Kumbukumbu 15 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 15:1-23

Mwaka Wa Kufuta Madeni

(Walawi 25:1-7)

115:1 Kum 31:10; Neh 10:31; Kut 23:10; Yer 34:14Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni. 2Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Bwana wa kufuta madeni umetangazwa. 315:3 Mwa 31:15; Kum 23:20; 28:12; Rut 2:10Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako. 415:4 Kum 28:5, 8Hata hivyo, hapatakuwepo maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana, 515:5 Kut 15:26; Kum 7:12; 28:1ikiwa tutamtii Bwana Mungu wenu kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo. 615:6 Kum 28:12-13, 44; Mit 22:7Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.

715:7 Mt 26:11; 18:30; 1Yn 3:17Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini. 815:8 Mt 5:42; Lk 6:34; Mdo 24:17; Law 25:35; Gal 2:10Afadhali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji. 915:9 Mt 20:15; Kut 22:23; Ay 5:15; Yak 5:4; Amo 5:11; Mit 28:22; Za 140:12Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonyesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Bwana dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi. 1015:10 2Kor 9:5; Kum 14:29; 24:19; Mt 25:40; Mdo 20:35; Rum 12:8; 1Tim 6:18; 1Pet 4:11Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Bwana Mungu wenu atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako. 1115:11 Mt 26:11; Mk 14:7; Yn 12:8Siku zote watakuwepo watu maskini katika nchi. Kwa hiyo ninawaamuru mwe na mikono iliyokunjuliwa kuwaelekea ndugu zenu, kuwaelekea maskini na wahitaji katika nchi yenu.

Kuwaacha Huru Watumwa

(Kutoka 21:1-18)

1215:12 Yer 34:14; Kut 21:2; Law 25:39Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru. 13Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu. 1415:14 Hes 18:27; Mit 10:22Mpe kwa uhuru kutoka zizi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka na kutoka mashinikizo yako ya kukamulia divai. Mpe kama vile ambavyo Bwana Mungu wako alivyokubariki. 1515:15 Kut 13:3; Yer 34:13; Kut 20:2; Kum 4:34; 9:26; 16:12; 24:18; Yer 16:14; 27:7Kumbukeni kuwa ninyi mlikuwa watumwa huko Misri naye Bwana Mungu wenu aliwakomboa. Ndiyo sababu nimewapa agizo hili leo.

1615:16 Kum 21:5-6Lakini mtumishi wako akikuambia, “Sitaki kukuacha,” kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako naye anaridhika nawe, 17ndipo utachukua chuma kidogo utoboe sikio lake mpaka hicho chuma kiingie kwenye ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako wa maisha. Ufanye vivyo hivyo kwa mtumishi wa kike.

1815:18 Isa 16:14; 21:16Usifikiri kuwa kuna ugumu kumwacha mtumishi wako huru, kwa sababu utumishi wake kwako kwa miaka hii sita umekuwa wa thamani mara mbili ya ujira wa mtumishi wa kuajiriwa. Naye Bwana Mungu wenu atakubarikia kwa kila kitu utakachofanya.

Wazaliwa Wa Kwanza Wa Wanyama

1915:19 Law 27:9; Kut 13:2; Mwa 4:4; Kut 22:30Wekeni wakfu kwa Bwana Mungu wenu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa makundi yenu ya ngʼombe na ya mbuzi na kondoo. Maksai walio wazaliwa wa kwanza msiwafanyize kazi, wala msinyoe manyoya ya wazaliwa wa kwanza wa kondoo. 2015:20 Law 7:15-18; Kum 12:5-7; 14:23Kila mwaka ninyi na jamaa zenu mtapaswa kuwala mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua. 2115:21 Kut 12:5; Law 22:19-25; Kum 17:1; Mal 1:8, 13Kama mnyama ana dosari, akiwa ni kilema au kipofu au kama ana kilema kibaya, kamwe usimtoe dhabihu kwa Bwana Mungu wenu. 2215:22 Kum 12:15, 22Itawapasa kumla ninyi wenyewe katika miji yenu. Wote wasio safi na walio safi kwa desturi za kiibada mwaweza kula kama vile mnavyokula paa au kulungu. 2315:23 Mwa 9:4; Kum 12:16; Eze 33:25; Law 7:26; 17:10Lakini kamwe msinywe damu; imwageni ardhini kama maji.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

申命记 15:1-23

安息年

1“每逢第七年末,你们要免除他人的债务。 2你们要这样做,所有债主都要免除同胞所欠的债务,不可向他们追讨,因为宣布免除债务的是耶和华。 3你们可以向外族人讨债,但无论同胞欠你什么债务,都要免除。 4-5只要你们听从你们上帝耶和华的话,谨遵我今天吩咐你们的诫命,祂必使你们在这片祂赐给你们作产业的土地上蒙福,你们中间不会有穷人。 6你们的上帝耶和华必照祂的应许赐福给你们,你们必借贷给多国,却不需要向他们借贷。你们必统治多国,却不被他们统治。

7“在进入你们的上帝耶和华将要赐给你们的土地后,如果你们居住的城中有贫穷的同胞,你们不可硬着心肠拒施援手。 8他们所需要的,你们要慷慨地借给他们。 9你们要谨慎,不可因为免除债务的第七年将近,就心怀恶念,对贫穷同胞冷眼相待,拒施援手。否则,他会求告耶和华,那时你们便有罪了。 10你们要慷慨给予,并且无怨无悔,因为耶和华必在你们所做的一切事上赐福给你们。 11你们居住的地方总会有穷人,所以我吩咐你们要慷慨地帮助贫穷或有需要的同胞。

12“如果你们的希伯来同胞,不论男女,卖身给你们做奴隶,他们要服侍你们六年,到第七年,你们要给他们自由。 13你们不可让他们空手离去, 14要慷慨地把你们的上帝耶和华赐给你们的羊、五谷和酒分给他们。 15要记住,你们曾在埃及做奴隶,你们的上帝耶和华拯救了你们。所以,我今天吩咐你们这样做。 16如果你们的奴隶因为爱你们和你们的家人,与你们相处融洽,不愿意离去, 17你们就要让他靠在门上,用锥子在他耳朵上扎个洞,他便终身成为你们的奴隶。对待婢女也要这样。 18你们释放奴隶时,不要不情愿,因为他们服侍你们六年,所做的是普通雇工的两倍。而且,你们的上帝耶和华也会在你们所做的一切事上赐福给你们。

头生的牛羊

19“你们要把头生的公牛和公羊分别出来,献给你们的上帝耶和华。不可用头生的公牛耕田,也不要剪头生公羊的毛。 20每年,你们全家要去你们的上帝耶和华选定的地方,在祂面前吃这些头生的牛羊。 21如果这些牛羊有什么残疾,如瘸腿、瞎眼或其他残疾,就不可献给你们的上帝耶和华。 22要在你们的城里吃这些牛羊。洁净的人和不洁净的人都可以吃,就像吃羚羊和鹿一样。 23但不可吃它们的血,要把血倒在地上,像倒水一样。