Kumbukumbu 18 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 18:1-22

Sadaka Kwa Makuhani Na Walawi

118:1 Yer 33:21; Hes 18:8, 20; 1Kor 9:13Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya Bwana za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao. 218:2 Hes 18:20; Yos 13:14Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi.

318:3 Kut 29:27; Law 1:5; 7:28-34; Hes 18:12Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo. 418:4 Kut 22:29; Hes 18:12Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu, 518:5 Kut 28:1; 29:9; Kum 10:8; Kut 29:9kwa kuwa Bwana Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la Bwana siku zote.

618:6 Hes 35:2-3; Kum 12:5Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo Bwana atapachagua, 718:7 1Fal 18:32; 22:16; Za 118:26anaweza akahudumu katika jina la Bwana Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za Bwana. 818:8 Hes 18:24; 2Nya 31:4; Neh 12:44, 47; 13:12Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake.

Matendo Ya Machukizo

918:9 Kum 9:5; 12:29-31; Law 18:3; 2Fal 21:2; 2Nya 28:3; 33:2; 34:33; Ezr 6:21; 9:11; Yer 44:4Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko. 1018:10 Law 18:21; 1Sam 15:23; Kut 7:11; Law 19:31; Kum 12:31Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi, 1118:11 Isa 47:9; Kut 22:18; 1Sam 28:13wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu. 1218:12 Law 18:24; Kum 9:4Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa Bwana, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana Bwana Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu. 1318:13 Mwa 6:9; 17:1; Za 119:1; Mt 5:48Kamwe msilaumiwe mbele za Bwana Mungu wenu.

Nabii

1418:14 2Fal 21:6Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, Bwana Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo. 1518:15 Mt 21:11; Lk 2:25-35; Yn 1:21; Mdo 3:22; 7:37; Hes 24:17; Isa 11:1; 61:1; Mt 11:3; 21:11; Lk 2:25-34; 4:16-22; 7:16; 24:19; Yn 4:19-26; 6:14; 7:40Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye. 1618:16 Kut 20:19; Kum 5:23-27Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba Bwana Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya Bwana Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.”

17Bwana akaniambia: “Wanachosema ni vyema. 1818:18 Mwa 20:7; Isa 2:3; 26:8; 51:4; Mik 4:2; Kut 4:12; Yn 4:25-26; 14:24; Mdo 3:22; Yn 17:8; 4:25; 8:28; 12:49, 50Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru. 1918:19 Kut 23:21; Law 19:12; 2Fal 2:24; Yos 22:23; Mdo 3:23; Ebr 12:25Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha. 2018:20 Kut 23:13; Kum 13:1-5; 17:12; Yer 14:14; 2:8; Zek 13:3Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.”

21Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na Bwana?” 2218:22 Kum 13:2; 1Sam 3:20; 1Fal 22:28; Yer 28:9Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la Bwana hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao Bwana hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.

Nueva Versión Internacional

Deuteronomio 18:1-22

Ofrendas para los sacerdotes levitas

1La tribu de Leví, a la que pertenecen los sacerdotes levitas, no tendrá patrimonio alguno en Israel. Vivirán de los sacrificios ofrecidos al Señor, pues esa es su herencia. 2Los levitas no tendrán herencia entre sus hermanos; el Señor mismo es su herencia, según les prometió.

3Cuando alguien del pueblo sacrifique un buey o un cordero, los sacerdotes tendrán derecho a la espaldilla, las quijadas y los órganos internos. 4También les darás las primicias de tu grano, tu vino y tu aceite, así como la primera lana que esquiles de tus ovejas. 5Porque el Señor tu Dios los eligió a ellos y a su descendencia, de entre todas tus tribus, para que estuvieran siempre en su presencia, ministrando en su nombre.

6Si un levita que viva en alguna de las ciudades de Israel, respondiendo al impulso de su corazón, se traslada al lugar que el Señor haya elegido, 7podrá ministrar en el nombre del Señor su Dios como todos los otros levitas que sirvan allí, en la presencia del Señor. 8Recibirá los mismos beneficios que ellos además de su patrimonio familiar.

Costumbres abominables

9Cuando entres en la tierra que te da el Señor tu Dios, no aprendas las costumbres abominables de esas naciones. 10Nadie entre los tuyos deberá sacrificar a su hijo o hija en el fuego ni practicar la adivinación, agorería o hechicería; 11tampoco hacer conjuros, servir de médium, practicar espiritismo o consultar a los muertos. 12Cualquiera que practique estas costumbres se hará abominable al Señor y por causa de ellas el Señor tu Dios expulsará de tu presencia a esas naciones. 13A los ojos del Señor tu Dios serás intachable.

El profeta

14Las naciones cuyo territorio vas a poseer consultan todo tipo de adivinadores, pero a ti el Señor tu Dios no te ha permitido hacer nada de eso. 15El Señor tu Dios hará surgir para ti y en medio de ti, de entre tus hermanos, un profeta como yo. A él sí lo escucharás. 16Eso fue lo que pediste al Señor tu Dios en Horeb, el día de la asamblea, cuando dijiste: «No quiero seguir escuchando la voz del Señor mi Dios ni volver a contemplar este enorme fuego, no sea que muera».

17Y me dijo el Señor: «Está bien lo que ellos dicen. 18Por eso levantaré entre sus hermanos un profeta como tú; pondré mis palabras en su boca y él les dirá todo lo que yo le mande. 19Si alguien no presta oído a las palabras que el profeta proclame en mi nombre, yo mismo le pediré cuentas. 20Pero el profeta que se atreva a hablar en mi nombre y diga algo que yo no haya mandado a decir morirá. Lo mismo sucederá al profeta que hable en nombre de otros dioses».

21Tal vez te preguntes: «¿Cómo podré reconocer un mensaje que no provenga del Señor?». 22Si lo que el profeta proclame en nombre del Señor no se cumple ni se realiza, será señal de que su mensaje no proviene del Señor. Ese profeta habrá hablado con presunción. No le temas.