Kumbukumbu 14 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 14:1-29

Vyakula Vilivyo Najisi Na Vilivyo Safi

(Walawi 11:1-47)

114:1 Yn 1:12; Rum 8:14; 9:8; Yer 16:6; Mwa 6:2-4; Kut 4:22-23; Gal 3:26; 1The 4:13Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa, 214:2 Mwa 28:14; Kut 8:22; 22:31; Isa 6:13; Mt 2:15; Law 20:26; Rum 12:1; Kum 7:6; 26:18-1914:2 Kut 19:5; 2Sam 7:23, 24kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.

314:3 Eze 4:14; Isa 65:4; Mdo 10:13; Rum 14:14Msile kitu chochote ambacho ni machukizo. 414:4 Mdo 10:14; Law 7:23; 11:2-45Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi, 514:5 Kum 12:15; Ay 39:1; Za 104:18kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani. 6Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua. 7Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada. 814:8 Law 5:12; 11:26-27Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.

9Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba. 10Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.

11Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi. 1214:12 Law 11:13Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu, 1314:13 Mwa 2:11; Isa 34:15kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote, 1414:14 Mwa 8:17kunguru wa aina yoyote, 15mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote, 16bundi, mumbi, bundi mkubwa, 1714:17 Za 102:6; Isa 13:21; 14:23; 34:11; Sef 2:14mwari, nderi, mnandi, 18korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.

19Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale. 2014:20 Law 20:25Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.

2114:21 Law 11:39; 14:2; 17:15; Kut 23:19; 22:31; Law 22:8; Eze 44:31Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu.

Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.

Zaka

2214:22 Mwa 14:20; Law 27:30; Hes 18:21; Neh 10:37; Kum 12:6, 17Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka. 2314:23 Kum 12:5, 17, 18; Za 4:7; 1Fal 3:2; Kum 4:10; Za 22:23; 33:8; Mal 2:5; Mit 3:13; Isa 8:13; Yer 32:38-41; Ebr 12:28Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima. 2414:24 Kum 12:21Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana), 2514:25 Mt 21:12; Yn 2:14basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua. 2614:26 Law 10:9; 23:40; Mhu 10:16-17; Kum 12:7-8Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi. 2714:27 Kum 12:19; Hes 18:20; 26:62; Kum 18:1-2; Rum 13:4; 15:27; 1Kor 9:1-14Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.

2814:28 Law 27:30; Kum 26:12Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu, 2914:29 Mwa 47:22; Hes 26:62; Kum 16:11; 24:19-21; Za 94:6; Isa 1:17; 58:6; Kum 6:11; 15:10; Za 41:1; Mit 22:9; Mt 3:10; Kum 10:18; Eze 22:7, 29; Lk 14:12; Ebr 13:2; Mal 3:10; Lk 11:41; 2Kor 9:6-11ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.

Japanese Contemporary Bible

申命記 14:1-29

14

神の民として

1あなたがたは神の民ですから、〔異邦人が偶像を拝むときするように〕体を傷つけたり、葬式の時に額をそったりしてはいけません。 2あなたがたは特別な民なのです。神様が地上のどの民よりも、あなたがたをご自分のものとしてお選びになったからです。

きよい動物と汚れた動物

3-5礼拝規定で汚れたものとみなされる動物を食べてはいけません。食べていい動物は次のとおりです。牛、羊、やぎ、鹿、かもしか、のろじか、野やぎ、くじか(大かもしかの一種)、大鹿、野羊。

6ひづめが分かれていて反芻する動物は、食べてかまいません。 7それ以外のものはだめです。らくだ、野うさぎ、岩だぬきなどは反芻しますが、ひづめが分かれていないので食べられません。 8その反対に、豚はひづめが分かれていますが、反芻しないので、やはり食べてはいけません。このような動物は死体にも触れてはいけません。

9水中の動物では、ひれとうろこのあるものは食べてかまいません。 10それ以外はみな汚れたものです。

11-18鳥は、次のものを除いて全部食べられます。はげわし、はげたか、黒はげたか、黒とび、はやぶさ、とびの類、からすの類全部、だちょう、よたか、かもめ、たかの類、ふくろう、みみずく、白ふくろう、ペリカン、野がん、鵜、こうのとり、さぎの類、やつがしら、こうもり。

19-20例外もありますが、羽のある昆虫類は汚れたもので、食べてはいけません。

21自然に死んだものは食べてはいけません。ただ、在留外国人は別です。その肉を彼らに与えても、売ってもかまいません。しかし、あなたがたは主にとってきよい者とされているのですから、食べてはいけません。

子やぎをその母の乳で煮てはいけません。

収穫の十分の一をささげよ

22毎年、収穫の十分の一をささげなさい。 23それを、主が聖所としてお選びになった場所へ持って行き、いっしょに食べなさい。穀物、新しいぶどう酒、オリーブ油、牛や羊の初子などの十分の一です。こうして、いつも神を第一にして生きることを学ぶのです。 24聖所が遠すぎてささげ物を持って行けないときは、 25それを売った代金を持って行きなさい。 26着いてから、その金で牛や羊、ぶどう酒や強い酒など、何でも欲しい物を買い、家族とともに主の前で楽しく食事し、祝い合いなさい。 27同じ町に住むレビ人にも、忘れずにその一部を分け与えなさい。レビ人には土地もなければ、収穫もないからです。

28三年ごとに、その年の十分の一のささげ物を、それぞれの地域の福祉に使いなさい。 29財産のないレビ人や外国人、町に住む未亡人や身寄りのない子に与えるのです。そうすれば、だれもが食べて満ち足り、主があなたも、あなたの仕事も祝福してくださいます。