Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”

201:20 Mit 11:18; 22:8; Mhu 8:12; Isa 3:10; Ebr 6:10Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi. 211:21 1Sam 2:35; 2Sam 7:11, 27-29; 1Fal 11:38; 14:10Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.

221:22 Mwa 41:1; Mdo 7:19Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”

New International Reader’s Version

Exodus 1:1-22

The Israelites Become Slaves in Egypt

1Here are the names of Israel’s children who went to Egypt with Jacob. Each one went with his family. 2Jacob’s sons were

Reuben, Simeon, Levi, Judah,

3Issachar, Zebulun, Benjamin,

4Dan, Naphtali,

Gad and Asher.

5The total number of Jacob’s children and grandchildren was 70. Joseph was already in Egypt.

6Joseph and all his brothers died. So did all their children. 7The people of Israel had many children. The number of them greatly increased. There were so many of them that they filled the land.

8Then a new king came to power in Egypt. Joseph didn’t mean anything to him. 9“Look,” he said to his people. “The Israelites are far too many for us. 10Come. We must deal with them carefully. If we don’t, there will be even more of them. Then if war breaks out, they’ll join our enemies. They’ll fight against us and leave the country.”

11So the Egyptians put slave drivers over the people of Israel. The slave drivers treated them badly and made them work hard. The Israelites built the cities of Pithom and Rameses so Pharaoh could store things there. 12But the worse the slave drivers treated the Israelites, the more Israelites there were. So the Egyptians became afraid of them. 13They made them work hard. They didn’t show them any pity. 14The people suffered because of their hard labor. The slave drivers forced them to work with bricks and mud. And they made them do all kinds of work in the fields. The Egyptians didn’t show them any pity at all. They made them work very hard.

15There were two Hebrew women named Shiphrah and Puah. They helped other women having babies. The king of Egypt spoke to them. He said, 16“You are the ones who help the other Hebrew women. Watch them when they get into a sitting position to have their babies. Kill the boys. Let the girls live.” 17But Shiphrah and Puah had respect for God. They didn’t do what the king of Egypt had told them to do. They let the boys live. 18Then the king of Egypt sent for the women. He asked them, “Why have you done this? Why have you let the boys live?”

19The women answered Pharaoh, “Hebrew women are not like the women of Egypt. They are strong. They have their babies before we get there.”

20So God was kind to Shiphrah and Puah. And the number of Israelites became even greater. 21Shiphrah and Puah had respect for God. So he gave them families of their own.

22Then Pharaoh gave an order to all his people. He said, “You must throw every Hebrew baby boy into the Nile River. But let every Hebrew baby girl live.”