Isaya 54 – NEN & HCV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 54:1-17

Utukufu Wa Baadaye Wa Sayuni

154:1 Isa 49:20; Gal 4:27; Mwa 21:6; Za 98:4; Isa 66:7; 49:20“Imba, ewe mwanamke tasa,

wewe ambaye kamwe hukuzaa mtoto;

paza sauti kwa kuimba, piga kelele kwa furaha,

wewe ambaye kamwe hukupata utungu;

kwa sababu watoto wa mwanamke aliyeachwa ukiwa ni wengi

kuliko wa mwanamke mwenye mume,”

asema Bwana.

254:2 Mwa 26:22; Isa 26:15; Kut 35:18; 39:40; Isa 49:19-20“Panua mahali pa hema lako,

tandaza mapazia ya hema lako uyaeneze mbali,

wala usiyazuie;

ongeza urefu wa kamba zako,

imarisha vigingi vyako.

354:3 Mwa 13:14; Isa 48:19; Ay 12:23; Isa 14:2; 60:4-11; 49:19Kwa maana utaenea upande wa kuume

na upande wa kushoto;

wazao wako watayamiliki mataifa

na kukaa katika miji yao iliyoachwa ukiwa.

454:4 Isa 30:10; Yoe 2:21; Isa 28:16; Mwa 30:23; Za 25:7; 119:39; Yer 22:21; Isa 47:8“Usiogope, wewe hutaaibika.

Usiogope aibu, wewe hutaaibishwa.

Wewe utasahau aibu ya ujana wako,

wala hutakumbuka tena mashutumu ya ujane wako.

554:5 Wim 3:3; Isa 41:14; 48:17; Rum 3:29; Hos 2:7-16; Za 149:2; Isa 51:13Kwa maana Muumba wako ndiye mume wako,

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake,

yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ni Mkombozi wako,

yeye anaitwa Mungu wa dunia yote.

654:6 Isa 49:14-21; 60:15; 62:4; Yer 44:2; Hos 1:10; Kut 20:14; Mal 2:14Bwana atakuita urudi

kana kwamba ulikuwa mke aliyeachwa na kuhuzunishwa rohoni;

kama mke aliyeolewa bado angali kijana

na kukataliwa,” asema Mungu wako.

754:7 Ay 14:13; Isa 26:20; 2Kor 4:17; Isa 27:8; Za 71:11; Isa 49:18“Kwa kitambo kidogo nilikuacha,

lakini kwa huruma nyingi nitakurudisha.

854:8 Isa 9:12; Yer 31:3; Za 92:2; Isa 26:20; Za 25:6; Isa 55:3; 63:7; Hos 2:19Katika ukali wa hasira

nilikuficha uso wangu kwa kitambo,

lakini kwa fadhili za milele

nitakuwa na huruma juu yako,”

asema Bwana Mkombozi wako.

954:9 Mwa 8:21; Mik 7:18; Eze 39:29; Isa 14:24; Kum 28:20; Isa 49:18“Kwangu mimi jambo hili ni kama siku za Noa,

nilipoapa kuwa maji ya Noa kamwe hayatafunika tena dunia.

Hivyo sasa nimeapa sitawakasirikia ninyi,

kamwe sitawakemea tena.

1054:10 Za 46:2; Ebr 12:27; Mwa 9:16; Kut 34:10; Ufu 6:14; Hes 25:12; Isa 55:7Ijapotikisika milima, na vilima viondolewe,

hata hivyo upendo wangu usiokoma kwenu hautatikisika,

wala agano langu la amani halitaondolewa,”

asema Bwana, mwenye huruma juu yenu.

1154:11 Isa 14:32; 29:6; 1Nya 29:2; Ufu 21:18; 21:19-20; Isa 26:18; 28:16; Kut 24:10“Ewe mji uliyeteswa, uliyepigwa kwa dhoruba na usiyetulizwa,

nitakujenga kwa almasi, nitaweka misingi yako kwa yakuti samawi.

1254:12 Ufu 21:21Nitafanya minara yako ya akiki,

malango yako kwa vito vingʼaavyo,

nazo kuta zako zote za vito vya thamani.

1354:13 Mik 4:2; Ebr 8:11; Law 26:6; Isa 11:9; 28:9; 48:18; Yn 6:45Watoto wako wote watafundishwa na Bwana,

nayo amani ya watoto wako itakuwa kuu.

1454:14 2Sam 7:10; Isa 9:4; 17:14; 26:2; Yer 30:20; Sef 3:17; Zek 9:8Kwa haki utathibitika:

Kuonewa kutakuwa mbali nawe;

hutaogopa chochote.

Hofu itakuwa mbali nawe;

haitakukaribia wewe.

1554:15 Isa 41:11-16Kama mtu yeyote akikushambulia,

haitakuwa kwa ruhusa yangu;

yeyote akushambuliaye

atajisalimisha kwako.

1654:16 Isa 44:12; 10:5; 13:5“Tazama, ni mimi niliyemuumba mhunzi,

yeye afukutaye makaa kuwa moto,

na kutengeneza silaha inayofaa kwa kazi yake.

Tena ni mimi niliyemwambia mharabu

kufanya uharibifu mwingi.

1754:17 Isa 29:8; Mdo 6:10; Isa 45:24-25; 41:11; 56:6-8; Zek 1:20-21; Isa 65:8-9Hakuna silaha itakayofanyizwa dhidi yako

itakayofanikiwa,

nawe utauthibitisha kuwa mwongo

kila ulimi utakaokushtaki.

Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana

na hii ndiyo haki yao itokayo kwangu,”

asema Bwana.

Hindi Contemporary Version

यशायाह 54:1-17

येरूशलेम के भविष्य की महिमा

1यह याहवेह की वाणी है,

“बांझ, तुम, जो संतान पैदा करने में असमर्थ हो, आनंदित हो.

तुम, जो प्रसव पीड़ा से अनजान हो,

जय जयकार करो,

क्योंकि त्यागी हुई की संतान,

सुहागन की संतान से अधिक है.

2अपने तंबू के पर्दों को फैला दो,

इसमें हाथ मत रोको;

अपनी डोरियों को लंबा करो,

अपनी खूंटियों को दृढ़ करो.

3क्योंकि अब तुम दाएं तथा बाएं दोनों ही ओर को बढ़ाओगे;

तुम्हारे वंश अनेक देशों के अधिकारी होंगे

और उजड़े हुए नगर को फिर से बसाएंगे.

4“मत डर; क्योंकि तुम्हें लज्जित नहीं होना पड़ेगा.

मत घबरा; क्योंकि तू फिर लज्जित नहीं होगी.

तुम अपनी जवानी की लज्जा को भूल जाओगे

और अपने विधवापन की बदनामी को फिर याद न रखोगे.

5क्योंकि तुम्हें रचनेवाला तुम्हारा पति है—

जिसका नाम है त्सबाओथ54:5 त्सबाओथ अर्थात् सेना के याहवेह—

तथा इस्राएल के पवित्र परमेश्वर हैं;

जिन्हें समस्त पृथ्वी पर परमेश्वर नाम से जाना जाता है.

6क्योंकि याहवेह ने तुम्हें बुलाया है

तुम्हारी स्थिति उस पत्नी के समान थी—

जिसको छोड़ दिया गया हो,

और जिसका मन दुःखी था,” तेरे परमेश्वर का यही वचन है.

7“कुछ पल के लिए ही मैंने तुझे छोड़ा था,

परंतु अब बड़ी दया करके मैं फिर तुझे रख लूंगा.

8कुछ ही क्षणों के लिए

क्रोध में आकर तुमसे मैंने अपना मुंह छिपा लिया था,

परंतु अब अनंत करुणा और प्रेम के साथ

मैं तुम पर दया करूंगा,”

तेरे छुड़ानेवाले याहवेह का यही वचन है.

9“क्योंकि मेरी दृष्टि में तो यह सब नोहा के समय जैसा है,

जब मैंने यह शपथ ली थी कि नोहा के समय हुआ जैसा जलप्रलय अब मैं पृथ्वी पर कभी न करूंगा.

अतः अब मेरी यह शपथ है कि मैं फिर कभी तुम पर क्रोध नहीं करूंगा,

न ही तुम्हें कभी डाटूंगा.

10चाहे पहाड़ हट जाएं

और पहाड़ियां टल जायें,

तो भी मेरा प्रेम कभी भी तुम पर से न हटेगा

तथा शांति की मेरी वाचा कभी न टलेगी,”

यह करुणामय याहवेह का वचन है.

11“हे दुखियारी, तू जो आंधी से सताई है और जिसको शांति नहीं मिली,

अब मैं तुम्हारी कलश को अमूल्य पत्थरों से जड़ दूंगा,

तथा तुम्हारी नीवों को नीलमणि से बनाऊंगा.

12और मैं तुम्हारे शिखरों को मूंगों से,

तथा तुम्हारे प्रवेश द्वारों को स्फटिक से निर्मित करूंगा.

13वे याहवेह द्वारा सिखाए हुए होंगे,

और उनको बड़ी शांति मिलेगी.

14तू धार्मिकता के द्वारा स्थिर रहेगी:

अत्याचार तुम्हारे पास न आएगा;

तुम निडर बने रहना;

डर कभी तुम्हारे पास न आएगा.

15यदि कोई तुम पर हमला करे, तो याद रखना वह मेरी ओर से न होगा;

और वह तुम्हारे द्वारा हराया जाएगा.

16“सुन, लोहार कोयले की आग में

हथियार बनाता है, वह मैंने ही बनाया है

और बिगाड़ने के लिये भी मैंने एक को बनाया है.

17कोई भी हथियार ऐसा नहीं बनाया गया, जो तुम्हें नुकसान पहुंचा सके,

तुम उस व्यक्ति को, जो तुम पर आरोप लगाता है, दंड दोगे.

याहवेह के सेवकों का भाग यही है,

तथा उनकी धार्मिकता मेरी ओर से है,”

याहवेह ही का यह वचन है.