Kumbukumbu 10 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 10:1-22

Vibao Vingine Vya Amri Kumi

(Kutoka 34:1-10)

110:1 Kut 34:2; 25:10Wakati ule Bwana aliniambia, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza uje kwangu juu mlimani. Pia utengeneze Sanduku la mbao. 210:2 Kut 25:16, 21; 2Nya 5:10; 6:11Nitaandika juu ya vibao maneno yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza, ambavyo ulivivunja. Kisha utaviweka ndani ya Sanduku.”

310:3 Kut 37:1-9; 34:4; 26:5Hivyo nikatengeneza Sanduku kwa mti wa mshita, nikachonga pia vibao vya mawe kama vile vya kwanza, kisha nikakwea mlimani nikiwa na vibao viwili mikononi mwangu. 410:4 Kut 24:12; 34:28; 20; 1; Kum 9:10; Yer 31:33Bwana akaandika juu ya hivi vibao kile alichokuwa amekiandika kabla, Amri Kumi alizokuwa amewatangazia juu mlimani, kutoka kwenye moto siku ile ya kusanyiko. Bwana akanikabidhi. 510:5 Kut 19:11; 25:10; 25:21; 34:29; 40:21; 1Sam 8:3; 1Fal 8:9Kisha nikashuka kutoka mlimani na kuweka vibao ndani ya Sanduku nililokuwa nimelitengeneza, kama Bwana alivyoniagiza, navyo viko huko sasa.

610:6 Hes 33:30; 27:13; 20:25-28; Kut 6:23(Waisraeli walisafiri kutoka visima vya Yaakani hadi Mosera. Huko Aroni alifariki na kuzikwa, naye Eleazari mwanawe akachukua nafasi yake kama kuhani. 710:7 Hes 33:32-34; Za 42:1; Wim 5:12; Isa 32:2Kutoka pale, walisafiri hadi Gudgoda wakaendelea mpaka Yotbatha, nchi yenye vijito vya maji. 810:8 Hes 3:6; 10:33; 16:9; Mwa 48:20; 1Nya 23:26; Kum 18:5; 21:5; Law 9:22Wakati huo Bwana aliteua kabila la Lawi kulibeba Sanduku la Agano la Bwana, kusimama mbele za Bwana ili kutoa huduma, na kutangaza baraka kwa Jina lake, kama wanavyofanya mpaka leo. 910:9 Hes 18:20; Eze 44:28Hiyo ndiyo sababu ya Walawi kutokuwa na sehemu wala urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama Bwana Mungu wao alivyowaambia.)

1010:10 Kut 33:17; 34:28; Kum 9:18-19; 25Basi nilikaa mlimani kwa siku arobaini usiku na mchana, kama nilivyofanya mara ya kwanza, pia Bwana alinisikiliza hata wakati huu. Haikuwa nia yake kuwaangamiza. 11Bwana akaniambia, “Nenda, ukawaongoze watu katika njia yao ili kwamba waweze kuingia na kuimiliki nchi ile niliyowaapia baba zao kuwapa.”

Mche Bwana

1210:12 Mik 6:8; Kut 20:20; 1Fal 2:3; 3:3; 4:4; Kum 5:32; 5:33; 6:13; 6:5; 11:13; 28:47; Mt 22:37; 1Tim 1:5; Za 100:2; Kum 6:5; Za 119:2; Kum 5:32Na sasa, ee Israeli, Bwana Mungu wako anataka nini kwako ila kumcha Bwana Mungu wako, kwenda katika njia zake, kumpenda na kumtumikia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote, 1310:13 Kum 4:2; 5:33; 6:25na kuyashika maagizo ya Bwana na amri zake ninazokupa leo kwa mafanikio yako mwenyewe?

1410:14 Za 148:4; Isa 19:1; Hab 3:8; Neh 9:6; Ay 35:5; Za 8:3; 89:11; 104:3; Kum 33:26; Za 115:16; 1Fal 8:27; Kut 19:5; Za 24:1; Mdo 17:24Mbingu, hata mbingu za juu sana, dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, ni mali ya Bwana Mungu wako. 1510:15 Kum 4:37; Za 105:6; 135:4; Hes 14:8; Rum 11:28; 1Pet 2:9Hata hivyo Bwana alikuwa na shauku na baba zako, akawapenda na akawachagua ninyi, wazao wao, kuliko mataifa yote, kama ilivyo leo. 1610:16 Mwa 17:11; Law 26:41; Kum 30:6; Yer 32:39; Kut 32:9; 9:13; Yer 4:4; Kum 9:6Kwa hiyo tahirini mioyo yenu, na msiwe na shingo ngumu tena. 1710:17 Yos 22:22; Za 135:9; 136:2; Dan 2:47; 11:36; Za 136:3; 1Tim 6:15; Kum 7:21; 1:17; Mal 2:9; Kut 23:8; Law 19:16; Efe 6:9Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye uweza na wa kutisha, ambaye hana upendeleo na hapokei rushwa. 1810:18 Kut 22:21, 22-24; 23:9; Law 19:33; Kum 27:19; Ay 29:13; Za 94:6; Isa 10:2; Yer 49:11; Hes 10:32Huwapigania yatima na wajane, humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi. 1910:19 Kum 7:12; Kut 22:21; Kum 24:19; Law 19:34; Eze 47:22-23Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri. 2010:20 Mt 4:10; Kum 11:22; 13:4; 30:20; Yos 23:8; Rut 1:14; 2Fal 18:6; Za 119:31; Isa 38:3; Kut 20:7; Za 63:11Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake. 2110:21 Kut 15:2; 1Sam 12:24; Za 126:2; 2Sam 7:23; Yer 17:14; Za 106:21-22Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe. 2210:22 Mwa 34:30; 46:26; Mdo 7:14; Mwa 12:2; Hes 10:36Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.

La Bible du Semeur

Deutéronome 10:1-22

L’Eternel pardonne

1Alors, l’Eternel m’a dit : « Taille-toi deux tablettes de pierre pareilles aux premières et viens me trouver sur la montagne ; tu fabriqueras aussi un coffre en bois. 2J’inscrirai sur les tablettes les paroles qui étaient gravées sur les premières que tu as brisées et tu les déposeras dans le coffre. » 3Je fabriquai donc un coffre en bois d’acacia et je taillai deux tablettes de pierre semblables aux premières. Après quoi, je gravis la montagne, les deux tablettes en main. 4L’Eternel écrivit sur les nouvelles tablettes comme il l’avait fait sur les premières, les dix commandements qu’il vous avait communiqués sur la montagne du milieu du feu, le jour où vous étiez assemblés, et il me les remit. 5Je m’en retournai et redescendis de la montagne. Puis je déposai les tablettes dans le coffre que j’avais fabriqué : elles y sont restées comme l’Eternel me l’avait ordonné.

6Les Israélites10.6 Les v. 6-9 se rapportent à des événements postérieurs à ceux du Sinaï. partirent des puits des descendants de Yaaqân pour Moséra. C’est là que mourut Aaron, et qu’il fut enseveli. Eléazar, son fils, lui succéda comme grand-prêtre10.6 Voir Nb 20.28 ; 33.38.. 7De là, ils partirent pour Goudgoda, puis de là pour Yotbata où abondent les cours d’eau10.7 Dernière marche dans le désert, la quarantième année de leurs pérégrinations.. 8C’est à cette époque que l’Eternel choisit la tribu de Lévi pour porter le coffre de l’alliance de l’Eternel et se tenir en sa présence, pour être à son service et pour bénir le peuple en son nom – comme elle l’a fait jusqu’à ce jour10.8 Voir Nb 3.5-8 ; 8.5-19.. 9C’est pour cela que la tribu de Lévi n’a reçu ni part, ni patrimoine foncier comme ses tribus sœurs ; c’est l’Eternel ton Dieu qui est son patrimoine, comme il le lui a promis.

10Moi donc, je suis resté sur la montagne pendant quarante jours et quarante nuits, comme la première fois10.10 Voir Ex 34.28.. Et cette fois-ci encore, l’Eternel m’exauça et renonça à vous détruire. 11Il me dit : « Lève-toi, va prendre la tête de ce peuple pour qu’ils partent à la conquête du pays que j’ai promis par serment à leurs ancêtres ! »

L’appel à changer de vie

12Et maintenant, Israël, qu’attend de toi l’Eternel ton Dieu ? Simplement que tu le craignes en suivant toutes les voies qu’il t’a prescrites, en l’aimant et en le servant de tout ton cœur et de tout ton être, 13en observant ses commandements et ses lois que je te prescris aujourd’hui pour ton bien. 14Voici : le ciel, et même les cieux les plus élevés, appartiennent à l’Eternel ton Dieu ainsi que la terre et tout ce qu’elle contient. 15Et pourtant, c’est uniquement à tes ancêtres que l’Eternel s’est attaché pour les aimer, et c’est leurs descendants, c’est-à-dire vous, qu’il a choisis parmi tous les peuples, comme vous le constatez aujourd’hui. 16Opérez donc aussi une circoncision dans votre cœur et ne vous rebellez plus contre l’Eternel ; 17car l’Eternel votre Dieu est le Dieu suprême et le Seigneur des seigneurs10.17 Titre repris en 1 Tm 6.15 ; Ap 17.14 ; 19.16., le grand Dieu, puissant et redoutable, qui ne fait pas de favoritisme10.17 Voir Ac 10.34 ; Rm 2.11 ; Ep 6.9. et ne se laisse pas corrompre par des présents. 18Il rend justice à l’orphelin et à la veuve et témoigne son amour à l’étranger en lui assurant le pain et le vêtement. 19Vous aussi, vous aimerez l’étranger parmi vous, car vous avez été étrangers en Egypte.

Israël face à un choix

Craindre l’Eternel

20C’est l’Eternel ton Dieu que tu craindras, c’est à lui que tu rendras un culte, à lui seul que tu t’attacheras, et si tu prêtes serment, c’est par son nom que tu le feras. 21Il est le sujet de tes louanges, il est ton Dieu ; c’est lui qui a accompli pour toi ces œuvres extraordinaires et redoutables dont tu as été témoin10.21 Voir Ex 7 à 12.. 22Tes ancêtres vinrent en Egypte au nombre de soixante-dix10.22 Voir Gn 46.27 ; Ex 1.5 ; Ac 7.14., et maintenant l’Eternel ton Dieu t’a rendu aussi nombreux10.22 Voir Gn 15.5 ; 22.17 ; Hé 11.12. que les étoiles du ciel.