Kumbukumbu 21 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 21:1-23

Upatanisho Kuhusu Mauaji

121:1 Hes 25:17; Za 9:12; Mit 28:17Kama mtu akikutwa ameuawa, naye amelala kwenye shamba katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki, wala haijulikani ni nani aliyemuua, 2wazee wenu na waamuzi watatoka na kupima umbali kutoka maiti alipolala mpaka kwenye miji ya jirani. 321:3 Hes 19:2Kisha wazee wa ule mji ulio karibu zaidi na yule maiti watamchukua mtamba ambaye hajapata kufanyishwa kazi na ambaye hajafungwa nira, 4na kumpeleka kwenye bonde ambalo halijapata kulimwa au kupandwa mazao na ambapo kuna chemchemi itiririkayo. Huko kwenye hilo bonde, wazee watamvunja yule mtamba shingo. 521:5 Mwa 48:20; Kut 39:43; Kum 17:8-11Makuhani, hao wana wa Lawi, watasogea mbele, kwa kuwa Bwana Mungu wenu, amewachagua kuhudumu na kutoa baraka katika jina la Bwana, na kuamua mashauri yote ya mabishano na mashambulio. 621:6 Mt 27:24; 1Nya 23:1321:6 Ay 9:30; Za 19:12; Yer 2:22; Mt 27:14; Ebr 9:10Ndipo wazee wote wa mji ulio karibu zaidi na huyo maiti watanawa mikono yao juu ya huyo mtamba ambaye shingo yake imevunjwa huko kwenye bonde, 721:7 2Sam 3:28nao watatangaza: “Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona likifanyika. 821:8 Hes 35:33-34; Yer 26:15; Eze 22:3; Yn 1:14Ee Bwana, ukubali upatanisho kwa watu wako Israeli, ambao umewakomboa, wala usiwahesabie watu wako hatia ya damu ya mtu asiyekuwa na hatia.” Nayo damu iliyomwagika itakuwa imefanyiwa upatanisho. 921:9 Kum 19:13Hivyo mtakuwa mmejitakasa wenyewe kutoka hatia ya kumwaga damu isiyokuwa na hatia, kwa kuwa mmefanya lile lililo sawa mbele za macho ya Bwana.

Kuoa Mwanamke Mateka

1021:10 Yos 21:44; 1Fal 8:46; 1Nya 9:1; Ezr 5:12; Yer 40:1; Eze 1:1; 17:12; Dan 2:25; Mik 4:10; 2Nya 32:8Mkienda vitani kupigana na adui zenu naye Bwana Mungu wenu akawatia adui mikononi mwenu, nanyi mkachukua mateka, 1121:11 Mwa 6:2; 34:8kama ukiona miongoni mwa mateka mwanamke mzuri wa sura nawe wavutwa naye, waweza kumwoa akawa mke wako. 1221:12 Law 14:9; Hes 8:7; 1Kor 11:5; Hes 6:9Mlete nyumbani mwako, anyoe nywele na kukata kucha zake, 1321:13 Za 45:10avue nguo alizokuwa amevaa alipotekwa. Baada ya kuishi nyumbani mwako na kumwombolezea baba yake na mama yake kwa mwezi mzima, ndipo utakapoweza kumwendea na kuwa mume wake naye atakuwa mke wako. 1421:14 Mwa 34:2; Amu 19:24Lakini kama hutaendelea kupendezwa naye, mwache aende popote anapotaka. Kamwe huwezi kumuuza au kumtendea kama mtumwa, kwa sababu utakuwa umemvunjia heshima.

Haki Ya Mzaliwa Wa Kwanza

1521:15 Mwa 4:19; 29:33Kama mwanaume ana wake wawili, naye anampenda mmoja na mwingine hampendi na wote wawili wamemzalia wana wa kiume, lakini mwana mzaliwa wa kwanza ni wa yule mke asiyempenda, 1621:16 1Nya 26:10; Rum 8:29wakati anapotoa wosia wa mali yake kwa wanawe, kamwe asitoe haki za mzaliwa wa kwanza kwa mwana wa mke ampendaye kwa upendeleo, badala ya mzaliwa hasa wa kwanza, ambaye ni mwana wa mke ambaye hampendi. 1721:17 2Fal 2:9; Isa 40:2; 61:7; Zek 9:12; Mwa 49:3; 25:31; Lk 15:12; 1Nya 5:1Ni lazima amkubali mwana wa mke asiyempenda kama mzaliwa wa kwanza kwa kumpa sehemu ya vile vyote alivyo navyo maradufu. Mwana huyo ni ishara ya kwanza ya nguvu za baba yake. Haki ya mzaliwa wa kwanza ni yake yeye.

Mwana Mwasi

1821:18 Za 78:8; Yer 5:23; Sef 3:1; Mit 30:17; Mwa 31:35; Mit 1:8; Isa 30:1; Efe 6:1-3; Kut 20:12; 21:15, 17; Law 19:3; 21:9Kama mtu ana mwana mkaidi na mwasi ambaye hamtii baba yake na mama yake, na hasikii wazazi wanapomrudi, 19baba yake na mama yake watamleta kwa wazee kwenye lango la mji wake. 20Watawaambia wazee, “Huyu mwanetu ni mkaidi na mwasi. Hatutii sisi, yeye ni mpotovu na mlevi.” 2121:21 Law 20:9; Kum 19:19; 1Kor 5:13; Kum 13:11; 1Sam 26:16Kisha wanaume wote wa mjini mwake watampiga kwa mawe mpaka afe. Ndivyo imewapasa kuondoa maovu kati yenu. Israeli yote itasikia hili na kuogopa.

Sheria Mbalimbali

2221:22 Kum 22:26; Mt 26:66; Mk 14:64; Mdo 23:29Kama mtu ana hatia ya kosa linalompasa kuuawa naye akauawa, mwili wake utaangikwa mtini, 2321:23 Yos 8:29; 10:27; Yn 19:31; Eze 39:12; Ezr 6:11; Es 2:23; 7:9; 8:7; 9:13, 25; Isa 50:11; Gal 3:13; Law 18:25kamwe msiuache mwili wake mtini usiku kucha. Hakikisheni mnauzika mwili wake siku ile ile, kwa sababu kila mtu anayeangikwa mtini yupo chini ya laana ya Mungu. Msiinajisi nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu.

Japanese Contemporary Bible

申命記 21:1-23

21

町の外での殺人

1主の与えてくださった約束の地で殺人事件があり、被害者は町の外で発見され、現場を目撃した者がいない場合は次のようにしなさい。 2まず、長老と裁判官が、死体から最も近い町はどこか調べます。 3どこかわかったら、その町の長老が、まだ農作業に使われたことのない雌の子牛を引いて、 4渓流のある開墾されていない谷間へ行き、そこで子牛の首を折ります。 5それから祭司たちが進み出ます。主は、聖所での仕事や人々を祝福することばかりでなく、争いごとや傷害事件が起きたとき、判断を下すためにも祭司を選ばれたのです。 6そこで、町の長老たちは子牛の上で手を洗いきよめ証言します。 7『被害者に手をかけたのは私たちではありません。私たちが全く知らないうちに事件は起きたのです。 8主よ、あなたが買い取られた民イスラエルを、どうぞお赦しください。私たちに、罪のない者を殺した罪を負わせないでください。』 9このように、主が正しいとみなされる方法で罪悪を取り除きなさい。

捕虜の娘との結婚

10主が敵をあなたの手に渡され、戦いに勝ち、捕虜を連れて引き揚げるとき、 11その中に美しい娘がいて妻にしたいと思ったなら、 12家へ連れ帰りなさい。娘は髪をそり、つめを切り、 13すっかり着替えをし、捕虜になった時に身に着けていた物を全部はずして、あなたの家で、自分の両親のために一か月の間、喪に服します。そのあとで結婚しなさい。 14彼女を好きでなくなったら、自由の身にして去らせなさい。彼女を辱めたのですから、売り払ったり、奴隷のように扱ったりしてはいけません。

長男の権利

15妻が二人あり、どちらにも子どもがある場合、長男の母親である妻は嫌いで、 16次男の母親である妻のほうを愛しているからといって、次男に長男としての財産を与えることはできません。 17嫌われている母親の子でも、父親には初めての子であり、長男の権利を持っているのだから、兄に弟の二倍の財産を与えなければなりません。

反抗的な息子

18いくら懲らしめても親の言うことを聞かない、強情で反抗的な息子は、 19町の長老のところへ連れて行きなさい。 20『息子は強情っ張りのうえに反抗的で、とても手に負えません。親の言うことなどそっちのけで、大酒ばかり飲んで、遊び暮らしています』と訴えるのです。 21そのあと、町の者が息子に石を投げつけて殺します。二度と若者たちがそんな親不孝をしないように見せしめとするためです。

木にかけられた者

22人が死刑に当たる罪を犯し、殺され、木にかけられる場合は、 23次の日までそのままにしてはいけません。その日のうちに埋葬しなさい。木にかけられた者は、神にのろわれた者だからです。あなたの神、主に与えられた地を汚してはいけません。