Kumbukumbu 17 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 17:1-20

117:1 Kut 12:5; Law 22:20; Kum 7:25; 15:21; Mal 1:8, 13Msimtolee Bwana Mungu wenu dhabihu ya maksai au kondoo ambaye ana dosari yoyote au hitilafu ndani yake, kwa kuwa hilo litakuwa chukizo kwake.

217:2 Kum 13:6-11Ikiwa mwanaume au mwanamke anayeishi kati ya mojawapo ya miji akupayo Bwana, anakutwa anafanya uovu mbele za Bwana Mungu wenu, kwa kuvunja Agano lake, 317:3 Yer 7:31; Kut 22:20; Mwa 1:16; 2:1; 37:9; Ay 31:26naye amekwenda kinyume na agizo langu kuabudu miungu mingine na kuisujudia, kama vile jua, mwezi au nyota za angani, 417:4 Kum 22:20; 13:12-14hili likiwa limeletwa mbele yenu, ni lazima kulichunguza kikamilifu. Ikiwa ni kweli na kuwa limehakikishwa kwamba hili ni chukizo lililofanyika katika Israeli, 517:5 Law 24:14mchukueni huyo mwanaume au mwanamke ambaye amelifanya tendo hili ovu kwenye lango la mji wenu na kumpiga mawe mtu huyo mpaka afe. 617:6 Hes 35:30; Kum 19:15; Mt 18:16; Yos 7:25; Yn 8:1717:6 Hes 35:30; Mt 18:16; Yn 8:17; 2Kor 13:1; 1Tim 5:19; Ebr 10:28Kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu mtu huyo atauawa, bali hakuna mtu atakayeuawa kwa ushuhuda wa shahidi mmoja tu. 717:7 Yn 8:7; Law 24:14; Mdo 7:58; Kum 13:5, 9; 1Kor 15:13Ni lazima kwanza mikono ya mashahidi itangulie kumuua huyo mtu, kisha mikono ya watu wote. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu.

Mahakama Za Sheria

817:8 Kut 21:6, 13; 2Nya 19:10; Kum 12:5; Za 122:3-5; Hag 2:11; Mal 2:7; Hes 35:11; Kum 19:17Kama mashauri yanaletwa katika mahakama zenu ambayo ni magumu zaidi kwenu kuyaamua, ikiwa ni umwagaji wa damu, madai au mashambulio, yapelekeni mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua. 917:9 Kum 24:8; 27:9; Kut 21:6; Mwa 25:22; Kum 19:17; Eze 44:24; Hag 2:11; Amu 4:5; 1Fal 3:16Nendeni kwa makuhani, ambao ni Walawi, na kwa mwamuzi ambaye atakuwa kazini wakati huo. Ulizeni kwao nao watawapa maamuzi. 10Ni lazima mtende sawasawa na maamuzi watakayowapa mahali Bwana atakapopachagua. Kuweni waangalifu kufanya kila kitu watakachowaongoza kufanya. 1117:11 Law 10:11; Kum 5:32; 25:1Fanyeni sawasawa na sheria wanayowafundisha na maamuzi wanayowapa. Msigeuke mkono wa kuume au kushoto kuacha kufanya yale wanayowaambia. 1217:12 Hes 15:30; 16:9-13; Mwa 17:14; Kum 13:11; 18:20; 19:20; 1Fal 18:40; Yer 14:14; Hos 4:4; Zek 13:3; Kum 13:5Mwanaume atakayeonyesha dharau kwa mwamuzi au kwa kuhani ambaye amewekwa kumtumikia Bwana Mungu wenu lazima auawe. Lazima mwondoe uovu katika Israeli. 1317:13 Kum 13:11Watu wote watasikia na kuogopa, nao hawatakuwa wenye kudharau tena.

Mfalme

1417:14 Hes 33:53; Yos 21:43; 1Sam 8:5-9; 19:20; 10:19Wakati utakapoingia katika nchi anayowapa Bwana Mungu wenu kuimiliki na kukaa humo, nanyi mkasema, “Na tumweke mfalme juu yetu kama mataifa yanayotuzunguka,” 1517:15 1Sam 16:3; 2Sam 5:3; Yer 30:21kuweni na uhakika wa kumweka mfalme juu yenu ambaye Bwana Mungu wenu atamchagua. Ni lazima atoke miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msimweke mgeni juu yenu ambaye si ndugu wa Kiisraeli. 1617:16 Isa 2:7; 30:16; 1Sam 8:11; 1Fal 4:26; 9:19; 10:26; 2Nya 1:14; Za 20:7; Isa 31:1; Yer 42:14; 1Fal 10:28-29; Eze 17:15; Kut 13:17Hata hivyo, kamwe mfalme asijipatie hesabu kubwa ya farasi kwa ajili yake mwenyewe, au kuwafanya watu warudi Misri ili kupata farasi zaidi, kwa maana Bwana amekuambia, “Hamtairudia njia ile tena.” 1717:17 Kut 34:16; 2Sam 5:13; 12:11; 1Fal 11:3; 2Nya 11:21; Za 31:3Kamwe asioe wake wengi, la sivyo moyo wake utapotoka. Kamwe asijilimbikizie kiasi kikubwa cha fedha na dhahabu.

1817:18 2Fal 11:12; Kum 31:9; 2Fal 22:8Atakapokuwa amekalia kiti cha ufalme wake, ajiandikie kwenye kitabu nakala ya sheria kwa ajili yake mwenyewe kutoka zile sheria za makuhani ambao ni Walawi. 1917:19 Yos 8; Za 119:97Atakuwa na nakala hiyo, naye ataisoma siku zote za maisha yake ili kwamba ajifunze kumheshimu Bwana Mungu wake na kufuata kwa uangalifu maneno yote ya sheria hii na amri hizi, 2017:20 Kum 5:32naye asijifikirie kuwa ni bora kuliko ndugu zake na kuipotosha sheria. Ndipo yeye na wazao wake watatawala katika ufalme wake kwa muda mrefu katika Israeli.

New International Version

Deuteronomy 17:1-20

1Do not sacrifice to the Lord your God an ox or a sheep that has any defect or flaw in it, for that would be detestable to him.

2If a man or woman living among you in one of the towns the Lord gives you is found doing evil in the eyes of the Lord your God in violation of his covenant, 3and contrary to my command has worshiped other gods, bowing down to them or to the sun or the moon or the stars in the sky, 4and this has been brought to your attention, then you must investigate it thoroughly. If it is true and it has been proved that this detestable thing has been done in Israel, 5take the man or woman who has done this evil deed to your city gate and stone that person to death. 6On the testimony of two or three witnesses a person is to be put to death, but no one is to be put to death on the testimony of only one witness. 7The hands of the witnesses must be the first in putting that person to death, and then the hands of all the people. You must purge the evil from among you.

Law Courts

8If cases come before your courts that are too difficult for you to judge—whether bloodshed, lawsuits or assaults—take them to the place the Lord your God will choose. 9Go to the Levitical priests and to the judge who is in office at that time. Inquire of them and they will give you the verdict. 10You must act according to the decisions they give you at the place the Lord will choose. Be careful to do everything they instruct you to do. 11Act according to whatever they teach you and the decisions they give you. Do not turn aside from what they tell you, to the right or to the left. 12Anyone who shows contempt for the judge or for the priest who stands ministering there to the Lord your God is to be put to death. You must purge the evil from Israel. 13All the people will hear and be afraid, and will not be contemptuous again.

The King

14When you enter the land the Lord your God is giving you and have taken possession of it and settled in it, and you say, “Let us set a king over us like all the nations around us,” 15be sure to appoint over you a king the Lord your God chooses. He must be from among your fellow Israelites. Do not place a foreigner over you, one who is not an Israelite. 16The king, moreover, must not acquire great numbers of horses for himself or make the people return to Egypt to get more of them, for the Lord has told you, “You are not to go back that way again.” 17He must not take many wives, or his heart will be led astray. He must not accumulate large amounts of silver and gold.

18When he takes the throne of his kingdom, he is to write for himself on a scroll a copy of this law, taken from that of the Levitical priests. 19It is to be with him, and he is to read it all the days of his life so that he may learn to revere the Lord his God and follow carefully all the words of this law and these decrees 20and not consider himself better than his fellow Israelites and turn from the law to the right or to the left. Then he and his descendants will reign a long time over his kingdom in Israel.