Isaya 57 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 57:1-21

Ibada Ya Sanamu Ya Israeli Iliyo Batili

157:1 Eze 21:3; 2Fal 22:20; Za 12:1; Isa 42:25Mwenye haki hupotea,

wala hakuna hata mmoja awazaye hilo moyoni mwake;

watu wanaomcha Mungu huondolewa,

wala hakuna hata mmoja anayeelewa

kuwa wenye haki wameondolewa

ili wasipatikane na maovu.

257:2 Isa 26:7; Kum 12:13Wale waendao kwa unyofu

huwa na amani;

hupata pumziko walalapo mautini.

357:3 Mal 3:5; Yak 4:4; Yer 2:20; Kut 22:18; Mt 16:4; Isa 1:20“Lakini ninyi:

Njooni hapa, ninyi wana wa wachawi,

ninyi wazao wa wazinzi na makahaba!

457:4 Isa 1:2Mnamdhihaki nani?

Ni nani mnayemcheka kwa dharau,

na kumtolea ndimi zenu?

Je, ninyi si watoto wa waasi,

uzao wa waongo?

557:5 Kum 12:2; 2Fal 16:4; Eze 16:20; Kum 18:10; Isa 1:29; Law 18:21; 18:2; Za 106:37-38Mnawaka tamaa katikati ya mialoni

na chini ya kila mti uliotanda matawi;

mnawatoa kafara watoto wenu kwenye mabonde

na chini ya majabali yenye mianya.

657:6 2Fal 17:10; Hab 2:19; Yer 44:18; 19:13; 7:18; 3:9; 7:18; 5:9-29; 9:9; 2:19“Sanamu zilizo katikati ya mawe laini ya mabondeni ndizo fungu lenu;

hizo ndizo sehemu yenu.

Naam, kwa hizo mmemimina sadaka za vinywaji,

na kutoa sadaka za nafaka.

Katika haya yote,

niendelee kuona huruma?

757:7 Yer 3:6; Eze 6:3; 23:41; 20:29; 20:27-28Umeweka kitanda chako juu kwenye kilima kirefu kilichoinuka,

huko ulikwenda kutoa dhabihu zako.

857:8 Eze 16:26; 23:7, 18; 23:18Nyuma ya milango yako na miimo yako

umeweka alama zako za kipagani.

Kwa kuniacha mimi, ulifunua kitanda chako,

umepanda juu yake na kukipanua sana;

ulifanya patano na wale ambao unapenda vitanda vyao,

nawe uliangalia uchi wao.

957:9 Law 18:21; 1Fal 11:5; Wim 4:10; Eze 23:16, 40Ulikwenda kwa Moleki57:9 Moleki alikuwa mungu aliyekuwa anaabudiwa na Waamoni; pia alijulikana kama Malkomu, Maloki au Kemoshi wa Moabu. ukiwa na mafuta ya zeituni,

na ukaongeza manukato yako.

Ukawatuma wajumbe wako mbali sana,

ukashuka kwenye kaburi57:9 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. lenyewe!

1057:10 Yer 18:12; Mal 3:14; Isa 47:13; Yer 2:25; 1Sam 2:4Ulikuwa umechoshwa na njia zako zote,

lakini hukusema, ‘Hakuna tumaini.’

Ulipata uhuisho wa nguvu zako,

kwa sababu hiyo hukuzimia.

1157:11 Mit 29:25; Eze 22:12; Yer 18:15; Es 4:14; Za 50:21; Yer 3:21; 1Fal 1:15; Isa 17:10“Ni nani uliyemhofu hivyo na kumwogopa

hata ukawa mwongo kwangu,

wala hukunikumbuka

au kutafakari hili moyoni mwako?

Si ni kwa sababu nimekuwa kimya muda mrefu

hata huniogopi?

1257:12 Eze 16:2; Mik 2:2-8; Isa 29:15; 66:18Nitaifunua haki yako na matendo yako,

nayo hayatakufaidi.

1357:13 Za 37:3-9; Yer 30:15; Isa 2:2-3; Yer 22:20; Amu 10:14; Za 118:8; Isa 65:9-11Utakapolia kwa kuhitaji msaada,

sanamu zako ulizojikusanyia na zikuokoe!

Upepo utazipeperusha zote,

pumzi peke yake itazipeperusha,

Lakini mtu atakayenifanya kimbilio lake,

atairithi nchi

na kuumiliki mlima wangu mtakatifu.”

Faraja Kwa Wenye Majuto

1457:14 Isa 62:10; Yer 18:15; Isa 11:16Tena itasemwa:

“Jengeni, jengeni, itengenezeni njia!

Ondoeni vikwazo katika njia ya watu wangu.”

1557:15 Kum 33:27; Ay 6:10; Mik 6:8; Za 90:2; 2Fal 22:19; Zek 2:13; Isa 52:13; Ay 16:19Kwa maana hili ndilo asemalo Aliye juu, yeye aliyeinuliwa sana,

yeye aishiye milele, ambaye jina lake ni Mtakatifu:

“Ninaishi mimi mahali palipoinuka na patakatifu,

lakini pia pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu

na mwenye roho ya unyenyekevu,

ili kuzihuisha roho za wanyenyekevu

na kuihuisha mioyo yao waliotubu.

1657:16 Za 85:5; Mik 7:18; Ebr 12:9; Isa 3:13-14; 54:9; Zek 12:1Sitaendelea kulaumu milele,

wala sitakasirika siku zote,

kwa kuwa roho ya mwanadamu

ingezimia mbele zangu:

yaani pumzi ya mwanadamu niliyemuumba.

1757:17 Isa 56:11; Yer 8:10; Isa 30:15; 53:6; 66:3Nilighadhibika na tamaa yake ya dhambi;

nilimwadhibu, nikauficha uso wangu kwa hasira,

na bado aliendelea katika njia zake za tamaa.

1857:18 Kum 32:39; 2Nya 7:14; Isa 49:13; Za 48:14; Isa 42:16; 48:17Nimeziona njia zake, lakini nitamponya,

nitamwongoza na kumrudishia upya faraja,

1957:19 Isa 51:16; Ebr 13:15; Efe 2:17; Mdo 2:39; Lk 2:14; Isa 32:17; 26:3nikiumba sifa midomoni ya waombolezaji

katika Israeli.

Amani, amani, kwa wale walio mbali

na kwa wale walio karibu,”

asema Bwana. “Nami nitawaponya.”

2057:20 Ay 18:5-21; Mwa 49:4; Efe 4:14; Yud 13; Za 69:14Bali waovu ni kama bahari ichafukayo,

ambayo haiwezi kutulia,

mawimbi yake hutupa takataka na matope.

2157:21 Isa 26:3; Eze 13:16; Isa 59:8; 48:22Mungu wangu asema,

“Hakuna amani kwa waovu.”

Hoffnung für Alle

Jesaja 57:1-21

Der Herr richtet die Gottlosen

1Menschen, die dem Herrn die Treue halten, kommen um, aber niemanden kümmert das. Sie werden aus dem Leben gerissen, aber niemand begreift, dass Gott sie dadurch vor noch schlimmeren Zeiten bewahren will. 2Sie haben ein aufrichtiges Leben geführt, nun ruhen sie in Frieden.

3»Ihr aber, ihr Hexensöhne«, ruft der Herr, »tretet vor, um euer Urteil zu hören, ihr Brut von Ehebrechern und Huren! 4Über mich macht ihr euch lustig. Gegen mich reißt ihr frech das Maul auf und streckt mir die Zunge heraus. Wisst ihr überhaupt, was ihr da tut, ihr bösartiges und verlogenes Pack?

5Ihr seid nur noch hinter euren Götzen her! Unter jeder Eiche und allen dicht belaubten Bäumen hurt ihr zu Ehren eurer Götzen. Ihnen opfert ihr sogar Kinder! In den Felshöhlen unten im Tal schlachtet ihr sie! 6Ihr verehrt die abgeschliffenen Kieselsteine im Bachbett. Sie allein bestimmen euer Schicksal – denkt ihr. Und darum opfert ihr ihnen Wein und gute Speisen. Und da sollte ich ruhig zusehen? 7Ihr steigt hinauf zur Spitze eines hohen Berges, um eure Opfer darzubringen. Dort schlagt ihr euer Lager auf. 8Ihr bringt magische Zeichen an der Innenseite der Tür und den Torpfosten an. Von mir aber habt ihr euch abgewandt. Wie eine Hure bezieht ihr euer Bett für einen anderen und richtet es schön für ihn her. Ihr handelt den Lohn aus, und schließlich geht ihr mit ihm ins Bett. Ihr habt sogar noch Spaß an dem, was ihr da seht und tut! 9Zum Götzen Moloch57,9 Wörtlich: König. – Vermutlich liegt hier ein Wortspiel vor, da sich das hebräische Wort für »König« nur geringfügig von dem Namen des kanaanitischen Götzen unterscheidet. pilgert ihr und bringt ihm kostbares Öl mit, dazu eine Menge wohlriechender Salben. Ihr schickt Boten auf eine lange Reise: Bis zur Totenwelt sollen sie vordringen. 10Euch ist keine Anstrengung zu groß, nie gebt ihr zu: ›Ach, das nützt doch alles nichts!‹ Nein – ihr kommt immer wieder zu Kräften, und darum gebt ihr nicht auf.

11Vor wem habt ihr denn solche Angst? Warum fürchtet ihr andere mehr als mich und betrügt mich? Warum habt ihr keinen Gedanken mehr für mich übrig, warum vergesst ihr mich? Doch nur, weil ich eurem Treiben so lange schweigend zugesehen habe. Deshalb denkt ihr wohl, ihr hättet von mir nichts zu befürchten.

12Doch ich werde euch nun zeigen, was eure Anstrengungen wirklich wert sind: Alle eure Mühe nützt euch gar nichts! 13Schreit nur um Hilfe – sollen sie euch doch helfen, eure vielen Götzen! Ein kleiner Windstoß reicht, um sie wegzublasen. Nur ein Hauch – und fort sind sie!

Doch wer bei mir Zuflucht sucht, der wird das Land erben und darf auf meinem heiligen Berg wohnen.«

Ich will mein Volk heilen

14Der Herr befiehlt: »Macht euch an die Arbeit, schnell! Baut eine Straße! Räumt meinem Volk alle Hindernisse aus dem Weg! 15Ich, der Hohe und Erhabene, der ewige und heilige Gott, wohne in der Höhe, im Heiligtum. Doch ich wohne auch bei denen, die traurig und bedrückt sind. Ich gebe ihnen neuen Mut und erfülle sie wieder mit Hoffnung. 16Ich will sie nicht ständig anklagen und nicht für immer zornig sein. Denn sonst würden sie vergehen, die Menschen, die ich doch selbst geschaffen habe. 17Ich war zornig über mein Volk wegen seiner Habgier. Darum bestrafte ich sie und wandte mich von ihnen ab. Aber sie taten weiterhin, was sie wollten, und gingen ihre eigenen Wege. 18-19Ich sah ihre Taten genau. Und doch will ich ihnen wieder zurechthelfen und sie führen. Die Trauernden werde ich trösten; ein Freudenlied lege ich ihnen in den Mund. Dann werden sie alle in Frieden leben, ob in der Nähe oder in der Ferne, denn ich will mein Volk heilen. Das verspreche ich, der Herr.

20Die Gottlosen aber sind wie das ungestüme Meer: Es kommt nicht zur Ruhe, seine Wellen wühlen immer wieder Dreck und Schlamm auf. 21Ja, alle, die sich gegen mich auflehnen, werden keinen Frieden finden. Darauf gebe ich mein Wort!«