Isaya 9 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 9:1-21

Kwa Ajili Yetu Mtoto Amezaliwa

19:1 2Fal 15:29; 1Nya 5:26; Law 26:24; Ay 15:24Hata hivyo, hapatakuwepo huzuni tena kwa wale waliokuwa katika dhiki. Wakati uliopita aliidhili nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, lakini katika siku zijazo ataiheshimu Galilaya ya Mataifa, karibu na njia ya bahari, kando ya Yordani:

29:2 Mt 4:15-16; Eze 5:8; Mal 4:2; Yn 8:12; Za 82:5; 107:10-14; 36:9; Isa 8:20; Efe 5:8Watu wanaotembea katika giza

wameona nuru kuu,

wale wanaoishi katika nchi ya uvuli wa mauti,

nuru imewazukia.

39:3 Ay 12:23; Isa 25:9; Kut 15:9; Za 119:162; 4:7; Yos 22:8Umelikuza taifa,

na kuzidisha furaha yao,

wanafurahia mbele zako,

kama watu wanavyofurahia wakati wa mavuno,

kama watu wafurahivyo

wagawanyapo nyara.

49:4 Amu 7:22-25; Nah 1:13; Isa 10:26-27; Mt 11:30; Isa 60:18; Ay 34:24; Isa 37:36-38; 14:24; Yer 2:20; Za 81:6Kama vile siku ya kushindwa kwa Wamidiani,

umevunja nira iliyowalemea,

ile gongo mabegani mwao na

fimbo yake yeye aliyewaonea.

59:5 Isa 2:4Kila kiatu cha askari kilichotumiwa vitani,

na kila vazi lililovingirishwa katika damu

vitawekwa kwa ajili ya kuchomwa,

vitakuwa kuni za kuwasha moto.

69:6 Ebr 13:20; Mwa 3:15; Ay 15:8; Amu 13:18; Mt 28:18; Za 24:8; Lk 2:14; Mwa 3:15Kwa maana, kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,

tumepewa mtoto mwanaume,

nao utawala utakuwa mabegani mwake.

Naye ataitwa

Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu,

Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.

79:7 Dan 2:44; Yn 12:34; Yer 23:5; 2Fal 19:31; Za 85:8; 1Kor 15:25; 2Sam 7:13Kuongezeka kwa utawala wake na amani

hakutakuwa na mwisho.

Atatawala katika kiti cha enzi cha Daudi

na juu ya ufalme wake,

akiuthibitisha na kuutegemeza

kwa haki na kwa adili,

tangu wakati huo na hata milele.

Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote

utatimiza haya.

Hasira Ya Bwana Dhidi Ya Israeli

8Bwana ametuma ujumbe dhidi ya Yakobo,

utamwangukia Israeli.

99:9 Isa 7:9; Eze 2:4; Zek 7:11; Isa 2:4Watu wote watajua hili:

Efraimu na wakazi wa Samaria,

wanaosema kwa kiburi

na majivuno ya mioyo,

109:10 Mwa 11:3; Amo 7:14; Lk 19:14; 1Fal 7:2-3“Matofali yameanguka chini,

lakini tutajenga tena kwa mawe yaliyochongwa,

mitini imeangushwa,

lakini tutapanda mierezi badala yake.”

119:11 Isa 7:8Lakini Bwana amemtia nguvu adui wa Resini dhidi yao

na kuchochea watesi wao.

129:12 Za 79:7; Isa 5:25; 2Fal 16:6; Ay 40:11Waashuru kutoka upande wa mashariki

na Wafilisti kutoka upande wa magharibi

wameila Israeli kwa kinywa kilichopanuliwa.

Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali,

mkono wake bado umeinuliwa juu.

139:13 Yer 5:3; Amo 4:6-10; Sef 1:16; 2Nya 28:22; Hag 2:17; Dan 9:13; Yer 50:4; Isa 17:7Lakini watu hawajamrudia yeye aliyewapiga,

wala hawajamtafuta Bwana Mwenye Nguvu Zote.

149:14 Isa 19:15; Ufu 18:8Kwa hiyo Bwana atakatilia mbali kutoka Israeli kichwa na mkia,

tawi la mtende na tete katika siku moja.

159:15 Isa 3:2-3; 5:13; 28:7; Ay 13:4; Eze 13:2, 22; Mt 24:24Wazee na watu mashuhuri ndio vichwa,

nao manabii wanaofundisha uongo ndio mkia.

169:16 Mt 15:14; 23:16, 24; Isa 3:12Wale wanaowaongoza watu hawa wanawapotosha,

nao wale wanaoongozwa wamepotoka.

179:17 Amo 8:13; Rum 3:13-14; Yer 13:14; Isa 32:6; Mik 7:2; Isa 5:25; Yer 9:21; 11:22; Isa 27:11; 5:25; Mt 12:34; Yer 48:15; 49:26Kwa hiyo Bwana hatawafurahia vijana,

wala hatawahurumia yatima na wajane,

kwa kuwa kila mmoja wao hamchi Mungu, nao ni waovu,

na kila kinywa kinanena upotovu.

Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali,

mkono wake bado umeinuliwa juu.

189:18 Za 83:14; Kum 29:23; Isa 1:31; 5:6Hakika uovu huwaka kama moto;

huteketeza michongoma na miiba,

huwasha moto vichaka vya msituni,

hujiviringisha kuelekea juu kama nguzo ya moshi.

199:19 Mik 7:2-6; Isa 13:9-13; Ay 40:11; Za 97:3; Isa 1:31; Yer 17:27; Isa 3:5Kwa hasira ya Bwana Mwenye Nguvu Zote

nchi itachomwa kwa moto,

nao watu watakuwa kuni za kuchochea moto.

Hakuna mtu atakayemhurumia ndugu yake.

209:20 Law 26:26; Ay 18:12; Isa 49:26; Zek 11:9Upande wa kuume watakuwa wakitafuna,

lakini bado wataona njaa;

upande wa kushoto watakuwa wakila,

lakini hawatashiba.

Kila mmoja atajilisha kwa nyama ya mtoto wake mwenyewe:

219:21 Amu 7:22; 12:4; 2Nya 28:6; Isa 5:25Manase atamla Efraimu,

naye Efraimu atamla Manase;

nao pamoja watakuwa kinyume na Yuda.

Hata kwa haya yote, hasira yake haijageukia mbali,

mkono wake bado umeinuliwa juu.

Hoffnung für Alle

Jesaja 9:1-20

1Das Volk, das in der Finsternis lebt, sieht ein großes Licht; hell strahlt es auf über denen, die ohne Hoffnung sind. 2Du, Herr, machst Israel wieder zu einem großen Volk und schenkst ihnen überströmende Freude. Sie sind fröhlich wie nach einer reichen Ernte; sie jubeln wie nach einem Sieg, wenn die Beute verteilt wird. 3So wie du Israel damals aus der Gewalt der Midianiter gerettet hast, so befreist du sie dann von der schweren Last der Fremdherrschaft. Du zerbrichst die Peitsche, mit der sie zur Zwangsarbeit getrieben werden. 4Die Soldatenstiefel, die beim Marschieren so laut dröhnen, und all die blutverschmierten Kampfgewänder werden ins Feuer geworfen und verbrannt.

5Denn uns ist ein Kind geboren! Ein Sohn ist uns geschenkt! Er wird die Herrschaft übernehmen. Man nennt ihn »Wunderbarer Ratgeber«, »Starker Gott«, »Ewiger Vater«, »Friedensfürst«. 6Er wird seine Herrschaft weit ausdehnen und dauerhaften Frieden bringen. Auf dem Thron Davids wird er regieren und sein Reich auf Recht und Gerechtigkeit gründen, jetzt und für alle Zeit. Der Herr, der allmächtige Gott, wird dies eintreffen lassen, leidenschaftlich verfolgt er sein Ziel.

Der Zorn des Herrn hat sich noch nicht gelegt

7Der Herr hat ein hartes Urteil über die Nachkommen von Jakob verhängt. Das Reich Israel wird es zu spüren bekommen, 8ja, es wird die Bewohner von Israel und die Einwohner Samarias treffen. Voller Hochmut prahlen sie: 9»Unsere Häuser aus Ziegelsteinen sind zwar zerstört, doch nun bauen wir uns neue aus Quadersteinen. Die knorrigen Maulbeerbäume wurden alle gefällt. Was soll’s, wir pflanzen Zedern dafür an!« 10Darum hat der Herr die Feinde von König Rezin stark gemacht und sie gegen Israel zum Krieg angestachelt. 11Die Syrer sind von Osten her ins Land eingefallen, und die Philister griffen von Westen an. Sie stürzten sich mit weit aufgerissenem Maul auf Israel und verschlangen ganze Stücke davon. Aber trotz allem hat sich Gottes Zorn nicht gelegt; noch ist seine strafende Hand erhoben.

12Der Herr, der allmächtige Gott, bestraft sein Volk hart, aber es kehrt nicht zu ihm zurück, ja, es fragt nicht einmal nach ihm. 13-14Darum wird der Herr an ein und demselben Tag Kopf und Schwanz von Israel abschlagen. Der Kopf, das sind die Führer des Volkes, die angesehenen Männer und Sippenoberhäupter; der Schwanz, das sind die angeblichen Propheten mit ihren falschen Weissagungen. Wie man die obersten Zweige der Palmen und die Binsen im Sumpf abschneidet, so wird Gott an einem Tag das ganze Volk vernichten. 15Denn die Führer dieses Volkes sind nichts als Verführer. Wer sich ihnen anvertraut, wird in die Irre geleitet. 16Darum verschont der Herr die jungen Männer nicht und hat kein Mitleid mit den Witwen und Waisen. Denn sie alle haben sich gegen ihn aufgelehnt, ihr ganzes Leben besteht aus Lug und Betrug. Aber noch hat sich Gottes Zorn nicht gelegt; noch ist seine strafende Hand erhoben.

17Durch ihre Gottlosigkeit sprechen sie sich selbst das Urteil. Ihre Bosheit gleicht einer lodernden Flamme, die Unkraut und Dornensträucher verzehrt und das dichte Unterholz im Wald in Brand steckt, bis schwarze Rauchsäulen aufsteigen. 18In seinem glühenden Zorn denkt der Herr, der allmächtige Gott, gar nicht daran, dieses Feuer einzudämmen. Zurück bleibt ein zerstörtes Land, ein Land, in dem jeder gegen jeden kämpft. Niemand kümmert sich um den anderen, 19jeder will nur seinen Hunger stillen. Gierig und rücksichtslos fällt man über alles Essbare her und wird trotzdem nicht satt. Am Ende zerfleischen sie sich gegenseitig: 20Die Leute vom Stamm Manasse stürzen sich auf den Stamm Ephraim, die von Ephraim gehen auf Manasse los, und zusammen fallen sie über Juda her. Und immer noch ist Gottes Zorn nicht gestillt; drohend schwebt seine Hand über diesem Volk.