Isaya 63 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 63:1-19

Siku Ya Mungu Ya Kisasi Na Ukombozi

163:1 Mwa 36:33; Amo 1:12; Yer 42:11; Sef 3:17; 2Nya 28:17; Isa 11:14; Ufu 19:13; Ay 9:4Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu,

kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu?

Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari,

anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake?

“Mimi ndimi, nisemaye katika haki,

mwenye nguvu wa kuokoa.”

263:2 Ufu 19:13; Mwa 49:11Kwa nini mavazi yako ni mekundu,

kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?

363:3 Amu 6:11; Ufu 19:15; Mao 1:15; Ufu 19:13; 14:19-20; Za 108:13“Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu;

kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami.

Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu

na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu;

damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu,

na kutia madoa nguo zangu zote.

463:4 Isa 1:24; Yer 50:15Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu,

mwaka wa ukombozi wangu umefika.

563:5 2Fal 14:26; Isa 41:28; 59:16; Za 44:3; Yn 16:32; Isa 33:2Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia,

nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada;

hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu,

na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.

663:6 Isa 29:9; Mao 4:21; Isa 34:3; Ay 40:12Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu,

katika ghadhabu yangu niliwalewesha,

na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”

Kusifu Na Kuomba

763:7 Isa 54:8; Efe 2:4; Kut 18:9Nitasimulia juu ya wema wa Bwana,

kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa,

sawasawa na yote ambayo Bwana

ametenda kwa ajili yetu:

naam, mambo mengi mema aliyoyatenda

kwa ajili ya nyumba ya Israeli,

sawasawa na huruma zake

na wema wake mwingi.

863:8 Mdo 9:4; Kut 14:19; 33:14; Kum 7:7-8; Ezr 9:9; Za 28:9; Ay 37:23Alisema, “Hakika wao ni watu wangu,

wana ambao hawatanidanganya”;

hivyo akawa Mwokozi wao.

963:9 Kut 14:19; 33:14; Kum 7:7-8; Ezr 9:9; Isa 48:20; Kum 1:31; 32:7; Za 28:9; Ay 37:23Katika taabu zao zote naye alitaabika,

na malaika wa uso wake akawaokoa.

Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa,

akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.

1063:10 Eze 20:8; Mdo 7:39-42; Efe 4:30; Za 106:40; 78:17; Isa 10:4; Yos 10:14Lakini waliasi,

na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake.

Hivyo aligeuka na kuwa adui yao,

na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.

1163:11 Kut 14:22, 30; Hes 11:17; Za 77:20Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita,

siku za Mose na watu wake:

yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari,

pamoja na wachungaji wa kundi lake?

Yuko wapi yule aliyeweka

Roho wake Mtakatifu katikati yao,

1263:12 Kut 14:21-22; Isa 11:15; Mwa 49:24aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu

kuwa katika mkono wa kuume wa Mose,

aliyegawa maji ya bahari mbele yao,

ili kujipatia jina milele,

1363:13 Kum 32:12; Yer 31:9; Kut 14:24; Za 119:11aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi?

Kama farasi katika nchi iliyo wazi,

wao hawakujikwaa,

1463:14 Kut 33:14; Kum 12:9kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho,

walipewa pumziko na Roho wa Bwana.

Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako

ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.

1563:15 Za 80:14; Mao 3:50; 1Fal 22:19; 2:26; Hos 11:8; Kum 26:15; Isa 64:12Tazama chini kutoka mbinguni ukaone

kutoka kiti chako cha enzi

kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu.

Uko wapi wivu wako na uweza wako?

Umetuzuilia wema wako na huruma zako.

1663:16 Ay 14:21; Gal 3:28; Isa 44:6; Kut 4:22; Yer 3:4; Yn 8:41; Isa 59:20Lakini wewe ni Baba yetu,

ingawa Abrahamu hatufahamu sisi

wala Israeli hatutambui;

wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu,

Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.

1763:17 Isa 6:10; 29:13; Hes 10:36; Mt 13:15; Mwa 20:13; Mao 3:9; Kut 4:21; 34:9Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako,

na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu?

Rudi kwa ajili ya watumishi wako,

yale makabila ambayo ni urithi wako.

1863:18 Law 26:31; Dan 8:24; Za 74:3-8; Kum 4:26; Isa 28:18; Lk 21:24; Dan 8:13Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu,

lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.

1963:19 Isa 43:7; Yer 14:9Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe,

kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.

Japanese Contemporary Bible

イザヤ書 63:1-19

63

神の復讐と救いの日

1エドムから来る、あの人はだれですか。

目にも鮮やかな深紅の衣を着て、

ボツラの町から来る、あの人はだれですか。

王の衣をまとい、威風堂々とやって来る、

あの人はだれですか。

「それは、あなたに救いを告げ知らせる主だ。

大きな力をもって救う主だ。」

2「どうしてお着物が、

ぶどうを踏みしぼったときのように真っ赤なのですか。」

3「わたしは、ひとりで酒ぶねを踏んだ。

手伝ってくれる者は一人もいなかった。

わたしは激しく怒り、

敵をぶどうのように踏みつぶした。

真っ赤になって怒り、敵を踏みにじった。

着物に染みついているのは、彼らの血だ。

4わたしの民のかたきを討ち、

虐げる者の手から救い出す時がついに来たのだ。

5わたしは辺りを見回したが、

彼らに手を貸す者は一人もいなかった。

わたしはあきれ返り、身のすくむ思いをした。

だから、だれの手も借りず、ひとりで復讐したのだ。

6わたしが怒って国々を踏みつけたので、

彼らはよろめき、倒れた。」

賛美と祈り

7私は神の恵みを人々に知らせます。

そのなさったすべてのことのゆえに神をたたえます。

私はまた、イスラエルに示された

神の深いあわれみを喜びます。

神は愛によって、あわれみを示したのです。

8「彼らはわたしのものだ。

彼らはもう二度と道を誤らない」

と、神は言いました。

こうして神は、彼らの救い主となったのです。

9彼らが苦しむとき、神はいつもいっしょに苦しみ、

彼らを救い出しました。

神は、ご自分の愛によって彼らを買い戻し、

彼らを高く掲げ、これまでずっと彼らを導きました。

10ところが、彼らは神に反抗し、

神の御霊を悲しませたのです。

それで神は、彼らの敵となり、彼らと戦ったのです。

11その時、彼らは神のしもべモーセが

イスラエルをエジプトから連れ出した時のことを

思い出し、叫びました。

「モーセを羊飼いに立てて、イスラエルの民を導き、

海を通らせた方は、どこにいますか。

ご自分の国の中に御霊を送られた神は、

どこにいますか。

12モーセが手をあげた時、

人々の見ている前で海を二つに分け、

ご自分の評判を永遠のものとした方は、

どこにいますか。

13人々に海の底を通らせたのは、どなたですか。

彼らは荒野を駆け巡る優秀な馬のように、

少しもつまずきませんでした。

14谷間で草を食べる家畜のように、

主の御霊は彼らに休息を与えました。」

こうして神は自ら、ご自分の名声を

不動のものとしたのです。

15ああ主よ、どうか天から見下ろして、

栄光に輝く聖なるお住まいから、

私たちに目を留めてください。

いつも示してくださった愛は、

どこへ行ったのですか。

神の力、あわれみ、同情は、

いったいどこにあるのですか。

16神が今でも私たちの父であることに、

変わりはありません。

たとえ、アブラハムとヤコブが私たちを見捨てても、

神は私たちの父であり、大昔からの救い主です。

17主よ、なぜ私たちを頑固にし、

罪を犯して神に背くようにされたのですか。

どうか、戻って来て、私たちを助けてください。

私たちは神のもの、どうしても神が必要です。

18エルサレムが私たちのものであった期間は、

なんと短かったことでしょう。

敵はこの都を破壊しました。

19ああ神よ、どうして私たちを、

主の名で呼ばれたことのない外国人のように

取り扱われるのですか。