Kumbukumbu 5 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 5:1-33

Amri Kumi

(Kutoka 20:1-17)

15:1 Kut 18:20Mose akawaita Israeli wote, akawaambia:

Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata. 25:2 Kut 19:5Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu. 35:3 Kum 11:2-7; Hes 26:63-65; Ebr 8:9; Mt 13:17Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo. 45:4 Kut 19:9, 18-19; 20:22; Kum 4:33, 36; 34:10; Hes 14:4Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima. 55:5 Gal 3:19; Mwa 3:10; Ebr 12:18-21; Kut 20:18-21; 20:18-21; Hes 16:48; Za 106:23; Yer 30:21(Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:

65:6 Kut 13:3; 29:46; Law 26:1; Kum 6:4; Za 81:10“Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.

75:7 Kut 20:3“Usiwe na miungu mingine ila mimi.

85:8 Law 26:1; Kum 4:15-16; Za 78:58; 97:7; Kut 20:4; Mdo 17:29Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji. 95:9 Hes 26:11; Kut 34:7; Hes 10:35; 14:18; Kut 34:7Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 105:10 Kut 34:2; Hes 14:18; Kum 7:9; Neh 1:5; Yer 32:18; Dan 9:4lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.

115:11 Za 139:20; Law 19:12; Kum 10:20; Mt 5:33-37Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.

125:12 Kut 16:23-30; 31:13; Mk 2:27-28; Kut 20:8Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza. 13Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote. 145:14 Mwa 2:2; Mt 12:2; Mk 2:17; Ebr 4:4; Ay 31:13; Yer 34:9-11; 17:21-24Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe. 155:15 Mwa 15:13; Kut 6:1; Za 108:6; Yer 32:21; Kum 4:34Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.

165:16 Mal 1:6; Kut 21:17; Law 19:3; Eze 22:7; Mt 15:4; 19:19; Mk 7:10; 10:19; Lk 18:20; Efe 6:2-3; Kum 4:40; 11:9; Mit 3:1-2Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.

175:17 Mwa 9:6; Law 24:17; Mhu 3:3; Yer 40:15; 41:3; Mt 5:21-22; 19:19; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9; Yak 2:11Usiue.

185:18 Law 20:10; Mt 5:27-30; 19:18; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9; Yak 2:11Usizini.

195:19 Law 19:11; Mt 19:19; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9Usiibe.

205:20 Kut 23:1; Mt 19:18; Mk 10:19; Lk 18:20Usimshuhudie jirani yako uongo.

215:21 Rum 7:7; 13:9Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”

225:22 Kut 20:21; 24:12; 31:18; Kum 4:13Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.

Woga Wa Watu Mlimani

(Kutoka 20:18-21)

235:23 Kut 3:16Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi. 245:24 Kum 4:34; 8:5; 11:2; Isa 53:4; Kum 3:24; Kut 19:19Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye. 255:25 Kut 20:18-19; Kum 18:16; Ebr 12:19Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi. 265:26 Kut 33:20; Kum 4:33; Amu 6:22-23; 13:22; Isa 6:5Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi? 275:27 Kut 19:8; 24:7Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”

285:28 Kum 18:17Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri. 295:29 Za 81:8, 13; Yos 22:5; Za 78:7; Kum 4:1-40; 12:25; 22:7; Isa 48:18; Kum 12:25; Yer 44:4; Mt 23:37; Lk 19:42; 2Kor 5:20; 6:1; 7:1; Ebr 12:25; Yn 15:14; Ufu 22:14Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!

305:30 Mal 4:4; Gal 3:19“Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao. 315:31 Kut 24:12Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”

325:32 Kum 4:29; 10:12; 17:11, 20; 28:14; Yos 1:7; 1Fal 15:5; 2Fal 22:2; Mit 4:27; Kum 10:12; Za 119:6; Mhu 8:12; 1Tim 4:8; Efe 6:3Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto. 335:33 Isa 3:10; Yer 7:23; 38:20; Lk 1:6; Kum 4:40Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.

New International Reader’s Version

Deuteronomy 5:1-33

The Ten Commandments

1Moses sent for all the Israelites. Here is what he said to them.

Israel, listen to me. Here are the rules and laws I’m announcing to you today. Learn them well. Be sure to obey them. 2The Lord our God made a covenant with us at Mount Horeb. 3He didn’t make it only with our people of long ago. He also made it with us. In fact, he made it with all of us who are alive here today. 4The Lord spoke to you face to face. His voice came out of the fire on the mountain. 5At that time I stood between the Lord and you. I announced to you the Lord’s message. I did it because you were afraid of the fire. You didn’t go up the mountain.

The Lord said,

6“I am the Lord your God. I brought you out of Egypt. That is the land where you were slaves.

7“Do not put any other gods in place of me.

8“Do not make statues of gods that look like anything in the sky or on the earth or in the waters. 9Do not bow down to them or worship them. I am the Lord your God. I want you to worship only me. I cause the sins of the parents to affect their children. I will cause the sins of those who hate me to affect even their grandchildren and great-grandchildren. 10But for all time to come I show love to all those who love me and keep my commandments.

11“Do not misuse the name of the Lord your God. The Lord will find guilty anyone who misuses his name.

12“Keep the Sabbath day holy. Do this just as the Lord your God has commanded you. 13Do all your work in six days. 14But the seventh day is a sabbath to honor the Lord your God. Do not do any work on that day. The same command applies to your sons and daughters, your male and female servants, your oxen, your donkeys and your other animals. It also applies to any outsiders who live in your towns. I want your male and female servants to rest, just as you do. 15Remember that you were slaves in Egypt. The Lord your God reached out his mighty hand and powerful arm and brought you out of there. So the Lord your God has commanded you to keep the Sabbath day holy.

16“Honor your father and mother, just as the Lord your God has commanded you. Then you will live a long time in the land he is giving you. And things will go well with you there.

17“Do not murder.

18“Do not commit adultery.

19“Do not steal.

20“Do not be a false witness against your neighbor.

21“Do not want to have your neighbor’s wife. Do not desire anything your neighbor owns. Do not desire to have your neighbor’s house or land, male or female servant, ox or donkey.”

22These are the commandments the Lord announced in a loud voice to your whole community. He gave them to you there on the mountain. He spoke out of the fire, cloud and deep darkness. He didn’t add anything else. Then he wrote the commandments on two stone tablets. And he gave them to me.

23The mountain was blazing with fire. You heard the voice coming out of the darkness. So your elders and all the leaders of your tribes came to me. 24You said, “The Lord our God has shown us his glory and majesty. We have heard his voice coming out of the fire. Today we have seen that a person can still stay alive even if God speaks with them. 25But why should we die? This great fire will burn us up. We’ll die if we hear the voice of the Lord our God again. 26We have heard the voice of the living God. We’ve heard him speaking out of the fire. Has any other human being ever heard him speak like that and stayed alive? 27Go near and listen to everything the Lord our God says. Then tell us what he tells you. We will listen and obey.”

28The Lord heard you when you spoke to me. He said to me, “I have heard what these people said to you. Everything they said was good. 29But I wish they would always have respect for me in their hearts. I wish they would always obey all my commands. Then things would go well with them and their children forever.

30“Go and tell them to return to their tents. 31But you stay here with me. Then I will give you all my commands, rules and laws. You must teach the people to obey them in the land I am giving them as their very own.”

32So be careful to do what the Lord your God has commanded you. Don’t turn away from his commands to the right or the left. 33Live exactly as the Lord your God has commanded you to live. Then you will enjoy life in the land you will soon own. Things will go well with you there. You will live there for a long time.