Kumbukumbu 30 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 30:1-20

Mafanikio Baada Ya Kumgeukia Bwana

130:1 Kum 11:26; Law 26:40-45; Kum 4:32; 29:28; 1Fal 8:47Wakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popote Bwana Mungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa, 230:2 Kum 4:29-30hapo wewe na watoto wako mtakapomrudia Bwana Mungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo, 330:3 Za 14:7; 53:6; 85:1; 126:4; Yer 30:18; 33:11; Eze 16:53; Yoe 3:1; Sef 2:7; Kum 13:17; Mwa 48:21; 11:4; Kum 4:27; Isa 11:11; Yer 12:15; 16:15; 26:4; 29:14; 48:47; 49:6ndipo Bwana Mungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya. 430:4 Isa 17:6; 24:13; 27:12; 40:11; 41:5; 49:5; 56:8; Eze 20:34, 41; 34:13; Za 19:6; Neh 1:8-9; Isa 11:12; 42:10; 43:6; 48:20; 62:11; Yer 31:8, 10; 50:2Hata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka huko Bwana Mungu wako atakukusanya na kukurudisha. 530:5 Yer 29:14; Kum 7:13Yeye Bwana atakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako. 630:6 Kum 6:24; 10:16; 6:5; Yer 32:29Bwana Mungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi. 730:7 Mwa 12:3; Kum 7:15Bwana Mungu wako ataweka laana hizi zote juu ya adui zako ambao wanakuchukia na kukutesa. 8Utamtii tena Bwana na kuzishika amri zake zote ninazokupa leo. 930:9 Yer 1:10; 24:6; 31:28; 32:41; 42:10; 45:4; Kum 28:63; Eze 34:27; Yer 32:41; 33:9; Sef 3:17; Lk 15:6, 10, 32; Yn 15; 11Ndipo Bwana Mungu wako atakapokufanikisha sana katika kazi zote za mikono yako na katika uzao wa tumbo lako, wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako. Bwana atakufurahia tena na kukufanikisha, kama alivyowafurahia baba zako, 1030:10 Kum 28:61; 4:29kama ukimtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake ambayo yameandikwa katika Kitabu hiki cha Sheria, na kumgeukia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.

Uzima Na Mauti

1130:11 Za 19:8; Isa 45:19-23; 63:1Ninachokuagiza leo sio kigumu sana kwako au usichokiweza. 1230:12 Mit 30:4; Rum 10:6; Yn 3:13Hakiko juu mbinguni, ili uulize, “Ni nani atakayepanda mbinguni kukileta na kututangazia ili tuweze kutii?” 1330:13 Ay 28:14; Rum 10:7Wala hakiko ngʼambo ya bahari, ili uulize, “Ni nani atakayevuka bahari kwenda kukichukua na kututangazia ili tupate kutii?” 1430:14 Kum 6:6; Rum 10:8La hasha! Lile neno liko karibu sana nawe; liko kinywani mwako na ndani ya moyo wako ili uweze kulitii.

1530:15 Mit 10:16; 11:9; 12:28; 3:1-2; Kum 28:11; Za 25:13; 106:5; Mwa 2:17; Kum 11:26Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo. 1630:16 Kum 6:5; 4:1; 32:17; Neh 9:29Ninakuamuru leo kwamba umpende Bwana Mungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, naye Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.

17Lakini kama moyo wako ukigeukia mbali ukawa huna utii, kama umevutwa kuisujudia miungu mingine na kuiabudu, 1830:18 Kum 8:19nakutangazia leo hii kwamba hakika utaangamizwa. Hutaishi maisha marefu katika nchi unayovuka Yordani kuiingia na kuimiliki.

1930:19 Kum 4:26; 11:26Leo ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yako kwamba nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana. Basi sasa chagueni uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi, 2030:20 Kum 6:5; 4:1; 8:3; 32:47; 10:20; Za 27:1; Yn 5:26; Mdo 17:28; Mit 3:22; Mwa 12:7; Za 37:3na ili upate kumpenda Bwana Mungu wako, uisikilize sauti yake na kuambatana naye. Kwa kuwa Bwana ndiye uzima wako, na atakupa wingi wa siku ili upate kuishi katika nchi aliyoapa kuwapa baba zako Abrahamu, Isaki na Yakobo.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

申命記 30:1-20

歸向耶和華必蒙福

1「當我向你們陳明的這些祝福和咒詛都應驗在你們身上時,如果你們在你們的上帝耶和華驅逐你們去的各國中回想這些話, 2歸向你們的上帝耶和華,你們及子孫照我今天的吩咐全心全意地聽從祂的話, 3祂必改變你們被擄的境遇,憐憫你們,把你們從祂驅逐你們去的列國招聚回來。 4即使你們被驅逐到天涯,你們的上帝耶和華也會把你們帶回來, 5帶到你們祖先的土地上,使你們擁有那片土地,比你們祖先更加人丁興旺、繁榮昌盛。 6你們的上帝耶和華要潔淨你們和你們子孫的心,好讓你們全心全意地愛祂,並且存活。 7你們的上帝耶和華要把所有的咒詛加在你們的仇敵及憎惡你們、迫害你們的人身上。 8你們必再次聽從耶和華,遵行今天祂藉我吩咐你們的一切誡命。 9-10倘若你們聽從你們的上帝耶和華的話,遵守這律法書上的誡命和律例,全心全意地歸向祂,祂必使你們凡事蒙福、兒女眾多、牛羊成群、五穀豐登。因為祂必樂意再次賜福你們,像從前賜福你們祖先一樣。

生死抉擇

11「我今天頒佈給你們的誡命,對你們來說不難遵行,也非遙不可及。 12這誡命並非在天上,以致你們說,『誰替我們上天取下來,講給我們聽,讓我們遵行呢?』 13這誡命也不在海的彼岸,以致你們說,『誰替我們過海取來,講給我們聽,好讓我們遵行呢?』 14這誡命近在咫尺,就在你口裡,在你心中,好讓你們遵行。

15「看啊,今天我把生死禍福擺在你們面前。 16我今天吩咐你們要愛你們的上帝耶和華,遵行祂的旨意,遵守祂的誡命、律例和典章,以便你們可以存活,人口興旺,在你們將要佔領的土地上蒙祂賜福。 17但倘若你們心中偏離,不肯聽從,被引誘去祭拜、供奉別的神明, 18我今天警告你們,你們必定滅亡,在約旦河對岸——你們將要佔領的土地上無法長久。 19今天,我叫天地為你們作證,我已把生死禍福擺在你們面前。選擇生命吧,以便你們及子孫可以存活。 20要愛你們的上帝耶和華,聽從祂的話,倚靠祂,因為祂是你們的生命,祂必使你們長久住在祂起誓賜給你們祖先亞伯拉罕以撒雅各的土地上。」