Kumbukumbu 34 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 34:1-12

Kifo Cha Mose

134:1 Hes 32:3; 21:10; Kum 32:49, 52; Yos 19:40-48; Amu 18:28Kisha Mose akaupanda mlima Nebo kutoka tambarare za Moabu mpaka kilele cha Pisga, ngʼambo ya Yeriko. Huko Bwana akamwonyesha nchi yote: kutoka Gileadi mpaka Dani, 234:2 Kut 23:31; Kum 11:24; Hes 34:6; Yos 15:12Naftali yote, nchi ya Efraimu na Manase, nchi yote ya Yuda mpaka bahari ya magharibi,34:2 Yaani Bahari ya Mediterania. 334:3 Mwa 12:9; 13:10; Amu 1:16; 3:13; 2Nya 28:15Negebu na nchi yote kuanzia Bonde la Yeriko, Mji wa Mitende, hadi Soari. 434:4 Mwa 28:13; 12:7; Yos 21:43; Kum 3:23, 27Kisha Bwana akamwambia, “Hii ndiyo nchi niliyomwahidi Abrahamu na Isaki na Yakobo kwa kiapo niliposema, ‘Nitawapa wazao wako.’ Nimekuruhusu uione kwa macho yako, lakini hutavuka kuingia.”

534:5 Hos 12:7; Yos 1:1-2; Mwa 25:8Naye Mose mtumishi wa Bwana akafa huko Moabu, kama Bwana alivyokuwa amesema. 634:6 Kum 3:29; Yud 9Mungu akamzika huko Moabu, katika bonde mkabala na Beth-Peori, lakini hakuna ajuaye kaburi lake lilipo mpaka leo. 734:7 Kut 7:7; Yos 14:10; Mwa 27:1; 15:15; Kum 31:2Mose alikuwa na umri wa miaka mia moja na ishirini alipofariki; hata hivyo nguvu ya macho yake haikufifia wala mwili wake haukudhoofika. 834:8 Hes 21:11; 20:29; Mwa 37:34; 50:3; 10; 50:3; 2Sam 11:27; 1Sam 25:1; Isa 57:1; Mdo 8:2Waisraeli wakaomboleza kwa ajili ya Mose kwenye tambarare za Moabu kwa siku thelathini, mpaka wakati wa kulia na kuomboleza ulipopita.

934:9 Mwa 41:38; Kut 28:3; 31:3; Isa 11:2; 1Fal 9:12; Kum 31:14; Mdo 6:6; Dan 6:3; Kum 27:18; Hes 11:17; 27:18Basi Yoshua mwana wa Nuni alijazwa roho ya hekima kwa sababu Mose alikuwa ameweka mikono yake juu yake. Kwa hiyo Waisraeli wakamsikiliza na wakafanya yale ambayo Bwana alikuwa amemwagiza Mose.

1034:10 Mwa 20:7; Kum 18:15-18; 5:4; Kut 33:11; Hes 12:6-8Tangu wakati huo, katika Israeli hajainuka nabii mwingine kama Mose, ambaye Bwana alimjua uso kwa uso, 1134:11 Kum 4:34; 7:19; Kut 11:3aliyetenda ishara zote zile za miujiza na maajabu ambayo Bwana alimtuma kuyatenda huko Misri, yaani kwa Farao na maafisa wake wote na nchi yake yote. 1234:12 Ebr 3:1-6; Kum 4:34Kwa kuwa hakuna mtu yeyote aliyewahi kuonyesha nguvu nyingi ama kutenda matendo ya kutisha ambayo Mose aliwahi kuyafanya mbele ya Israeli yote.

Hoffnung für Alle

5. Mose 34:1-12

Mose stirbt

1Nachdem Mose die Israeliten gesegnet hatte, verließ er die moabitische Steppe und stieg gegenüber von Jericho auf den Nebo, einen Gipfel des Berges Pisga. Dort zeigte ihm der Herr das ganze Land, das die Israeliten bekommen sollten: die Landschaft Gilead bis zum Gebiet von Dan, 2die Gebiete der Stämme Naftali, Ephraim und Manasse, das ganze Land Judas bis zum Mittelmeer, 3die Wüste Negev im Süden und die Ebene von der Palmenstadt Jericho bis hinab nach Zoar. 4Der Herr sprach zu ihm: »Dies ist das Land, das ich Abraham, Isaak und Jakob für ihre Nachkommen versprochen habe. Du wirst nicht hineingehen, aber ich wollte, dass du es mit eigenen Augen siehst.«

5Darauf starb Mose, der Diener des Herrn, dort im Land Moab, wie der Herr es bestimmt hatte. 6Der Herr selbst begrub ihn in einem Tal bei Bet-Peor. Niemand hat je das Grab gefunden.

7Bei seinem Tod war Mose 120 Jahre alt. Bis zuletzt waren seine Augen klar und seine Lebenskraft ungebrochen. 8Dreißig Tage lang hielten die Israeliten in der moabitischen Steppe für ihn die Totenklage.

9Dann trat Josua, der Sohn von Nun, an seine Stelle. Er war vom Geist Gottes erfüllt und besaß große Weisheit, seit Mose ihm die Hände aufgelegt hatte. Die Israeliten hörten auf ihn, wie der Herr es ihnen durch Mose befohlen hatte.

10Nach Mose hat es in Israel keinen Propheten mehr gegeben, dem der Herr von Angesicht zu Angesicht begegnet ist. 11Nie wieder sind so große Wunder durch einen Menschen geschehen; nichts lässt sich mit dem vergleichen, was Mose im Auftrag des Herrn in Ägypten vollbracht hat, um dem Pharao, seinen Hofbeamten und seinem ganzen Land Gottes Macht zu beweisen. 12Niemand hat seitdem so schreckliche und gewaltige Dinge vor den Augen aller Israeliten getan wie er.