Isaya 8 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 8:1-22

Ashuru, Chombo Cha Bwana

18:1 Kum 27:8; Ay 19:23; Yer 20:3; 51:60; Isa 30:8; 8:3; Hos 1:4Bwana akaniambia, “Chukua gombo kubwa, uandike juu yake kwa kalamu ya kawaida jina: Maher-Shalal-Hash-Bazi.8:1 Maher-Shalal-Hash-Bazi maana yake ni Haraka kuteka nyara, Upesi kwenye hizo nyara. 28:2 2Fal 16:10; Yos 24:22; Rut 4:9; Yer 10:10-12; 32:10Nami nitawaita kuhani Uria, na Zekaria mwana wa Yeberekia kama mashahidi wangu waaminifu.”

38:3 Kut 15:20; Mwa 3:15Kisha nikaenda kwa nabii mke, naye akapata mimba, akazaa mwana. Kisha Bwana akaniambia, “Mwite huyo mtoto Maher-Shalal-Hash-Bazi. 48:4 Isa 7:8, 16; Mwa 14:15; Isa 7:8Kabla mtoto hajaweza kusema ‘Baba yangu’ au ‘Mama yangu,’ utajiri wa Dameski na nyara za Samaria zitachukuliwa na mfalme wa Ashuru.”

5Bwana akasema nami tena:

68:6 Neh 3:15; Isa 5:24; 7:1; Yn 9:7“Kwa sababu watu hawa wamekataa maji ya Shilo yatiririkayo taratibu

wakamfurahia Resini na mwana wa Remalia,

78:7 Isa 7:20; Dan 11:40; Nah 1:8; 2Nya 28:20; Isa 17:12-13; 30:28; Yos 3:15; Isa 10:16kwa hiyo Bwana yu karibu kuleta dhidi yao

mafuriko makubwa ya Mto:8:7 Yaani Frati.

yaani mfalme wa Ashuru na fahari yake yote.

Yatafurika juu ya mifereji yake yote,

yatamwagikia juu ya kingo zake zote,

88:8 Isa 7:14; 28:15; 18:6; 46:11; Yer 4:13; 48:40na kufika hadi Yuda, yakizunguka kwa kasi juu yake,

yakipita katikati na yakifika hadi shingoni.

Mabawa yake yaliyokunjuliwa

yatafunika upana wa nchi yako,

Ee Imanueli!”8:8 Imanueli maana yake Mungu yu pamoja nasi.

98:9 Isa 17:12-13; Eze 38:7; 38:3; Zek 14:2-3; Ay 34:24; Yer 46:3; 6:4; Zek 14:2; Yos 6:5Inueni kilio cha vita, enyi mataifa,

na mkavunjwevunjwe!

Sikilizeni, enyi nyote nchi za mbali.

Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe!

Jiandaeni kwa vita, nanyi mkavunjwevunjwe!

108:10 Ay 5:12; Isa 7:7, 14; Rum 8:31; Mit 19:21; Mt 1:23Wekeni mikakati yenu, lakini itashindwa;

fanyeni mipango yenu, lakini haitafanikiwa,

kwa maana Mungu yu pamoja nasi.8:10 Kiebrania ni Imanueli.

Mwogope Mungu

118:11 Eze 3:14; 2:8; 1:3Bwana alisema nami mkono wake wenye nguvu ukiwa juu yangu, akinionya nisifuate njia za taifa hili. Akasema:

128:12 Isa 36:6; 7:2; 20:5; 1Pet 3:14; Mt 10:28“Usiite fitina kila kitu ambacho watu hawa hukiita fitina,

usiogope kile wanachokiogopa,

wala usikihofu.

138:13 Hes 20:12; Isa 29:23; Kut 20:20Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye peke yake

ikupasaye kumheshimu kuwa mtakatifu,

ndiye peke yake utakayemwogopa,

ndiye peke yake utakayemhofu,

148:14 Rum 9:33; Eze 11:16; Isa 24:17-18; Za 118:22; Yer 6:21; Lk 2:34; Isa 4:6; Lk 20:18; Eze 3:20naye atakuwa mahali patakatifu;

lakini kwa nyumba zote mbili za Israeli atakuwa

jiwe lile linalosababisha watu kujikwaa

na mwamba wa kuwaangusha.

Kwa watu wa Yerusalemu,

atakuwa mtego na tanzi.

158:15 Lk 20:18; Isa 28:13; 59:10; Rum 9:32; Mt 4:19; Lk 20:18; Isa 59:10Wengi wao watajikwaa;

wataanguka na kuvunjika,

watategwa na kunaswa.”

168:16 Dan 8:26; 12:4; Yer 32:14; Rut 4:7; Isa 29:11-12Funga ushuhuda na kutia muhuri sheria

miongoni mwa wanafunzi wangu.

178:17 Kum 31:17; Za 27:14; 22:5; Ebr 2:13Nitamngojea Bwana,

ambaye ameificha nyumba ya Yakobo uso wake.

Nitaliweka tumaini langu kwake.

188:18 Mwa 33:5; Ebr 2:13; Kut 3:12; Lk 2:34; Eze 12:6; 24:24; 4:3; Kum 28:46; Eze 12:11; Za 9:11Niko hapa, pamoja na watoto ambao Bwana amenipa. Sisi ni ishara na mfano wake katika Israeli, kutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayeishi juu ya Mlima Sayuni.

198:19 1Sam 28:8; Isa 29:4; Hes 27:21; Law 19:31Wakati watu wanapowaambia ninyi kutafuta ushauri kwa waaguzi na wenye kuongea na mizimu, ambao hunongʼona na kunungʼunika, je, watu wasingeuliza kwa Mungu wao? Kwa nini watake shauri kwa wafu kwa ajili ya walio hai? 208:20 Mik 3:6; Isa 60:2; 1:10; Rut 4:7; Lk 16:29; Isa 9:2; 59:9; 9:2Kwa sheria na kwa ushuhuda! Kama hawatasema sawasawa na neno hili, hawana mwanga wa mapambazuko. 218:21 Ay 18:12; Kut 22:28; Ay 30:3; Ufu 16:11Watazunguka katika nchi yote, wakiwa na dhiki na njaa. Watakapotaabika kwa njaa, watapatwa na hasira kali, nao, wakiwa wanatazama juu, watamlaani mfalme wao na Mungu wao. 228:22 Ay 15:24; 3:13; Isa 5:30; Ufu 16:10; Mt 25:30Kisha wataangalia duniani na kuona tu dhiki na giza, hofu na huzuni tupu, nao watasukumiwa kwenye giza nene kabisa.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Isaías 8:1-22

Asiria, el instrumento del Señor

1El Señor me dijo: «Toma una tablilla grande y, con un estilete común, escribe sobre ella: “Tocante a Maher Salal Jasbaz”.8:1 En hebreo, Maher Salal Jasbaz significa Pronto al saqueo, presto al botín; también en v. 3. 2Yo convocaré como testigos confiables al sacerdote Urías y a Zacarías hijo de Jeberequías».

3Luego tuve relaciones con la profetisa, y ella concibió y dio a luz un hijo. Entonces el Señor me dijo: «Ponle por nombre Maher Salal Jasbaz. 4Antes de que el niño aprenda a decir “papá” y “mamá”, la riqueza de Damasco y el botín de Samaria serán llevados ante el rey de Asiria».

5El Señor volvió a decirme:

6«Por cuanto este pueblo ha rechazado

las mansas corrientes de Siloé

y se regocija con Rezín

y con el hijo de Remalías,

7el Señor está a punto de traer contra ellos

las impetuosas crecidas del río Éufrates:

al rey de Asiria con toda su gloria.

Rebasará todos sus canales,

desbordará todas sus orillas;

8pasará hasta Judá, la inundará,

y crecerá hasta llegarle al cuello.

Sus alas extendidas, ¡oh Emanuel!,8:8 En hebreo, Emanuel significa Dios con nosotros; véase también v. 10.

cubrirán la anchura de tu tierra».

9Escuchad esto, naciones,

todas las naciones lejanas:

¡Alzad el grito de guerra,

y seréis destrozadas!

¡Preparaos para la batalla,

y seréis despedazadas!

¡Preparaos para la batalla,

y seréis desmenuzadas!

10Trazad vuestra estrategia,

pero será desbaratada;

proponed vuestro plan,

pero no se realizará,

porque Dios está con nosotros.8:10 Dios está con nosotros. Lit. Emanuel; véase v. 8.

Hay que temer a Dios

11El Señor me habló fuertemente y me advirtió que no siguiera el camino de este pueblo. Me dijo:

12«No digáis que es conspiración

todo lo que llama conspiración esta gente;

no temáis lo que ellos temen,

ni os dejéis asustar.

13Solo al Señor Todopoderoso

tendréis por santo,

solo a él debéis honrar,

solo a él habéis de temer.

14El Señor será un santuario.

Pero será una piedra de tropiezo

para las dos casas de Israel;

¡una roca que los hará caer!

¡Será para los habitantes de Jerusalén

un lazo y una trampa!

15Muchos de ellos tropezarán;

caerán y serán quebrantados.

Se les tenderán trampas,

y en ellas quedarán atrapados».

16Guarda bien el testimonio;

sella la ley entre mis discípulos.

17El Señor ha escondido su rostro

del pueblo de Jacob,

pero yo esperaré en él,

pues en él tengo puesta mi esperanza.

18Aquí me tenéis, con los hijos que el Señor me ha dado. Somos en Israel señales y presagios del Señor Todopoderoso, que habita en el monte Sión.

19Si alguien os dice: «Consultad a las pitonisas y a los agoreros que susurran y musitan; ¿acaso no es deber de un pueblo consultar a sus dioses y a los muertos, en favor de los vivos?», 20yo os digo: «¡Ateneos a la ley y al testimonio!» Para quienes no se atengan a esto, no habrá un amanecer.

21Vosotros os enfureceréis cuando, angustiados y hambrientos, vaguéis por la tierra. Levantando los ojos al cielo, maldeciréis a vuestro rey y a vuestro Dios, 22y, clavando la mirada en la tierra, solo veréis aflicción, tinieblas y espantosa penumbra; ¡seréis arrojados a una oscuridad total!